Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Jamaa hawana nguzo hawa,nimelipia february 2018 mpaka leo naskia mboyoyo tu
 
achaneni na tanesco fungeni umeme wa solar ambao uko intergrated na wind turbine, mchana unapokea umeme jua na umeme upepo usiku unapokea umeme upepo. hamna sijui luku imeisha sijui umeme umekatika? unafunga umeme siku hiyo hiyo unatumia siku hiyo hiyo.
huo umme wa solar ni bei gani kunifungia kwa taa5. computer, friji, na radio na pasi inagharimu kiasi gani? friji ni dogo la kawaida la matumizi ya nyumbani
 
Jana nimemtuma kijana wangu kwenda kupata namba ya kumbukumbu TANESCO Mkuranga akaelezwa kuwa network inasumbua aache no za simu mambo yakiwa tayari atajulishwa.

Naye akachukua za TANESCO Mkuranga, kila akiwapigia jibu, bado network haijarudi, sisi tupo kwenye mradi mpya, huku tunatangaziwa kuwa mwisho ijumaa.

Kila kitu kifanywe kwa ueledi, anayefata Huduma TANESCO kaacha kutoa Huduma sehemu nyingine ili tuumuunge mkono Mh Rais tupunguze njoo kesho ili tusonge Mbele.
Shukrani,
Malipo yamefanyika Leo ,hii nategemea kupata Huduma ya Umeme hivi karibuni.

Nawapongeza saaaaaaaaaaana.
 
Tanesco inaweza kuwa ni miongoni mwa kampuni ambayo wafanyakazi wake wanapenda rushwa kuliko zote. Nimelipia umeme bado tu kuja kuunganishiwa na sihitaji nguzo mmoja wao kaniambia nitoe hela nje ya yale malipo halali niunganishiwe. Shirika hovyo kabisa hili
 
Tupate namba za waziri husika nahisi ndo atatatua kero zetu ila si hawa walagai wakubwa kwa wateja wao. Mpaka sasa tangu nimelipia nguzo hawataki kuniunganishia umeme. Naolewao nikimtambua muhusika mkuu anaeweza kuwatumbua ntamueleza bayana. Yaani nguzo zinapitishwa mbeleyangu kwenda kwa jirani hala naambiwa nguzo hazipatikani
 
Yaani TANESCO mnachokifanya ndo mnaoifanya hii nchi isiendelee. Kwanini mnatufanya watanzania wote kama hatuna akili timamu? Kwani huduma hizi mnatoa bure? Kila kukicha ni malalamiko na rushwa zimewatawala.

Tanesco Songea mnachokifanya sio, hao wateja mnaowazungusha kila siku na kuwadai 20,000/= ili surveyors wafike kupima ya nini?

HII NI RUSHWA, TENA YA WAZI WAZI. MTAKUFA NA TAMAA ZENU NA UMASKINI WENU. Ipo siku tutaheshimiana tu, dawa yenu inachemka.
 
Yaani huku mbeya nimefungiwa umeme wakanipa unit 10 zikaisha nikaenda tanesco kuisajili mita no yangu, ili nijunulie umeme wangu nashangaa nazungushwa mpaka sasa ni siku ya nne hii nakaa giza wanashindwa nisajili......hata hizo unit 50 za bure nimenyimwa
 
Mtaalamu tunatakiwa kutolea taarifa Tanesco waya za umeme zikishuka au kutepeta kwa kimo kiasi gani toka ardhini na hasa kwa waya za kutoka nguzo moja hadi nyingine
 
Taratibu zipoje nataka mita yetu kwa mzee iwe tarrif 4 ,,maana kwa siku natumia unit 2.5,,,,,,,, TANESCO ,,04202888667. ,,,,,ila sikuizi Tanesco mnastahili pongezi suala la kukatika mara kwa mara umeme limeisha kabisa kwa mkoa wa Dar,
 
Back
Top Bottom