Ziwa Nyasa limeporwa kikamilifu?

Ziwa Nyasa limeporwa kikamilifu?

Binafsi hiki kitu kilinifikilisha Sana enzi za jk na kujaribu kufuatilia habari mbalimbali, mwishowe nilifika kwenye ukweli mchungu ya kwamba ziwa nyasa lote ni la Malawi ingawaje wagawaji wa mipaka kipindi hicho yaani wakoloni walifanya makosa ya ugawaji kwa kutozingatia baadhi ya kifungu. Kifungu hicho ni kwamba mipakani Kama Kuna ziwa au bahari basi mpaka lazima upite katikati ili kila nchi inufaike na maji. Kwa kuzingatia kifungu hicho wareno ambao walikuwa watawala wa msumbiji walikaa mezani na waingereza ambao walikuwa watawala wa Malawi na kukubaliana kuchora mpaka upya ndiyo maana utaona katika ziwa,msumbiji na Malawi mpaka umepita katikati. Lakini kipindi hayo yanafanyika Tanganyika na Malawi zote zilikuwa chini ya waingereza, kwahiyo hawakuona haja ya kubadili mpaka yote ni makoloni yao na hali hiyo iliendelea mpaka hizi nchi zikapata uhuru. Sasa Malawi hawataki kukaa mezani kugawana ziwa nyasa wanadai kwa mujibu wa mipaka ya mkoloni ziwa ni mali yao, ni kweli lakini mbona walikubali kufanya marekebisho enzi za wakoloni Kati yao na msumbiji? Hii inaonesha haki haikutendeka ndiyo maana Hilo liliwezekana ila halikufanyika enzi za muingereza kwa sababu hakuona haja ya kufanya hivyo nchi zote mbili ziko chini yake. Sasa tukae mezani tugawane ziwa,Malawi hawataki wanasema tufuate mpaka wa wakoloni. Tukumbuke mgogoro huu upo tangu enzi za Nyerere na Kamuzu Banda
Dah! Kwahiyo suluhisho ni nini mkuu?
 
Safi sana! mleta mada tusaidie kujua!
Hoja hapa ni mpaka kuonesha ziwa lote lipo Malawi!
Miaka michache nyuma waliweka alama nyekundu katikati ya ziwa kuonesha ziwa hilo bado linazozaniwa na mataifa mawili... Leo ile alama nyekundu haipo na mpaka umesogezwa kwa kumega zaidi ya kilomita 20 za nchi yetu.

Umeelewa?
 
Ni busara kufanya tafiti na angalau hata kujua chanzo cha huo mzozo, kabla ya kuandika kitu usichokielewa kwa ufasaha. Ikumbukwe mzozo
wa mpaka katika hilo ziwa, ulikuwa toka tunapata uhuru.Aliyekuwa raisi wa kwanza wa taifa hili, marehemu Julius K. Nyerere alizozana na marehemu raisi Kamuzu wa Malawi na mpaka wakaitana majina.Na viongozi wengine waliofuata waliingia katika majadiliano kuhusu mpaka
bila mafanikio na ilifikia wakati likapelekwa kwa wasuluhishi wa kimataifa wakati wa uongozi wa raisi Jakaya Kikwete ila mrejesho sikufanikiwa kuupata.
Mrejesho ndio huo ramani imebadilishwa kwa kukwapua kilomita 20 ndani ya nchi yetu
 
Kama Wamalawi wanafanya exploration ya mafuta katikati ya Ziwa huku sisi tuko kimya tukiwa tumezubaa bila kupinga kwa nguvu zote basi maana yake ni kuwa watatengeneza precedence na reality on the ground na itazoeleka, kisha baada ya hapo watosegea ndani ya maji tunayodai ni yetu, na kisha watasogea mdogomdogo kuelekea upande wetu.
HUU NI MUDA MUAFAKA WA KUPINGA KWA NGUVU ZOTE EXPLORATION YA MALAWI KWENYE MAJI TUNAYODAI NI YETU, TUKIZUBAA HAO JAMAA WANACHEZA LONGTERM PLAN, WATAENDELEA KUSOGEA MDOGO MDOGO HUKU WAKIJIDAI WANATAFITI MAFUTA!

Ni lazima tupinge sasa hiyo move yao, la sivyo miaka 50 ijayo hatutakuwa na basis ya kuclaim hilo ziwa!
Tena serikali ya Malawi imeshaanza mazungumzo na kampuni la Uingereza kuja kuchimba hizo rasilimali
 
Natamani vita ije ili mshindi akabidhiwr ziwa nyasa.......,
 
Achana na google maps, kwani ile meli iliyopona ajali hivi karibuni ilikuwa inafanya safari kwenye ziwa gani? Jiulize unaweza kufanya safari kwenye ziwa ambalo huna umiliki nalo?
 
huo ote ni udhaifu wa mwendazake.
anahangaika na kuiba hela za wafanyabiasha na kununua wapinzani kwa kuogopa kunyang'anywa madalaka huku wenzake wanabadirisha ramani.
dipromasia zimemshinda na kila kitu hovyo.
 
Ni ujinga wamalawi kutaka ziwa lote liwe lao. Ni kutafuta migogoro ya kipuuzi tu isiyo na kichwa wala miguu. Ni tamaa na kutumika tu
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Iko hivi, kipindi kulivyoibuka vita ya maneno kati yetu na Malawi niliangalia mpaka wetu na Malawi kupitia picha za satellite nikaona mpaka huo umepita katikati ya ziwa Nyasa.

Siku chache mbeleni nikaangalia tena nikaona mpaka upo pale pale lakini sehemu hiyo/mpaka huo ukiwa umebadilishwa rangi kuwa nyekundu.

Kuchorwa mpaka huo kwa rangi nyekundu ni kuashiria kuna mzozo ambao umoja wa mataifa haujaelewa ni nani hasa mwenye haki na eneo hilo kati ya Tanzania na Malawi.

Tangu 2015 sikuwahi kuchungulia tena eneo hilo, ila leo nimeangalia mpaka huo kupitia camera za satellite nikashtuka baada ya kuona mpaka huo umehamishwa alafu wakabadili na jina la ziwa hilo na kuliita ziwa Malawi 😠

Yaani kwa kifupi lile ziwa hatuna mamlaka nalo tena! Tumeporwa kilomita nyingi sana za mraba huku serikali yetu ikiwa haijui kinachoendelea juu ya ziwa hilo lenye utajiri wa gesi, mafuta na spish za samaki zaidi ya 1500.

Mpaka huo umehamishwa kutoka katikati ya ziwa hadi kwenye fukwe za nchi yetu huku wakibadili kabisa jina la ziwa letu na kuliita ziwa Malawi kama inavyoonekana kwenye picha.

View attachment 1804817

Linganisha na mpaka ambao tuliachiwa na wakoloni katika picha hii.

View attachment 1804818

Ikumbukwe kwamba miaka michache kipindi cha serikali ya Jakaya kikwete tulikuwa na mzozo Malawi kuhusiana na hili ziwa hadi kukatokea vitisho vya kuingia vitani kila nchi ikidai italinda mpaka wake. Malawi wakidai ziwa lote ni lao huku Tanzania tukidai mpaka wa wakoloni ambao ulipita ndani ya ziwa huku sisi tukiwa na eneo lenye upana zaidi ya Malawi.

Hii maana yake nini? Sisi ni wapole sana au hatupo tayari kulinda mipaka yetu?

Kwanini wazungu wameridhia kumega nchi yetu na kuikabidhi Malawi?

Naomba serikali yetu tukufu itoe maelezo kuhusu hili jambo maana sio dogo.

Tukiendelea kunyamaza kuna siku watasema mkoa wa Mbeya ni wao
Sasa inakuwaje kuhusu gesi, labda mabeberu wamegundua hatuna mbinu mpya,kwa uzoefi wa gesi ilivyoporwa na uchina,defense unit wako wapi?
 
Ramani iko hivo miaka mingi kabla hata ya Google earth. Kuna siku kwenye ofisi ya ubalozi wa Ujerumani nchini Tanzania ilionekana ramani yenye kuonesha ziwa lote liko Malawi. Ramani za kimataifa zinaliita ziwa Malawi badala ya Nyasa, ni kama uamue kuliita ziwa Nyanza utaliita mwenyewe wengine wataendelea kuliita Victoria.

Malawi wakileta ushahidi wao lazima tutumie akili kuupinga. Sio kukariri resolution ya UN iliyo generalized. UN hawakugawa hizi nchi, waliogawana Tz na Malawi ni Wajerumani waliokuwa German East Africa (ikiwemo Tanganyika) na Waingereza waliokuwa Malawi. Ukitazama Heligoland treaties mbili ndio mpaka ule umewekwa. Sheria za mipaka ya Afrika zinaheshimu mgawanyo wa wakoloni bila kuubadilisha. Sasa Malawi wana treaty ya kwanza inayoonesha ziwa lote ni lao. Treaty ya pili inayoonesha ziwa linagawanywa tulitakiwa tuwe nayo sisi. Hatuna

Angalizo: Nimetumia memories za zamani nilivyoelewa hili suala. Sina uhakika sana
 
Back
Top Bottom