bagamoyo au mtu yeyote mwenye kibao cha Ashura kilichoimbwa na sambulumaa pls nakiomba
Wakati wa utoto ilikuwa bendi yangu bora. Mpaka leo nikisikiliza nyimbo zao sizichokiPia kuna Orch. Marquiz Original,kundi hili liliundwa miaka ya 70 na wanamuziki waliotoka katika jimbo la Shaba nchini Zaire(DRC) waliingia nchini wakiitwa Orchestre Super Gabby,baada ya kuingia nchini walibadilisha jina na kuanza kuitwa Orchestra Maquis du Zaire/Marquis Original.....Mitindo waliyoitumia ni pamoja na Ogelea Piga Mbizi,Zembwela na Sendema.....Ukumbi waliokuwa wakipiga(uwanja wao wa nyumbani) ni Lang'ata Social Hall pale Kinondoni(FM Club ambapo kwa sasa ni kanisa).....Hawa pia walikuwa wanaujua muziki hasa kutokana na aina ya muziki mchanganyiko wa kizaire(kavasha) na vionjo vya kitanzania walivyopiga....
Bendi hii ilitamba na nyimbo nyingi sana,nyimbo kama Mayanga,Ngalula,Makumbele,Mpenzi Luta,Mpenzi Scola,Karubandika,Seya,Tipwatipwa,Kisabengo,Wakati nilikuwa mdogo,Bi Sofia,Hali ngumu,Ni wewe pekee,Kibulwa,Huba wangu,Mapenzi sio masihara,Wanaume wa leo,Clara,Mayasa,Wema wangu,Double double,Mabruki,Anjelu,Balimwacha,Kazi yangu Baharia,Mapenzi ya pesa na nyingnie nyingi....Hawa jamaa wanaweza kuwa wanaongoza Tanzania kwa kuwa na nyimbo nyingi sana....
Bendi hii imewahi kuwa na wanamuziki kama Tshimanga Kalala Assosa,Issa Nundu,Mukumbule Lulembo 'Parash',Mbuya Makonga 'Adios',Ilunga Banza Mchafu.Dekula Kahanga 'Vumbi',Bobo Sukari,Fredito Butamu,Mbwana Kocks,Kabea Badu,Mutombo Lufungula Audax,Matei Joseph,Kaumba Kalemba,Mukuna Roy,Berry Kankonde,William Maselenge,Seif Said,Nguza Vicking,Kyanga Songa,Kasaloo Kyanga,Kiniki Kieto na wengine kibao..............
Hakika ya kale ni dhahabu...
Huo wimbo upo youtube, nenda ksuchukue.Naomba audio ya wimbo wa zahir zorro photo album
Kama una maneno ya wimbo wa KIKO KIDS ya tabora chini ya Marehemu Salum Zahoro " MWAMTETEA BURE.....ohoohooo. hohohooo mwacheni huyooo, yaelekea hana kosa, kosa gani alilotenda, bure bure mwamfatafata..............Salama wakuu?,ni jumapili nyingine tulivu....
Leo naomba tujikumbushe bendi zetu zilizotamba sana miaka ya 80 na 90,bendi ambazo ama zimekufa ama zinaendelea kusuasua na ambazo ukisikiliza muziki wake leo hii unatamani ungerudisha wakati nyuma.
Kwa kuanzia tuanze na hawa Orchestra Vijana Jazz,bendi ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Umoja wa vijana wa CCM,bendi hii ilikuwa ikitumia mitindo ya Sindimba, Hekaheka, Heka koka, Watoto wa nyumbani, Air Pambamoto (awamu ya kwanza na ya pili) na baadae mtindo wa Saga Rhumba.
Kwangu mimi bendi hii ndiyo ilikuwa chaguo langu hasa. Ukitaka kuujua ukali wa bendi hii sikiliza nyimbo kama Chiku, Mary Maria, Penzi lamea penye penzi,Shemeji,Bujumbura,Ilikuwa lifti,Tambiko la Pambamoto, Adza(Aza), Ngapulila, Ogopa Tapeli, Mwisho wa Mwezi, Penzi haligawanyiki,Wivu, Malaine, Nyongise, Shoga,Theresa, V.I.P, Mama Chichi na nyingine nyingi tu tamu.
Bendi hii imewahi kuundwa na wanamuziki kama Hemed Maneti 'Chiriku', Hamza Kalala 'Komando', Manitu Mussa, Issa Chikupele, Hassan Dalali, Hassan Shaw, Ally Jamwaka, Abuu Semhando, Bakari 'Baker' Semhando, Mhina Panduka 'Toto Tundu', Adam Bakari 'Sauti ya zege', Eddy Sheggy, Shaban Yohana 'Wanted', Rashid Pembe 'Profesa', Kida Waziri,Beno Villa Anthony,Rahma Shally,Jerry Nashon 'Dudumizi',Suleiman Mbwembwe,Shaban Dogodogo,Aggrey Ndumbalo, John Kitime, Abdallah Mgonahazelu, Freddy Benjamin, Mohammed Gotagota, Said Hamis 'Misukosuko', Athumani Momba na wengine kibao.
Habari zaidi, soma=>Mashairi ya Kiswahili ya Nyimbo zote za Maquis du Zaire
Naomba audio ya wimbo wa zahir zorro photo album
Huu kuupata huku si rahisiNaomba audio ya wimbo wa Nash mc penati ya mwisho
Ok mkuu, acha mimi nikupe mistari miwili mitatu ya kuanzia ili uniangalizie nyimbo hizi mbili katika maktaba ya wazee.Ungeweka maneno mawili matatu yaendayo ya kibao hicho cha Ashura ningeweza kubashiri ni wimbo gani na nani kaupiga kama ni Sambulumaa band au bendi nyingine.
Maktaba ya wazee wetu imesheheni nyimbo nyingi, na uhakika ukiongeza nusu mstari wa wimbo huo, tutaweza ku upload hapa JF .
Mkuu kuna mwamba kaweka hapo chini katika post ya mwisho kabisa namba 1,595 ila bado haujamtumia ili na sisi tuupate kupitia post yako.Ungeweka maneno mawili matatu yaendayo ya kibao hicho cha Ashura ningeweza kubashiri ni wimbo gani na nani kaupiga kama ni Sambulumaa band au bendi nyingine.
Maktaba ya wazee wetu imesheheni nyimbo nyingi, na uhakika ukiongeza nusu mstari wa wimbo huo, tutaweza ku upload hapa JF .
Mkuu Balantanda hizi nyimbo mbili hauna au haujawahi kuzisikia? Nyimbo hizo ni
Bana congoMimi natafuata jina la wimbo mmoja nadhan ni wenge bcbg, unaimbwa "baswahili batakingalaba titi, eliiiiii mamaaaa eliiii maamaaa