Zile risiti za baa mnazopewa na namba za simu msizidharau, zifanyieni kazi

Zile risiti za baa mnazopewa na namba za simu msizidharau, zifanyieni kazi

Boss upo?
Hivi wale ndugu zetu kule posta bado wapo?
Kuna siku nilipita mida ya asbh,nikachungulia sikuwaona.

Nipo mkuu. Walirudi kiwizi wizi, nikaenda kununua miwili kabisa wakipotea nibaki na maisha. Maybe weekend hasa jumapili?
 
Kumezuka na wimbi jipya ingawa kwangu la zamani kidogo

Ukienda sehemu ya kula na kunywa wakati wa kulipa unapewa billi

Kwa juu imeandikwaa namba yanguu ni hii hapa.

Kuna mdada leo amepatata kazi.

Nilijaribu kumwombea kazi sehemu mbali mbali leo alipiga mchana njoo sehemu nikauliza kuna shida dada akasema hapana mungu kaniona wooh, kufika nikamkuta ana nguo za moja ya mabasi yaendayo Moshi.

Nikamwambia umeanza lini akajibu leo ndio nimeingia na safari naanza jumatatu ijayo.

Ilikuwaje nilipita sehemu mwezi na nusu uliopita huyu mdada aalikuwa anatoa huduma baadae akanipa karatasi ya bill kusoma nkaona namba nkawaza huyu sijamwomba namba wacha nijue ana shida gani. Nkaongea nae akasema atanipigia kesho yake.

Alipopiga niilikuwa busy nkamwomba ntampigia..Nilipopiga akajieleza sana akaomba msaada amesoma mpaka form four ametafuta kazi kila sehemu amekosa wapo waliojaribu kumtumia kumpa kazi wakamtosa....

Nikamweleza ntakujulisha lii uje sehemu na vyeti vyako mdada alifanya hivyo ..Nikapeleka w kwenye mabasi mbali mbali wakasema wakihitaji watampigia.

Hamada nilishassaahau kabisa niliposikia hili nilisema msidharau zile namba sio kila mmoja anataka ukamtumie wengine wana shida wanashindwa kujieleza wakiwa kazini.

Otherwise msaidie mwenzie uje kusaidiwa mbele ya safari, tenda wema uende zako ...Nimemhaidi ntatumia basi yako kwenda na kurudi na familia yangu December.

Styblsd

Letslovelead
Kumbuka akienda kuiba au kufanya tukio lolote la kihalifu ,wewe ndiye utakuwa wa kwanza kutiwa nguvuni.

Kumbuka kilichomkuta Feruzi kwenye wimbo wake wa Wema wangu umeniponza.
 
Nipo mkuu. Walirudi kiwizi wizi, nikaenda kununua miwili kabisa wakipotea nibaki na maisha. Maybe weekend hasa jumapili?
Aiseee
Yaani sikuwaona kabisa na ilikuwa weekend
Ama Kwa vile ilikuwa asubuhi?

Nataka nijaribu jioni
Nikiwakosa sijui ntakuwa mgeni wa nani🥺.
 
Kwenye basi hakuna tipu?
Sema ukweli wwe toka lini ulikata ticket ukatoa tipu kwa konda!!? Lakini Walevi kila siku wanatoa tipu na bado wanabambikiziwa bili lakini kwa kua wako tungi wao wanatoa tu majuto kesho atajijua anaanzaje siku yake mpya!!
 
Back
Top Bottom