Ziwa Nyasa limeporwa kikamilifu?

Ziwa Nyasa limeporwa kikamilifu?

Nakubaliana na wewe. Sisi cha kufanya ni kusema malawi wanapotosha umma na dunia kwa kuchapisha ramani zinazoonesha uongo.
Yes, tukinyamazia mwisho lazima hili eneo lije kuleta matatizo makubwa pande zote mbili
 
Hata jina la Nyasa si la kwao pia maana huwa nasikia nchi yao wanajiita Nyasaland
 
Nadhani hakuna jipya hapo, shughuli za kiuchumi zinaendelea kama kawaida. Meli, uvuvi na ulinzi, nothing to fear, google map kubadili mipaka ni sawa watu wanasema zanzibar ni jamhuri huru wakati huko duniani passport na nyaraka ni tanzania 🇹🇿
Fuatilia kwa makini huu mgogoro utagundua baadae huu mgogoro utatuelemea.

Wenzetu wao wanaweka mpangilio fulani huko umoja wa mataifa ili waonekane wana haki na eneo lote
 
Wamalawi wanajidanganya
Huwezi kudai maji yaliyopakana na vijiji vya nchi nyingine kuwa wakienda kuchota maji kwenye ziwa hilo basi wako nchi jirani.
Hatuwezi kukubali ujinga huo!

Ila ubaya wa hii kitu, mabeberu wanaweza kuitumia kutublackmail ili tuwape concensions kadha wa kadha la sivyo watambue kuwa ziwa lote ni mali ya Malawi
Kwenye hilo ziwa kuna oil na gesi ndo maana jamaa wamefanya hivyi na wameshaanza kifanya exploration kwenye sehemu iliokua mpaka na Tanzania yaani kati mati ya ziwa
 
Fuatilia kwa makini huu mgogoro utagundua baadae huu mgogoro utatuelemea.

Wenzetu wao wanaweka mpangilio fulani huko umoja wa mataifa ili waonekane wana haki na eneo lote
Kuonekana una haki haimaanishi hiyo haki unayo, kumbukumbu za mgogoro na sehemu ulipofikia zipo. Sasa huwezi kukurupuka kivyako vyako ukaendelea na mipangilio yako ya kumiliki ziwa zima, labda ulimiliki kimoyomoyo. Kasheshe ni pale utatakapotaka kulimiliki kivitendo ndo sebene linapoanza kuchezwa hapo na ile ngoma ya sindimba, naamini wamalawi bado wanaupenda ugali..
 
ramani iko hivyo miaka yote tangu tunapata uhuru.wakoloni ndio walichora hivyo ila Tanzania tuliikataa hiyo ramani kutokana na sheria ya kimataifa inayosema kama kuna, water body mpakani basi mpaka ni katikati ya hiyo water body ili nchi zote zinazopakana zitumie resources za hiyo water body ndio maana huu mgogoro upo tangu tunapata uhuru
 
ramani iko hivyo miaka yote tangu tunapata uhuru.wakoloni ndio walichora hivyo ila Tanzania tuliikataa hiyo ramani kutokana na sheria ya kimataifa inayosema kama kuna, water body mpakani basi mpaka ni katikati ya hiyo water body ili nchi zote zinazopakana zitumie resources za hiyo water body ndio maana huu mgogoro upo tangu tunapata uhuru
Nafikiri walifanya hivyo kwa kuona Tanganyika ina water bodies nyingi hivyo kutaka nchi za ndani ndani na zenyewe ziambulie waterbodies kidogo sema walichokosea wangemega kabisa na meneo ya nchi kavu ya huku Tanganyika ili wananchi wanaozunguka hilo ziwa wanufaike vizuri na kutokuwepo migogoro.
 
Kwenye hilo ziwa kuna oil na gesi ndo maana jamaa wamefanya hivyi na wameshaanza kifanya exploration kwenye sehemu iliokua mpaka na Tanzania yaani kati mati ya ziwa

Kama Wamalawi wanafanya exploration ya mafuta katikati ya Ziwa huku sisi tuko kimya tukiwa tumezubaa bila kupinga kwa nguvu zote basi maana yake ni kuwa watatengeneza precedence na reality on the ground na itazoeleka, kisha baada ya hapo watosegea ndani ya maji tunayodai ni yetu, na kisha watasogea mdogomdogo kuelekea upande wetu.
HUU NI MUDA MUAFAKA WA KUPINGA KWA NGUVU ZOTE EXPLORATION YA MALAWI KWENYE MAJI TUNAYODAI NI YETU, TUKIZUBAA HAO JAMAA WANACHEZA LONGTERM PLAN, WATAENDELEA KUSOGEA MDOGO MDOGO HUKU WAKIJIDAI WANATAFITI MAFUTA!

Ni lazima tupinge sasa hiyo move yao, la sivyo miaka 50 ijayo hatutakuwa na basis ya kuclaim hilo ziwa!
 
Atakuwa anaungwa mkono na Ujerumani na washirika wake
 
Tuanzie kwenye mipaka ya Tanganyika kwa pale ilipo sasa tulirithishwa kwa kutumia mkataba wa mipaka iliyowekwa mwaka gani?

Na kwa nini tuliipokea hiyo huku tukijua himaya zetu za utawala wa mababu zinavuka mipaka hiyo ya wakoloni?

Na je wakati tunapewa uhuru tuliambiwa mipaka yetu ni ipi?

Kwa katizo la hoja hasa kwa dhana ya Zanzibar na Sultanate area.
Je zile zinazosemekana kilometer 16 (au 16 miles?) za nchi kavu kutokea bahari ya hindi si za Tanganyika?

Ila Somewhere kwa kuwa England ilitawala Uganda, Kenya, Tanganyika, Malawi, Zambia na Zimbwe; walikuwa hawajali sana mipaka ya maeneo kwa kadri walivyokabidhiwa na watangulizi wao hasa kwa maeneo ya majini. Hiyo ilichangia kuvuruga mipaka iliyowekwa na wajerumani.
Again Somewhere else, ilikubaliwa kwamba kwa nchi zinazopakana kwa water bodies basi pale kati kati ya eneo la maji pawe ndio mpaka.

Na huo ndio msimamo wa Tanzania.
```````````````````````````````````````````````````
Tanzania haiwezi kuwa mlinzi wa vyanzo vya maji halafu isitumie maji hayo!

Swali je kulingana na miamba ya chini kuendelea kuserereka na hivyo kusababisha matetemeko ya ardhi, volcano, na utitio wa Ardhi. Je ikiwa itatokea Ardhi ya let say mkoa wa Njombe hasa kule Ludewa ikatitia na maji yakajaa eneo lote la mkoa wa Njombe na Mbeya (sorry for Ngoni, Wakinga and Wanyanyakusa, I assure you haitatokea), je ikitokea sasa, endapo wa juu sana kaamua tutatuimia hii kanuni ya kuwa katikati ya eneo la maji ndio uwe mpaka?
Maana tectonic plates zinaendelea zake chini kwa chini kwenye Rift Valley of East Africa!
Asante sana mkuu
 
Hotel ya Mwamunyange ipo Ngonga kwenye makutano ya mto Kiwira na ziwa, kwa pembeni kidogo kuna makutano ya mto Songwe na ziwa ambao ni mpaka wa nchi hizi mbili,hakuna hata fujo za majini.
Ajabu ni kuwa, watu wa Nkatabay na Mbambabay, Kyela na Karonga huu mgogoro ni kama hauwahusu kwa uhusiano walio nao. Wanaishi kindugu kabisa.
Mgogoro ni wa mataifa ya Ulaya baada ya kutamani rasilimali zilizopo chini ya ziwa hilo.

Wanawatumia viongozi wa Malawi huku raia wakiwa fresh tu
 
Ishu hapo ni mafuta na gesi kifupi Mzungu hapo amefanikiwa kuingiza mgogoro (boko haramu) hivo lazima adili na jeshi moja tofauti akidili na majeshi mawili na la tz kwakua litakua na haki ya kuingilia kupambania mpaka wetu ziwani
otherwise....
Atafanya amefanya makubaliano na wakuu wa vipenyo ili diplomatically wakubali matokeo ili wapate mgao
Mgogoro unaonesha Uingereza ndio inatengeneza huu mgogoro ikishirikiana na viongozi wa Malawi
 
Chanzo cha hii ramani ni kipi, maana kwa ufahamu wangu kuna kamati iliundwa na Umoja wa Afrika bado inaendelea kushughulikia hili suala baada ya Malawi kupeleka malalamiko kuwa hili ziwa ni mali yao, juu ya jina la ziwa kuwa ziwa Malawi, watu wa malawi wamekuwa wakiliita hili ziwa kwa jina hilo kwa miaka mingi tu. Lakini ikumbukwe pia hili ziwa halimilikiwi na Malawi na Tanzania pekee yao, Msumbiji pia wamo so mipaka haiwezi badilika kirahisi kiasi hicho!
Chanzo cha hii ramani ni wazungu wenyewe kwa kutumia picha za satellite wameonesha ziwa lote ni la Malawi
 
Wabongo wanachukuliaga vitu rahisi sana,ila mwishoni wanabak kulia kumbe ni mambo ya kudharau. Heb waza mtoto anaezaliwa na kuona mipaka ikiwa hivyo. Baada ya miaka 50 halijaporwa? Nani atasema hakuona mipaka? Hapo mazingira yametengenezwa ya kizazi hata kingine kipate urahisi wa kulichukua kwa maneno tu.

Kwa sababu sisi tunaangalia na kuwaza leo hatuna habari na kesho ndio maana
Ndio tatizo letu kubwa!

Ramani imebadilishwa kwa nchi yetu kumegwa raia wanasema mbona maisha yapo kawaida... Ukija kwa viongozi ndio kabisa hata hawaelewi kama mambo yamefika huko 😢
 
Back
Top Bottom