VOICE OF MTWARA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 2,987
- 1,954
kuna wimbo mwingine unaimbwa; watoto wamekuja juuuuuuuuu, wanataka nyumba (mali) yaooooo
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
huo wimbo ulipigwa na bendi ya washirika utunzi wa hayati adam bakarkuna wimbo mwingine unaimbwa; watoto wamekuja juuuuuuuuu, wanataka nyumba (mali)
yaooooo
Huu Wimbo mbona upo humu Chifu?, angalia post namba 240...kuna wimbo mwingine unaimbwa; watoto wamekuja juuuuuuuuu, wanataka nyumba (mali) yaooooo
Watoto wamekuja Juu....
Hayati Adam Bakari ' Sauti ya Zege' na Washirika Tanzania Stars 'Watu njatanjata'
Ningali bado najiuliza usiku na mchana, na mume wangu kanitoka upweke umenizunguka...
Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao, Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao....
Na kila nikifikiria jinsi nilivyotabika, na malezi ya watoto ingawa sikuwazaa...
Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao, Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao....
Ningali bado najiuliza usiku na mchana, na mume wangu kanitoka upweke umenizunguka...
Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao, Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao...
Na kila nikifikiria jinsi nilivyotabika, na malezi ya watoto ingawa sikuwazaa...
Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao, Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao....
Adam Bakari:
Kila nilifanyalo wao haliwapendezi, na wala hawakumbuki usia wa baba yao;
Kila nilifanyalo wao haliwapendezi, na wala hawakumbuki usia wa baba yao;
Marehemu aliusia wasinitupetupe, na wala wasininyanyase mama....ooh mama...
Marehemu aliusia wasinidharau, na wala wasininyanyase mama....ooh mama...
Majirani wameshauri eti nirudi nyumbani kwani sina baba wala mama, jama niende kwa nani....
Wengine wameshauri eti niwashitaki wakati nyumbani ni mali yao, Jama nifanye nini....
Marehemu aliusia wasinitupetupe, na wala wasininyanyase mama....ooh mama...
Marehemu aliusia wasinidharau, na wala wasininyanyase mama....ooh mama...
Marehemu aliusia wasinitupetupe, na wala wasininyanyase mama....ooh mama...
Marehemu aliusia wasinidharau, na wala wasininyanyase mama....ooh mama...
Mkuu Balantanda heshima kwako jinsi ulivotukumbusha mbali sana. Infact mm mpaka sasa ni mdau wa muziki huu wa Vijana wa Zamani na ninaburudishwa sana na kuguswa na hisia nisikiapo muziki huu.
Naombeni mnisaidie kujua huu wimbo unaoitwa "
Joyce" umeimbwa na nani na bend gani na Je! nawezaje kuupata maana niliinao umeishia nusu, wakati nnaupenda mnooo...
Wimbo wenyewe unaimba hv...
">Ondoa mawazo yako nimekwishakusamehe
Mimi nakukanya Joyce usirudie tena
uliyoyafanya zamani ni mabaya sana
sasa yamekwisha Joyce usitende tena< "
rudia tena
-Unavoendelea ndio cjui saidieni wadau
Salama wakuu?,ni jumapili nyingine tulivu....
Leo naomba tujikumbushe bendi zetu zilizotamba sana miaka ya 80 na 90,bendi ambazo ama zimekufa ama zinaendelea kusuasua na ambazo ukisikiliza muziki wake leo hii unatamani ungerudisha wakati nyuma.......
Kwa kuanzia tuanze na hawa Orchestra Vijana Jazz,bendi ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Umoja wa vijana wa CCM,bendi hii ilikuwa ikitumia mitindo ya Sindimba,Hekaheka,Heka koka,Watoto wa nyumbani,Air Pambamoto(awamu ya kwanza na ya pili) na baadae mtindo wa Saga Rhumba.....
Kwangu mimi bendi hii ndiyo ilikuwa chaguo langu hasa......Ukitaka kuujua ukali wa bendi hii sikiliza nyimbo kama Chiku,Mary Maria,Penzi lamea penye penzi,Shemeji,Bujumbura,Ilikuwa lifti,Tambiko la Pambamoto,Adza(Aza),Ngapulila,Ogopa Tapeli,Mwisho wa Mwezi,Penzi haligawanyiki,Wivu,Malaine,Nyongise,Shoga,Theresa,V.I.P,Mama Chichi na nyingine nyingi tu tamu....
Bendi hii imewahi kuundwa na wanamuziki kama Hemed Maneti 'Chiriku',Hamza Kalala 'Komando',Manitu Mussa,Issa Chikupele,Hassan Dalali,Hassan Shaw,Ally Jamwaka,Abuu Semhando,Bakari 'Baker' Semhando,Mhina Panduka 'Toto Tundu',Adam Bakari 'Sauti ya zege',Eddy Sheggy,Shaban Yohana 'Wanted',Rashid Pembe 'Profesa',Kida Waziri,Beno Villa Anthony,Rahma Shally,Jerry Nashon 'Dudumizi',Suleiman Mbwembwe,Shaban Dogodogo,Aggrey Ndumbalo,John Kitime,Abdallah Mgonahazelu,Freddy Benjamin,Mohammed Gotagota,Said Hamis 'Misukosuko',Athumani Momba na wengine kibao...
Mimi nitafurahi zaidi kama nitapata mtu atakeyenipa "title" za nyimbo ambazo ziliimbwa na bendi zetu miaka hiyo ya themanini na tisini, yaani zile zilizoimbwa kwa lugha za asili za makabila yetu. Nimezitafuta sana lakini nimshindwa kuzipata.
Wakati huo wa u "teen", mimi nilikuwa nikiwajua band iliyokuwa ikipiga pale Splendid, nna uhakika kuna watu wa Dar wazamani watapakumbuka hapo, The Rifters, walikuwa vijana wa Kariakoo, kinaDodger, Salah, Marehem Abdallah Matimbwa, na wengine siwakumbuki, tulikuwa tukienda siku za jumapili saa nane mchana (enzi hizo thubutu tutoke usiku) unaachiwa radhi!
Baada ya hao nawakumbuka "The Sunburst", enzi za bahari beach, ilikuwa raha sana siku za Jumapili tukienda family nzima anaetaka beach aende anaetaka mziki haya tena...
Hawa Sunburst ndio hasa walianzisha huu mtindo unapjulikana sasa wa "mduara" kwenye dance za mziki wa kisasa. Nakumbuka walikuwa na nyimbo zao wakiziita za kitoto, kama vile "Ukuti" na mingineo ambayo kuikumbuka m kwa mara moja inakuwa shida.
Namkumbuka Muimbaji wao James, sijui yuko wapi huyu, nilimuona Kariakoo around 2005, halafu namkumbuka "Drummer boy" John Rocky, huyu yupo na namuona ona sana na baiskeli yake (hajabadilika in spite of age), na niliwahi muona miaka miwili mitatu nyuma akipiga drums pale Moevenpick halafu nikamuona Kempinski. Sijawahi kumuona Drummer boy better than him mpaka hii leo kwa huku kwetu. Namkumbuka pia mpiga wao bass maarufu Bashir, huyu ni mtoto wa yule mzee wa kizanzibari maarufu, gwiji la mziki Marehem Iddi farhan, inasemekana huyu Mzee Farhan watoto zake woote, zaidi ya kumi ni musicians (wakike na wakuime pamoja na mama yao) na inasemekana mpaka wafanyakazi wa nyumbani kwao (house girls na boys) nao pia ni musicians, isitoshe, mpaka majirani zao wengi wamefundishwa mziki na huyo mzee ama wanawe. Huyu Bashiri alikuwa na ndugu zake wanne Audu, Jaffar, Fresh na dada yao Jamila akipiga drums ) nilikuwa nikiwaona wakipiga ala tofauti hapo Sunburst.
Jamani hizo ni late 60s na 70s.
Nani anazikumbuka bendi hizi, za watoto wa mjini (in real sense)?