Elections 2015 Zitto: Sitagombea Urais wala Ubunge 2015

Elections 2015 Zitto: Sitagombea Urais wala Ubunge 2015

Hitimisho lako ni zito sana, una ushahidi wowote kwamba hivi ndivyo alivyo, au ndio mtindo huohuo wa hisia kuzibadilisha kuwa kweli? Wazungu wanasema: 'we suspect in others what we feel in ourselves'. Yaani wakati mwingine binadamu huwa tunawaza kitu fulani akilini mwetu na kujiona sisi tulivyo na kudhani na kujiaminisha kwamba hivi ndivyo walivyo watu wengine. Angalia ndugu yangu usije ukawa hivyo ulivyo ukadhani na wengine ndivyo walivyo!!
Dr Mkumbo, Mayu hili ndilo janga hasa la vijana wetu, mna kazi sana nyie walimu, nadhani kwenye mtaala wetu msisitize watu kusoma walau Philosophy, hata kama sio matawi yote, walau logic, general psychology, ethics na epistemology, hata CL ikiangaliwa vizuri. Ukiangalia sasa watu hawajadili masuala ya msingi, wanajadili watu, yaani umbeya. Ukifuatilia majadiliano hususani watu wanaotoka chama fulani ambao kwangu nadhani ndio wanapaswa kuwa kielelezo bora ndio wamekuwa wachafuaji wa hadhi na heshima za watu, eti kwa kuwa anasupport chama kilichokinyume na wewe. Kama ni utani wa kisiasa sawa, wenye chombo waanzishe sehemu ya watani, tujue kwamba ni utani tucheke na tuendelee na kazi. Lakini kama ni kuongelea watu hii ni hatari sana, kuliko hata wauza unga.
 
CDM watakuja kujua umuhimu wa Zitto baadaye. Zitto ni jembe sana ndani ya CDM Hana siasa za maji taka Kama akina Lissu, Lema na Sugu. Hakuna asiyejua mchango wa Zitto kwa CDM. Hawa vijana akina Lema hawajengi CDM Bali wamekidhoofisha sana chama kwa siasa zao za maji taka. Pumzika kaka pumzika Zitto.

Shelui lakini huyu Lema unayedai kwamba haijengi Chadema si ndiye huyu anayewahenyesha ccm Arusha hadi amewazidi nguvu? Matokeo ya uchaguzi wa udiwani ambapo ccm mliangukia pua si ilikuwa ni matokeo ya kazi nzuri ya kuijenga Chadema inayofanywa na Lema, sasa wewe unawezaje kuthubutu kudanganya watu kuwa anaidhoofisha Chadema? Bila shaka umeshindwa tu kukiri kwamba LEMA ndiye kiboko yenu pamoja na kutumia nguvu nyingi za ccm, serikali kupitia kwa mkuu wa mkoa pamoja na jeshi la polisi lakini kamanda Lema amaewaelemea sana.
 
Ni ngumu kupata jipya katika siasa na utawala/uongozi wa nchi yetu kwa mazingira kama haya. Mlikuwa mnapiga vitu vya siasa vizuri hata matumaini yakaturudi,ni nani aliyeleta ulozi?
 
Ni kweli zitto ni mtu makini sana kwa siasa za ndani lakini napata maswali mengi ni nini kinamfanya asiendelee na siasa na kutaka kufundisha vyuo vikuu,mimi naamini huwenda amekatishwa tamaa na mambo furani furani,mimi namshauri akaze buti
 
Sasa kama CDM wameshamvuruga afanyeje?

si yeye kajivuruga....?si mara kibao humu tulikuwa tukiwaambia kuwa dogo ni psychopathic.

Si alisema ana mwito na uzalendo sana, CDM wameuondoa, si alisema anazo sifa zote za kuwa Amir Jeshi mkuu wa hii nchi?Si alisema ataua hadi panya watu wakiingia ktk njia zake......


Tunasubiri next funny move.....sijui km ya Makamba ?
 
Kama hii habari ni ya kweli...na nasisitiza neno "kama", basi Zitto Kabwe ni aidha kigeugeu au asiejua anacho kitaka. Kwenye 2008 alitamkaga kauli kama hii hii ya kusema asinge gombea ubunge 2010 na kwamba angetaka kuwa lecturer. Matokeo yake akagombea. Mwaka wa jana kwenye kipindi cha Makutano show cha Fina Mango akatangaza na sauti yake ikasikika akisema kwamba anataka kuja kuwa raisi wa nchi baadae kwani uwezo anao. Sasa leo hii anarudia yale ya 2008 na kumbuka 2008 ilikua miaka miwili kabla ya uchaguzi mkuu kama ilivyo sasa.

Kama ni kweli Zitto it's time to put up or shut up.
 
Poleni sana..Drama za hilo jembe lenu hazijaaisha....hana umuhimu wowote zaidi ya kujitafutia umuhimu wa kuibukia.Jembe gani sasa km amekulia ktk chama hadi sasa hajajua anafit wapi?Watz wenye hata PHD na first classes kibao ni watu wa hovyo sana.Sijui Zitto hadi sasa ana nini cha tofauti na loosers za CCM.

Soon utasikia anacheza dili za kijinga km za makamba mwenzie ktk "un holy trinity Makamba, Zitto, Jussa".Watoto wa Uswazi ni wepesi sana kupanda na kuanguka ghafla.

Hakuna mtu asiye na mchango anaweza kukubalika sehemu, na mara nyingine ni chama kukutumia kwa kutuma ktk mambo mengi kutegemea na mazingira na hii ni sehemu ya majukumu ya kazi.


Sijui nani atafundishwa na Zitto ....zaidi ya material things biasness yake ktk vitu vyenye different school of thought.Wanafunzi wataishia kuwa km wa Haroub Othman.

'Nicolas kwa nini Zito tu awe biased na si wewe? Nadhani jichunguze nawe. Nadhani tatizo kubwa kwetu ni kuwaona wenzetu ni tatizo pasipokujiangalia kwa kina endapo nasi hatuko sehemu ya hilo tatizo.
 
CDM watakuja kujua umuhimu wa Zitto baadaye. Zitto ni jembe sana ndani ya CDM Hana siasa za maji taka Kama akina Lissu, Lema na Sugu. Hakuna asiyejua mchango wa Zitto kwa CDM. Hawa vijana akina Lema hawajengi CDM Bali wamekidhoofisha sana chama kwa siasa zao za maji taka. Pumzika kaka pumzika Zitto

U r right shelui, huyu jamaa amefanya mengi sana nchi hii kupitia ubunge wake na wananchi wengi tumeliona hilo bila ya kujali itikadi zetu za siasa, wabunge wengine wa chadema ukiacha halima mdee wamekuwa watu kama wa vijiweni kwani kutwa kulalamika na kukashifu bila ya kutoa mawazo chanya yenye kusaidia nchi, najiuliza mbowe, lissu, na lema hadi leo to be honest sijawahi kusikia mchango wao kama wabunge wenye kusaidi nchi hii ukiacha na makelele yao kila siku, wabadilike tumechoka, huo siyo upinzani ni utoto
 
ukweli gan mkuu, ukweli huonekana hausemwi, uwongo husemwa. Huna sababu ya kutumia nguvu nyingi kutuambia tuone aliyoyafanya Zitto. Kama yapo tutamhukumu kwayo..

Mimi ni muumini wa performaance ya kiongozi wa chama ndani ya chama. Zitto hajafanya lolote kwaa kipindi kirefu kuijenga chadema zaidi amekuwa mtu anaeleta tension na niseme amegundua weakness iliyopo chadema na anaitumia hiyo kuwanyanyasa.

Mfano chadema inapigwa propaganda ya Udini kuwa ni chama cha wakristo. Zitto ni muislam (anitumia hii turufu kuwaacha chadema kwenye mkesha zitto akiondoka itachafua political climate).. Chadema inapigwa propaganda ya ukabila na ukanda (Zitto analijua hili coz yeye ni wa kigoma na muha, anawalaza chadema usiku kucha milango wazi kuombea asiharibu political climate). Chadema inapigwa propaganda ya viongozi wake kukimbia shule..yeye ana shule hivyo kumdeny nayo inawasumbua chadema.

Zitto awepo ndani ya chadema, aondoke ndani ya chadema bado sufferings za chadema zitaremain constant. Ndio maana nasema Zitto ashajiona ni zaidi ya taasisi, anapenda hata jambo alilolifanya chadema lisisemwe chadema wameamua hivi, anataka lisemwe Zitto kaamua hivi. Ni mjinga.


Hakuna kitu kama hicho,
Chuki zenu binafsi
 
Nadhani hamna cha kuongea piteni lumumba kamateni chenu mrudi kwenu mkalale tu.nonses
 
CDM watakuja kujua umuhimu wa Zitto baadaye. Zitto ni jembe sana ndani ya CDM Hana siasa za maji taka Kama akina Lissu, Lema na Sugu. Hakuna asiyejua mchango wa Zitto kwa CDM. Hawa vijana akina Lema hawajengi CDM Bali wamekidhoofisha sana chama kwa siasa zao za maji taka. Pumzika kaka pumzika Zitto
Kuwa busy na chama chako kinachoelekea kufa mkuu...mambo ya Zitto mbona ni madogo sana ukifananisha na fujo zilizopo hapo kijani?
 
Poleni sana..Drama za hilo jembe lenu hazijaaisha....hana umuhimu wowote zaidi ya kujitafutia umuhimu wa kuibukia.Jembe gani sasa km amekulia ktk chama hadi sasa hajajua anafit wapi?Watz wenye hata PHD na first classes kibao ni watu wa hovyo sana.Sijui Zitto hadi sasa ana nini cha tofauti na loosers za CCM.



Soon utasikia anacheza dili za kijinga km za makamba mwenzie ktk "un holy trinity Makamba, Zitto, Jussa".Watoto wa Uswazi ni wepesi sana kupanda na kuanguka ghafla.

Hakuna mtu asiye na mchango anaweza kukubalika sehemu, na mara nyingine ni chama kukutumia kwa kutuma ktk mambo mengi kutegemea na mazingira na hii ni sehemu ya majukumu ya kazi.


Sijui nani atafundishwa na Zitto ....zaidi ya material things biasness yake ktk vitu vyenye different school of thought.Wanafunzi wataishia kuwa km wa Haroub Othman.

Mwanasiasa mzuri siku zote anatakiwa kuwa na malengo ya mbali na kuyatekeleza

Hii tabia ya kuwa opportunist ni mbaya sana na ndicho kinachowagharimu Zitto,Jussa na January Makamba

Wapo tayari kwa lolote ilimradi wanapata umaarufu

zito angetulia vizuri na chadema angefika mbali.akina Tundu Lissu wameibuka na kasi yao ya kujenga chama inatisha.January ni mnafiki ila yuko makini hata siku moja hawezi kukihujumu chama chake na ndiyo maana hata ile petition ya bungeni kumng'oa waziri mkuu hakusaini.

hapa anafuatilia weeee halafu kesho utamsikia anatoa press statement
 
Ninawasikitikia sana vijana wenzangu wa nchi hii, kwakweli ni aina ya vijana ambao hawaamini kuwa hawaamini wanachokiamini,

Mtu yeyote anaweza kuwageuza akili zao vyovyote apendavyo,

Namshukuru sana kamanda mwenzangu Ben Saanane kwa kusimamia nakuiishi imani yake bila kutetereka,

Niliwahi kuandika na ninatembea nakuishi katika imani hii kuwa Zitto Kabwe Naibu Katibu wangu wa Chadema ni "Mnafiki" namba moja kati ya wanafiki wote nchini wanaoishi kwa siasa!

Haya hapa chini yataishi na kutembea kichwani na moyoni mwangu daima!

Binafsi naitafakari kauli ya Zitto Zuberi Kabwe na ninafurahi kuona kuwa kile nilichoonya kuwa kijana mwenzangu anatumiwa vibaya na ccm sasa kimetimia.
Wakati akihojiwa katika kipindi kiitwacho, Exclusive interview na Millard Ayo cha Clouds FM
Amesema hivi nanukuu “Wazee wetu walitusaidia kutupatia maendeleo ya kisiasa, sasa ni jukumu letu kuleta maendeleo ya kiuchumi. Ila naomba nisisitize, jukumu hili haliwezi kutekelezwa na mtu yeyote aliyezaliwa kabla ya uhuru, na ninatangaza kuwa nitagombea urais mwaka 2015?

Naunga mkono kwamba vijana tujitokeze kuleta maendeleo kwa taifa letu, lakini napingana vikali kauli “jukumu hili haliwezi kutekelezwa na mtu yeyote aliyezaliwa kabla ya uhuru”


Kwanza mimi nasema amewatukana wazee wote Tanzania, huku ni kukosa busara heshima na hana sifa ya Uongozi kwani ni mbaguzi. Wapo Wazee waliozaliwa kabla ya uhuru na wanailetea Tanzania maendeleo na wapo wapuuzi waliozaliwa baada ya uhuru ni wapuuzi wa kutisha yeye akiwemo. Zitto hana busara kwa hili


Amejisemea bila kufikiri. Ana maanisha hata kama mtu ni msomi kama akina Dr Slaa, Dr Gharibu Bilali mtaalamu wa nyuklia na Prof Lipumba hawawezi kusaidia isipokuwa wale waliozaliwa baada ya uhuru? Huu ni uhuni wa kawaida wa Zitto ambaye hujitahidi kujionyesha kama thinker wakati siyo hasa ikizingatiwa hata akiwa shule alipita hivyo hivyo.

Nadhani kwa thinker mzuri hana haja ya kuwatenga watu kwa umri wao bali tabia zao hasa linapokuja suala zima la ujenzi wa taifa. Mbona tuna vijana waliozaliwa baada ya uhuru kama yeye mwenyewe Zitto na wengine lakini bado ni mafisadi???

Kitendo cha kutangaza nia ya kugombea urais 2015 sio kibaya kwakuwa ni haki yake kikatiba, lakini kutangaza nje ya ya utaratibu wa chama chake huu ni uhaini kwa chama. Zitto anajua anachokifanya, na anajua matokeo yake lakini ni jambo la kusikitisha kuwa hajui madhara yake kwake.


Katika tafakuri yangu kwa mapana ya nera, nikamkumbuka mwalimu wangu pale Moscow Urusi, Prof Radav Metbarg aliyenifundisha uhandis wa umeme, huyu alinidokeza aina ya binadamu, hakika ilikuwa muhimu sana ndio maana leo imenijia akilini nikalazimika kuzama kimang’amuzi zaidi, nimefanya hivyo ili nimtambue huyu mtu aitwae Zitto Kabwe kiundani zaidi, Katika aina za binadamu Zitto ni wa aina ya Sanguine, hii ni kwamujibu wa tabia zake za kisiasa. Hakika naamini watu wa aina hii ni hatari hasa ukiwasogeza jirani na uongozi popote pale basi wanaouwezo na msukumo mkubwa wa kukupindua. Hiyo ni sehemu ya sifa ya watu wa aina hiyo na kwa ujumla ni waroho wa madaraka.


Lakini najiuliza kwani Magharibi mwa Tanzani ndiko aina hii ya watu inapatikana kweli au yeye ni chipuzi tu? Nikiangalia wenye tabia zake nawaona kama Kafulia, Mkosamali na Shibuda. Lakini sitaki kujikita katika dhana hiyo ya ukanda bali nasimamia kuwa hao ni chipuzi la aina hiyo ya tabia za binadamu ambao ni hatari hasa uwasogezapo katika vyeo vya juu basi huutaka ufalme hata kwa njia ya uasi tu. Muono wangu ni kuwa Zitto hautaki urais na anajua fika kuwa kwa mujibu wa katiba iliyopo yeye hastahili kugombea URAIS, ila kwa gharama kubwa amejichimbia msituni kukihujumu chama chake kilichomlea na kumfanya leo ajione fahali la masika.


Ninarudia tena Zitto hana nia ya urais, nasema hana hata chembe za kuutaka urais ila analengo moja tu nalo nikukivuruga Chama chake tu. Mwili wa Zitto upo Chadema ila moyo wake upo ccm palipo panono, kweli pesa mwanaharamu.


Lakini wadadisi wa siasa za Afrika tunapaswa kulaumiwa sana, tulipopokea mageuzi ya siasa za kidemokrasia na kuziacha siasa zetu za kiimla lakini tulishindwa kupokea hata miundo ya siasa hizo, mathalani vyama vya siasa vyenye ukwasi wa kidemokrasia huwa na utaratibu wa kutengeneza viongozi wa chama, kitaifa na viongozi wa kimataifa. Hili nadhani hata Hayati Mzee Nyerere alifanikiwa kuliasisi lakini baada ya kufariki mabaka demokrasia wamebaka na kubuni mifumo ya kuzalisha watawala sio kuzalisha viongozi tena.


Hili lisiwe turufu kwa Zitto, naamini anatambua njia aipitayo na madhaifu ya muundo huu wa vyama vyetu vya siasa. Ningefurahi na ninaamini wadadisi wote wa siasa za Afrika wangefurahi pia kama Zitto angeanzisha harakati za kuboresha muundo wa vyama vyetu vya siasa hususani Chama chake cha Chadema kilichobeba tumaini kuu la wazalendo na wengi wa nchi hii. Je ccm ya leo bado inautaratibu wa kuandaa vijana kwaajili ya siasa za kesho? kwaajili ya urais? kwaajili ya wanadiplomasia wa kimataifa wakesho? Chadema je? UDP je? NCCR je?


Jambo la kumshukuru Mungu nikuwa Chadema wanajua kila anachokifikiria kufanya, anachokifanya, anakolalia, anakoamkia, anakokutania na wafadhiri wa uasi huu na kila kitu. Kwaujumla chama kinamjua utosi hadi unyayo.

Chadema wamekuwa wakipigana vita mbili kwa mda mrefu, vita hiyo ni ya nje (ccm) na ndani (Zitto, Shibuda na mamluki wengine) lakini mda wote chadema imeshinda na itashinda na itaendelea kushinda daima kwakuwa ni vita kati ya wema na ubaya kumbuka na elewa kuwa kwenye wema Mungu yupo.

Ninachoamini katika siasa duniani ni kuwa hakuna aliyejuu ya chama chake.
 
Zito anaona mbali, mawaziri hawatakuwa wabunge, so anajipanga.
Indirectly anamsapoti kijana mwenzie ili akiingia tu, naye anashika wizara.
 
si yeye kajivuruga....?si mara kibao humu tulikuwa tukiwaambia kuwa dogo ni psychopathic.

Si alisema ana mwito na uzalendo sana, CDM wameuondoa, si alisema anazo sifa zote za kuwa Amir Jeshi mkuu wa hii nchi?Si alisema ataua hadi panya watu wakiingia ktk njia zake......


Tunasubiri next funny move.....sijui km ya Makamba ?
hata kuwa mwalimu pia ni mwito wa uzalendo.

Kusema hagombei leo haina maana kuwa hatagombea miaka ijayo.
 
Ninawasikitikia sana vijana wenzangu wa nchi hii, kwakweli ni aina ya vijana ambao hawaamini kuwa hawaamini wanachokiamini,

Mtu yeyote anaweza kuwageuza akili zao vyovyote apendavyo,

Namshukuru sana kamanda mwenzangu Ben Saanane kwa kusimamia nakuiishi imani yake bila kutetereka,

Niliwahi kuandika na ninatembea nakuishi katika imani hii kuwa Zitto Kabwe Naibu Katibu wangu wa Chadema ni "Mnafiki" namba moja kati ya wanafiki wote nchini wanaoishi kwa siasa!

Haya hapa chini yataishi na kutembea kichwani na moyoni mwangu daima!

Unaweza kumfananishe na nani? Babu?
 
Mbona hizo sifa walizo zitaja hapo huyu dr. Wa injili slaa hana. Sasa hao cdm watamweka nani?
 
Back
Top Bottom