Ziwa Nyasa limeporwa kikamilifu?

Ziwa Nyasa limeporwa kikamilifu?

Mambo ni mdogomdogo mkuu. Kama ramani imebadilishwa kuna siku ya tutapigwa marufuku

Jirani akimega kiwanja chako usipomchukulia hatua kali, atavunga jamii ikishazoea kwamba eneo alilomega ni lake ndipo anakuja kuweka uzio

Nakubaliana na wewe. Sisi cha kufanya ni kusema malawi wanapotosha umma na dunia kwa kuchapisha ramani zinazoonesha uongo.
 
Nadhani hakuna jipya hapo, shughuli za kiuchumi zinaendelea kama kawaida. Meli, uvuvi na ulinzi, nothing to fear, google map kubadili mipaka ni sawa watu wanasema zanzibar ni jamhuri huru wakati huko duniani passport na nyaraka ni tanzania 🇹🇿
 
Wamalawi wanajidanganya
Huwezi kudai maji yaliyopakana na vijiji vya nchi nyingine kuwa wakienda kuchota maji kwenye ziwa hilo basi wako nchi jirani.
Hatuwezi kukubali ujinga huo!

Ila ubaya wa hii kitu, mabeberu wanaweza kuitumia kutublackmail ili tuwape concensions kadha wa kadha la sivyo watambue kuwa ziwa lote ni mali ya Malawi
Kwa ramani ambazo Malawi wanazitumia ziwa Nyasa linaonekana hivyo na wao wanaliita Lake Malawi. Lakini kwa ramani za mitaala ya Tanzania ziwa Nyasa limegawanyika kwa dotted lines. Ukiona dotted lines kwenye ramani maana yake hiyo border iko kwenye dispute.

Hata Malawi kipindi cha Muluzi kurudi nyuma walikuwa wanaweka dotted lines, lakini alipokuja yule Rais Mwanamama wa kwanza wa Malawi, Joyce Banda akaja na ajenda ya kuwa ziwa ni la Malawi pekee kadri ya Heligoland Treaty ya 1870.

Najua maongezi ya umiliki wa ziwa Nyasa yanaendele kati ya nchi zetu 2 chini ya uratibu wa Ex President wa Mozambique Joachim Chissano
 
Tuanzie kwenye mipaka ya Tanganyika kwa pale ilipo sasa tulirithishwa kwa kutumia mkataba wa mipaka iliyowekwa mwaka gani?

Na kwa nini tuliipokea hiyo huku tukijua himaya zetu za utawala wa mababu zinavuka mipaka hiyo ya wakoloni?

Na je wakati tunapewa uhuru tuliambiwa mipaka yetu ni ipi?

Kwa katizo la hoja hasa kwa dhana ya Zanzibar na Sultanate area.
Je zile zinazosemekana kilometer 16 (au 16 miles?) za nchi kavu kutokea bahari ya hindi si za Tanganyika?

Ila Somewhere kwa kuwa England ilitawala Uganda, Kenya, Tanganyika, Malawi, Zambia na Zimbwe; walikuwa hawajali sana mipaka ya maeneo kwa kadri walivyokabidhiwa na watangulizi wao hasa kwa maeneo ya majini. Hiyo ilichangia kuvuruga mipaka iliyowekwa na wajerumani.
Again Somewhere else, ilikubaliwa kwamba kwa nchi zinazopakana kwa water bodies basi pale kati kati ya eneo la maji pawe ndio mpaka.

Na huo ndio msimamo wa Tanzania.
```````````````````````````````````````````````````
Tanzania haiwezi kuwa mlinzi wa vyanzo vya maji halafu isitumie maji hayo!

Swali je kulingana na miamba ya chini kuendelea kuserereka na hivyo kusababisha matetemeko ya ardhi, volcano, na utitio wa Ardhi. Je ikiwa itatokea Ardhi ya let say mkoa wa Njombe hasa kule Ludewa ikatitia na maji yakajaa eneo lote la mkoa wa Njombe na Mbeya (sorry for Ngoni, Wakinga and Wanyanyakusa, I assure you haitatokea), je ikitokea sasa, endapo wa juu sana kaamua tutatuimia hii kanuni ya kuwa katikati ya eneo la maji ndio uwe mpaka?
Maana tectonic plates zinaendelea zake chini kwa chini kwenye Rift Valley of East Africa!
 
Hii habari inaleta taharuki.
Nitaenda mwenyewe hadi Kyela-Matema Beach nitafikia hoteli ya Jenerali Mwamunyange nione kama haturuhusiwi kugusa hayo maji.
Hotel ya Mwamunyange ipo Ngonga kwenye makutano ya mto Kiwira na ziwa, kwa pembeni kidogo kuna makutano ya mto Songwe na ziwa ambao ni mpaka wa nchi hizi mbili,hakuna hata fujo za majini.
Ajabu ni kuwa, watu wa Nkatabay na Mbambabay, Kyela na Karonga huu mgogoro ni kama hauwahusu kwa uhusiano walio nao. Wanaishi kindugu kabisa.
 
Hotel ya Mwamunyange ipo Ngonga kwenye makutano ya mto Kiwira na ziwa, kwa pembeni kidogo kuna makutano ya mto Songwe na ziwa ambao ni mpaka wa nchi hizi mbili,hakuna hata fujo za majini.
Ajabu ni kuwa, watu wa Nkatabay na Mbambabay, Kyela na Karonga huu mgogoro ni kama hauwahusu kwa uhusiano walio nao. Wanaishi kindugu kabisa.
Wanasiasa ndio wachoganishi. Wananchi hata hawajui chochote.
 
Hotel ya Mwamunyange ipo Ngonga kwenye makutano ya mto Kiwira na ziwa, kwa pembeni kidogo kuna makutano ya mto Songwe na ziwa ambao ni mpaka wa nchi hizi mbili,hakuna hata fujo za majini.
Ajabu ni kuwa, watu wa Nkatabay na Mbambabay, Kyela na Karonga huu mgogoro ni kama hauwahusu kwa uhusiano walio nao. Wanaishi kindugu kabisa.
Halafu ukiwa hapo hotelini kwa Mwamunyange, tunatumiwa sms kwenye simu zinasema Welcome to Malawi.
 
Mkuu fuatilia huo mgogoro utaona kuna mazingira tunatengenezewa ya kuporwa hilo eneo.
Mbona ile rasi ya Crimea uwekezaji unaendelea kama kawaida japo liliporwa kibabe mwaka 2014?
Ishu hapo ni mafuta na gesi kifupi Mzungu hapo amefanikiwa kuingiza mgogoro (boko haramu) hivo lazima adili na jeshi moja tofauti akidili na majeshi mawili na la tz kwakua litakua na haki ya kuingilia kupambania mpaka wetu ziwani
otherwise....
Atafanya amefanya makubaliano na wakuu wa vipenyo ili diplomatically wakubali matokeo ili wapate mgao
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Iko hivi, kipindi kulivyoibuka vita ya maneno kati yetu na Malawi niliangalia mpaka wetu na Malawi kupitia picha za satellite nikaona mpaka huo umepita katikati ya ziwa Nyasa.

Siku chache mbeleni nikaangalia tena nikaona mpaka upo pale pale lakini sehemu hiyo/mpaka huo ukiwa umebadilishwa rangi kuwa nyekundu.

Kuchorwa mpaka huo kwa rangi nyekundu ni kuashiria kuna mzozo ambao umoja wa mataifa haujaelewa ni nani hasa mwenye haki na eneo hilo kati ya Tanzania na Malawi.

Tangu 2015 sikuwahi kuchungulia tena eneo hilo, ila leo nimeangalia mpaka huo kupitia camera za satellite nikashtuka baada ya kuona mpaka huo umehamishwa alafu wakabadili na jina la ziwa hilo na kuliita ziwa Malawi 😠

Yaani kwa kifupi lile ziwa hatuna mamlaka nalo tena! Tumeporwa kilomita nyingi sana za mraba huku serikali yetu ikiwa haijui kinachoendelea juu ya ziwa hilo lenye utajiri wa gesi, mafuta na spish za samaki zaidi ya 1500.

Mpaka huo umehamishwa kutoka katikati ya ziwa hadi kwenye fukwe za nchi yetu huku wakibadili kabisa jina la ziwa letu na kuliita ziwa Malawi kama inavyoonekana kwenye picha.

View attachment 1804817

Linganisha na mpaka ambao tuliachiwa na wakoloni katika picha hii.

View attachment 1804818

Ikumbukwe kwamba miaka michache kipindi cha serikali ya Jakaya kikwete tulikuwa na mzozo Malawi kuhusiana na hili ziwa hadi kukatokea vitisho vya kuingia vitani kila nchi ikidai italinda mpaka wake. Malawi wakidai ziwa lote ni lao huku Tanzania tukidai mpaka wa wakoloni ambao ulipita ndani ya ziwa huku sisi tukiwa na eneo lenye upana zaidi ya Malawi.

Hii maana yake nini? Sisi ni wapole sana au hatupo tayari kulinda mipaka yetu?

Kwanini wazungu wameridhia kumega nchi yetu na kuikabidhi Malawi?

Naomba serikali yetu tukufu itoe maelezo kuhusu hili jambo maana sio dogo.

Tukiendelea kunyamaza kuna siku watasema mkoa wa Rukwa ni wao
Hili ni Swala na Waziri wa mambo ya ndani na Nje kulishughulikia kwa Haraka
 
Chanzo cha hii ramani ni kipi, maana kwa ufahamu wangu kuna kamati iliundwa na Umoja wa Afrika bado inaendelea kushughulikia hili suala baada ya Malawi kupeleka malalamiko kuwa hili ziwa ni mali yao, juu ya jina la ziwa kuwa ziwa Malawi, watu wa malawi wamekuwa wakiliita hili ziwa kwa jina hilo kwa miaka mingi tu. Lakini ikumbukwe pia hili ziwa halimilikiwi na Malawi na Tanzania pekee yao, Msumbiji pia wamo so mipaka haiwezi badilika kirahisi kiasi hicho!
 
Ishu hapo ni mafuta na gesi kifupi Mzungu hapo amefanikiwa kuingiza mgogoro (boko haramu) hivo lazima adili na jeshi moja tofauti akidili na majeshi mawili na la tz kwakua litakua na haki ya kuingilia kupambania mpaka wetu ziwani
otherwise....
Atafanya amefanya makubaliano na wakuu wa vipenyo ili diplomatically wakubali matokeo ili wapate mgao
Na hili ni tatizo la Kuwa na serikali masikini, kwani kwa miaka 60 sasa hatujachukua hata hatu kuwekeza kwenye hayo maziwa, hata kuweka Boti za wanajeshi Kufanya doria kuweka maboya Kuchora ramani ya nchi yetu na kuiweka Kwenye satellite, hivyo vitu vinahitaji pesa, na serikali haina pesa, Umasikini ni laana sana
 
IMG_20210601_170710.jpg

Upana wa km 20 umemegwa bado urefu
 
Back
Top Bottom