Mpira wa sasa ni mgumu ukilinganisha na wa zamani bwana. Msipende kubadilisha vitu,, nikikuuliza pele alizipataje zile goli 1000 utanijibu nini?
Kwa sasa hata goli 500 asingefikisha ukweli ndio huo, na ukizingatia sheria zilivyo ngumu kipindi hiki acha kabisa
wa pele tunaweza danganya hapa sababu hatujauona ila wa kina zidane, figo nimeuona na wa kina ronaldo na messi nimeuona si kweli kwamba wa sasa ni mgumu.
nikupe tu homework
1. barcelona wana Beki kama puyol sasa hivi?
2. Madrid wana Beki kama Hierro, Carlos, salgado?
3. Man U wana Beki kama Ferdinand na Vidic na Evra?
4. Ac Milan wana Beki kama Nesta na Maldini?
5. Arsenal wana Beki kama Campbell na Tony Adams?
6. Chelsea wana beki kama Terry na Carvalho?
7. inter wana beki kama Lucio, zanetti na cannavaro?
8. bayern wanayo tena beki ya kina Lahm, lizarazu, sagnol na kuffour?
Hapo nimejaribu kukuonyesha mabeki wazuri miaka ya 90 hadi 2006 club kubwa ambao walicheza na kina Zidane, Ronaldo etc hao ni mabeki tu bado holding midfield za kina Gatusso, cambiaso, keane, viera, makelele, ze roberto etc
ukija makipa kina khan, dida, casilas, toldo, buffon, peter schimichel etc
kulikuwa na quality za hali ya juu. ndio maana wachezaji wote walikuwa hawana goli nyingi, sasa hivi nimetoa ushahidi comment ya juu, Messi na Ronaldo ndio wana consistency ila wachezaji kibao wanafika level ya goli 50.
mwaka ulioisha Harry kane ndio muingereza wa kwanza kufikisha Goli 50, kwa logic zetu Harry kane ni mchezaji bora kupata kutokea? Hana kombe hata moja ila magoli 50 anayo, hii inathibitisha sasa hivi ni rahisi kufunga.
muangalie ibra, cavani, suarez, dosti, falcao, na wengine wengi kwa vipindi tofauti wametupia magoli mengi ambayo hao ma legend hawajawahi je ina maana na wao nj bora?
quantity ni bora kuliko quality?