Elections 2015 Zitto: Sitagombea Urais wala Ubunge 2015

Elections 2015 Zitto: Sitagombea Urais wala Ubunge 2015

January Makamba? Kweli elimu imeshuka. Walifadhiliwa na nani hao wanachuo?
 
Hakuna kitu kama hicho,
Chuki zenu binafsi

Honest speaking Zitto hana tofauti na Samwel Sitta, wote ni watendaji wazuri sanaa lakini madumila kuwili na wapenda sifa binafsii.. Sina chuki na Zito wala Sitta na nawakubali sanaa wao kama wao ila as part of team hawa ni majangaa... Hapo ndio kwenye challange CDM inamtumiaje Zitto, chonde viongozi wa chadema hebu kaeni na huyu kijana muone mnaweza kumsaidi vipi ili atimize ndotto zake, kwa fikra zangu ndani ya CDM zitoo anazidi kufunikwa na vijana kama kina Lisuu, Mnyika, Lemaa na 2015 si ajabu akafunikwa moja kwa mojaa.. Siasa ni kazi na Zito ni mmoja kati wanasiasa vijana waliofanikiwa kupitia chadema ila hilo halitoshi kwake (job satisfaction) kuna kikubwa zaidi anakihitaji toka kwa viongozi wenzake (sifa, kutambuliwa kama ana mchango mkubwa ndani ya CDM),, hali tunayoiona sasa hivi ni kama kapuuzwa na hakuna tena kiongozi anayemshobokea... Mbowe na Dr Slaa lazima mkumbuke na jukumu kubwa na kuendelea kuwalea vijana wenu na kuwarudisha kwenye mstari ikiwa ni pamoja na kuwapa majukumu (madaraka) na sio vyeo visivyokuwa na madaraka. Kwa mtizamo wangu na hata ukiangalia Maslow's pyramid Zito anaipenda CDM ila amechoka na hana shida ya hela au mali anachokitaka ni kutambuliwa, kuthaminiwa na kupewa madaraka..
Zito kumbuka una nafasi kubwa zaidi ya kukua ndani ya chadema na kufikia kilele cha mafanikio kama utaweza kujirekebisha na ukafanya kazi kama team na hata pale unapokuwa na tofauti na viongozi wenzako ni busara kusubiri vikao na mkalijadili humo kuliko kutoka na mismamo binafsi kama ya mwenzako sitta na kuwafanya wengine kwenye chama waonekane hawajui nini wanachofanya...
 
Nashangaa sana mwanasiasa kama Zitto kuingiliwa kwenye email, maana kwa bongo obviously atakua amefanyiwa Phishing tu, kama sio hivo siamini kamamkuna mtu atakua amemtumia trojan ili kupata logs zake since kumpata isingekua kirahisi unless jamaa kapitia email ya chadema ambayo iko public, still google wangeiscan na kuitoa sasa which comes to the fact kua hawa wanasiasa nahisi wanahitaji elimu ya jinsi ya kujilinda against online threats maana mambo kama haya yanavoenda kijingajinga hivi ni kupigizanakwlele na kuchafuana tu, kwa hizo info hapo juu inaonekana wazi kabisa kua ni iutoka kwenye email ya Jamaa, but still siwezi comment alichifanya alikua anafikiria nini maana kuna wakati mtu unafanya kitu ukiwa unajua unafanya nini ili mwishowe upate matokeo ambayo ni mazuri japo hukupitia direct way... Personal privacy ipewe heahima yake jamani
 
Mtu complex hawezi toa maelezo mepesi kiasi hiki,kwan mbunge hawezi kufundisha???!!!!
Si anakaa Dar jimbo lipo Kigoma sasa atashindwa kuishi Mwanza kwenye vyuo na aendelee huko kanda ya ziwa???!!

If this is true ,he should come out clean!!!!!

Kwa uwezo wake na matumaini ya baadhi ya watu juu yake ni sawa na dereva kugomea safari katikati ya msitu!!!!

Aseme safari ngumu.??????
Gari bovu????!
Uwezo wa kuendesha umeshuka??!!!
Konda na tanboi hawampi ushirikiano safarini???!!!!
Nia ilikuwa sio kufika???!!!
Alitaka tu kuonekana akilitoa basi kituoni????!!!!!
Alitaka kuendesha magari katika kampuni ya kimataifa ila ilikiwa ni lazima aendeshe basi kwanza???

Ukiwa mwanasiasa Tanzania ni lazima kufanya kazi hiyo hadi ugombee/uwe Uraisi/Raisi?

Ukiwa mwanasiasa Tanzania ni lazima kufanya kazi hiyo hadi siku Mungu atakapochukua Roho yako?
 
Kwa mimi naonavyo Zitto anakurupuka kufanya maamuzi kama hayo lakn itafika mahali atakanusha na kuipinga kauli yake. CDM wala haiwezi tetereka kisa zitto kaamua kujipumzisha na siasa. Daima CDM IKO IMARA KWANI INA VIJANA WAZURI KAMA MNYIKA LEMA MAWAZO BASIL LEMA LISSU MDEE MSIGWA SUGU WENJE KIWIA HAO KWA UCHACHE TU. Kuna vijana mamilioni ndani na nje ya nchi wanauwezo wakukijenga chama na kukiendeleza hata kwenye kushika hatam ya uongozi wa nchi hii. Kama kaamua kwa moyo mwacheni akapumzike.
 
CDM watakuja kujua umuhimu wa Zitto baadaye. Zitto ni jembe sana ndani ya CDM Hana siasa za maji taka Kama akina Lissu, Lema na Sugu. Hakuna asiyejua mchango wa Zitto kwa CDM. Hawa vijana akina Lema hawajengi CDM Bali wamekidhoofisha sana chama kwa siasa zao za maji taka. Pumzika kaka pumzika Zitto

Mkuu shelui salama?
 
Honest speaking Zitto hana tofauti na Samwel Sitta, wote ni watendaji wazuri sanaa lakini madumila kuwili na wapenda sifa binafsii.. Sina chuki na Zito wala Sitta na nawakubali sanaa wao kama wao ila as part of team hawa ni majangaa... Hapo ndio kwenye challange CDM inamtumiaje Zitto, chonde viongozi wa chadema hebu kaeni na huyu kijana muone mnaweza kumsaidi vipi ili atimize ndotto zake, kwa fikra zangu ndani ya CDM zitoo anazidi kufunikwa na vijana kama kina Lisuu, Mnyika, Lemaa na 2015 si ajabu akafunikwa moja kwa mojaa.. Siasa ni kazi na Zito ni mmoja kati wanasiasa vijana waliofanikiwa kupitia chadema ila hilo halitoshi kwake (job satisfaction) kuna kikubwa zaidi anakihitaji toka kwa viongozi wenzake (sifa, kutambuliwa kama ana mchango mkubwa ndani ya CDM),, hali tunayoiona sasa hivi ni kama kapuuzwa na hakuna tena kiongozi anayemshobokea... Mbowe na Dr Slaa lazima mkumbuke na jukumu kubwa na kuendelea kuwalea vijana wenu na kuwarudisha kwenye mstari ikiwa ni pamoja na kuwapa majukumu (madaraka) na sio vyeo visivyokuwa na madaraka. Kwa mtizamo wangu na hata ukiangalia Maslow's pyramid Zito anaipenda CDM ila amechoka na hana shida ya hela au mali anachokitaka ni kutambuliwa, kuthaminiwa na kupewa madaraka..
Zito kumbuka una nafasi kubwa zaidi ya kukua ndani ya chadema na kufikia kilele cha mafanikio kama utaweza kujirekebisha na ukafanya kazi kama team na hata pale unapokuwa na tofauti na viongozi wenzako ni busara kusubiri vikao na mkalijadili humo kuliko kutoka na mismamo binafsi kama ya mwenzako sitta na kuwafanya wengine kwenye chama waonekane hawajui nini wanachofanya...
Well said mkuu, Zitto ana kitu kinachomsumbua 'distinction' ambacho kwa kila mtu makini hukihitaji, ila ninavyomuona hadi sasa bado hajaamua ni kipi kati ya siasa na taaluma kitakachomfikisha huko, namshauri awe makini wakati wa kuchagua njia sahihi asipokuwa makini mwisho anaweza kufikiri njia yeyote inaweza kumfikisha, which is very wrong.
 
Tambueni CDM SIO ZITTO MBOWE DR SLAA WALA MNYIKA. Hao tumewapa uongozi tu ndani ya chama hvyo akiondoka hata mmoja CDM ITAENDELEA KUWEPO TENA IMARA KAMA SASA.
 
Hongera Zitto kwa kuwaonyesha CCM siasa za kisasa. Muda bado upo kwa umri wako kurudi kulitumikia taifa. Hatutaki design za akina Malecela, Kingunge, Lowasa na wengine wengi tu CCM kufikiri wao ni wabunge maisha yao yote (Mugabe style). No wonder wengine wameaibishwa na vijana wadogo kama akina Lusinde.

Kama kweli CCM wanaona kuwa ni Zitto tu peke yake kwa sasa ndiyo anaweza kuwa Rais wa nchi, kwa nini wasikae chini na kuwashauri kutushauri wananchi kuwa na mgombea mmoja tu wa Urais (Zitto) kwa manufaa ya taifa letu??

Akina Ritz, chama, FF na HAMY-D mnajifanya ni furaha ya kaskazini wakati ni furaha ya CCM. Hivi kwa nini hamshangai Zitto kauchunia huu mkanda. Jaribuni kuangalia mtego uko wapi maana Zitto juzi tu aliwaambia kuwa hatakiacha chama alichokijenga!! Hajasema hatagombea nafasi kwenye chama, remember!!??
 
Last edited by a moderator:
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe (CHADEMA), amesema hafikirii kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho wala ubunge katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.

Alisema mwaka 2015, ndio mwaka wa mwisho kujihusisha na siasa ambapo dhamira yake ni kutafuta chuo ambacho ataweza kufundisha masomo ya uchumi na maliasili.

Bw. Kabwe aliyasema hayo hivi karibuni katika mahojiano maalumu na gazeti hili siku chache baada ya viongozi 105 kutoka Vyuo Vikuu 30 nchini, kupendekeza majina ya wanasiasa wanaofaa kuwania urais mwaka 2015.

Jina la Bw. Kabwe, lilishika nafasi ya pili katika mchujo huo ambapo Mbunge wa Bumbuli, mkoani Tanga ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Bw. January Makamba, alishika nafasi ya kwanza kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mwanasiasa aliyeshika nafasi ya tatu katika mchujo huo alikuwa Mbunge wa Ubungo, Dar es Salaam, Bw. John Mnyika (CHADEMA).

"Hiki ni kipindi cha mwisho kwangu kujihusisha na siasa kwani nimechoka nazo, nitatafuta chuo nikafundishe na kama nitakosa ni bora nikalime michikichi... sihitaji urais," alisema.

Katika mkutano wa wanafunzi hao, walisema Bw. Makamba ana sifa zote za kuwa rais wa nchi kamaatagombea nafasi hiyo mwaka 2015 ili aweze kulikomboa Taifa ambalo hivi sasa linakabiliwa na matukio mengi ya uvunjifu wa amani.

Wanafunzi hao walikwenda mbali zaidi na kuyataja baadhi ya matukio hayo kuwa ni pamoja na vurugu, kutekwa kwa watu wasio na hatia, kufanyiwa vitendo vya ukatili, kumwagiwa tindikali na kupungua kwa mtangamano wa kijamii.

Mwenyekiti wa mkutano huo ambao ulifanyika mkoani Morogoro ambaye pia ni Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Kampasi ya Mbeya, Bw. Theonest Theophil, alisema Bw. Makamba alipata kura 72 ambapo Bw. Kabwe alipata kura 20.

Bw. Theophil alisema sifa za kiongozi wanayemtaka kwanza awe kijana mwenye fikra mpya, atakayeleta matumaini mapya, kuwaunganisha Watanzania, asiyeendekeza siasa za kikanda, mdini na mkabila.

Sifa nyingine ni kiongozi mwadilifu asiye na rekodi ya kutuhumiwa mahali popote kwa vitendo viovu, mtulivu, mwenye busara na anayepima kauli zake.


Source: Majira

Naona dogo amejitambua, alikuwa hafai kabisa kwa nafasi ya Urais. Yeye atulie tu ajilie vile alivyochuma kwenye siasa kwa miaka 10. Dogo ni tajiri hasa.
 
Mhhhh: Mkuu, mbona umesha hukumu kabisa hapo?....ngoja tuone ni mapema mno kutoa maneno makali kama hayo....Lazima kutakua na jambo NYETI tu.
Mtu complex hawezi toa maelezo mepesi kiasi hiki,kwan mbunge hawezi kufundisha???!!!!
Si anakaa Dar jimbo lipo Kigoma sasa atashindwa kuishi Mwanza kwenye vyuo na aendelee huko kanda ya ziwa???!!

If this is true ,he should come out clean!!!!!

Kwa uwezo wake na matumaini ya baadhi ya watu juu yake ni sawa na dereva kugomea safari katikati ya msitu!!!!

Aseme safari ngumu.??????
Gari bovu????!
Uwezo wa kuendesha umeshuka??!!!
Konda na tanboi hawampi ushirikiano safarini???!!!!
Nia ilikuwa sio kufika???!!!
Alitaka tu kuonekana akilitoa basi kituoni????!!!!!
Alitaka kuendesha magari katika kampuni ya kimataifa ila ilikiwa ni lazima aendeshe basi kwanza???
 
Kuna wakati Mhe.Zitto Kabwe alisema anautaka urais na kuapa kutogombea ubunge, hii ya kutokuutaka tena urais inatia shaka.Ni vema nivute subira kwenye hili maana lolote laweza kutokea.
 
zito hanalolote anasubli mwaka 2015 aje na sababu wananchi wamemuomba kama 2010 alivyofanya.
 
Mhhhh: Mkuu, mbona umesha hukumu kabisa hapo?....ngoja tuone ni mapema mno kutoa maneno makali kama hayo....Lazima kutakua na jambo NYETI tu.


Sijahukumu mkuu nimesema IF THIS IS TRUE HE SHOULD COME OUT CLEAN!!!Istand to be corrected
 
Nicholas, tatizo la uchambuzi wa matatizo ya psychology ni kwamba hakuna mzima. naweza nikachambua word selection yako katika argumentation zako nyingi hapa nikakuta wewe pia ni mgonjwa. Kwa hiyo tofauti zetu ni degrees--au pengine niseme viwango vya kuumwa. Hilo linazusha haja ya kuvumiliana katika ubinadamu wetu. Lakini pia ukifanya individual cost-benefit analysis ya hatma ya mwisho ya maamuzi ya mtu ndiyo hupunguza hukumu ya tendo lenye sura ya wehu. Hii ndiyo dhana inayotumiwa kuruhusu vita.

bottom line ya uamuzi wa zitto ni nini kwake at individual level? kwanza ataepuka migogoro ya kisiasa ambayo ni mingi. anataka kazi isiyokuwa na migogoro mingi. anataka amani at individual level. kuna wehu gani katika kutafuta a peaceful life? nadhani ni vizuri ukifuta kauli....usimwite zitto psychopath. hii kauli si sahihi.


Chadema sometimes inaleta ukakasi sana na hawa wanaojiita ni makamanda wake,
Hivi na wewe ndan ya chadema hii ni nani hasa??
Kwa maana unaonekana kuwa ni msemaji wa chama huku mara nyingi ukiongea mambo yasiyo na kichwa wala miguu,

Sasa huyo unaemsema,wewe na wenzako watokwa povu mmefanya nin ndan ya chadema cha kutaka kuuaminisha umma wa watanzania kuwa mna say ndan ya chama,,na mko na saut ya kupinga mazur aliyoyafanya Zitto??

Besides mahusiano yake na viongoz wake wa juu yako positive na hakuna mgogoro huo mnaoushapulia nyinyi,vijana kama nyinyi mtambue kuwa mnayo nafas ya kufanikiwa maishan lakini si kwa kutegemea kusafiria nyota na mafanikio ya watu wengine,

The revolution is inside of you,kama una amin ivo sion umuhim wa kuja kumwagika povu hapa
 
Kabisa,
Na kwa kias kikubwa sana CHADEMA kinapitia wakati mgum sana kwa sasa,asilimia kubwa ya vijana sampuli hiyo wamekimbizia matumain kwa CHADEMA moja kwa moja na kuacha kuhangaika kufanya kazi na kutafuta namna ya kujikwamua na utumwa wa fikra,

Wanadhani kama CHADEMA kikiingia madarakani kitakuwa kinawajaza pesa mifukoni,haitafanya hivyo,

Ikiingia Madarakan kwa ridhaa ya wananchi itachofanya ni kusimamia sera zake na kuahid kile kilichokuwa kinasemwa kwa wananchi,

Wao wanadhani kwa kukaa bila kufanya kazi na kushabikia shabikia basi maisha yao yatabadilika once chadema kikichukua inchi,wanashindwa kuelewa maisha ni haya haya,na kila siku watu wanakufa na kuzaliwa,
Tumaini Makene naomba wewe kama msemaji wa chama uchukue jukumu la kuwakemea hawa waganga njaa na wachumia tumbo wanaodhani kukesha kuwalamba lamba miguu viongoz wa juu wa chama basi itawarahishia maisha hapo baadae,

Mfano ni hawa vijana wababishaji na wenye njaa kali kama Yericko & Saa nane,itoke kauli ya uhakika dhidi ya hawa vijana,

Wanajenga taswira mbovu ya chama ili hali hawana influence yyte na by the way hakuna tuh anaewatambua kwa namna yoyote ile,

Wana kua ni taswira ya chama hali ya kuwa wao wana taswira zao binafsi zilizofifia na kukosa matumain,

Waambie wasitegemee kubebewa na taasis,wajenge identity yao,pia waache ufitini na udanganyifu kwa kutumia nembo ya chama,

WANATIA KICHEFU CHEFU
Kiongozi we mbaya yani umepoteza kabisa huyo mlamba miguu ya watu (Benn saanane) huyo mwengine hajielewi wala simshangai (yericko) she is nothing kabisa.hawa vijana kweli ndio chanzo kikubwa cha mimi kuichukia CDM kwasababu inawalea vijana wapenda majungu na kufitinisha, hutumia majina ya watu kupata attention
Benn Saanane hataki kusikia kabisa kijana mwenzake anauwezo zaidi yake,anajihisi he is very smart sababu masters ya INDIA.
Saanane fanya yako acha kua mtumwa wa kufatilia maisha ya watu. free yourself kijana
 
Habari njema kwa Ben maana yeye kila siku anapambana na Zitto ndani ya CDM badala ya kukijenga chama. Naona huyu Ben anatumika sana na Babu kumpaka matope Zitto.

CDM mbaya wenu sio Zitto Bali ni sera zenu za maji taka zisizokuwa na kichwa wala mkono. Cha moto mtakiona came 2015 na hamtaambulia kitu tuombe uzima.

mawazo ya wendawazimu hayana manufaa kwa walio timamu,yeye kasema hafikrii kugombea nafasi yeyote katka siasa mnaanza kupiga ramuli kama mlivyozoea,katiba yenyewe wenda ikamtupa nje,na kama urais anahujumiwa je? ubunge nao nani anamhujumu?kaokoteni mengine mlete haya yalishazoeleka.
 
Ukiwa mwanasiasa Tanzania ni lazima kufanya kazi hiyo hadi ugombee/uwe Uraisi/Raisi?

Ukiwa mwanasiasa Tanzania ni lazima kufanya kazi hiyo hadi siku Mungu atakapochukua Roho yako?


Hivi mtu kama umeelogwa au mnaogopa kuhoji hii political tubulance nchini???!!
Kama aliomba kura za wananchi then lazima wakati wa kuondoka atoe neno la shukurani sio kukurupuka kama mtu anakimbia nyuki na sisi tukubali tu!!!!

Kasome hierarchy of needs then ujue ulipofikia mimi bila ya kujibiwa hayo maswali siku akiamua kuachia siasa ntamuweka kundi ambalo ntalitaja siku hiyo!!!!
 
Ukiwa mwanasiasa Tanzania ni lazima kufanya kazi hiyo hadi ugombee/uwe Uraisi/Raisi?

Ukiwa mwanasiasa Tanzania ni lazima kufanya kazi hiyo hadi siku Mungu atakapochukua Roho yako?


During old school days we used to read a phrase and later on asked to give it a tittle!!! Ever asked your teacher on its significance????!!!
 
Back
Top Bottom