Ziara ya Rais Samia Agosti 1, 2024 yasimamisha shuguli za kiuchumi jijini Dar es Salaam

Ziara ya Rais Samia Agosti 1, 2024 yasimamisha shuguli za kiuchumi jijini Dar es Salaam

Boi Manda

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2023
Posts
388
Reaction score
506
Tarehe 01 Agosti, 2024 rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hasani amesafiri kwa Treni ya kisasa ya SGR kutoka Darisama kuelekea Dodoma kwenye uzinduzi wa safari kutoka Dar Es Salaam kwenda Dodoma

Dhiara hiyo ya rais samia ilianza asubuhi ya tarehe 1 Agosti akitokea Ikulu ya magogoni na ujumbe mkubwa wa mawaziri, rais wa Zanzibar, marais wastaafu na wadau wengine wa septa ya usafiri na machawa akina baba Levo kuelekea Dodoma

Kutokana na mfululizo mrefu wa vingozi hao barabara ya Sokoine drive ilifungwa na askari wa barabarani (Traffic) kutoka saa moja asubuhi mpaka saa tano kuruhusu viongozi mbali mbali kufika stesheni ya Dar kwa ajili ya kusafiri na treni ya mwendokasi kuelekea Dodoma

Kitendo hicho kimesababisha biashara za kiuchumu kusimama jijini Dar kwa muda wote huo kutokana na foleni na barabara nyingi zinaongia mjini kufungwa

Mwananchi mmoja allyetokea Mbagala kuja maeneo ya Mnazi Mmoja Kitumbini kufuata mabero ya mitumba ili ende kuuza kwenye meza yake Mbagla alilalamika kuzuiwa kwa daladala kuingia katikati ya mji kwa ajili ya kupisha msafara wa rais na wapambe wake kupita njia ya sokoine drive kuja stesheni kupanda SGR

Mfanyabiashara huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa amelazimika kutembea kwa miguu kutoka Polisi Ufundi mpaka Mnazi Mmoja ili kununua mabero kwenda kuuza Mbagala

Alisema ameishiwa na mzigo leo alitoka asubuhi kuja mnazi mmoja kununua mabero ya nguo za mtumba lakini ameathiriwa na foleni kubwa mno na kuchelewa kufannya biashara yake kwa wakati

Pia wafanyakazi wengi wa Bandari wamelalamika kuchelewa kufika kazini kutokana na foleni kubwa nyakati za asubuhi na kulazika kutembea kwa miguu umbali mrefu mpaka kufika Kazini kwao Bandarini

Ikumbukwe kuwa uchumi wa nchi unategemea Bidhii zinazoshuka kutoka Bandari na TRA makusanyo yao makubwa ya kodi yanatoka Bandarini

Inasemekana na wataalam wa uchumi kuwa makusanyo ya kodi ya TRA asimia 70% yanatoka Bandari ya Darisalama

Mfanyabiashara mmoja wa Posta alisema kuwa kulikuwa na sababu gani rais kutokea Dar kwenda kuzindua SGR Dodoma na kwamba kwanini asingepanda ndege akaenda Dodoma kufanya uzinduzi huo?

Mfanyabiasha mwingine alisema kuwa anashangaa kuona uongozi umetokea Dar mji wa kibiashara wakati viongozi wote makazi yao ni Dodoma na kuhoji kuwa kwa nini wasingemaliza uzinduzi huo huko huko Dodoma mpaka waje Dar mji wa kibiashara kuathiri utendajikazi wa watu?

Comasava
 
Wakienda na ndege mnasema wanachezea hela, wakitumia ma v8 mnasema wanachezea kodi, wamejirundika wote kwenye litreni bado mnalalamika, hivi ulitaraji kutoka ikulu hadi stesheni wateembee? Kwa miguu?
 
Wakienda na ndege mnasema wanachezea hela, wakitumia ma v8 mnasema wanachezea kodi, wamejirundika wote kwenye litreni bado mnalalamika, hivi ulitaraji kutoka ikulu hadi stesheni wateembee? Kwa miguu?
Kwann wasizindulie Dodoma? Si angepanda akawasha horn watu wakapiga makofi na hotuba ya uzinduzi ikafanyika na safari zikaendelea? Bongo bwana!
 
Kwani ameizindulia wapi bwashee?

Ujinga upo kwenye kuzifanya shughuli za watu wote zisimame kwa muda mrefu, kisa kupisha kiongozi. Huo upuuzi mbona haupo kwenye nchi za wenzetu?

Nchi nyingine kwani hazina viongozi wa kitaifa? Mataifa mengi, watu hawasimishwi zaidi ya nusu saa kupisha msafara wa kiongozi. Lakini kwetu huku, kwenye nchi ya malimbukeni yasiyojua thamani ya muda, kuna wakati watu wanasimamishwa zaidi ya masaa 4 eti kupisha msafara wa kiongozi wa Kitaifa. Kule Mwanza iliwahi kutokea, Makamu wa Rais bado yupo Igunga (zaidi ya kilometa 300 toka Mwanza), Nzega; cha ajabu, tayari Shinyanga mpaka Mwanza, watu wameanza kusimamishwa wasitumie barabara. Watu walikaa pembeni kwa zaidi ya masaa 6. Mpaka Makamu wa Rais Dr. Mpango alichukia na kuukemea uwendawazimu huo.

Karibuni hapa, kuna ndugu yangu alikuwa mkoani Geita, siku hiyo ilikuwa apande ndege Mwanza kuja Dar, alisimamishwa barabarani kwa masaa 3, kisa Biteko anaenda jimboni kwake. Akachelewa ndege. Huo ndio ujinga wa watawala wetu. Mtu kila siku alikuwa anapita barabara kawaida akiwa na watumiaji wengine, kuteuliwa tu, amepewa cheo fulani, wanadamu wengine wote wanakuwa hawana maana. Mbona ambulance na magari ya zimamoto huwa tunayapisha, na hakuna ambaye huwa anasimamishwa?
 
Wakienda na ndege mnasema wanachezea hela, wakitumia ma v8 mnasema wanachezea kodi, wamejirundika wote kwenye litreni bado mnalalamika, hivi ulitaraji kutoka ikulu hadi stesheni wateembee? Kwa miguu?
Wangeenda kupandia Pugu stesheni basi au wangesafori usiku wa saa tano wakati watu wengi wameshatoka makazi njia nyingine kwa nini mawazari wasingetumia usafari mmoja wa min bus wote kwa pamoja ili kuepusha misafara mirefu?
 
Ujinga upo kwenye kuzifanya shughuli za watu wote zisimame kwa muda mrefu, kisa kupisha kiongozi. Huo upuuzi mbona haupo kwenye nchi za wenzetu?

Nchi nyingine kwani hazina viongozi wa kitaifa. Mataifa mengi, watu hawasimishwi zaidi ya nusu saa kupisha msafara wa kiongozi. Lakini kwetu huku, kwenye nchi ya malimbukeni yasiyojua thamani ya muda, kuna wakati watu wanasimamishwa zaidi ya masaa 4 eti kupisha msafara wa kiongozi wa Kitaifa. Kule Mwanza iliwahi kutokea, Makamu wa Rais bado yupo Igunga (zaidi ya kilometa 300 toka Mwanza), Nzega, Shinyanga mpaka Mwanza, watu wameanza kusimamushwa wasitumie barabara. Mpaka Makamu wa Rais Dr. Mpango alichukia na kuukemea uwendawazimu huo.

Karibuni hapa, kuna ndugu yangu alikuwa mkoani Geita, siku hiyo ilikuwa apande ndege Mwanza kuja Dar, alisimamishwa barabarani jwa masaa 3, kisa Biteko anaenda jimboni kwake. Akachelewa ndege. Huo ndio ujinga wa watawala wetu. Mtu kila siku alikuwa anapita barabara kawaida akiwa na watumiaji wengine, kuteuliwa tu, amepewa cheo fulani, wanadamu wengine wote wanakuwa hawana maana. Mbona ambulance na magari ya zimamoto huwa tunayapisha japo hakuna ambaye huwa anasimamishwa?
Well said
 
Wangeenda kupandia Pugu stesheni basi au wangesafori usiku wa saa tano wakati watu wengi wameshatoka makazi njia nyingine kwa nini mawazari wasingetumia usafari mmoja wa min bus wote kwa pamoja ili kuepusha misafara mirefu?
Kila mtu anataka kukaa siti ya mbele
 
Tarehe 01 Agosti, 2024 rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hasani amesafiri kwa Treni ya kisasa ya SGR kutoka Darisama kuelekea Dodoma kwenye uzinduzi wa safari kutoka Dar Es Salaam kwenda Dodoma

Dhiara hiyo ya rais samia ilianza asubuhi ya tarehe 1 Agosti akitokea Ikulu ya magogoni na ujumbe mkubwa wa mawaziri, rais wa Zanzibar, marais wastaafu na wadau wengine wa septa ya usafiri na machawa akina baba Levo kuelekea Dodoma

Kutokana na mfululizo mrefu wa vingozi hao barabara ya Sokoine drive ilifungwa na askari wa barabarani (Traffic) kutoka saa moja asubuhi mpaka saa tano kuruhusu viongozi mbali mbali kufika stesheni ya Dar kwa ajili ya kusafiri na treni ya mwendokasi kuelekea Dodoma

Kitendo hicho kimesababisha biashara za kiuchumu kusimama jijini Dar kwa muda wote huo kutokana na foleni na barabara nyingi zinaongia mjini kufungwa

Mwananchi mmoja allyetokea Mbagala kuja maeneo ya Mnazi Mmoja Kitumbini kufuata mabero ya mitumba ili ende kuuza kwenye meza yake Mbagla alilalamika kuzuiwa kwa daladala kuingia katikati ya mji kwa ajili ya kupisha msafara wa rais na wapambe wake kupita njia ya sokoine drive kuja stesheni kupanda SGR

Mfanyabiashara huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa amelazimika kutembea kwa miguu kutoka Polisi Ufundi mpaka Mnazi Mmoja ili kununua mabero kwenda kuuza Mbagala

Alisema ameishiwa na mzigo leo alitoka asubuhi kuja mnazi mmoja kununua mabero ya nguo za mtumba lakini ameathiriwa na foleni kubwa mno na kuchelewa kufannya biashara yake kwa wakati

Pia wafanyakazi wengi wa Bandari wamelalamika kuchelewa kufika kazini kutokana na foleni kubwa nyakati za asubuhi na kulazika kutembea kwa miguu umbali mrefu mpaka kufika Kazini kwao Bandarini

Ikumbukwe kuwa uchumi wa nchi unategemea Bidhii zinazoshuka kutoka Bandari na TRA makusanyo yao makubwa ya kodi yanatoka Bandarini

Inasemekana na wataalam wa uchumi kuwa makusanyo ya kodi ya TRA asimia 70% yanatoka Bandari ya Darisalama

Mfanyabiashara mmoja wa Posta alisema kuwa kulikuwa na sababu gani rais kutokea Dar kwenda kuzindua SGR Dodoma na kwamba kwanini asingepanda ndege akaenda Dodoma kufanya uzinduzi huo?

Mfanyabiasha mwingine alisema kuwa anashangaa kuona uongozi umetokea Dar mji wa kibiashara wakati viongozi wote makazi yao ni Dodoma na kuhoji kuwa kwa nini wasingemaliza uzinduzi huo huko huko Dodoma mpaka waje Dar mji wa kibiashara kuathiri utendajikazi wa watu?

Comasava
Kusimamisha shughuli za uchumi ndiyo furaha yako na unaona ni sifa njema wakati serikali inahitaji kodi kutoka kwa haohao mliosimamisha shughuli zao.

Kuna watu wa ajabu sana, Morogoro maofisi ya serikali yamefungwa tangu saa 2 asubuhi, Rais amefika kwenye tukio saa 8 mchana, imagine watu wameteseka kiasi gani
 
Wangeenda kupandia Pugu stesheni basi au wangesafori usiku wa saa tano wakati watu wengi wameshatoka makazi njia nyingine kwa nini mawazari wasingetumia usafari mmoja wa min bus wote kwa pamoja ili kuepusha misafara mirefu?
Mni bus mbli,tatu na sgr na wananchi wakiwemo ipi rahisi?
 
Tarehe 01 Agosti, 2024 rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hasani amesafiri kwa Treni ya kisasa ya SGR kutoka Darisama kuelekea Dodoma kwenye uzinduzi wa safari kutoka Dar Es Salaam kwenda Dodoma

Dhiara hiyo ya rais samia ilianza asubuhi ya tarehe 1 Agosti akitokea Ikulu ya magogoni na ujumbe mkubwa wa mawaziri, rais wa Zanzibar, marais wastaafu na wadau wengine wa septa ya usafiri na machawa akina baba Levo kuelekea Dodoma

Kutokana na mfululizo mrefu wa vingozi hao barabara ya Sokoine drive ilifungwa na askari wa barabarani (Traffic) kutoka saa moja asubuhi mpaka saa tano kuruhusu viongozi mbali mbali kufika stesheni ya Dar kwa ajili ya kusafiri na treni ya mwendokasi kuelekea Dodoma

Kitendo hicho kimesababisha biashara za kiuchumu kusimama jijini Dar kwa muda wote huo kutokana na foleni na barabara nyingi zinaongia mjini kufungwa

Mwananchi mmoja allyetokea Mbagala kuja maeneo ya Mnazi Mmoja Kitumbini kufuata mabero ya mitumba ili ende kuuza kwenye meza yake Mbagla alilalamika kuzuiwa kwa daladala kuingia katikati ya mji kwa ajili ya kupisha msafara wa rais na wapambe wake kupita njia ya sokoine drive kuja stesheni kupanda SGR

Mfanyabiashara huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa amelazimika kutembea kwa miguu kutoka Polisi Ufundi mpaka Mnazi Mmoja ili kununua mabero kwenda kuuza Mbagala

Alisema ameishiwa na mzigo leo alitoka asubuhi kuja mnazi mmoja kununua mabero ya nguo za mtumba lakini ameathiriwa na foleni kubwa mno na kuchelewa kufannya biashara yake kwa wakati

Pia wafanyakazi wengi wa Bandari wamelalamika kuchelewa kufika kazini kutokana na foleni kubwa nyakati za asubuhi na kulazika kutembea kwa miguu umbali mrefu mpaka kufika Kazini kwao Bandarini

Ikumbukwe kuwa uchumi wa nchi unategemea Bidhii zinazoshuka kutoka Bandari na TRA makusanyo yao makubwa ya kodi yanatoka Bandarini

Inasemekana na wataalam wa uchumi kuwa makusanyo ya kodi ya TRA asimia 70% yanatoka Bandari ya Darisalama

Mfanyabiashara mmoja wa Posta alisema kuwa kulikuwa na sababu gani rais kutokea Dar kwenda kuzindua SGR Dodoma na kwamba kwanini asingepanda ndege akaenda Dodoma kufanya uzinduzi huo?

Mfanyabiasha mwingine alisema kuwa anashangaa kuona uongozi umetokea Dar mji wa kibiashara wakati viongozi wote makazi yao ni Dodoma na kuhoji kuwa kwa nini wasingemaliza uzinduzi huo huko huko Dodoma mpaka waje Dar mji wa kibiashara kuathiri utendajikazi wa watu?

Comasava
Magali yamesomba Wana mboga mboga Kila Kona ya dar mpaka inje ya dar nilikuwepo hakuna dar iliosimama walilaImisha kufunga Hadi mnada wa pugu Ili wapate wahuzuliaji ACHA kabisa uongo
 
Back
Top Bottom