Zembwela wa Wasafi FM: Kutokana na hii Kero ya Tozo Lukuki natabiri 90% ya Wabunge hawatorudi tena Bungeni 2025

Zembwela wa Wasafi FM: Kutokana na hii Kero ya Tozo Lukuki natabiri 90% ya Wabunge hawatorudi tena Bungeni 2025

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
"Kama kweli Watanzania wakijielewa na kutuliza Akili zao na kwa hali ninayoiona sasa Mitaani kutokana na Hasira za Tozo Lukuki huku Maisha yao yakizidi kuwa magumu kuna Uwezekano 90% ya Wabunge hatutokuwa nao tena Bungeni mwaka 2025" amesema Mtangazaji wa Wasafi FM Hillary Daud a.k.a Zembwela leo Asubuhi katika 'Segment' yao ya Magazeti.
 
"Kama kweli Watanzania wakijielewa na kutuliza Akili zao na kwa hali ninayoiona sasa Mitaani kutokana na Hasira za Tozo Lukuki huku Maisha yao yakizidi kuwa magumu kuna Uwezekano 90% ya Wabunge hatutokuwa nao tena Bungeni mwaka 2025" amesema Mtangazaji wa Wasafi FM Hillary Daud a.k.a Zembwela leo Asubuhi katika 'Segment' yao ya Magazeti.
Hayo ni maoni ya Zembwela na wenzake, wewe unaamini kama kweli Watanzania watajielewa na Kwa maumivu ya tozo na ugumu wa maisha walionao, ni asilimia ngapi watarudi 2025?
 
Hayo ni maoni ya Zembwela na wenzake, wewe unaamini kama kweli Watanzania watajielewa na Kwa maumivu ya tozo na ugumu wa maisha walionao, ni asilimia ngapi watarudi 2025?
Kwa Umbumbu ( Uzuzu ) wa Wapiga Kura wengi ( siyo Wote ) wenye Unafiki mwingi na Njaa kali najua 98% ya Wabunge wa sasa Watarejea tena Bungeni.
 
Mnawasingizia watanzania. Wawekeeni tume huru ndio mtajua kuwa issue ni kanga na kofia au tume huru.

Sugu Moto Chini ashindwe uchaguzi na dokta halafu useme ni kwa vile wananchi wamehongwa kofia
 
Wabunge wengi watakaopungua ni wale walioingia kwa influence ya Magufuli.

Team Mgaso itaweka watu wake almost kila mahali.

Ndio maana kule juu wamejipanga kuhakikisha hilo linatokea.
Kwani hao waliyoingia kwa influence ya huyo uliyomtaja,wana uwezo wowote....wote ni wale wale

Nyie mjiandae wkt wa uchaguz matamasha ya wasanii,singeli, bongo movie mtayasahau yote

Ova
 
Maoni Zembwela na kubaliana nayo kwani kila anayekatwa Tozo ktk mafao kama mm tuko wengi na wanaotumia ndugu zao fedha ni wengi pia na kama ni wengi hawa jamaa watapita kwa njia ipi.
Na tukumbuke moto wa kudai Katiba Mpya ndo umeanza kukolezwa na hapo anaporudi Lisu ndo upepo unabadilika kabisa kwa chama changu ccm
 
Sema hawatarudi kwa kuwa mtetezi wao aliyewafanya wapite bila kupingwa yuko udongoni. Hii ni sababu ya kwanza. Ya pili ndio issues za tozo
 
Hakika Mkuu na hapa ndipo Wasiwasi wangu mkubwa uliko kwani ninavyojua ni kwamba duniani kote hakuna Watu ( Raia ) Wanafiki kama Watanzania ( Waswahili )
Salute mkuu you hit the point home, watanzania ni WANAFIKI, uongo, mazuzu na uoga wa kuogopa vivuli vyao!,bila push back came 2025 itakua kama CD 💿, utapigwa wimbo ule ule!wengi wanalalamika humu kwenye soft landing, mara ohoooo ajira, tumeonewa makazini, interview hazikua fair etc etc, push back in zero, ccm wapo tayari to take this country down as far as wanabaki madarakani, huu ndio ukweli!
 
Shida ni moja,
Wapiga kura wengi wapo vijijini ktk kilimo cha mkono.Kwahiyo hawajui habari za mbolea wala trekta na zaidi wao hawajui habari za tozo kwani hawafanyi biashara wala mihamala!

Hapa ndo chimbo la wanasiasa washenzi hupenyea!

Labda wale wa majimbo ya mijini ndo wajipange sawasawa!
 
Back
Top Bottom