Zijue namba za magari ya Tanzania! Pamoja na namba maalum za magari ya viongozi, Serikali na Taasisi za Umma kwa ujumla

Hayo Magari ya # 12 hapo huwa yanapita njia gani Mkuu kwani binafsi japo niko ' down town ' kwa ' miongo ' mitatu sasa ya Uhai wangu lakini sijawahi kubahatisha kuyaona japo nina hamu sana niyaone.
Mitaa ya makumbusho barack obama na sarrender mkuu
 
Nimejifunza kitu.mungu akubariki muandaaji wa hii thread
 
Namba za magari ni mpangilio wa kuweza kutambua magari kwa sababu za usalama barabarani na kwenye matukio tofauti.Serikali na idara husika huweza kubadilisha mfumo wa namba za magari.
Kwa mfano wale tulio "wahenga"magari ya serikali yalikuwa na plate number inayoanzia na GT ikimaanisha Government of Tz,kila mji mkuu wa mkoa uliwa na namba zake kwa magari binafsi. Kwa mfano Mbeya - MB, Moshi -MS Tanga TA DSM - DS Arusha- AR Tabora -TB n.k. siku za karibuni tumebadilisha mfumo wa namba za magari kulingana na ule wa SADC mfano T 666 CCC
Siku za nyuma magari yanayotumia DFP yalikuwa yanatumia TX
 

10: FT (fire Tanzania) sio sahihi. Inabidi iwe
ZT (zimamoto Tanzania)

12:E 1, E 2, inamaanisha hizo ni gari Za escort. Escort 1 (E 1) escort 2, (E 2)
 
4. Jaji Mkuu wa Tanzania
Gari la Jaji Mkuu wa Tanzania huwa na herufi JM kwenye kibao chake


Kuna jingine limeandikwa JK, tukaambiwa ni Jaji Kiongozi, je tofauti yao ni nini?
 


Mkuu, hapa ungeongezea kuwa number plates zao zinatofautiana kwa rangi,
UN - Blue
Balozi - Green
 
14. Magereza Tanzania
Magari ya Magereza ya Tanzania huwa na kibao chenye kuanziwa na herufi MT kisha hufuatiwa na namba kadhaa mbele yake kwenye kibao cha magari hayo



Kuna moja nilikuta lina namba za mpangilio huu lakini kibao chake ni chekundu likiwa na bendera, mengine yana kibao chenye rangi hiyo na maandishi rangi hiyo, ila ni RAC, hayo ni magari ya watu gani?
 
Inakuwaje pale unakuta gari jipya kabisa lakini namba za zamani, kwa mfano kuna V8 moja mpya kabisa ina namba T804AVB
 
Escort 1 for president and so on


Kuna mmoja alikuwa analiosha gari la namna hiyo Benz pale Kijitonyama, akawakodishia jamaa kwenda walikokuwa wanakwenda sikujua kama lilikuwa ni gari la huko!!!!
 
Umesahau kuna magari huwa nayaona mitaa ya keko pale msd,mitaa ya Victoria (bagamoyo rd) kule wazo kama unaenda madale ya usajili wa UT afu plate number zake zimeandikwa kama za polisi...kwani hizo nazo niza serikali?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…