mchakavumlasana
JF-Expert Member
- Mar 9, 2011
- 389
- 212
Na gharama ya nguzo moja ni kiasi gani?Bei inategemea na umbali hivyo ndank ya mita 30 ni 321000 mijini na 177000 vijijini.ikizidi hapo inategemea na umbali uliopo
Kaka nguzo tatu ulilipia kiasi gani?Mm nimelipia nguzo 3 mwezi was September leo mwezi wa June miezi 10 karibia milioni 2 nilizolipa kwa miezi 10 ningezifanyia Biashara zingenisaidia
Tanesco ikiendelea kubaki kama ilivyo, hata angekuja rais mkali namna gani, hata ungeweka watendaji wakuu wachapa kazi kiasi gani, bado ufanisi hautapatikana! Tanesco inatakiwa igawanywe na shughuli zingine zibinafisishwe. Mfano Tanesco ya leo inatakiwa kuwa mzalishaji na msafirishaji tu wa umeme. Suala la usambazaji linatakiwa kubinafisishwa kabisa ili kuongeza tija ya kuwapatia watanzania umeme kwa haraka na kwa bei za kiushindani. Naamini kungekuwepo na makampuni binafsi ya kusambaza umeme, malalamiko mengi yasingekuwa ya kuchelewa kufungiwa umeme. Makampuni yangefanya kazi kibiashara zaidi, bei zingekuwa za kiushindani zaidi...huenda zingekuwa chini ya hizi za sasa na huduma ingepatikana kwa haraka sana. Hivyo watanzania wengi sana wangepata huduma ya umeme kwa wakati. Kama kuna wadau wa serikali au wizara husika humu na mambo haya ya umeme, nawashauri waufanyie kazi ushari wangu, utatuletea maendeleo ya haraka sana kwenye sekta ya nishati ya umeme.TANESCO inahitaji kuongozwa na mtu aina ya Kimei au Mchechu.
Shirika limekosa visionary leaders wanaenda kwa mazoea tu.
Hahahahaha Mkuranga ni MOTOOOOOO, hatimaye surveyor amepita kwenye himaya yangu na kufanya uchunguzi na kupitisha tayari kwa hatua nyingine.Nashukuru kwa maelekezo mazuri, niliyoyasoma humu. Maana nimechukua fomu Mkuranga nikaelekezwa nizikamilishe kisha watapita maeneo yetu.
Lkn imekuwa kimya,na maelekezo humu yananitaka nikabidhi ofisi ya TANESCO ktk eneo langu wao ndiyo watapanga kuja kufanya ukadiriaji Wa malipo.
Kesho narudisha fomu zangu kwa utaratibu huu niliyosoma.
Ushauti wako haufuatwi na Tanesco itaendelea kua pasua kichwa. Bora enzi za Filischemi MrambaTanesco ikiendelea kubaki kama ilivyo, hata angekuja rais mkali namna gani, hata ungeweka watendaji wakuu wachapa kazi kiasi gani, bado ufanisi hautapatikana! Tanesco inatakiwa igawanywe na shughuli zingine zibinafisishwe. Mfano Tanesco ya leo inatakiwa kuwa mzalishaji na msafirishaji tu wa umeme. Suala la usambazaji linatakiwa kubinafisishwa kabisa ili kuongeza tija ya kuwapatia watanzania umeme kwa haraka na kwa bei za kiushindani. Naamini kungekuwepo na makampuni binafsi ya kusambaza umeme, malalamiko mengi yasingekuwa ya kuchelewa kufungiwa umeme. Makampuni yangefanya kazi kibiashara zaidi, bei zingekuwa za kiushindani zaidi...huenda zingekuwa chini ya hizi za sasa na huduma ingepatikana kwa haraka sana. Hivyo watanzania wengi sana wangepata huduma ya umeme kwa wakati. Kama kuna wadau wa serikali au wizara husika humu na mambo haya ya umeme, nawashauri waufanyie kazi ushari wangu, utatuletea maendeleo ya haraka sana kwenye sekta ya nishati ya umeme.