Zitto Kabwe: Rais Samia ametembea kwenye maneno yake, haikuwa rahisi

Zitto Kabwe: Rais Samia ametembea kwenye maneno yake, haikuwa rahisi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzungumza na viongozi wa vyama vya siasa leo Januari 3, 2022, (Rais Samia: Vyama vya siasa ruksa kufanya Mikutano ya hadhara ) kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ametoa neno:

"Wakati Rais Samia anakula kiapo kwa mara ya kwanza aliahidi kukutana na wanasiasa na kutengeneza mazingira ya siasa zenye tija.

“Rais ametembea kwenye maneno yake na vitendo vilivyofanyika ni lazima apongezwe, haikuwa kazi rahisi sote tunajua.

“Wakati tunafanya mkutano wa kwanza wa vyama Desemba 2021, maneno yalikuwa mengi sana, baadaye tulipofanya mkutano wa Kituo cha Demokrasia (TCD) maneno yalikuwa pia, ni lazima apongezwe.

“Ni wajibu wetu kutumia majukwaa kuwasemea Watanzania, tutatumia majukwaa ya kisiasa na huo ndio wajibu wetu, nadhani tumeanza vizuri mwaka wa mageuzi ya kisiasa.”
 
Baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzungumza na viongozi wa vyama vya siasa leo Januari 3, 2022, (Rais Samia: Vyama vya siasa ruksa kufanya Mikutano ya hadhara ) kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ametoa neno:

"Wakati Rais Samia anakula kiapo kwa mara ya kwanza aliahidi kukutana na wanasiasa na kutengeneza mazingira ya siasa zenye tija.

“Rais ametembea kwenye maneno yake na vitendo vilivyofanyika ni lazima apongezwe, haikuwa kazi rahisi sote tunajua.

“Wakati tunafanya mkutano wa kwanza wa vyama Desemba 2021, maneno yalikuwa mengi sana, baadaye tulipofanya mkutano wa Kituo cha Demokrasia (TCD) maneno yalikuwa pia, ni lazima apongezwe.

“Ni wajibu wetu kutumia majukwaa kuwasemea Watanzania, tutatumia majukwaa ya kisiasa na huo ndio wajibu wetu, nadhani tumeanza vizuri mwaka wa mageuzi ya kisiasa.”

Akina mdude chadema , wataweza siasa za kistaarabu??
 
Ukiona ccm wameruhusu mikutano ujuwe katiba mpya hakuna.
 
Wapinzani uchwara, ni heri tujue moja kwamba na nyinyi ni Mafisiemu sio kucheza na Saikolojia yetu.
Hamna mbele wala nyuma mpo mpo tu kama sigara kali.
Kila siku mnapiga trip ikulu kama Gari tipa la mavi.​
walipowaingiza barabarani kufanya fujo hamkuingia barabarani, mlipoambiwa mbaki mita 200 mlinde kura mkagoma sasa mlitaka wafanyeje ?
 
Ngoja tuone kama na sarakasi za polisi kwenye kutoa vibali zitaisha!
 
Kuna watu bado mnawafuatilia hao the so called 'wapinzani'.. bora mtafute kazi ya kufanya.
 
Wewe unawaza viti vya ubunge, wenzako wanawaza kuimarisha na kujenga chama nchi nzima. Majimbo yapo tu, ila Uhuru wa kufanya siasa Tena kwa kulindwa na Polisi ni muhimu Sana.
Hao wengine ni wale wanaowaza matumbo tu. Utasikia wanakwambia eti Katiba Mpya inaleta ugali🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom