Ziara ya Rais Samia Ufaransa: Tanzania yasaini Mkataba wa Mkopo wa Masharti nafuu wa Euro Milioni 178

Hivi youtong zinatutoa jasho tunaongeza na Renault ya mfaransa
 
CC. Ndugai huko aliko, basi hizo € 80 mil ziwafikie hata wakulima 5,000 tu jamani
 
Hivi huko Ulaya hawahitaji misaada maana ni sisi tu ndio tunapewa misaada na mikopo.

Kama kweli uchumi wa buluu unalipa na tuna hizo rasilimali bahari kwanini tusizisimamie vyema na kupata faida yake bila kukopa.

Kwanini tusaini makubaliano na Ufaransa wakati bahari yetu wala hata haipo karibu na Ufaransa.

Au ufaransa ndio atanufaika na uchumi wa bahari yetu??
 
Kushindwa kulipa bilioni 10 wakati ule haimaanishi wanashindwa kulipa sasa. Uchumi ni somo linalofundishwa darasani, ukiwaweka katika nafasi wachumi na wakapewa uhuru wa kufanya kazi bila ya siasa kuwaingilia tegemea matokeo chanya ya ukuaji wa uchumi.

Mauritius wanaishi kwa kutegemea utalii tu na pato lao la taifa ni kubwa kuliko la Tanzania. Hivyo kila kitu kinaanzia kichwani, kibaya ni kuwa na akili za kukariri. Kwamba walishindwa miaka ya nyuma kulipa deni basi milele uwezo wao wa kulipa haupo!.
 
Bora huyu anatutangazia yule aliyeondoka alikua anachukua kimya kimya halafu miradi anatuambia anatekeleza kwa frdha za ndani.
 
Nchi hii ingejiwekeza katika wawekezaji wakubwa ambao wangesaidia kupatikana kwa ajira kwa wananchi na upatikanaji wa huduma za kijamii kwa gharama ndogo kuliko mikopo mikopo mikopo aaaaaah Mama badilisha mfumo
 
178,000,000 £ ni sawa na 467,509,776,760.00 TSH. Hizi kwa serikali fisadi ninkuzigawa na kuzitafuna tu, mwisho hata hiyo BRT sijui ni phase gani haitakamilika kwa wakati.
Halafu wanafuikaji wa huo mkopo ndo utasikia nani kama mama sijui anaupiga mwingi sana mama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…