Zijue sababu za Kimkakati zilizoifanya Yanga SC ya Mwakalebela Kuzungumza na Vyombo vya Habari jana

Zijue sababu za Kimkakati zilizoifanya Yanga SC ya Mwakalebela Kuzungumza na Vyombo vya Habari jana

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
1. Uongozi kwa Kushirikiana na GSM Kukwepa Lawama na kuwalazimisha Mashabiki wao waone wanaowakwamisha ni TFF na Kamati zake.

2. Kutaka Kuwatishia Waamuzi ( hasa huyu wa leo dhidi ya Mtibwa FC ) awaogope na awapendelee ili washinde Mechi yao.

3. Kumuhusisha kwa Kumtaja hadi Kumzungumzia Msemaji wa Simba SC Haji Manara ni Mbinu ya kutaka Kumtoa Manara katika Mstari ili asiihamasishe Simba SC kuelekea katika Mechi yake muhimu dhidi ya Al Ahly Siku ya Jumanne ijayo tarehe 23 February Benjamin Mkapa Stadium.

4. Kutaka Kuficha Madhaifu ya Wachezaji wao Wabovu ambao waliwasajili kwa Mbwembwe kumbe ni Wagonjwa tupu na sasa wanaiingiza tu Gharama zisizo za lazima Yanga SC.

5. Baada ya Kupima na Kukiangalia Kikosi cha Simba SC na Kugundua kuwa kina 99% ya kuwa Mabingwa tena hivyo wameanza Kutupa Shutuma zao TFF na katika Kamati yake ili Kuwajenga Kisaikolojia Wanachama na Mashabiki wao ikitokea hawachukui Ubingwa ( na ambao hawauchukui kweli ) basi wasiumie Mioyo sana.

6. Ndani ya Yanga SC kuna Fukuto Kubwa la uhaba wa Pesa huku Wachezaji wazawa wakiwa na Bifu na Wachezaji wageni wa Yanga SC ambao inasemekana ndiyo Wanadekezwa na Kusikilizwa mno na Wadhamini GSM huku Wazawa wakiwa wanabung'aa bung'aa tu kama Mbuzi wa Mpemba Makonde Kituoni Mbezi Beach.

7. Kwa kujua kuwa Walishawaaminisha Uwongo Mashabiki wao wengi Mbumbumbu ( japo siyo wote ) kuwa Sakata la Mchezaji Bernard Morisson litaisha kwa Faida ya Yanga SC na linasubiriwa kwa hamu njia ( mbinu ) pekee waliyoiona ni kila mara Kulizungumzia ( Kuligusia ) ili wana Yanga SC wawaamini Viongozi na Mfadhili wao GSM wakati ukweli umeshajulikana kuwa huko CAS Yanga SC hawana chao na hata Maamuzi yakitoka bado yataipa Simba SC ushindi.

Huwezi kukutana na Upuuzi (Uhayawani ) huu ndani ya Timu zinazojitambua kama za Azam FC au Gwambina FC au KMC FC au Coastal Union FC au Simba SC au hata Namungo FC.

Najua leo Yanga SC itashinda Mechi yao kwa idadi Kubwa ya Magoli dhidi ya Mtibwa FC Kuanzia Goli 2 au 3 na mpaka hata 4. Baada ya Mechi Kumalizika nitaweka kila Kitu hadharani kwani nina Taarifa za chini ya Kapeti kwa Kilichofanyika.
 
Kumbe maadui wa mpira wetu wapo miongoni mwetu watanzania, sasa huu utakua mpira au vita ..watu kwanini hawapendi kuwajibika na matokeo yao mabovu , wanataka kuharibu ligi ya mpira Tanzania ..na ndio kwanza tumeanza kutangaza ligi yetu nchi za nje
Walaumu Yanga SC na siyo Simba SC au TFF na Kamati zake au Bernard Morisson au Mimi All - Rounder tafadhali.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] daaah fiston hamna kitu pale kudadake!++
Sio kweli jamaa.
Fiston ni watu wawili na nusu.
Sema nini apewe muda na Kaze mpaka sasa bado ajapanga vema kikosi chake mwisho wa huu mzunguko wa pili,anabahatisha sana.
 
Back
Top Bottom