Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unajua humo kwenye shule za msingi kiasi gani mmomonyoko wa maadili unaendelea kwa kuwa tu, huko majumbani wanakotokea watoto hakuna anayewapa elimu hiyo? Unajua kuwa ubakaji na ulawiti wa watoto unaanzia majumbani kwa 60% kisha unahamia mashuleni na kusambaza? Unajua kuwa kwa mshangao huo sambamba na mkutano wa wananchi Leo hii wote mtajua mengi msiyoyajua? Na mikakati itokanayo na ziara hii itaokoa taifa lote? Waza wa upana na kutoka nje ya box.Waziri mzima unakuja hapa kujinasibu kwa kuzindua mradi wa vyumba vitatu, VYUMBA😂
ma ma mae walai nchi hii ni kama tumelaaika, hivi kwa haraka haraka tu msafara wako kuanzia mafuta, posho na mengineyo inagharimu kiasi gani.
Hivyo vitu vya kipuuzi, vinafaa kuzinduliwa hata na katibu kata huko, mngekuwa serious hata mwenyekiti wa kijiji anaweza zindua hii kitu.
Nyie viongozi ndio mnatifelisha pakubwa, taifa linakwama kwa ajili yenu, uwajibikaji zero, badala mfanye ya maana muonekano, mnashindwa mnakimbilia kuonekana katika vitu vidogo,
Ndio maana mpaka leo taifa linajengewa vyoo kwa misaada.
Miaka 60+ ya uhuru ila ukichora graph ya maendeleo yetu vs muda ni inasikitisha.
Haya kila la kheri kwenye uzinduzi, na kwa kiwa mnatuongozamaiti zinazotembea, msipate shaka endeleeni kula cake ya taifa.
Swali zuri Sana, nitakuja kulijibu nikianzia na uzinduzi wa mkakati wa tarehe 15 Mei 2024 Dodoma, pale viwanja vya Chinangali Park, ambapo mawaziri wa kisekta na wawakilishi wa Wakuu wa Mikoa walikuwa wanatoa ahadi zao. Sema HUKUFUATILIA. Ila Leo ngoja kwanza tumalize kuzindua mafuriko ya miradi huku Tabora kisha tutakuja na kwenye ajenda hii. Huwa napenda Sana maswali kama haya maana yanaongezea sauti kwenye uwepo wa mikakati kwani, pengine huwa kuna baadhi yetu hatufuatilii hata kurasa za wizara na taarifa za habari hivyo, maswali kama haya huturejesha kwenye kusema tena na tena, ahsante Sana 🇹🇿😍
Nitampigia Kura, huyu Dada Hana makuuuWe cheka tu ila 2025 rais ni Dkt. Gwajima D