Zitto Kabwe: Ubadhirifu wa 2020/21 ni mara mbili ya mwaka uliotangulia. Kulikuwa na ubadhirifu kwa jina la uzalendo

Zitto Kabwe: Ubadhirifu wa 2020/21 ni mara mbili ya mwaka uliotangulia. Kulikuwa na ubadhirifu kwa jina la uzalendo

View attachment 2194749


Kuna watu walikuwa wanajifanya wazalendo mpaka kupiga wengine risasi. Lakini ni wazalendo gani wanampiga mtu risasi akiwakosoa, wanataifisha pesa za watu kwenye bank, waharibu biashara na uwekezaji wa watu, wanajipendelea na kutumia pesa ya umma kujenga kwao na kufikia mpaka kuweka mbuga, wanaiba kura kwa kupitia usalama na Polisi, wanatumia pesa nje ya budget, wana rekodi maadui wao wa kisiasa, wanauwa waandishi wa habari wanao wapinga, wanadanganya Watanzania kuhusu covid……
Kweli “uzalendo” ndio kichaka cha wezi wa awamu ya 5.
 
Wapi nimeandika anachosema Zitto dhidi ya Magufuli sio sahihi?

Nisome unielewe hasa paragraph ya pili.

Ukitoka hapo ndio uone unafiki wa huyo Zitto anapopigia kelele uwepo wa tatizo kila siku, lakini akiambiwa aungane na wanaotaka solution anawakimbia, mimi sio mjinga.
Nimekuelewa.
 
Ni kweli kabisa Magufuli alikuwa na siasa za uongo:
• Alitudanganya amejenga flyovers
• Alitudanganya amejenga SGR
• Alitudanganya amehamishia serikali Dodoma
• Alitudanganya amejenga vituo vya afya na hospital za willaya na rufaa
• Alitudanganya amekarabati shule kongwe
• Alitudanganya elimu bure
• Alitudanganya kufufua shirika la ndege, reli, na kukarabati na kujenga reli mpya
• Alitudanganya anajenga na kupanua miundombinu ya barabara
• Alitudanganya anajenga bwawa la Mwl Nyerere
• Alitudanganya anapambana na rushwa, mafisadi, wauza madawa ya kulevya na uhakifu mwingine
• Name them

Ni kweli kabisa alitudanganya na aliendesha siasa za uongo na ulaghai.

Nakuuliza katika hayo, kipi cha pekee ambacho watawala waliotangulia hawakufanya?

Daraja la juu la Ubungo, mchakato wake ulianza tangu awamu ya 4. Na je, hilo ni daraja la kwanza kujengwa Tanzania?

Reli ambayo mpaka leo haijafika hata Dodoma, hivi unaifahamu reli ya uhuru (ilijengwa na wakoloni), SGR ya TAZARA, ni kilometer elfu ngapi?

Elimu bure hii ambayo haina hata ubora, waulize waliosoma miaka ya nyuma, ambapo ukiwa university ulikiwa unapewa high learning allowance. Shule za msingi na sekondari, wanafunzi walikuwa wanapewa madaftari, kalamu na vitabu bure.

Hivi unajua kuwa tuliwahi kununua ndege 13 mpya, zote jet, siyo hizi za mchanganyiko na pangaboi? Suala siyo kununua bali ni kufanya shirika liweze kutoa huduma na kutengeneza faida, kitu ambacho mpaka leo tumeshindwa.

Kwenye ujenzi wa barabara za lami, una ujasiri wa kusema wakati wa utawala wa Magufuli ndiyo zimejengwa sana? Awamu ya 4, zilijengwa 12,000km, awamu ya 5 zimejengwa 2,800km. Zipi ni nyingi kwa uelewa wako?

Hilo bwawa la umeme la Nyerere ndiyo la kwanza? Unayajua mabwawa ya Kidatu, Mtera, Kihansi, mitambo ya kufua umeme wa gas?

Kuhusu kupambana na rushwa na ufisadi na wizi, umejiuliza Sabaya anafanya nini jela? Amejiuliza Makonda utajiri wake mkubwa uliupataje? Umesoma report ya CAG juu ya wizi na ufisadi mkubwa uliofanywa na utawala wa Magufuli? Magufuli aliwahadaa watu, na kujifanya mkali sana, watu wakawa waoga, akatumia nafasi hiyo yeye na watu wake kufanya ufisadi mkubwa unaowekwa wazi sasa na report za CAG.

Hospitali za wilaya na vituo vya afya, hivi unafahamu kuwa hospitali na vituo vya afya, vyote vilivyojengwa wakati wa Magufuli, ukiviweka pamoja, thamani yake haifikii hospitali moja tu kama ile ya Mloganzila au Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete?

Unajua kuwa aliuporomisha ukuaji wa uwekezaji toka 28% mpaka 4%? Unajua kuwa aliporomosha ukuaji wa utalii toka 15% mpaka 3.6%? Unafahamu kuwa alidondisha thamani ya mauzo ya mazao ya kilimo kwa 50%?

Ni mjinga pekee yake, ndiye anaweza kuamini kuwa eti Magufuli alifanya mambo makubwa kuliko utawala mwingine wowote uliopita.

Mtu unazungumzia kufuta ada mashuleni, huzungumzii aliyezijenga. Umazungumzia ukarabati wa hospitali, huzungumzii alizijenga hizo hospitali, wewe kweli ni mzima?

Kama kuna jambo pekee alilofanikiwa kwa kiasi kikubwa Magufuli, basi ni kutengeneza kundi la wajinga ambao hata ukawaonesha guni la mahindi na kibaba, watakuambia kibaba kina ujazo mkubwa zaidi kuliko gunia.
 
Huu ufisadi wa Magufuli ndio unamuuma sana Zitto zaidi ya ule wa Escrow, EPA nk

Huyu mmoja alikuwa anaiba huku anajiita mzalendo ili kutudanganya, yule mwingine alikuwa anaiba kimya kimya, hawa kwangu wote ni wezi tu.

Najua Zitto anashindwa kumlaumu yule mmoja kwasababu aliwahi kusema huyo alikuwa ni sawa na baba yake, anamfichia aibu.

Anajua kulalamika kama vile ni mzalendo wa kweli, kumbe akiambiwa habari za Katiba Mpya naye hataki kuzisikia. Maana yake huyu mnafiki anataka tuendelee kuibiwa na marafiki zake ili nae agaiwe, ila tukiibiwa na wale wasio rafiki zake ndio anaumia.

Kuendelea kumshangilia huyu tapeli na hizi kelele zake za kila siku kwa Magufuli ni kujidumaza akili tu, anawazubaisha wajinga, na kwa ujinga wao wanazidi kumshangilia.
Umeongea vema mkuu!

Kwa msomi na mwanauchumi kama Zitto, ni vema angebainisha ufisadi anaousema kipengele baada ya kipengele na kutwambia hizo pesa zilikuwa zikipelekwa wapi?

Zitto analalamika tuu bila kusema nini ni nini...!!
 
Nakuuliza katika hayo, kipi cha pekee ambacho watawala waliotangulia hawakufanya?

Daraja la juu la Ubungo, mchakato wake ulianza tangu awamu ya 4. Na je, hilo ni daraja la kwanza kujengwa Tanzania?

Reli ambayo mpaka leo haijafika hata Dodoma, hivi unaifahamu reli ya uhuru (ilijengwa na wakoloni), SGR ya TAZARA, ni kilometer elfu ngapi?

Elimu bure hii ambayo haina hata ubora, waulize waliosoma miaka ya nyuma, ambapo ukiwa university ulikiwa unapewa high learning allowance. Shule za msingi na sekondari, wanafunzi walikuwa wanapewa madaftari, kalamu na vitabu bure.

Hivi unajua kuwa tuliwahi kununua ndege 13 mpya, zote jet, siyo hizi za mchanganyiko na pangaboi? Suala siyo kununua bali ni kufanya shirika liweze kutoa huduma na kutengeneza faida, kitu ambacho mpaka leo tumeshindwa.

Kwenye ujenzi wa barabara za lami, una ujasiri wa kusema wakati wa utawala wa Magufuli ndiyo zimejengwa sana? Awamu ya 4, zilijengwa 12,000km, awamu ya 5 zimejengwa 2,800km. Zipi ni nyingi kwa uelewa wako?

Hilo bwawa la umeme la Nyerere ndiyo la kwanza? Unayajua mabwawa ya Kidatu, Mtera, Kihansi, mitambo ya kufua umeme wa gas?

Kuhusu kupambana na rushwa na ufisadi na wizi, umejiuliza Sabaya anafanya nini jela? Amejiuliza Makonda utajiri wake mkubwa uliupataje? Umesoma report ya CAG juu ya wizi na ufisadi mkubwa uliofanywa na utawala wa Magufuli? Magufuli aliwahadaa watu, na kujifanya mkali sana, watu wakawa waoga, akatumia nafasi hiyo yeye na watu wake kufanya ufisadi mkubwa unaowekwa wazi sasa na report za CAG.

Hospitali za wilaya na vituo vya afya, hivi unafahamu kuwa hospitali na vituo vya afya, vyote vilivyojengwa wakati wa Magufuli, ukiviweka pamoja, thamani yake haifikii hospitali moja tu kama ile ya Mloganzila au Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete?

Unajua kuwa aliuporomisha ukuaji wa uwekezaji toka 28% mpaka 4%? Unajua kuwa aliporomosha ukuaji wa utalii toka 15% mpaka 3.6%? Unafahamu kuwa alidondisha thamani ya mauzo ya mazao ya kilimo kwa 50%?

Ni mjinga pekee yake, ndiye anaweza kuamini kuwa eti Magufuli alifanya mambo makubwa kuliko utawala mwingine wowote uliopita.

Mtu unazungumzia kufuta ada mashuleni, huzungumzii aliyezijenga. Umazungumzia ukarabati wa hospitali, huzungumzii alizijenga hizo hospitali, wewe kweli ni mzima?

Kama kuna jambo pekee alilofanikiwa kwa kiasi kikubwa Magufuli, basi ni kutengeneza kundi la wajinga ambao hata ukawaonesha guni la mahindi na kibaba, watakuambia kibaba kina ujazo mkubwa zaidi kuliko gunia.
Wasomi nyinyi mmekuwa wehu?

Utwambie, Ni wapi pesa zimepigwa na kwenda wapi na ni shi ngapi?

Unaposema vituo vya afya ni mpango wa awamu ya NNE unamaana gani? Je zingelibaki kuwa ni mpango tuu au?

Eti reli ungependa kuiona ikichukua miaka na miaka, jinga kabisa wewe, teknologia ya karine hizo ulinganishe na Leo?

Lipi bora kwako, mipango ya awamu ya NNE kuendelezwa na kukamilishwa na au kubakia kuwa mipango tu hata awamu ya tano, ungechagua lipi pimbi wewe?

Ni wajinga wachache hasa wezi, fisadi, wala rusha, wauza ngada na feki vyeti ndio mnaog'aa sharubu kushambulia kazi za mwamba, na hata hivyo, hambadirishi chochote masikioni mwa mamilioni ya watanzania

Kunyweni sumu iwapo mmechukizwa na kazi zake mwamba JPM
 
Nikusahihishe hapo Kweny flyover.. Tanzania bado hatujawa na flyovers. Pale tazara tuna flying bridge, na ubungo tuna flying bridge!! Fika angalau Kenya utajua nn maana ya flyovers!!!
Ni kweli kabisa Magufuli alikuwa na siasa za uongo:
• Alitudanganya amejenga flyovers
• Alitudanganya amejenga SGR
• Alitudanganya amehamishia serikali Dodoma
• Alitudanganya amejenga vituo vya afya na hospital za willaya na rufaa
• Alitudanganya amekarabati shule kongwe
• Alitudanganya elimu bure
• Alitudanganya kufufua shirika la ndege, reli, na kukarabati na kujenga reli mpya
• Alitudanganya anajenga na kupanua miundombinu ya barabara
• Alitudanganya anajenga bwawa la Mwl Nyerere
• Alitudanganya anapambana na rushwa, mafisadi, wauza madawa ya kulevya na uhakifu mwingine
• Name them

Ni kweli kabisa alitudanganya na aliendesha siasa za uongo na ulaghai.
 
Wewe bila shaka ni kipofu wa akili.

Ni nini cha pekee alichofanya Magufuli ambacho hakijawahi kufanyika huko nyuma?

Kama una akili na ufahamu na uwezo wa kufuatilia mambo, utagundua kuwa Magufuli alikuwa anaendesha siasa za uwongo kuwahadaa wajinga wamwone kuwa anafanya mambo makubwa sana ambayo hayajawahi kufanyika, wakati hakuna hata moja lililokuwa jipya.
Wewe ndio kipofu mkuubwa wake, kwa sababu yaliyojaa moyoni mwako ni chuki tuu dhidi ya unayemsema
 
Kuna wakt naunga mkono Sana regime ya magufuli na kumpenda Sana na kujuta kumpoteza mtu Kam huyu lkn Sasa Kuna wakt nikiona udhalimu wake huu namchukia mbya Sana kifup Ni kuwa Kuna 50 nzur za magu na Kuna 50 mbaya za kwake pia

Mbaya Ni nyingi sana
 
Wacha kuremba remba awamu ya 5 walikuwa wezi sana
Hizo ni propaganda tu, awamu ipi ambayo haina dosari kwenye ripoti ya CAG? Na si kila dosari kwenye ripoti ya CAG inamaanisha wizi umefanyika.
 
Kuna wakt naunga mkono Sana regime ya magufuli na kumpenda Sana na kujuta kumpoteza mtu Kam huyu lkn Sasa Kuna wakt nikiona udhalimu wake huu namchukia mbya Sana kifup Ni kuwa Kuna 50 nzur za magu na Kuna 50 mbaya za kwake pia

Mbaya Ni nyingi sana
Duu! Yaani nzuri 50 na mbaya 50, alafu unasema mbaya ni nyingi sana!
 
Huu ufisadi wa Magufuli ndio unamuuma sana Zitto zaidi ya ule wa Escrow, EPA nk

Huyu mmoja alikuwa anaiba huku anajiita mzalendo ili kutudanganya, yule mwingine alikuwa anaiba kimya kimya, hawa kwangu wote ni wezi tu.

Najua Zitto anashindwa kumlaumu yule mmoja kwasababu aliwahi kusema huyo alikuwa ni sawa na baba yake, anamfichia aibu.

Anajua kulalamika kama vile ni mzalendo wa kweli, kumbe akiambiwa habari za Katiba Mpya naye hataki kuzisikia. Maana yake huyu mnafiki anataka tuendelee kuibiwa na marafiki zake ili nae agaiwe, ila tukiibiwa na wale wasio rafiki zake ndio anaumia.

Kuendelea kumshangilia huyu tapeli na hizi kelele zake za kila siku kwa Magufuli ni kujidumaza akili tu, anawazubaisha wajinga, na kwa ujinga wao wanazidi kumshangilia.
Mkuu umepiga za uso, chuki yote hii kwa Magu ni kwa kuwa hakupata fursa ya ulaji..........huyu naona yuko ki-fursa zaidi kuliko anavyotaka kuaminisha watu kwamba yupo kutetea maslahi ya wanyonge, mtu anayetetea wanyonge hawezi kamwe kupinga hoja ya katiba mpya....
 
Huu ufisadi wa Magufuli ndio unamuuma sana Zitto zaidi ya ule wa Escrow, EPA nk

Huyu mmoja alikuwa anaiba huku anajiita mzalendo ili kutudanganya, yule mwingine alikuwa anaiba kimya kimya, hawa kwangu wote ni wezi tu.

Najua Zitto anashindwa kumlaumu yule mmoja kwasababu aliwahi kusema huyo alikuwa ni sawa na baba yake, anamfichia aibu.

Anajua kulalamika kama vile ni mzalendo wa kweli, kumbe akiambiwa habari za Katiba Mpya naye hataki kuzisikia. Maana yake huyu mnafiki anataka tuendelee kuibiwa na marafiki zake ili nae agaiwe, ila tukiibiwa na wale wasio rafiki zake ndio anaumia.

Kuendelea kumshangilia huyu tapeli na hizi kelele zake za kila siku kwa Magufuli ni kujidumaza akili tu, anawazubaisha wajinga, na kwa ujinga wao wanazidi kumshangilia.
Kama viongozi watarajiwa wa nchi hii ndio Hao basi tufahamu kuwa nchi INA ombwe kubwa sana la viongozi bora !! Sijui tunatokaje kama Taifa !!
 
Ni kweli kabisa Magufuli alikuwa na siasa za uongo:
• Alitudanganya amejenga flyovers
• Alitudanganya amejenga SGR
• Alitudanganya amehamishia serikali Dodoma
• Alitudanganya amejenga vituo vya afya na hospital za willaya na rufaa
• Alitudanganya amekarabati shule kongwe
• Alitudanganya elimu bure
• Alitudanganya kufufua shirika la ndege, reli, na kukarabati na kujenga reli mpya
• Alitudanganya anajenga na kupanua miundombinu ya barabara
• Alitudanganya anajenga bwawa la Mwl Nyerere
• Alitudanganya anapambana na rushwa, mafisadi, wauza madawa ya kulevya na uhakifu mwingine
• Name them

Ni kweli kabisa alitudanganya na aliendesha siasa za uongo na ulaghai.
Mkuu unafikiri hawaelewi haya? Ni kwamba huu ni mkakati maalumu wa kumchafua tu, kwa kuwa awamu nyingine hazikufanya hata nusu ya hayo, hata hii tuliyonayo haiwezi kufanya hata robo ya awamu ya tano.

Kutokana na hayo wameamua kuja na mkakati maalumu wa kumchafua ili ionekane kwamba hakuna kilichofanyika, ni aibu tu wanaona maana wanashangaa kuwa aliwezaje kufanya hayo bila tozo wala kuwapigia magoti wazungu? Wao kutwa kuwapigia magoti wazungu lakini bado mambo hayaendi.

Enzi za Magufuli mara kadhaa tuliona wanabana matumizi kwa kusitisha sherehe fulani za kitaifa na pesa kupelekwa kwenye shughuli za maendeleo, leo huwezi sikia hilo, Wananchi tunalia hali ngumu wao ni kutumia "Helicopter" na kusafiri kwa makundi kwenda kwenye nchi za watu, ni mwendo wa kulamba asali tu.
 
Kwenye hi dunia nimegundua kuna ukweli na wasema ukweli wa aina mbili, wengine huuusema ukweli kwa nia njema kabisa while wengine huusema ukweli kwa nia OVU au HILA, kwangu mimi zitto anaangukia KUNDI la pili. Kuna wasema ukweli huku wakiwa na chuki binafsi na huyo wanae mtolea huo ushahidi wa huo ukweli wanao usema. Mengi ya haya yalio onwa na CAG wapinzani hasa Lissu walipigia sana kelele manunuzi yasio fata sheria, walipigia sana kelele hata ujenzi wa uwanja wa ndege Chato, kama kumbukumbu zangu zipo sahihi, zitto nilimsikia akilalamikia ujenzi wa SGR to Mwanza kwamba sio sahihi (namuunga mkono ) akipendekeza SGR iende Kigoma kuliko Mwanza (namuunga mkono hapa pia ) but pamoja na sababu nzuri alizozitaja kuhusu SGR to Kigoma kwamba is more beneficial than Mwanza but again alikua na HILA, KWAO kule, alikua na conflict of interest kama Magufuli tu
 
Zitto ni mdini sana na ni mnafiki aliyepitiliza chadema walifanya jambo jema kumtema mchawi huyu.
uko sawa,udini upo sana lipo kundi la dini huwa haliangalii udini lingine udini sna kwasasa mwendo huu umeshamiri japo kama hauonekani lkn ndo ukwerii.
 
Kama angekuwa ni mdini hasingechangisha ujenzi wa msikiti kanisani.na huo ufisadi unaozungumzia hamna ushahidi wowote kama hizo jela zilienda wapi?
Nyie wafuasi wa Magufuli Ni matahira kweli, report ya CAG hujaisoma au?!
 
Kama awamu ya tano waliiba hivyo na bado tukaona tangibles hizo,vipi serikali ya awamu ya nne na sita ambazo Ni Safi kabisa hazikuiba lakini hatuoni kinachofanyika zaidi ya utumbuaji was kina ma rope , escrow, EPA,meremeta, symbion,IPTL,bwawa huko TANGA nk,zito ndo mpiga filimbi was makambà,like dodoki la nyerere katika speech yake mbeya mwaka 1995 ili mulenga Nani kweli ?
 
View attachment 2194749


Kuna watu walikuwa wanajifanya wazalendo mpaka kupiga wengine risasi. Lakini ni wazalendo gani wanampiga mtu risasi akiwakosoa, wanataifisha pesa za watu kwenye bank, waharibu biashara na uwekezaji wa watu, wanajipendelea na kutumia pesa ya umma kujenga kwao na kufikia mpaka kuweka mbuga, wanaiba kura kwa kupitia usalama na Polisi, wanatumia pesa nje ya budget, wana rekodi maadui wao wa kisiasa, wanauwa waandishi wa habari wanao wapinga, wanadanganya Watanzania kuhusu covid……
Watakwambia tumejenga sgr sijui flyover and such upuuzi kuhalalisha upigaji..

Hivi Serikali haiwezi mkamata mlipaji mkuu wa serikali ya awamu ya 5?

Ujue hawa ndio walikuwa wanawaambia watu kwamba eti ni zamu yetu.Haiwezekani Tzn hii imegeuka shamba la bibi..

Kiongozi wao na yule mshenzi mwenye shutuma za kunyika watu haki ya kuishi walikuwa wanajizungusha makanisani na kujifanya wanamjua Sana Mungu kumbe ni majambazi..

Inatia hasira Sana mbwa hao 👇

Screenshot_20220420-213234.png


Screenshot_20220420-213038.png
 
Back
Top Bottom