ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

Balantanda tafadhali huu wimbo uliitwaje?
Bado na asili navyo na kamwe sitobadilika
Japo kuwa unajitamba na cheo kujiongezea
Bure utakonda na mwili kukupooza
Umejiingiza katika mambo
Mambo ya siyo kuhusu
Mwiba huchoma kote kote
Si rahisi kukosa
Wewe bado bwana mdogo hata chini hujakaa
 
Kuna mwingine unasema "wengi wamelazwa hospitalini na kuwekewa P.O.P shauri yako Hawae,Hawae P.O.P aah P.O.P......"
Nani anakumbuka umepigwa na nani?
 
Habarini, leo nimepanda daladala nikasikia nyimbo mbili za bendi fulani za zamani, nilikuwa dogo ila nilikuwa najitambua! Nimeusikia wimbo huu nimekumbuka mbali sana tabora, nimeshawishika nitafute hizi nyimbo na zingine za kina hamza kalala komando ila sijui pa kuzipata.
Nimesikia hizi nyimbo mbili chini ktk daladala ila sizijui majina wala walioimba nikajikuta nimesafirishwa mpaka miaka ya 90s.
-Bwana mwangusi nakupa pole sana watu hao ni walaghai wanaitwa matapeli......

Mwingine huu;

-hunijali kwa chumvi hunijali kwa sukari tabu nyingi ninapata na watoto......

-Vijana wengi hukosa adabu iieee wakishajua huyo si mama yake ieeee humdharau na kumsimanga iiieeeee.......

Old is gold!!
 
Salama wakuu?,ni jumapili nyingine tulivu....

Leo naomba tujikumbushe bendi zetu zilizotamba sana miaka ya 80 na 90,bendi ambazo ama zimekufa ama zinaendelea kusuasua na ambazo ukisikiliza muziki wake leo hii unatamani ungerudisha wakati nyuma.......

Kwa kuanzia tuanze na hawa Orchestra Vijana Jazz,bendi ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Umoja wa vijana wa CCM,bendi hii ilikuwa ikitumia mitindo ya Sindimba,Hekaheka,Heka koka,Watoto wa nyumbani,Air Pambamoto(awamu ya kwanza na ya pili) na baadae mtindo wa Saga Rhumba.....

Kwangu mimi bendi hii ndiyo ilikuwa chaguo langu hasa......Ukitaka kuujua ukali wa bendi hii sikiliza nyimbo kama Chiku,Mary Maria,Penzi lamea penye penzi,Shemeji,Bujumbura,Ilikuwa lifti,Tambiko la Pambamoto,Adza(Aza),Ngapulila,Ogopa Tapeli,Mwisho wa Mwezi,Penzi haligawanyiki,Wivu,Malaine,Nyongise,Shoga,Theresa,V.I.P,Mama Chichi na nyingine nyingi tu tamu....

Bendi hii imewahi kuundwa na wanamuziki kama Hemed Maneti 'Chiriku',Hamza Kalala 'Komando',Manitu Mussa,Issa Chikupele,Hassan Dalali,Hassan Shaw,Ally Jamwaka,Abuu Semhando,Bakari 'Baker' Semhando,Mhina Panduka 'Toto Tundu',Adam Bakari 'Sauti ya zege',Eddy Sheggy,Shaban Yohana 'Wanted',Rashid Pembe 'Profesa',Kida Waziri,Beno Villa Anthony,Rahma Shally,Jerry Nashon 'Dudumizi',Suleiman Mbwembwe,Shaban Dogodogo,Aggrey Ndumbalo,John Kitime,Abdallah Mgonahazelu,Freddy Benjamin,Mohammed Gotagota,Said Hamis 'Misukosuko',Athumani Momba na wengine kibao...
Hizi nyimbo zinapatikanaje?
 



Hiyo bwana mangushi ni Ogopa matapeli ilipigwa na hao Vijana Jazz, ninayo kwenye Kompyuta yangu online nimeicheki sikuipata.
Habarini, leo nimepanda daladala nikasikia nyimbo mbili za bendi fulani za zamani, nilikuwa dogo ila nilikuwa najitambua! Nimeusikia wimbo huu nimekumbuka mbali sana tabora, nimeshawishika nitafute hizi nyimbo na zingine za kina hamza kalala komando ila sijui pa kuzipata.
Nimesikia hizi nyimbo mbili chini ktk daladala ila sizijui majina wala walioimba nikajikuta nimesafirishwa mpaka miaka ya 90s.
-Bwana mwangusi nakupa pole sana watu hao ni walaghai wanaitwa matapeli......

Mwingine huu;

-hunijali kwa chumvi hunijali kwa sukari tabu nyingi ninapata na watoto......

-Vijana wengi hukosa adabu iieee wakishajua huyo si mama yake ieeee humdharau na kumsimanga iiieeeee.......

Old is gold!!
 
Kuna mwingine unasema "wengi wamelazwa hospitalini na kuwekewa P.O.P shauri yako Hawae,Hawae P.O.P aah P.O.P......"
Nani anakumbuka umepigwa na nani?
cc Balantanda anaweza kutusaidia kupata huu wimbo wa MINUO YA MAQUIS DU ZAIRE ORIGINAL mkuu naomba msaada wako Kwa hisani yako kiuungwana tu
 
Amani Iwe nanyi wakuu,
Baada ya Kuteseka na Kuhangaika huku na kule mitandaoni nikitafuta ni wapi nitapata Ku-download ngoma zote za hapo kitambo na kukosa, basi nimeona nifungue Blog yangu ZILIPENDWA ambapo kila muda naweka Nyimbo mbali mbali zilizowahi kuwika hapa Barani Africa. Nyumbani ndio kwa Sana.
Hivyo basi wale wadau wote wa Muziki wa Kale Tukutane >>> HAPA <<<
Wadau wote wa KILWA JAZZ, MSONDO, JUWATA, SUPER RAINBOW, TABORA JAZZ, SUPER MATEMBELE, IN AFRICA, MASHROOM, LESS WANYIK/SIMBA WA NYIKA nk BOFYA >>> HAPA twende Pamoja.

Shukran.
 
Safi sana ushauri toa e mail au namba za simu ili wadau waweze kutumia nyimbo nyingine ambazo wanazo kwa kupitia whatsapp au e mail
 
Back
Top Bottom