nanjilinji
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 1,203
- 563
Waeleze wapenzi wafute , kabla ya mp3 waweke . ili wazifaidi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yaliyopita si ndwele - Washirika Tanzania Stars (Utunzi wake 'Komando' Hamza Kalala)
Nimekusamehe lakini sitokusahau visa ulivyonitendea Kalala ee eeh,visa ulivyonitendea Kalala ee eeh
Ulinikana ee wakati mi na shida,ukasahau yote tuliyofanya nawe,wakati unaelewa hakuna Komando wa shida,wakati unaelewa hakuna Bingwa wa shida,leo nakukumbusha shida huja na kupita,yaliyopita si ndwele tugange yajayo kakaa mimi nakusamehe lakini sitokusahau,lalalala lalalala laaaa,lalalala lalalala mimi nimekusamehee,lalalala lalalala laaaa,lalalala lalalala mimi nimekusamehee
(Eddy Sheggy) Nimekusamehe lakini sitokusahau
Nimekusamehe lakini sitokusahau visa ulivyonitendea Kalala ee eeh,visa ulivyonitendea Kalala ee eeh
Ulinikana ee wakati mi na shida,ukasahau yote tuliyofanya nawe,wakati unaelewa hakuna Komando wa shida,wakati unaelewa hakuna Bingwa wa shida,leo nakukumbusha shida huja na kupita,yaliyopita si ndwele tugange yajayo kakaa mini nakusamehe lakini sitokusahau,lalalala lalalala laaaa,lalalala lalalala mimi nimekusamehee,lalalala lalalala laaaa,lalalala lalalala mimi nimekusamehee
Rafiki wa kweli ni yule asiyekutupa ee kwenye dhiki na faraja mko wote mko wote,kwenye dhiki na faraja oooh oooh,uliniacha nateseka peke yangu peke yangu,pasipo msaada wowote kaka oo oooh,pasipo msaada wowote kaka oo oooh,lakini mola muweza wa yote(wa yote) kaninusuru na matatizo yamepita o kaka,kweli nimekusamehe lakini sitokusahau,yaliyopita si ndwele tugange yajayo kaka,kweli nimekusamehe lakini sitokusahau,yaliyopita si ndwele tugange yajayo kaka,lalalala lalalala laa,lalalala lalalala mimi nimekusamehe,alalala lalalala laa,lalalala lalalala mimi nimekusamehe
Nawatakiwa maandalizi mema ya Krismas na Mwaka mpya 2014
Nawatakia Heri ya Mwaka mpya wa 2014 wadau wote wa Jukwaa hili..
Kila la heri...
Nawatakia Heri ya Mwaka mpya wa 2014 wadau wote wa Jukwaa hili..
Kila la heri...
Nzuri mkuu....Balantanda, kama ukiniwekea mashairi ya wimbo: Shahada ya Uvumilivu. Tunaambiwa ni kisa cha kweli.Naomi wa DDC,Ukewenza/ Kulala Sebuleni-Washirika. Pia Vijana Jazz: Top Queen, Visa vya mume( nikipika ugali unasema una mabuja, nikipika wali unasema una mawe, sema kinachokukera bwanaa ee),daa hadi raha. Shoga, V.I.P, Kapu la mjanja. Bantu Group- Baba Jane 1&2, mwaka mpya. Bimalee- Busu pande tatu, Makulata. Kama mzee John Kitime yumo humu jamvini yumo aje atupe uhondo. Huu music wa kubana sauti umenichosa sana. Na kwa bahati mbaya TBC nao wamekuwa .com, ni nadra sana kupiga nyimbo hizi. Hata vipindi ambavyo ilikuwa ni kichochoe cha nyimbo hizi havipo tena, labda kutokana na mabadiliko wa technology. Vipindi kama,jambo, pole kwa kazi,kombora, mchana mwema, misakato, club rahaleo show, chaguo la msikilizaji n.k. Ikumbukwe kuwa huwezi kukumbuka muziki wa dansi usihusishe RTD.
bala, huwakumbuki mzinga troupe ya moro? Waliibuka na kibao kiitwacho mazoea yanikondesha kilichotungwa na kuimbwa na issa mrisho kwa sauti nzuri sana. Kibao hicho kikipigwa hata leo utadhani ni cha jana. Baadhi ya masahiri ni haya
mazoea yananikondesha eee
sio kama nimelishwa kizizi, labda,
laini siamini alijua matatizo
hata mjusi hata kinyonga,
wao hula vijidudu hai
hasa vyenye kurukaruka, mbona yeye hana mbawaaaa
anapata riziki yakeee, sembuse mimi mwanadamu
bala, umtaja kurugenzi jazz, bila shaka ni ile ya arusha iliyokuwa na kibao kikali sana wivu
wivu ukizidi nyumbani mapenzi yapunguaa
wivu usiyo na maana waleta hasara
umefanya kitu gani, bibi umemkataza kufanya kazi
ati sababu wachelelewa nyumbani....
Kibwagizo
maisha ya leo, ni kufanya kazi
mke na mume, kusaidiana
Nzuri mkuu....
Nyimbo nyingi ulizozitaja zipo humu....Fuatilia thread toka mwanzo mpaka hapa...