Zitto Kabwe atoa hoja nzito juu ya uwekezaji wa DP World Tanzania

Zitto Kabwe atoa hoja nzito juu ya uwekezaji wa DP World Tanzania

Nimesikiliza kwa makini sana alichozungumza Zitto Kabwe juu ya hili suala la DP World.

Kwanza ningependa kumpongeza Zitto Kabwe kwa kazi nzuri sana anayoendelea kufanya, kwenye hili ametenda haki na ameonesha ukomavu wa hali juu kama kiongozi wa Chama cha Upinzani (ACT Wazalendo).

Ameweza kuondoa ukakasi kwa maneno machache sana na rahisi mno ambayo kila mtu anaweza kuelewa.

ZK anasema, kwenye jambo hili ni vyema tukatofautisha kati ya hisia na facts, ingawa hawapingi wazungumzao kwa kutumia tu hisia, kwani hisia nazo ni muhimu bali tunapaswa tuwe makini zaidi ili tuepuke upotoshaji ambao kama umejitokeza siku kadhaa nyuma.

Kwenye suala hili, ZK anasema kwamba kulikuwa na sababu za makusudi za upotoshaji, ambazo lengo lake ni kuleta hataruki (confusion) kwa jamii kwa maslahi ya kisiasa.

ZK anasema kwamba kupitia chama chake cha ACT Wazalendo, wametoa tamko linalowaeleza wananchi ni kitu gani kinakwenda kujadiliwa Bungeni. Nipongeze hatua hii kwani kwani vyama vingine mfano CHADEMA, kwenye hili kimekuwa mstari wa mbele kupotosha umma kuliko kuelimisha umma, Hongera ZK kwa hili.

ZK anaendelea, Kinachokwenda kujadiliwa Bungeni ni MoU ambayo imetoka hadharani, MoU ile, ni makubaliano kati ya serikali mbili (Dubai na Tanzania) ambapo makubaliano hayo sasa, yanatoa ruhusa ya serikali yetu kwenda kujadiliana hayo mambo yanayohusu uwekezaji wa DP World, na huko kwenye hayo majadiliano, ndipo tunapaswa tuwe makini kwa sababu ndio tutakapokuwa na masharti yote ya mkataba wa utekelezaji.

ZK kwa umakini wa hali ya juu anasema kwamba, hiki ambacho kinakwenda kujadiliwa Bungeni, "is simply the framework agreement" ambayo ina muda mahususi. ZK anasema, amesoma Kamati ya Bunge inayohusika moja kwa moja na jambo hili, na ripoti ya azimio la ambalo linakwenda kujadiliwa Bungeni inasema kwamba, "Serikali ya Tanzania itahakikisha kuwa, mamlaka ya bandari haitapokea maombi mengine kwenye maeneo ya ushirikiano yaliyoanishwa katika kiambatanisho namba 1 awamu ya kwanza mkapa hapo mazungumzo katika ya TPA na DP World yatakakuwa yamesitishwa au baada ya kupita kipindi cha miezi 12 baada ya kusainiwa kwa MoU".

Sasa basi, ili tuweze kupata mkataba wa utekezaji, ni hadi Bunge lijadili MoU na kutoa ridhaa kwa TPA kuanza majadiliano na DP World ili kuandaa mkataba wa utekelezaji (HGA), sasa kama itatokea TPA na DP World wameshindwana kwenye majadiliano ndani ya kipindi tajwa, serikali inaweza kutafuta kampuni nyingine ya kuwekeza kwenye bandari zetu.

ZK anaendelea kusema kwamba, mjadala wa Bunge juu ya MoU hii ndio muhimu zaidi, yaani ndio msingi mkuu wa HGA, kupitia hapa ndio tunaweza kujua kwamba tunaliwa au tunakula, kwahiyo ni muhimu sana Wananchi kwamba kinachokwenda kuamuliwa na Bunge, sio kuwapa DP World uendeshaji wa bandari zetu, bali kinachokwenda kuazimiwa, ni kuipa ruhusa serikali kuanza majadiliano na DP World, na kama majadiliano hayo yakishindikana, azimio lote halipo tena. Nguvu zetu,tuwekeze kwenye majadiliano ambayo yanakwenda kutupa mkataba wa utekelezaji.

Kwa ufafanuzi huu wa @zittokabwe ,kama mtu hatoelewa basi, na unaua kabisa hoja muflisi za mkataba usiokua na kikomo na mkataba wa miaka 100.
Tulilijua hili... atafuatia Lipumba kisha sheikh Kishki!! Tunajua mpambano umehamia misikitini!
 
kwanini serikali inataka kuingia mkataba na kampuni yenye tuhuma kwenye nchi mbalimbali ilizowai kufanya kazi za bandari?
DP World ni kampuni kubwa sana na inawashindani wengi sana, inafanya kazi na zaidi na ya nchi 60, ni kawaida kuwa shutuma na shutuma sio tuhuma. Hebu onesha kesi moja tu, ambayo DP World ilishindwa na kutozwa faini. Kampuni kubwa na shutuma sio kigezo cha kutofanya biashara, sio jambo baya, ni kawaida, hata wewe kesho unaweza kupewa shutuma, ila haina maana una makosa, ni shutuma tu.
 
Nimesikiliza kwa makini sana alichozungumza Zitto Kabwe juu ya hili suala la DP World.

Kwanza ningependa kumpongeza Zitto Kabwe kwa kazi nzuri sana anayoendelea kufanya, kwenye hili ametenda haki na ameonesha ukomavu wa hali juu kama kiongozi wa Chama cha Upinzani (ACT Wazalendo).

Ameweza kuondoa ukakasi kwa maneno machache sana na rahisi mno ambayo kila mtu anaweza kuelewa.

ZK anasema, kwenye jambo hili ni vyema tukatofautisha kati ya hisia na facts, ingawa hawapingi wazungumzao kwa kutumia tu hisia, kwani hisia nazo ni muhimu bali tunapaswa tuwe makini zaidi ili tuepuke upotoshaji ambao kama umejitokeza siku kadhaa nyuma.

Kwenye suala hili, ZK anasema kwamba kulikuwa na sababu za makusudi za upotoshaji, ambazo lengo lake ni kuleta hataruki (confusion) kwa jamii kwa maslahi ya kisiasa.

ZK anasema kwamba kupitia chama chake cha ACT Wazalendo, wametoa tamko linalowaeleza wananchi ni kitu gani kinakwenda kujadiliwa Bungeni. Nipongeze hatua hii kwani kwani vyama vingine mfano CHADEMA, kwenye hili kimekuwa mstari wa mbele kupotosha umma kuliko kuelimisha umma, Hongera ZK kwa hili.

ZK anaendelea, Kinachokwenda kujadiliwa Bungeni ni MoU ambayo imetoka hadharani, MoU ile, ni makubaliano kati ya serikali mbili (Dubai na Tanzania) ambapo makubaliano hayo sasa, yanatoa ruhusa ya serikali yetu kwenda kujadiliana hayo mambo yanayohusu uwekezaji wa DP World, na huko kwenye hayo majadiliano, ndipo tunapaswa tuwe makini kwa sababu ndio tutakapokuwa na masharti yote ya mkataba wa utekelezaji.

ZK kwa umakini wa hali ya juu anasema kwamba, hiki ambacho kinakwenda kujadiliwa Bungeni, "is simply the framework agreement" ambayo ina muda mahususi. ZK anasema, amesoma Kamati ya Bunge inayohusika moja kwa moja na jambo hili, na ripoti ya azimio la ambalo linakwenda kujadiliwa Bungeni inasema kwamba, "Serikali ya Tanzania itahakikisha kuwa, mamlaka ya bandari haitapokea maombi mengine kwenye maeneo ya ushirikiano yaliyoanishwa katika kiambatanisho namba 1 awamu ya kwanza mkapa hapo mazungumzo katika ya TPA na DP World yatakakuwa yamesitishwa au baada ya kupita kipindi cha miezi 12 baada ya kusainiwa kwa MoU".

Sasa basi, ili tuweze kupata mkataba wa utekezaji, ni hadi Bunge lijadili MoU na kutoa ridhaa kwa TPA kuanza majadiliano na DP World ili kuandaa mkataba wa utekelezaji (HGA), sasa kama itatokea TPA na DP World wameshindwana kwenye majadiliano ndani ya kipindi tajwa, serikali inaweza kutafuta kampuni nyingine ya kuwekeza kwenye bandari zetu.

ZK anaendelea kusema kwamba, mjadala wa Bunge juu ya MoU hii ndio muhimu zaidi, yaani ndio msingi mkuu wa HGA, kupitia hapa ndio tunaweza kujua kwamba tunaliwa au tunakula, kwahiyo ni muhimu sana Wananchi kwamba kinachokwenda kuamuliwa na Bunge, sio kuwapa DP World uendeshaji wa bandari zetu, bali kinachokwenda kuazimiwa, ni kuipa ruhusa serikali kuanza majadiliano na DP World, na kama majadiliano hayo yakishindikana, azimio lote halipo tena. Nguvu zetu,tuwekeze kwenye majadiliano ambayo yanakwenda kutupa mkataba wa utekelezaji.

Kwa ufafanuzi huu wa @zittokabwe ,kama mtu hatoelewa basi, na unaua kabisa hoja muflisi za mkataba usiokua na kikomo na mkataba wa miaka 100.
Zitto huyu huyu anayetaka tusiwaguse Wazanzibar kwenye jambo ili tusionekane Wabaguzi ? Wadanganye Wajinga sana .
 
Kama kawaida ya watanzania hakuna wasichokijua, Kkla kitu wanajua. Unaeza mkuta mtu anashabikia kuwa katiba ibadilishwe (of course ni kweli) lakin ukimuuliza kuhusu katiba iliyopo hajui kifungu chochote, watu wanatumia hisia badala la logic, Mtu kaleta Mada badala ya watu kutoa hoja, wanatoa kashfa. Yaan watanzania ni wepesi wa kukosoa sana lakini hawawezi toa njia mbadala. Sijui ni Ujuaji ulokithiri, uvivu kutafuta maarifa au mtu asionekane yuko nyuma.

Ni rahisi Tanzania mtu kupinga kitu, kama tu yeye hakifahamu bila kujitathimin kuwa yapo mengi hayafahamu na anapaswa kujifunza.

Kama Taifa tunasafari ndefu ya kwenda.


Ni vyema kujibu hoja kwa hoja.
 
Wakina nani? Mbona hakuna mkataba bado? MoU sio Mkataba...
Kwahiyo kile kipande cha mkataba kipengele cha kutoruhusiwa kuvunja mkataba hata itokee nini, hata wavunje masharti ya mkataba , ni forgery?
EEA5EC86-2038-43B0-8AF2-4FB79C49DC6F.jpeg
 
Back
Top Bottom