Zitto: "Majibu ya Sumari ni 'ovyo ovyo'"; atakiwa kufuta kauli!

Tatizo CCM wamezoea kufunika, panaponuka pamoja na wao weneyewe kuelewa kuwa pananuka watasema pananukia, ili mradi tu wanafanikisha wanachokitaka.
 
Spika katoa majibu juu ya issue ya Mh. Zitto kalaza kiporo hadi next week ndio apange namna ya kumshughulikia.

Suala la Seleli bado anazidi kilimung'unya limemshinda Home boy wake nalo anadai bado makatibu wa bunge wanafunua mavitabu kuona kama fedha zilishapitishwa lakini inaonekana wazi hakuna kitu wanaficha.

Six bado analalama eti magazeti yanamchonganisha na Serikali kwa kudai anawachonganisha na mawaziri na baadhi ya wabunge.

My rule

Kwanini wabunge wasimpige chini tu huyu spika kama waingereza walivyompiga chini spika wao Martin
amekuwa mnafiki mno.
 
Safi sana Zitto kaza buti urudishe sifa zako ilizozipoteza kamua tunataka waongezeke tene ili CCM wazidi kuumia
 


Kwa hili naona unatoka nje ya mstari..............
 
Kwanini wabunge wasimpige chini tu huyu spika kama waingereza walivyompiga chini spika wao Martin
amekuwa mnafiki mno.

Sawa kabisa Huyu baba SIX anaharibu bunge na kuelemea upange mmoja
watu wa kwao urambo wanamchukia saaana hana msaada kwao jamani jamani hawa wabunge sijui neseme nini hawana msaada wowote wanatesa tu wanachi
 
This is shaping up a showdown in Dodoma between Zitto and the masses on the one side and Sitta and the status quo on the other.

They better recognize, or else they will restore the "martyrdom" status all over again after the Dowans brouhaha.
 
Wakuu tusiwe tunachanganya vitu hapa kwa sababu tu tunataka ujumbe fulani ufike.. Na ubaya wake ni kwamba inaonyesha sisi wenyewe tunapuyanga tu bila kutazama sheria..
Nitarudia tena kusema hivi hakuna sheria ndani ya Tanzania ktk miiko na maadili ya viongozi inayomkataza kiongozi kumiliki shirika wala swala lolote linalohusiana na Conflict.. Azimio la Zanzibar lipo kisheria na linadunda kama kawa hivyo fikra zetu ktk kutafuta haki ni lazima zianze na Azimio hilo na sio kurukia kulaumu kiongozi ambaye anamiliki shirika kisheria..

Hata kama mimi ningekuwa nafasi ya huyu waziri Sumari pewngine ningekuwa namiliki shirika kwa sababu huvunji sheria, mbali na hivyo hakuna kiongozi hata mmoja nchini ambaye hamiliki shirika binafsi as a sole Ownership, Partnership, ama a Corporate..hakuna! kama ipo naomba mnipe kifungu cha sheria kinacholifuta/tengua Azimio la Zanzibar..

Hivyo tuwe waangalifu na sheria zetu kabla ya kupakaza ili mradi mtu fulani aonekane mbaya..
Tumeona majibu ya wakubwa kuhusiana na Azimio hilo kwamba muswada ndio kwanza unaandaliwa ili kufikishwa bungeni...pengine hadi kufikia bunge lipitishe sheria hiyo itakuwa 2015.
 
nguvu ya dr.slaa na zitto bungeni inaonesha jinsi gani wabunge wa ccm wako weak sana kiasi cha kwamba wanapata jazba na kutoa maneno ya kitoto bungeni.tuombe tu mwakani wabunge wa upinzani waongezeke tuone sasa wabunge wa ccm watavyokua wanaropoka matusi ndani ya bunge kwa hasira.
 
Nilivyomsikiliza Sitta, nimegundua kuwa kuna jambo kubwa nyuma ya hili sakata. Kwa manno ya Sitta, inamaanisha kuwa baada ya kumaliza kupitisha bajeti mwaka jana, wizara ikaenda kuongeza vifungu vya fedha kwenye vvifungu ambavyo havikupangiwa fedha na ndio maana vitabu vya bajeti vilivyopo bungeni havionyeshi kama fedha zilitengwa kwa ajili ya miradi hii wakati nakala ya vile vya wizara vinaonyesha fedha zimetengwa. Kwa kawaida, vitaby vya bajeti vinavyobaki kwenye nmaktaba ya Bunge ni vile ambavyo vimefanyiwa marekebisho yote. sasa hapa sakata linageuka kwa sababu upo uwezekano mkubwa kuna forgery imefanyika kuonyesha kuwa fedha zilitengwa wakati hazikutengwa
 


Sawa IT SPECIALIST! MWENYEWE UNAONA UNATOA POINT KWELI. Na wewe unaleta hoja za hovyo hovyo
 
Azimio la Zanzibar lipo kisheria na linadunda kama kawa hivyo fikra zetu ktk kutafuta haki ni lazima zianze na Azimio hilo na sio kurukia kulaumu kiongozi ambaye anamiliki shirika kisheria..
Nakuunga mkono Mkandara,

Siku za nyuma niliwahi kusema hili, kuwa kiini cha tatizo ni kuja kwa azimio la Zanzibar, ambalo hata Mwalimu wakati fulani aliwahi kulizungumzia.

Tatizo ni kuwa wengi wetu hatupendi kufanya homework zetu ki sawasawa, na hii pengine ni kutokana na mfumo wetu wa elimu kwa sasa, ambao kwa namna fulani unatuwezesha kufaulu mitihani tu bila ya kuelimika kwa kiwango sawa na kufaulu huko.
 

My SHY, please changia issue iliyopo, kwamba majibu ya waziri ni hovyo hovyo or not, sio kumzungumzia Zitto na mambo ya kwenu huko.
 
Wengi wataitwa majina ya ajabu kama tusipobadilika: Wa kuogopa sio rais bali wananchi eti !!!!

Wakubwa wetu kuitwa jina la jamaa yule anayebweka hivi ni ajali au ndio majaliwa na hatima ya uongozi wa nchi ulioshindwa kuwaridhisha wananchi.

Hivi bado tunafunga macho katika dunia ya televisheni na intaneti ambayo inamuonesha mvulana na msichana wa Tanzania leo jinsi ambavyo viongozi wengine walivyofanya na wanavyofanya kazi kiasi ambacho nchi zao na miji yao ni pepe katika dunia ? Kisha anajikuta katika 'jehenamu ya Tanzania' kwanini asikerwe kwanini hatimaye kilichofichwa moyoni kwa sababu ya utamaduni wa kizamani na uliopita na wakati wa kuheshimu hata wezi, mafisadi, wahuni, wanaodhulumu wananchi, wababaishaji, wasiochangia chochote katika kubadili maisha ya aliyehai leo na atakayekuwa hai kesho ???

Hili halitofautiani sana na mawasiliano kuhusu gonjwa la HIV/Aids ambalo linatokana na kitu kinachofanyika kila siku kwa njia halali au haramu. Kabla ya jana tulikuwa waoga hata kuligusia wakubwa kwa wakubwa, kununua kondomu dukani ilikuwa kazi, kumwambia kijana kwamba ana zama muhimu katika maisha yake hapo baadaye na zinaweza kumjenga au kumbomoa kutokana na atakavyozitumia ilikuwa shida, lakini leo mbona kwa wengine limekuwa jambo la kawaida la kimaisha na vijana wengi wananusurika kwa hilo !!!

ANCHOTUAMBIA MHESHIMIWA SAAAANA BW. ZITTO NI KUWA SERIKALI YETU INAUGUA UKIMWI -(ukosefu wa kutenda, imani (huruma), menejimenti (bora) na (kutimiza) wajibu ipasavyo!)...na wanaoharibu kazi na kuvunja imani kwa serikali hawajibishwi na wanalelewa na kudekezwa vibaya zaidi na chama fulani na watawalal wetu. Wende hawa wakaulize yaliyowasibu vyama vingine vilivyotamalaki miaka 30, 40, 50 au zaidi nini kiliwafika wananchi walipofunguka macho na kusema: 'kumbe hawa wazembe, wezi, wababaishaji wakubwa !'

Miaka ya kuogopa asiyekuogopa imekwisha. Kama waziri hatuogopi ila anamuogopa tu mkubwa wake wa kazi na katugeuza sisi watwana wake siku inakuja tutampasha ipasavyo! Kuanzia, sisi hatuna sababu ya kumuogopa anayejifanya bwana mkubwa na baa wetu, ila tuna kila sababu ya kumuogopa anayejifanya na kuonekana kweli ni mtumwa na mtumishi wetu. Miaka imebadilika someni kwenye ukuta mtaziona ishara wajemeni!

Papaa Mawani upo ? Wamegee watu vipande vyao. Maana tatizo la nchi hii sio kwamba hatuna watu wanaoweza kuendesha nchi vizuri na kwa mafanikio makubwa bali wanaopewa nafasi hizo wengi wao ni makapi na karunguyeye wa kwamfugambwa au sio. Tukiwa siriazi hata kama ni lazima kutupa mbali uchama na unafiki na ukabila wake hivi kweli tutashindwa kuwa na watu wanaoweza kuigeuza Tanzania ndani ya miaka mitatu tu. Lakini, huweji juwa bado labda hatima ya watawala ndio imeandikwa ipitie njia hii au sio ?

Heshima, utukufu, ukubwa jamani utatoka wapi kama hamuwajibiki kuyafanya yale tuliyowatuma ????

Na hatukuunda vyama, serikali, bunge au mahakama au vyombo vya habari ili vilindane katika uzembe, wizi, ufisadi na ubabaishaji wao katika kazi bali viwajibishane katika hayo ili tuwaridhishe wananchi na tupate haki na ridhaa yao ya kweli kuwaongoza kihalali na kiungwana.
 
Jamii haijengwi kwa maneno kama ya zitto na wale wote wanaosupport ushambenga wake , haijengwi kwa maneno matupu na majina vivuli ya watu wenye ajenda za siri kwa nchi hii
Gooooosh shy are you high??????????????????
 

kuna wakati nikikumbuka nia ya huyu mbunge kijana kuacha kugombea ubunge huwa najiuliza tumpate wapi kama huyu tena?
kama walivyowahi kujiuliza farao na viongozi wa serikali yao baada ya kusikia hekima za yusuph ingawa hakuwa mmisri mwenzao.
 
SHY is sick; proved from the word here; anaumwa yule muacheni; ndio maana hata darasa la wachovu; bado kuna wa kwanza na wa mwisho; VERY LOW
 
Last edited:
I see Tanzania moving into darkness. By now it is 60% dark and only 20% is brighter, 10% bright and 10% fading.

60% Dark: The government as leading pillar of the nation is corrupt. Every six of anything that the government is doing is corrupt and it doesn't want its poor people know.

20% Brighter: The remaining portion of the things that we see every government in the world is doing, Tanzania inclusive. Things like; formal meetings (bunge, mahakama etc), formal leaders' trips (outside and inside the country), Formal ceremonies (public holidays, mwenge etc).

10% Bright: Politics of puppeting its people and influencing other countries politically (politics of South Africa for instance is 'just' copy & paste from that of Tanzania).

10% Fading: Love and unit that our forefathers had left us. Now, Zitto is quoting that out of 10 Tanzanians, only 2 are trusting each other, no matter being a wife and husband.10% Fading:

Where is the country heading, God!
 


Asante sana Rufiji. Mungu akubaki sana kwa kuleta ukweli juu ya hili kampuni lake la Solomon Stockbrokers Ltd. Sasa najiuliza, je ali-declare conflict of interest mbele ya umma wakati Wizara anayoiongiza ndiyo ina dhamana ya kusimamia shares zote za serikali kupitia wakala anayehusika CMSA?? Noamba turejee prospectus zote za uuzaji wa shares za NMB na CRDB je Solomon hawakuwa among selected brokers??? Appendix 1 - List of selling agents wa CRDB shares wako 8 na Solomon Stock Brokers Ltd ni wa kwanza. Katika NMB Selling agents wako 8 pia na Solomon Stockbrokers Ltd ni ya 8. Sasa je hii ni serikali gani?. Huyu Jeremiaha Sumary ni owner kabisa wa hii kampuni i.e majority shareholder na kwa kuwa ni yake. Inakuwaje inashiriki dili la kuuza hisa, au kuna mwenye evidence hapa kama alishauza share zake kabisa na kuwa si kampuni yake?? Kwanza waandishi wa habari hebu tumlipue huyu jamaa. Tunataka tumsome vizuri. Asituletee mambo mbofu mbofu na hovyo hovyo hapa.
 

Hivi tuna stipulation za ku declare hizi conflicts of interest? Nilishawahi kuuliza kama tunayo equivalent ya "Securities and Exchange Commission" ya US?

Hii ingetuletea miongozo na policing ya mambo mengi, kuanzia DECI like Ponzi schemes mpaka declaration of conflicts of interest.

Hatuwezi hata kuipa kazi hii au kuunda idara moja hapo Wizara ya Fedha? Kadiri ya uchumi wetu unavyoingia katika ma sophistication ya stock markets and what not ndivyo tunavyohitaji chombo kama hiki zaidi na zaidi.

http://www.sec.gov/
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…