Ziwa Nyasa limeporwa kikamilifu?

Ziwa Nyasa limeporwa kikamilifu?

Fuatilia kwa makini huu mgogoro utagundua baadae huu mgogoro utatuelemea.

Wenzetu wao wanaweka mpangilio fulani huko umoja wa mataifa ili waonekane wana haki na eneo lote
Yawezekana ila kiuhalisia ni ngumu Malawi 🇲🇼 kulob hata kule mahakamani. Ukishakua mnyonge at one point utakua mpira wa kona
Refer: 🇰🇪 vs somalia 🇸🇴
China 🇨🇳 vs japan 🇯🇵
Kenya 🇰🇪 vs uganda 🇺🇬
Siyo rahisi kukubali kuachia kipande cha ardhi maana leo ukiwapa uhuru mfano mtwara wawe republic maana yake umefungua mlango kwa kaskazini etc nao kujitangazia
 
Ramani iko hivo miaka mingi kabla hata ya Google earth. Kuna siku kwenye ofisi ya ubalozi wa Ujerumani nchini Tanzania ilionekana ramani yenye kuonesha ziwa lote liko Malawi. Ramani za kimataifa zinaliita ziwa Malawi badala ya Nyasa, ni kama uamue kuliita ziwa Nyanza utaliita mwenyewe wengine wataendelea kuliita Victoria.

Malawi wakileta ushahidi wao lazima tutumie akili kuupinga. Sio kukariri resolution ya UN iliyo generalized. UN hawakugawa hizi nchi, waliogawana Tz na Malawi ni Wajerumani waliokuwa German East Africa (ikiwemo Tanganyika) na Waingereza waliokuwa Malawi. Ukitazama Heligoland treaties mbili ndio mpaka ule umewekwa. Sheria za mipaka ya Afrika zinaheshimu mgawanyo wa wakoloni bila kuubadilisha. Sasa Malawi wana treaty ya kwanza inayoonesha ziwa lote ni lao. Treaty ya pili inayoonesha ziwa linagawanywa tulitakiwa tuwe nayo sisi. Hatuna

Angalizo: Nimetumia memories za zamani nilivyoelewa hili suala. Sina uhakika sana
Nadhani haupo sahihi hapo kwenye Nyanza/ Victoria
Refer swaziland 🇸🇿/ eSwatin
Nikukumbushe pia DRC 🇨🇩 ya leo ilikua Zaire ya zamani kama vile upper volta kwenda Burkina faso 🇧🇫
mara baada ya kuuwawa kashoji kule turkey 🇹🇷 uingereza wakabadili jina la mtaa ulipo ubalozi wa Saudi Arabia 🇸🇦 kuwa jina la huyo mhanga, leo ukituma chochote kinachotumia adress ya eneo hilo utatatumia kashoji 😁
 
Wandugu,
Toeni taharuki zenu, hiyo ramani iko hivyo hata kabla ya Tanganyika kupata uhuru wake.
Ni ramani ilichorwa na wakoloni. Haiongezi wala kuondoa kitu.

Ila historia inawapiga chenga wengi
 
Acha upotoshaji hiyo ramani ipo hivyo siku zote huo mgogoro upo lakini haujapatiwa ufumbuzi bado.Malawi wanang’ang’ania mkataba wa Heligoland unaosema mpaka Upo ufukweni.Upande wa Malawi linaitwa ziwa Malawi kwetu ni ziwa Nyasa,Upande wa Msumbiji wanaliita ziwa Niasa.Malawi hawawezi kufanya shughuli yoyote ya uchimbaji mafuta na gas maana itaanzisha upya mgogoro na pengine vita.Hivyo Sio kweli kwamba wamechukua ziwa kinyemela.
 
There is now no doubt at all about the boundary. We know that not a drop of water of the Lake Nyasa belongs to Tanganyika…”

Julias K. Nyerere 1960
 
T14 Armata mkuu nakukumbusha tu Wayahudi walikuja Palestina kimasihara kwa sasa impact yao inaonekana dunia nzima.

Miaka 50 ijayo Malawi itasema ziwa lote lao,nani atapinga? Viongozi wa nyakati hizo za 2070 wote watakuwa wamezaliwa wakiona mipaka ikiwa hivyo,wataanzaje kukataa?

Kiufupi Nyerere sio mjinga kugombea hilo ziwa na kufanikiwa angekuwa fala asingelupata.

Miaka michache iliyopita wakenya walikua wanadai mlima upo kwao kwa kufuata mpaka wa unaopinda endeo la Taveta na kijiografia inaonekana,lakini kwanini Nyerere aliwazid akili? Sababu hakuchukulia mambo kirahisi.

Kisiwa cha Pemba kiko Kenya nani anakataa? Ukinyoosha mstari utakiona wap? Kwanin Nyerere alikomaa kikawa TZ? Hana akili au ni mwizi?

Dah leo nimegundua kwanini Tanzania inaongoza kwa migogoro ya ardhi, kumbe watu wanachukulia powa afu badae maji yakiwa shingoni ndio wananza kutafutana mchawi nani.
 
Amkeni Kuna sehemu tumelala kabisa Kwenye ulinzi wa mipaka ya inchi yetu hii ji jukumu la serikali sio la kukalia kimya
Screenshot_20210602-014611_Maps.jpg
 
Si tuingie vitani tu zipigwa aisee Kwan kuna tatizo gan majeshi tunayo tatizo nn aisee tunapiga mpaka mji mkuu na makao makuu ya malawi au tupeleke bibalaka huko waingie madalakani tubadili mipaka
 
Binafsi hiki kitu kilinifikilisha Sana enzi za jk na kujaribu kufuatilia habari mbalimbali, mwishowe nilifika kwenye ukweli mchungu ya kwamba ziwa nyasa lote ni la Malawi ingawaje wagawaji wa mipaka kipindi hicho yaani wakoloni walifanya makosa ya ugawaji kwa kutozingatia baadhi ya kifungu. Kifungu hicho ni kwamba mipakani Kama Kuna ziwa au bahari basi mpaka lazima upite katikati ili kila nchi inufaike na maji. Kwa kuzingatia kifungu hicho wareno ambao walikuwa watawala wa msumbiji walikaa mezani na waingereza ambao walikuwa watawala wa Malawi na kukubaliana kuchora mpaka upya ndiyo maana utaona katika ziwa,msumbiji na Malawi mpaka umepita katikati. Lakini kipindi hayo yanafanyika Tanganyika na Malawi zote zilikuwa chini ya waingereza, kwahiyo hawakuona haja ya kubadili mpaka yote ni makoloni yao na hali hiyo iliendelea mpaka hizi nchi zikapata uhuru. Sasa Malawi hawataki kukaa mezani kugawana ziwa nyasa wanadai kwa mujibu wa mipaka ya mkoloni ziwa ni mali yao, ni kweli lakini mbona walikubali kufanya marekebisho enzi za wakoloni Kati yao na msumbiji? Hii inaonesha haki haikutendeka ndiyo maana Hilo liliwezekana ila halikufanyika enzi za muingereza kwa sababu hakuona haja ya kufanya hivyo nchi zote mbili ziko chini yake. Sasa tukae mezani tugawane ziwa,Malawi hawataki wanasema tufuate mpaka wa wakoloni. Tukumbuke mgogoro huu upo tangu enzi za Nyerere na Kamuzu Banda
Rudi tena usome historia ya mpaka katika ziwa Nyasa hiki ulichoandika siyo sahihi.

Tanganyika ilikuwa chini ya ujerumani na mpaka wa mwanzo wakati Tanganyika likiwa koloni la ujerumani unafahamika ulikuwa unajumuisha Ziwa Malawi.

Kasome vizuri the Heligolland Treaty utapata mwanga
 
Kwahiyo wewe ndiyo unajua kuliko mtoa mada kwa hiki ulichoandika ?
 
Tukiendelea kunyamaza kuna siku watasema mkoa wa Mbeya ni wao
Wewe Jamaa una mihemko ya aina fulani.

Kwani historia ya hapo tokea zamani huijui? Hizo ramani ndio leo umeanza kuziona?

Sasa unalia tunapoteza ziwa, wananchi wetu hawaendelei na shughuli zao humo ziwani; umesikia mitumbwi yao ikizamishwa?

Yaani unataka tujadili hapa jambo ambalo huna ufahamu nalo?.

Wewe unajiita 'kijana wa jana'; hivi kweli utakosa kujua historia ya hapo?

Unatafuta kupotezea watu muda bure!
 
Muhimu ni kujenga ukuta unaoelea,wanajeshi tuliona wanaliweza hili,mianzi kibao tunayo, na kama hilo haliwezekani tuna milima mirefu kuliko kina cha Ziwa Nyasa hii milima dongo lake litumike kujaza ndani ya ziwa kwa kilomita tunazozitaka,halafu tuone.
 
Back
Top Bottom