Zitto Kabwe: Anayefikiri Tanzania itapata Katiba Mpya bila kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi hana ubongo

Zitto Kabwe: Anayefikiri Tanzania itapata Katiba Mpya bila kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi hana ubongo

" Yeyote yule anayefikiri kuwa Tanzania itapata katiba mpya bila kwanza kuwa na Tumehuru ya uchaguzi hana ubongo" Zitto


Zitto anaongea REALPOLITIK.

Tume huru ya uchaguzi ni “offer” ambayo CCM wameamua kuitoa baada ya kutafakari kwa undani sana mkakati wa kupunguza kasi au kuzima kabisa kadhia ya madai ya katiba mpya. Credit to mtoto wa mkulima. Kura ya turufu iko kwenye madaraka ya Rais. That’s the brightest red line.

Kwa mantiki, anachosema Zitto ni nonsense. Ili kuipata hiyo Tume huru, lazima mabadiliko ya msingi yafanyike kwenye Katiba.

Lakini, kiuhalisia, Tume huru ya “mwendokasi” inaweza kupatikana kama wadau watakuwa tayari kufanya “compromise” na watawala katika mambo ya msingi kwa ahadi kuwa mengine yatamaliziwa baadaye.
 
Tanzania inahitaji katiba mpya. Tume huru na mihimili imara inayojiamini na kujisimamia ni matunda ya katiba imara yenye kubeba maslahi ya nchi.
 
" Yeyote yule anayefikiri kuwa Tanzania itapata katiba mpya bila kwanza kuwa na Tumehuru ya uchaguzi hana ubongo" Zitto

Ameanzia wapi hata akatoa kauli hii...?

Nina hakika kuna maneno umeacha na ukatupia (quote) sentensi hii moja tu..

Naamini kuna mahali Zitto kaanzia na kuna mahali alimalizia..

Otherwise, mimi binafsi nakubaliana na Zitto 100% katika mantiki ya hoja yake...

Mabadiliko yoyote ya kisiasa ni process. CCM wanaongoza serikali. Kwa hiyo obviousily, hawa ndio wanaohodhi mabadiliko haya....

So long as CCM wanaelekea kukubali kukaa mezani na kujadiliana namna ya kwenda mbele katika issue hii, basi ikikubalika kuwa tuanze na NEC huru, basi tukubaliane na hilo...

Lililo muhimu ni kutumia historia kuepuka makosa kama yaliyotokea Zanzibar na "ZEC huru chini ya JECHA" ambayo pamoja na "uhuru" huo wa tume, bado CCM walipata upenyo wa kuharibu uchaguzi mkuu wa 2015...!!

Aidha inaeleweka kuwa, ni ngumu sana kubadili muundo na mfumo wa upatikanaji wa NEC huru bila kufanya mabadiliko kadhaa ya kikatiba...

Je, tunadhani Zitto Kabwe halijui hili...?

Mimi siamini kuwa hajui. Otherwise, on one way or another he's absolutely right, kwamba one step forward kupata katiba mpya ni kuanza na NEC huru kwa maana ya huru kwelikweli...
 
Msimamo wako kuwa anaye kupinga anafanya hivyo kwa sababu ya maslahi yake ( sio dhambi) na kuwa ni mbishi tu kwa asili kunaonyesha hauna nia dhabiti ya kukubali ukweli kuwa na misimamo tofauti sio dhambi. Ingawa unasema kila mtu ana haki kuwa na mawazo tofauti una maanisha kuwa hayo mawazo tofauti lazima yaendane na ya kwako. Hiyo sio demokrasia.

Amandla...
Sasa wewe hutaki niwe na mawazo yangu? Kama nawaza kwamba anayepinga anapinga kwa sababu ya njaa yake kwa nini uone sina haki ya kuwa na mawazo hayo!

Ni wewe hapa ndiye unayeweka hiyo dhana ya "kuwa na mawazo tofauti kuwa dhambi", umeona wapi nilipoandika hivyo.

Sasa utategemea vipi "mawazo tofauti, lazima yaendane na yakwangu", hilo litawezekana vipi?
 
Hii na sawa na kuulizwa kuku na yai nani alianza.
Kuna wakati ya kupasa kuingiza kichwa kwanza Kabla ya kutumbukiza mabega na hatimaye na mkia wake.

Kuna mazingira waweza kuingia mzima mzima na isiwe tabu. Lakini upo wakati lazima uingie kidogo kidogo. Unaweza chelewa lakini mwisho utaingia mzima.

Kwa mazingira ya sasa ni ngumu kuingiza mwili wote. Labda tuendelee kukosa yote tena kama ilivyo kuwa 2014/2015

Kuna wakati inatulazimu kuifuata njia yao ili kufika mwisho wa safari yako hata ikiwa ni kwa kuchelewa.
 
Zitto wamekulishwa nini this time. Tume huru ni zao la katiba hakuna mbadala wa hilo.
 
Sasa wewe hutaki niwe na mawazo yangu? Kama nawaza kwamba anayepinga anapinga kwa sababu ya njaa yake kwa nini uone sina haki ya kuwa na mawazo hayo!
Ni wewe hapa ndiye unayeweka hiyo dhana ya "kuwa na mawazo tofauti kuwa dhambi", umeona wapi nilipoandika hivyo.

Sasa utategemea vipi "mawazo tofauti, lazima yaendane na yakwangu", hilo litawezekana vipi?
I am done.

Amandla...
 
Katiba Inasema Tume Ikimtangaza mgombea kuwa ni Rais Hakuna Mamlaka yeyote kuhoji
Tume huru itasaidiaje au unataka ubunge Katiba?!
 
ACT na Zitto wanafikiri tumesahau, marehemu aliwahi kusema ogopa sana Mungu na Teknolojia.

09201360-9938-42A9-AB6F-74207CB39FCB.jpeg
 
Niaje Msela...
Mbona Matusi tena ?

Anayefikiri tofauti ni haki yake (Fikra Huru); Hayo mambo ya kuambiana kukosa Ubongo ni Kukosa Ubongo
Huyo mtu mnayemwambia ana ubongo wa kuku mimi najaua kwanini anasema tuanze na tume huru ya uchaguzi , inawezekana anataarifa nyeti ya uchelewewashwaji wa makusudi wa kupata katiba mpya ili rais alieyeko madarakani aoengezewe muhula wa 2 mpaka 2030 bila kupingwa , hiyo ndiyo agenda wanayo push ccm nyuma ya pazia .....
 
Back
Top Bottom