Raphael focus
JF-Expert Member
- Nov 4, 2018
- 779
- 4,564
Habari ya muda huu wanajanvi!
Kama mada inavyo jieleza hapo juu.
Hizi ni njia tatu bora na rahisi za kupunguza kitambi ambazo huitaji kwenda jimu au kukimbia kwenye ukingo wa bahari.
NJIA YA KWANZA: kopa mkopo mkubwa benki
Kwa wewe unaehitaji kupunguza kitambi kopa mkopo benki, zile presha za kupigiwa simu kila mara na benki ku kumbushia deni lao kwa mwezi mzima. Kumbuka utakapokuwa umekopa mkopo haijalishi ni kiasi gani, kama utakuwa umepewa mkataba wa miaka mitano kulejesha mkopo maana yake utakuwa umepigiwa simu kwa miaka mitano mfurulizo.
NJIA YA PILI: tembea na mwenza wa mwanajeshi
Maana yake kama wewe ni kidume tembea na mke wa mwanajeshi, kama wewe ni dada unasifika mjini kwa kubeba waume za watu tembea na mume wa mwanajeshi.
Hapa kutokana na zile pilika pilika za kutafutwa na mikwaju na kuruka fensi. Mara umekaa mjeshi anakutokea barazani, hapa ndo pale unapoamuwa kupitia uwani kwa sababu ya presha.
NJIA YA TATU: nunua gari bovu
Ulishasikia gari ya M1.8? au laki saba? Yaani gari ambayo hutaki kuagiza kutoka Japan, gari ambayo hutaki kununua kwenye yadi, ila gari utakayo nunua ni kutoka mikononi mwa mtu.Gari ambayo ukiwa ndani unaona lami kupitia matundu huku kwenye madimbwi ya maji ukipita kwa tahadhari kubwa.
Hapa mpela mpela wake pale inapozima na unaamuwa kushuka ili uisukume .Ghafla unamuona trafiki anakuja kuikagua ile gari ambayo haina hata vibali ile presha yake sasa hapo kitambi ndo kinakata ghafla.
ONGEZA NA ZAKO.
Kama mada inavyo jieleza hapo juu.
Hizi ni njia tatu bora na rahisi za kupunguza kitambi ambazo huitaji kwenda jimu au kukimbia kwenye ukingo wa bahari.
NJIA YA KWANZA: kopa mkopo mkubwa benki
Kwa wewe unaehitaji kupunguza kitambi kopa mkopo benki, zile presha za kupigiwa simu kila mara na benki ku kumbushia deni lao kwa mwezi mzima. Kumbuka utakapokuwa umekopa mkopo haijalishi ni kiasi gani, kama utakuwa umepewa mkataba wa miaka mitano kulejesha mkopo maana yake utakuwa umepigiwa simu kwa miaka mitano mfurulizo.
NJIA YA PILI: tembea na mwenza wa mwanajeshi
Maana yake kama wewe ni kidume tembea na mke wa mwanajeshi, kama wewe ni dada unasifika mjini kwa kubeba waume za watu tembea na mume wa mwanajeshi.
Hapa kutokana na zile pilika pilika za kutafutwa na mikwaju na kuruka fensi. Mara umekaa mjeshi anakutokea barazani, hapa ndo pale unapoamuwa kupitia uwani kwa sababu ya presha.
NJIA YA TATU: nunua gari bovu
Ulishasikia gari ya M1.8? au laki saba? Yaani gari ambayo hutaki kuagiza kutoka Japan, gari ambayo hutaki kununua kwenye yadi, ila gari utakayo nunua ni kutoka mikononi mwa mtu.Gari ambayo ukiwa ndani unaona lami kupitia matundu huku kwenye madimbwi ya maji ukipita kwa tahadhari kubwa.
Hapa mpela mpela wake pale inapozima na unaamuwa kushuka ili uisukume .Ghafla unamuona trafiki anakuja kuikagua ile gari ambayo haina hata vibali ile presha yake sasa hapo kitambi ndo kinakata ghafla.
ONGEZA NA ZAKO.