Zipo sababu za kutosha za kulilalamikia Jeshi la Polisi kusapoti Chama Tawala kwa asilimia kubwa

Zipo sababu za kutosha za kulilalamikia Jeshi la Polisi kusapoti Chama Tawala kwa asilimia kubwa

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
4,016
Reaction score
6,759
Yawezekanahiyo Video wanapasha misuli joto ama yawezekana wanafurahi pamoja kama watanzania, silipingi hili kwa sababu amani , umoja na mshikamano ndo jambo la msingi. Lakini content ya hiyo Nyimbo inalenga kukisifia chama tawala pia.

Tuache mambo ya kamanda Shana, wacha yale ya aliyekuwa OCD wa Hai na mengineyo. Lawama zinazotumwa kwa jeshi la polisi ni za msingi mno. Mihemko inawazidi na kushindwa kuficha Hisia za ulipaji wa fadhila kwa Chama Tawala.

Wahusika hatufahamu ni lini watajirekebisha. Hatujui ni lini mfumo wa sheria utabadilika at least Jeshi hili liwe taasisi huru ya kidemokrasia yenye dhima ya kweli ya Usalama wa Mali na Raia. Hatujui ni lini litaacha kuwa na sura ya kisiasa. Hii Video ni kosa kubwa sana la kimaadili na linalochafua Jeshi husika.

 
Back
Top Bottom