ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

Nenda YouTube search "eddie nassor" mtumie msg wimbo unaotaka ataupload,

Nina shida na KAPU LA MJANJA, JANJA YA NYANI pamoja na KULALA SEBULENI( uke wenza huu ni Washirika Tanzania Stars) hizo zingine mbili ni Vijana Jazz
 
Nina shida na KAPU LA MJANJA, JANJA YA NYANI pamoja na KULALA SEBULENI( uke wenza huu ni Washirika Tanzania Stars) hizo zingine mbili ni Vijana Jazz

Kapu la Mjanja - Vijana Jazz

Ndege wa rangi moja huruka pamoja ee, Uliona wapi Bundi kwenye kundi la Njiwa eee,
Ndege wa rangi moja huruka pamoja ee, Uliona wapi Bundi kwenye kundi la Njiwa eee,
Uliona wapi Bundi kwenye kundi la Njiwa eee...

Wamekususa wenzio, wamekuchoka ee, visa si visa balaa hakukaliki mamaa,
Wamekususa wenzio, wamekuchoka ee, visa si visa balaa hakukaliki mamaa,

Mwenzio kakuamini, kakufanya kama ndugu,
Mwenzio kakuamini, kakufanya kama ndugu,
Kumbe usingizi hupati udenda wakutoka,
Kumbe usingizi hupati udenda wakutoka, kaka ee kaka ee
Wamtamani mkewe, kaka wee, kaka wee
Wamtamani shemeji, kaka wee , kaka wee, yoyoo...aibuuu

Kimasomaso umejitoa, Oooo Kimasomaso umejitoaaaa,
Kimasomaso umejitoa, Oooo Kimasomaso umejitoaaaa,
Umemtamkia shemejio neno la mapenzi, Umemtamkia shemejio nipe nikate kiu..
Oooh aibu imekupa, Oooh aibu Mazabe imekupata...

Shetani kamuingia kakukubalia, Shetani kamuingia kakukubalia,
Dunia haina siri mwenyewe katambua ee, Dunia haina siri mwenyewe katambua ee,
Kaka ee kaka ee, kakufukuza nyumbani, Kaka ee kaka ee, kakufukuza kwake,
Kaka ee kaka ee, na utakula nini, Kaka ee kaka ee, sasa utalala wapi, Kaka ee kaka ee yoyoo, aibuu,

Ona sasa huna pa kula na kulala, Umekuwa kama Bundi ukionekana mkosi,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Elewa Kapu kama hilo Mjinga hatii mkono,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Elewa Kapu kama hilo Mjinga hatii mkono,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Mwenye mali ameshagukuta Dunia haina siri,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Mwenye mali ameshagukuta Dunia haina siri,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Hiyo kiu gani Zege ya kumtamani shemejiyo,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Umebaki kuwayawaya wamekususa wenzio,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Umebaki kuwayawaya wayawaya wayawaya....

Nawe nami, Bara mpaka Pwani, Pambamoto shambuliaaa....
Nawe nami, Bara mpaka Pwani, Pambamoto shambuliaaaaaaa....
 
Nina shida na KAPU LA MJANJA, JANJA YA NYANI pamoja na KULALA SEBULENI( uke wenza huu ni Washirika Tanzania Stars) hizo zingine mbili ni Vijana Jazz
Kulala Sebuleni : Washirika Tanzania Stars

Mume wangu ana matatizo, yanayonifanya nikonde siku hadi siku mimi mwenzenu,
Mume wangu ana matatizo, yanayonifanya nikonde siku hadi siku mimi mwenzenu,
Kuniletea mke mwenzangu ndani ya nyumba, si jambo la kushangaza hilo,
Kinachoniuma moyoni ni kulala sebuleni oo, mimi na watoto jama,
Kuniletea mke mwenzangu ndani ya nyumba, si jambo la kushangaza hilo,
Kinachoniuma moyoni ni kulala sebuleni oo, mimi na watoto jama,

Yeye na mke mwenzangu hunisumbuasumbua, wanaporudi kutoka kwenye starehe zao,
Yeye na mke mwenzangu hunisumbuasumbua, wanaporudi kutoka kwenye starehe zao,

Kuniletea mke mwenzangu ndani ya nyumba, si jambo la kushangaza hilo,
Kinachoniuma moyoni ni kulala sebuleni oo, mimi na watoto jama,

Amesahau kama mimi ni mzazi mwenziwe, sijawahi kuona mume kumfanyia mke kama hivyo,
Nashindwa kudai talaka nimemzoea ee, naomba ushauri kwenu wenzangu, nifanyeje,

Kuniletea mke mwenzangu ndani ya nyumba, si jambo la kushangaza hilo,
Kinachoniuma moyoni ni kulala sebuleni oo, mimi na watoto jama,

Najitazama kwenye kioo mimi (mwenzenu eeeh), uzuri bado ninao mimi oooh (jama oooooh),
Najiuliza nina kasoro gani (mwenzenu eeeeh), Machozi yanidondoka mimi ooooh (jama oooooh),
Najitazama kwenye kioo mimi (mwenzenu eeeh), uzuri bado ninao mimi oooh (jama oooooh),
Najiuliza nina kasoro gani (mwenzenu eeeeh), Machozi yanidondoka mimi ooooh (jama oooooh),

Kwa nini mume wangu ananinyanyasa mimi eeeeh...

Kuniletea mke mwenzangu ndani ya nyumba, si jambo la kushangaza hilo,
Kinachoniuma moyoni ni kulala sebuleni oo, mimi na watoto jama......
 
Yap....Elly Longomba alifariki siku nyingi, tena alikufa baada tu ya kutoa/kuurudia upya wimbo wa baba yake Lovy Longomba wimbo wa 'Elly wangu' ambao alimshirikisha Papy Nguza 'Papy Kocha'...

Nakikumbuka sana kibao cha Bana Beta cha Beta Musica......Hii bendi ilitamba na kupotea ghafla...Wanamuziki waliounda bendi hii Ibonga Katumbi Jesus, Richard Mangustino, Totoo Ze Bingwa na Donat Zinga Nkuvu na mcheza shoo mahiri mwanama Salm Abeid 'Mama lao',,,
Balantanda nimesikitika kusikia kuwa Elly Longomba kuwa alifariki. She knew how to dance the ikinda nkoi....
 
Kulala Sebuleni : Washirika Tanzania Stars

Mume wangu ana matatizo, yanayonifanya nikonde siku hadi siku mimi mwenzenu,
Mume wangu ana matatizo, yanayonifanya nikonde siku hadi siku mimi mwenzenu,
Kuniletea mke mwenzangu ndani ya nyumba, si jambo la kushangaza hilo,
Kinachoniuma moyoni ni kulala sebuleni oo, mimi na watoto jama,
Kuniletea mke mwenzangu ndani ya nyumba, si jambo la kushangaza hilo,
Kinachoniuma moyoni ni kulala sebuleni oo, mimi na watoto jama,

Yeye na mke mwenzangu hunisumbuasumbua, wanaporudi kutoka kwenye starehe zao,
Yeye na mke mwenzangu hunisumbuasumbua, wanaporudi kutoka kwenye starehe zao,

Kuniletea mke mwenzangu ndani ya nyumba, si jambo la kushangaza hilo,
Kinachoniuma moyoni ni kulala sebuleni oo, mimi na watoto jama,

Amesahau kama mimi ni mzazi mwenziwe, sijawahi kuona mume kumfanyia mke kama hivyo,
Nashindwa kudai talaka nimemzoea ee, naomba ushauri kwenu wenzangu, nifanyeje,

Kuniletea mke mwenzangu ndani ya nyumba, si jambo la kushangaza hilo,
Kinachoniuma moyoni ni kulala sebuleni oo, mimi na watoto jama,

Najitazama kwenye kioo mimi (mwenzenu eeeh), uzuri bado ninao mimi oooh (jama oooooh),
Najiuliza nina kasoro gani (mwenzenu eeeeh), Machozi yanidondoka mimi ooooh (jama oooooh),
Najitazama kwenye kioo mimi (mwenzenu eeeh), uzuri bado ninao mimi oooh (jama oooooh),
Najiuliza nina kasoro gani (mwenzenu eeeeh), Machozi yanidondoka mimi ooooh (jama oooooh),

Kwa nini mume wangu ananinyanyasa mimi eeeeh...

Kuniletea mke mwenzangu ndani ya nyumba, si jambo la kushangaza hilo,
Kinachoniuma moyoni ni kulala sebuleni oo, mimi na watoto jama......

Umenikuna sana. Audio clip ya wimbo huu nitapata wapi?
 
Kapu la Mjanja - Vijana Jazz

Ndege wa rangi moja huruka pamoja ee, Uliona wapi Bundi kwenye kundi la Njiwa eee,
Ndege wa rangi moja huruka pamoja ee, Uliona wapi Bundi kwenye kundi la Njiwa eee,
Uliona wapi Bundi kwenye kundi la Njiwa eee...

Wamekususa wenzio, wamekuchoka ee, visa si visa balaa hakukaliki mamaa,
Wamekususa wenzio, wamekuchoka ee, visa si visa balaa hakukaliki mamaa,

Mwenzio kakuamini, kakufanya kama ndugu,
Mwenzio kakuamini, kakufanya kama ndugu,
Kumbe usingizi hupati udenda wakutoka,
Kumbe usingizi hupati udenda wakutoka, kaka ee kaka ee
Wamtamani mkewe, kaka wee, kaka wee
Wamtamani shemeji, kaka wee , kaka wee, yoyoo...aibuuu

Kimasomaso umejitoa, Oooo Kimasomaso umejitoaaaa,
Kimasomaso umejitoa, Oooo Kimasomaso umejitoaaaa,
Umemtamkia shemejio neno la mapenzi, Umemtamkia shemejio nipe nikate kiu..
Oooh aibu imekupa, Oooh aibu Mazabe imekupata...

Shetani kamuingia kakukubalia, Shetani kamuingia kakukubalia,
Dunia haina siri mwenyewe katambua ee, Dunia haina siri mwenyewe katambua ee,
Kaka ee kaka ee, kakufukuza nyumbani, Kaka ee kaka ee, kakufukuza kwake,
Kaka ee kaka ee, na utakula nini, Kaka ee kaka ee, sasa utalala wapi, Kaka ee kaka ee yoyoo, aibuu,

Ona sasa huna pa kula na kulala, Umekuwa kama Bundi ukionekana mkosi,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Elewa Kapu kama hilo Mjinga hatii mkono,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Elewa Kapu kama hilo Mjinga hatii mkono,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Mwenye mali ameshagukuta Dunia haina siri,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Mwenye mali ameshagukuta Dunia haina siri,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Hiyo kiu gani Zege ya kumtamani shemejiyo,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Umebaki kuwayawaya wamekususa wenzio,
Elewa Kapu la Mjanja ,Mjinga hatii mkono, Umebaki kuwayawaya wayawaya wayawaya....

Nawe nami, Bara mpaka Pwani, Pambamoto shambuliaaa....
Nawe nami, Bara mpaka Pwani, Pambamoto shambuliaaaaaaa....

Kaka, daaaah, ungepata audio clip watu wakamsikia Eddy Sheggy( R.I.P) jinsi alivyoimba vizuri huu wimbo hadi raha aisee.
Huu wimbo ulirudiwa na sauti ya Eddy Sheggy- R.I.P. iliimbwa na dada mmoja. Kwangu binafsi hawakuutendea haki wimbo huu. Lakini nyimbe zingine ambazo Eddy Sheggy aliiamba na baadae watu wakazirudia KIMAKOSA ni: Kulala Sebuleni, Kapu la Mjanja, Nimekusamehe( Utunzi wa Hamza Kalala, akiwa Washirika, ulirudiwa kimakosa na Kalala Junior)
 
Msaada wenu wana jf msaada wa rekodi ya nyimbo hizi za zilipendwa online 1. DALILI-MSONDO NGOMA 2. CHEUSI MAGALA NO.1-OTTU JAZZ 3. MALARIA-MSONDO NGOMA 4. NIPELEKE KWA BABA NO.2-OTTU JAZZ 5. SI WAZURI BINADAMU-MLIMANI PARK ORCHESTRA Kama kuna mdau ataweza kuniaploadia online au anafahamu link ambayo nitaweza kuzipata nyimbo hizi, nitashukuru sana

Hiyo namba tano; wimbo unaitwa Binadamu hana wema na umeimbwa na OSS. Unaweza kuupata kwenye link hiyo chini.

BINADAMU HANA WEMA/SHUKRANI KWA MJOMBA-OSS - BongoCelebrity
 
Wakuu mimi natafuta sana nyimbo mbili za Ottu/Msondo Ngoma,ya kwanza ni Sekuntonza na ya pili ni Arabia fadhili. Kwa yeyote mwenye nazo naomba aweke hapa na ningefurahi zaidi kama ningepata na Video pia ya Arabia fadhili.
 
Wakuu mimi natafuta sana nyimbo mbili za Ottu/Msondo Ngoma,ya kwanza ni Sekuntonza na ya pili ni Arabia fadhili. Kwa yeyote mwenye nazo naomba aweke hapa na ningefurahi zaidi kama ningepata na Video pia ya Arabia fadhili.


SHUKRANI KUBWA kwa:


  1. Video hizo Kwa hisani ya Africha Entertainment wa YouTube
  2. Director aliyeandaa video: KING DODOO La BOUCHE wa DSM
  3. Band: Msondo Ngoma Band Contact band manager Mr. Kibiriti Telephone +255 (0)655921223
 
mnanionesha njia ya kwetu-sikinde
naomi-sikinde
makulata-bima lee
neema-bima lee
masafa marefu-tuncut almasi
selina-sikinde
talaka ya hasira-sikinde
nawashukuru wazazi-sikinde
shingo ya upanga-jamhuri jazz
asha-tabora jaz
mfaume- sikinde
 
kuna wimbo unasema:-

Naikumbuka siku ileeee ulipokuja asubuhi na mapema,
ukifoka kwa ukali , kwamba ni mimi niliyetaka vunja ndoa yako.

Namshukuru baba mwenye nyumba,
aliyelizua panga lako,
lisishuke maungoni na kunipa kilema cha maisha.

Chorus:-

ukweli ulikuja kwa hasira sana (ehhh bwana ehhh)
bila kufahamu undani wa mambo yenyewe.


wimbo huo nautafuta sana, sikumbuki jina lake wala walioupiga



NI wimbo wa Msondo na mtunzi ni marehemu Nico Zengekalaambaye pia aliimba. Wimbo unaitwa "Kilema Cha Maisha."
 
Mie natafuta nyimbo za TOM MALANGA:
1.AMIGO
2.AFRO
3.BARUA.
Na pia natafuta nyimbo za yule mwanamziki mkongwe(marehemu kwa sasa)ni msambaa wa VUGA Lushoto na kwa jinsi nilivyokua nampenda mwaka 2010 nilisafiri mpaka kijijini kwao nikaliona kaburi lake.
wimbo wake ninao upenda zaidi unaitwa Mwisho wa mwezi.Hapa namuongerea EDDY SHEGGY.
 
Naona Bendi za miaka ya 1970, 1960 zimeamua kurudi uwanjani kama video hizi ''live'' za Atomic Jazz iki-perform jana 09.12.2014:

  1. Tanga's Atomic Jazz band veterans in action ''Tanzania Yetu'' : Tanga's Atomic Jazz band veterans in action https://www.youtube.com/watch?v=aDylte-9mQQ&list=UUEPDRLEx1hH201ZrSVbKGNA
  2. Tanga's Atomic Jazz band veterans in action ktk wimbo ......?? (Msaada vijana wa zamani) https://www.youtube.com/watch?v=ZruAlNhC_So&list=UUEPDRLEx1hH201ZrSVbKGNA

Video zote kwa hisani kubwa ya MUHIDIN MICHUZI wa YouTube
 
mimi kuna wimbo siujui jina lake na wala sijui bendi gani iliimba,naupenda sana na ningependa kama kuna anayeufahamu japo anitajie jina lake na bendi iliyoimba.

Wimbo wenyewe una baadhi ya maneno yafuatayo

"Tanzania yetu ndiyo nchi ya kujivunia,naye mwalimu Nyererer ndiye wetu muhifadhi......."
 
Back
Top Bottom