Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Cut-out ni kifaa cha umeme ambacho kina unganisha cable ya umeme ya tanesco na wiring ya mteja. Yaani hapa ndipo pale umeme wa tanesco unakutana na wiring system ya mteja inapoanzia.

Kazi yake ni kuhakikisha kuwa kuwa umeme unahitaji mteja unapita salama kwenda kwenye nyumba yako.

Inaunganishwa direct kwenye umeme unaokuja kwako mteja na ina kitu kinaitwa ‘main fuse’. Hii husaidia kuhakikisha kiwango sahihi cha umeme kinaingia kwenye nyumba yako.

Kama umeme ukiwa mwingi unataka kuingia kwenye nyumba yako hiyo main fuse inafanya isolation ili umeme huo usiingie kwenye nyumba ili vitu visiungue na hapo inafanya kuzuia umeme usiingie kwako kwa kiwango kikubwa kwa ku trip na umeme kukata kwemye jengo kukiwa na overload ya voltage.
Ubarikiwe sn mkuu.

Nitaiweka hii kitu kumbe.
 
@chaliifrancisco, TANESCO kuna swali jingine hapa. mie ni muhanga wa kusubiria umeme kwa muda mrefu katika maeneo tofauti. sehemu ya kwanza ni dsm na ya pili ni ikonda njombe kwenye mradi wa REA(umeme vijijin).

kwa dsm nimeletewa nguzo mbili kama wiki moja imepita, je swali langu ni tuuendelee kusubiria tena miezi sita mingine au kuna unafuu wa muda.
kwa kule kijijini pana hitaji nguzo moja lakini nakaribia miezi 9.

kingine nawapa Pongezi maana niliwalaumu bure lakini kuna mfanyakazi wa tanesco alinielewesha japo aliambulia yale maneno ya KA-TA
Mkuu kuna upungufu wa material hasahasa nguzo hivyo kwakuwa umeshasambaziwa nguzo ujenzi wake basi sio siku nyingi kwakuwa kwa wateja wa nguzo huwa wanasambaza kwanza nguzo wakija wanasimamisha na kuwasha umeme. Kama nguzo wameleta hapo chekelea tu

Kuhusu hiyo ya REA siwezi kukupa jibu la uhakika ila ukishalipia kwenye REA wala Tanesco wanakuwa hawahusiki maana hata hela uliyolipa ni VAT na inaenda TRA wala sio kwa Tanesco.

Ukishalipa Tanesco hukabidhi kazi yako kwa contractor aliyepewa tender na REA kwa sehemu husika na huyo mkandarasi ndie naehusika kuja kufunga umeme wala sio Tanesco.
 
HATUA YA KWANZA-:- MAOMBI YA MWANZO

Je mteja anaweza kuchukua fomu ofisi yeyote ya tanesco?

Mteja anaweza kuchukua fomu ya maombi ya umeme katika ofisi yeyote ya shirika bila kujali kuwa eneo hilo linahudumiwa na ofisi husika. Ila atapaswa kurudisha ofisi ya maeneo ambayo makazi yake yapo ili kurahisisha kufanyiwa vipimo (service line survey)

JE KUNA GHARAMA ZOZOTE KATIKA UCHUKUAJI WA FOMU?

Fomu za maombi ya umeme zinatolewa bure kabisa kwa wateja wote.

VITU MUHIMU VYA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHUKUA FOMU

1. Hakikisha umeme umefika maeneo yako na kama ni mradi uwe umekamilika.

2. Hakikisha mtandao wa nyaya ndani ya nyumba yako (wiring) umefanyika kupitia mkandarasi aliyesajiliwa.

3. Kitambulisho kinachomtambulisha muombaji wa umeme mfano leseni ya udereva, hati ya kusafiria, kitambulisho cha kazi (hii inasaidia shirika kumtambua mteja husika)

4. Kwa mwombaji wa mita ya ziada (meter separation) jina litakalotumika ni la mwenye nyumba kama linavyosomeka katika mita ya awali. Vinginevyo mteja atapaswa kutumia uthibitisho wa ruhusa ya mwenyenyumba kama atakuwa ni mpangaji. Lazima mteja aje na namba ya mita (kama zipo zaidi ya moja aje nazo zote) ili kuhakiki kama kuna yenye deni.


5. Kwa waombaji wanaomba kwa ajili ya ofisi, makapuni au taasisi za serikali au binafsi anapaswa kuja na leseni ya biashara, tin namba, udhibitisho wa usajili wa kampuni. Au udhibitisho wa ofisi ya serikali husika.

6. Kwa wapangaji wa nyumba za taasisi au makampuni waje na barua za waliopangisha zinazoonyesha kuwe wenye nyumba hizo wameridhia mita husika iwe na jina la mpangaji husika.

7. Shirika linapenda kuwaomba wamiliki wa nyumba kupenda kufika ofisi zetu wenyewe ili kuzuia udanganyifu ambao umekuwa ukifanywa na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu

HATUA YA PILI KUWEKA MCHORO, PICHA NA KUINGIA MAKUBALIANO YA KUFUNGIWA UMEME NAKUREJESHA FOMU

Endapo mteja atakidhi vigezo na masharti ya hatua ya mwanzo na kupatiwa fomu ya maombi ya mwanzo anatakiwa afanye yafuatayo

1. Kuisoma fomu kwa umakini mkubwa na kukubailiana na vigezo namba moja mpaka kumi na mbili. Mteja akijiridhisha kuwa amekubaliana na masharti yote ataweka sahihi sehemu husika (ukurasa wa pili wa fomu ya maombi ya umeme)

2. Kumpatia mkandarasi aliyesajiliwa ili achore mchoro wa mtandao wa nyaya (wiring diagram) wa nyumba husika pamoja na kugonga muhuri. (gharama ni makubaliano baina ya mteja na mkandarasi husika), wakandarasi wanapatikana kwenye ofisi zao maeneo mbalimbali, orodha ya waliosajiliwa pia inapatikana kwenye ofisi za tanesco. Mteja anapaswa kupewa orodha na kuchagua mkandarasi anayemtaka yeye.

3. Mteja atapaswa kuweka picha moja ya mwombaji wa umeme

4. Kisha mteja atarudisha fomu hiyo iliyokamilika ofisi ya eneo ambalo makazi yake yako (inayomudumia)

HATUA YA TATU- KUFANYIWA VIPIMO (SURVEY)

Mara baada ya mteja kurejesha fomu iliyojazwa kikamilifu, mteja atapangiwa tarehe ya kufanyiwa vipimo (survey). Mafundi watafika kwenye nyumba au sehemu inayoombewa umeme ili kutathimini gharama atakazolipia mteja kwa kuzingatia umbali wa eneo ilipo miundombinu ya umeme kama nguzo na transfoma na uwezo wa umeme huo kuunganisha kwa wateja wapya.

HATUA YA NNE: - KUPATIWA MAKADIRIO YA GHARAMA KIASI GANI ALIPE ILI AFUNGIWA UMEME

Mara baada ya kufanyiwa tathimini mteja anaweza kupatiwa makadirio ya gharama ya kiasi gani alipe ili kufungiwa umeme. Makadirio haya huweza kutumwa kwa njia ya nukushi, ujumbe mfupi wa meneno, barua pepe au mteja kufika ofisini na kuchukua barua. Viwango vya muda wa kutoa makadirio kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini:

MAELEZO

Muda wa makadirio

Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)

Ndani ya siku 7 za kazi

Ujenzi wa njia ya nyongeza unahitajika (mita 30- 100)

Ndani ya siku 10 za kazi

Kama mfumo mpya wa usambazaji unahitajika kujegwa au mfumo wa umeme mkubwa unahitajika kuongezwa kwa ajili ya kiwanda au biashara kubwa (kama hakuna mfumo wa kumuunganishia mwombaji) (zaidi ya mita 100)

Ndani ya siku 14 za kazi

HATUA YA TANO: - KUFANYA MALIPO

Mteja atafika ofisi ya tanesco ili kupatiwa namba ya kumbukumbu (reference number) itakayomuwezesha kufanya malipo bank, mteja atafanya malipo na atapatiwa stakabadhi ya malipo bank (risiti kwa njia ya ujumbe mfupi- sms) (kwa sasa ni bank ya nmb tu), wateja wanahimizwa kufanya malipo yote bank na si kwa mtu mwingine yeyote. Malipo yote yatakayofanyika nje ya mfumo uliwekwa hayatambulika na tanesco. Mteja akishafanya malipo bank husika hatatakiwa kurudi tena tanesco bali tanesco watakuwa na taarifa zake zote na kinachofuata ni kumfungia umeme.

HATUA YA SITA:-KUUNGANISHIWA UMEME

Mara baada ya mteja kufanya malipo viwango vya muda wa kumfungia umeme vitakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali hapo chini.

MAELEZO

Muda wa kufungiwa

Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)

Ndani ya siku 30 za kazi

Ujenzi wa njia ya nyongeza itahitajika

(mita 30- 100)

Ndani ya siku 60 za kazi

KAMA MFUMO MPYA WA USAMBAZAJI UNAHITAJIKA KUJEGWA AU MFUMO WA UMEME MKUBWA UNAHITAJIKA KUONGEZWA KWA AJILI YA KIWANDA AU BIASHARA KUBWA (KAMA HAKUNA MFUMO WA KUMUUNGANISHIA MWOMBAJI) (ZAIDI YA MITA 100)

Ndani ya siku 90 za kazi

KWA MAULIZO WASILIANA NASI

Kituo cha huduma kwa wateja: - 0768985100/0222194400

Barua pepe: customer.Service@tanesco.Co.Tz

Facebook: www.Facebook.Com/tanesco yetu

Twitter: - www.Twitter.Com/tanesco yetu

Tovuti; www.Tanesco.Co.Tz
Tunashukuru kuna maeneo kule moshi vijijini ambayo yalibahatika kuwa na umeme tooka enzi za mwalimu na kila uchwao kule nyumba zinajengwa na mahitaji ya umeme kuongezeka sasa mdau kero yake inakuja baadhi ya maeneo ambayo nimeshuhudia kwa macho yangu umeme wake ule mwanga ni bora uwashe chemli au mshumaa yaani ni mdogo tena unaumiza macho tena ikifika majira ya jioni ambapo uhitaji huongezeka ukiwasha taa zingine haziwaki kabisa tembeleeni huko vijijini hasa vunjo mkajionee
 
TANESCO kwanaza nawashukuru kwa kuwa na account yenu humu jamii f. Naomba kuuliza haya maswali. Mosi IPI ni gharama halisi ya kuunganisha Umeme wa REA vijijini? Pili, Mimi nipo katika kijijini cha Itale wilayani Ileje ambapo kwa sasa ndo Umeme umeanza kuunganishwa na tumetozwa sh elfu sabini na saba (77000) kwa kila anayetaka kuunganishwa Umeme na mkandarasi anasema elfu 27 ni ya TANESCO na elfu 50 ni ya mkandarasi. Je, ni halali hiyo? Tatu huwa hatoi list na anaandika jina tu na kwa kuwa inakuwa na uongozi wa kata na kijijini basi watu hukubali tu, je utaratibu unakuwaje? Mwisho napenda niuombe uongozi wa TASESCO ebu mtusaidie sisi wanakijiji cha Itale -Ileje maana wengi naona wataliwa fedha na wahuni kupitia mgongo wa wakandarasi uchwara.
 
Tunashukuru kuna maeneo kule moshi vijijini ambayo yalibahatika kuwa na umeme tooka enzi za mwalimu na kila uchwao kule nyumba zinajengwa na mahitaji ya umeme kuongezeka sasa mdau kero yake inakuja baadhi ya maeneo ambayo nimeshuhudia kwa macho yangu umeme wake ule mwanga ni bora uwashe chemli au mshumaa yaani ni mdogo tena unaumiza macho tena ikifika majira ya jioni ambapo uhitaji huongezeka ukiwasha taa zingine haziwaki kabisa tembeleeni huko vijijini hasa vunjo mkajionee
Hao watoe taarifa hapo Himo (kama sijakosea) kuna low voltage na Tanesco watafanya Voltage improvement kwa ku upgrade size ya transformer au kuweka TF jingine
 
Mkuu kuna upungufu wa material hasahasa nguzo hivyo kwakuwa umeshasambaziwa nguzo ujenzi wake basi sio siku nyingi kwakuwa kwa wateja wa nguzo huwa wanasambaza kwanza nguzo wakija wanasimamisha na kuwasha umeme. Kama nguzo wameleta hapo chekelea tu

Kuhusu hiyo ya REA siwezi kukupa jibu la uhakika ila ukishalipia kwenye REA wala Tanesco wanakuwa hawahusiki maana hata hela uliyolipa ni VAT na inaenda TRA wala sio kwa Tanesco.

Ukishalipa Tanesco hukabidhi kazi yako kwa contractor aliyepewa tender na REA kwa sehemu husika na huyo mkandarasi ndie naehusika kuja kufunga umeme wala sio Tanesco.
huko ikonda nililipa kwa tanesco ila nilivyowasumbua sana wakaniambia mradi upo chini ya REA, na REA haina fedha tena mpaka mwaka mpya wa fedha nkachoka.
 
TANESCO kwanaza nawashukuru kwa kuwa na account yenu humu jamii f. Naomba kuuliza haya maswali. Mosi IPI ni gharama halisi ya kuunganisha Umeme wa REA vijijini? Pili, Mimi nipo katika kijijini cha Itale wilayani Ileje ambapo kwa sasa ndo Umeme umeanza kuunganishwa na tumetozwa sh elfu sabini na saba (77000) kwa kila anayetaka kuunganishwa Umeme na mkandarasi anasema elfu 27 ni ya TANESCO na elfu 50 ni ya mkandarasi. Je, ni halali hiyo? Tatu huwa hatoi list na anaandika jina tu na kwa kuwa inakuwa na uongozi wa kata na kijijini basi watu hukubali tu, je utaratibu unakuwaje? Mwisho napenda niuombe uongozi wa TASESCO ebu mtusaidie sisi wanakijiji cha Itale -Ileje maana wengi naona wataliwa fedha na wahuni kupitia mgongo wa wakandarasi uchwara.
Mkuu kama unatozwa 77k hiyo ni bei ya kuunganishiwa umeme kwa maeneo ya kijijini.

Hiyo 150 inaenda Tanesco kama uko vizuri kihisabati basi uki calculate VAT ya hiyo 150 k ni 27k na sio kwamba inaenda REA bali kodi ya ongezeko la thamani inaenda TRA na sio REA
 
Tanesco nyie no waongo,labda maeneo mengine ya nchi. NIKO NYAMONGO NIMELIPA UMEME TA NGIA JANUARY MWISHONI NADHANI, KUTOKA KWENYE NGUZO NI MITA KAMA 88.KILA NIKIFUATILIA NI KISWAHILI TU.NA SIO MIMI TU HATA JIRANI YANGU NAYE NI LAINI YA SNGLE,MPAKA KESHO. LABDA MSEME LINGINE NIWAELEWE.NIKO NYAMONGO TARIME, 0756847424
 
huko ikonda nililipa kwa tanesco ila nilivyowasumbua sana wakaniambia mradi upo chini ya REA, na REA haina fedha tena mpaka mwaka mpya wa fedha nkachoka.
Basi usiilaumu tanesco. REA ni wakala wa kusambaza umeme vijijini hivyo jaribu kuulizia REA kwanini hawaunganishi umeme
 
Hatumuelewi Meneger wa Tanesco Bagamoyo kuna mitaa ya pale pale Bagamoyo mjini kama Sengerema na Kimara ng'ombe haina umeme almost 10 years now, its too much na imeanza kuwa na nyumba nyingi kwa miaka hyo hyo 10, Cha kushangaza ujenzi wa chuo ulioanza miaka ya hivi karibuni tayari una transfoma lake binafsi. You guys mnafanya kazi kwa masilahi ya walipa kodi au watumia kodi, matukio ya wizi yanazidi kuongezeka maeneo hayo. Na cha kushangaza zaidi maeneo ya mitaa mingine ambayo nyumba ziko more separated ndio yamepata umeme, mjali wananchi jamani huku mikoa mingine tunashuhudia mpaka nyumba za nyasi zina umeme....inakuwaje mitaa ya mjini/wilayani bagamoyo ikose.
 
Tanesco nyie no waongo,labda maeneo mengine ya nchi. NIKO NYAMONGO NIMELIPA UMEME TA NGIA JANUARY MWISHONI NADHANI, KUTOKA KWENYE NGUZO NI MITA KAMA 88.KILA NIKIFUATILIA NI KISWAHILI TU.NA SIO MIMI TU HATA JIRANI YANGU NAYE NI LAINI YA SNGLE,MPAKA KESHO. LABDA MSEME LINGINE NIWAELEWE.NIKO NYAMONGO TARIME, 0756847424
Kuwa mvumilivu mkuu, utapata umeme soon. Chamuhimu epuka vishoka ambao wanaharibu taswira ya Tanesco kwa kutapeli wateja, usitoe hela yako kwa cash, mpesa au tigo pesa. Malipo yote halali yanafanyika bank na unapata receipt.
 
Hatumuelewi Meneger wa Tanesco Bagamoyo kuna mitaa ya pale pale Bagamoyo mjini kama Sengerema na Kimara ng'ombe haina umeme almost 10 years now, its too much na imeanza kuwa na nyumba nyingi kwa miaka hyo hyo 10, Cha kushangaza ujenzi wa chuo ulioanza miaka ya hivi karibuni tayari una transfoma lake binafsi. You guys mnafanya kazi kwa masilahi ya walipa kodi au watumia kodi, matukio ya wizi yanazidi kuongezeka maeneo hayo. Na cha kushangaza zaidi maeneo ya mitaa mingine ambayo nyumba ziko more separated ndio yamepata umeme, mjali wananchi jamani huku mikoa mingine tunashuhudia mpaka nyumba za nyasi zina umeme....inakuwaje mitaa ya mjini/wilayani bagamoyo ikose.
Mkuu kama mpo wananchi wengi kuanzia 20 basi andikeni barua kuomba mradi maeneo ya kwenyu na surveyor atakuja kupima maradi ili muweze kuletewa umeme huko
 
Unatetea upuuzi?,au wewe Surveyor?..
Ndio na huwa sipendi rushwa, na ndio maana najaribu kuwaelewesha wateja njia sahihi.

Hao wanaopenda rushwa ni vishoka mkuu ila watu tunaojaua kazi zetu na wenye maadili ya kazi hatufanyi hivo
 
Mkuu kama mpo wananchi wengi kuanzia 20 basi andikeni barua kuomba mradi maeneo ya kwenyu na surveyor atakuja kupima maradi ili muweze kuletewa umeme huko
Hapana tunaomba makao makuu wafanye mawasiliano na meneja huyo wa Tanesco Bagamoyo kuhusu kero ya maeneo hayo ya Sengerema na Kimarang'ombe hayo majibu unayotoa mkuu ni majibu rahisi sana kama nilivyotangulia kusema hapo awali maeneo hayo yana nyumba bora zaidi ya 100 ambazo hazina umeme na wenyew walisema barua ya kuomba mradi ni baada ya kufikia watu 50 na sio 20 lakini hivi tunavyoongea kuna nyumba zaidi ya 100 hazina umeme na ni nyumba bora kabisa kama barua nadhani zimeshaandikwa zaidi hata ya 10 labda saizi tuandike tuadress USAID watupe msaada, tunashangaa hata huu umeme wa rea wa vijijini sisi tunakosa.....ni aibu kubwa sana
 
Hapana tunaomba makao makuu wafanye mawasiliano na meneja huyo wa Tanesco Bagamoyo kuhusu kero ya maeneo hayo ya Sengerema na Kimarang'ombe hayo majibu unayotoa mkuu ni majibu rahisi sana kama nilivyotangulia kusema hapo awali maeneo hayo yana nyumba bora zaidi ya 100 ambazo hazina umeme na wenyew walisema barua ya kuomba mradi ni baada ya kufikia watu 50 na sio 20 lakini hivi tunavyoongea kuna nyumba zaidi ya 100 hazina umeme na ni nyumba bora kabisa kama barua nadhani zimeshaandikwa zaidi hata ya 10 labda saizi tuandike tuadress USAID watupe msaada, tunashangaa hata huu umeme wa rea wa vijijini sisi tunakosa.....ni aibu kubwa sana
Chamuhimu andikeni barua kwenda kwa meneja wa tanesco pwani ikiwa na list ya wateja wanaotaka umeme mtapata tu
 
huyo anayejibu ni tanesco au kishika.Vishoka ndo wabba mlungula kwa mabs na wanatngnzw na mabs haohao wa tanyesco
 
Meter ikishafungwa sehemu hata ukitaka kuhama huwezi kuihamisha labda iwe within the sama plot (yaani mfano mita ipo chumbani unataka kuihamishia barazani au kuna nyumba nyingine kwenye the same plot)

Kama unahamia kwingine hapo meter hurudi Tanesco na wewe huko unapohamia utafanya maombi yakupata meter mpya

Asante chaliifrancisco kwa maelezo yako mazuri. Japo sijajua kama unajibu kama miongoni mwa wahusika wa TANESCO au kama mtu mwenye uzoefu na mambo ya Tanesco.

Labda nikuulize swali la ziada, iwapo Mita inarudi Tanesco je nitalazimika kuilipia upya? Au kwa malipo yale ya awali yatatosha kuniwezesha kufungiwa mita hiyo au nyingine mahali pengine baada ya kukamilisha ujazaji wa form unaoonesha eneo langu jipya (mahali ninapotaka ifungwe baada ya kuhama/kuacha eneo/ofisi ya awali).
 
Asante chaliifrancisco kwa maelezo yako mazuri. Japo sijajua kama unajibu kama miongoni mwa wahusika wa TANESCO au kama mtu mwenye uzoefu na mambo ya Tanesco.

Labda nikuulize swali la ziada, iwapo Mita inarudi Tanesco je nitalazimika kuilipia upya? Au kwa malipo yale ya awali yatatosha kuniwezesha kufungiwa mita hiyo au nyingine mahali pengine baada ya kukamilisha ujazaji wa form unaoonesha eneo langu jipya (mahali ninapotaka ifungwe baada ya kuhama/kuacha eneo/ofisi ya awali).
Mimi ni mwananchi wa kawaida tu kama wewe na kweli nina uzoefu na masuala ya Tanesco.

Kuna tabia ya sisi watanzania wengu kutopenda kusoma au kuomba kueleweshwa mambo. Ukifanya application ya maombi ya umeme ile form unayopewa ina maelezo yakutosha na kuna kipengele kinaeleza kuwa "material yote kuanzia kwenye nguzo mpaka kwenyr meter vitabaki kuwa mali ya Tanesco"

Kwanini mali ya Tanesco!?
Jibu: Tanesco wanatoa huduma ya umeme na hawauzi meter wala nguzo wala nyaya, wao wanasambaza huduma ya umeme na wewe unacholipia ni gharama kwaajili ya kupatiwa huduma ya umeme na sio gharama kwaajili yakuuziwa nguzo au meter.

Kwa mantiki hiyo basi kama uli sign ule mkataba ina maana ulisoma na kuridhia yaliyoandikwa na hivyo hupasi kupinga pale utakapoambiwa kuwa huwezi kuhamisha hiyo meter kwakuwa sio mali yako na huko unapoenda kama utahitaji umeme lazima ufanye maombi upya na kulipia gharama kama kawaida.

Kuhusu kupungua kwa gharama ni katika ku upgrade tu kutoka labda single phase kuenda three phase katika nyumba hiyo hiyo. Mfano una meter ya single phase lakini matumizi yako yameongezeka na hiyo haikidhi load uliyonayo basi utafanya maombi ya kuomba umeme na contractor wako atachora mchoro wa wiring na kuonyesha vifaa vilivyopo na total load kisha baada ya taratibu zote ile gharama ya three phase service line itachukuliwa kisha itatolewa ile uliyolipia mwanzo (single phase)

Mfano kama ulilipia 500 kupata single phase na gharama ya three phase ni 2000 basi watafanya 2000-500 na utalipia 1500
 
Back
Top Bottom