Ziwa Nyasa limeporwa kikamilifu?

Ziwa Nyasa limeporwa kikamilifu?

Ukiona hivyo ujue tulishindwa hiyo kesi kwenye kile kikao cha usuruhirishi. Shida iko kwenye serikali yetu haina uwazi hata kidogo,hata kwa jambo la hatari kama hili,ilipaswa wananchi wajulishwe ile kesi ya usuruhishi kuhusu hilo umefikia wapi?. Zaidi hatuna habari na hayo mambo. Tulikuwa tunapambana kumbana sana Mbowe na watu wake.
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Iko hivi, kipindi kulivyoibuka vita ya maneno kati yetu na Malawi niliangalia mpaka wetu na Malawi kupitia picha za satellite nikaona mpaka huo umepita katikati ya ziwa Nyasa.

Siku chache mbeleni nikaangalia tena nikaona mpaka upo pale pale lakini sehemu hiyo/mpaka huo ukiwa umebadilishwa rangi kuwa nyekundu.

Kuchorwa mpaka huo kwa rangi nyekundu ni kuashiria kuna mzozo ambao umoja wa mataifa haujaelewa ni nani hasa mwenye haki na eneo hilo kati ya Tanzania na Malawi.

Tangu 2015 sikuwahi kuchungulia tena eneo hilo, ila leo nimeangalia mpaka huo kupitia camera za satellite nikashtuka baada ya kuona mpaka huo umehamishwa alafu wakabadili na jina la ziwa hilo na kuliita ziwa Malawi 😠

Yaani kwa kifupi lile ziwa hatuna mamlaka nalo tena! Tumeporwa kilomita nyingi sana za mraba huku serikali yetu ikiwa haijui kinachoendelea juu ya ziwa hilo lenye utajiri wa gesi, mafuta na spish za samaki zaidi ya 1500.

Mpaka huo umehamishwa kutoka katikati ya ziwa hadi kwenye fukwe za nchi yetu huku wakibadili kabisa jina la ziwa letu na kuliita ziwa Malawi kama inavyoonekana kwenye picha.

View attachment 1804817

Linganisha na mpaka ambao tuliachiwa na wakoloni katika picha hii.

View attachment 1804818

Ikumbukwe kwamba miaka michache kipindi cha serikali ya Jakaya kikwete tulikuwa na mzozo Malawi kuhusiana na hili ziwa hadi kukatokea vitisho vya kuingia vitani kila nchi ikidai italinda mpaka wake. Malawi wakidai ziwa lote ni lao huku Tanzania tukidai mpaka wa wakoloni ambao ulipita ndani ya ziwa huku sisi tukiwa na eneo lenye upana zaidi ya Malawi.

Hii maana yake nini? Sisi ni wapole sana au hatupo tayari kulinda mipaka yetu?

Kwanini wazungu wameridhia kumega nchi yetu na kuikabidhi Malawi?

Naomba serikali yetu tukufu itoe maelezo kuhusu hili jambo maana sio dogo.

Tukiendelea kunyamaza kuna siku watasema mkoa wa Mbeya ni wao
Acha kudanganywa na hiyo mipaka ya Satelite
 
wamalawi wasije kutumiwa kutaka kuchota gesi yetu na nchi kubwa. wakifanya hivyo watatusumbua .
maana kama labda wameshindwa kuchota kupitia tanzania watapitia malawi ili tu wafanikiwe lengo lao .
 
Nimeenda kuangalia nimekuta kweli Roho imeniuma kweli, inawezekanaje hii?
Inauma sana. Mpaka wetu ulitakiwa upite hapa kama zamani
Screenshot_20210602-094720.png
Screenshot_20210602-094720.png

Uzuri ukiangalia hapo, mpaka wa Zambia ulio katikati ya maji unaelekeza kabisa vile ramani ilikua hapo kabla
 
Acha kudanganywa na hiyo mipaka ya Satelite
Wewe upo dunia ya wapi? Satellite ndio hipima karibia kila kitu siku hizi hadi viwanja.
Kama camera za satellite zimeelekezwa kupitisha mpaka pembeni ya ziwa ujue wale wale waliokufanya mtumwa wanaihakikishia dunia kwamba hatuna mamlaka na hilo ziwa tena.

Ni suala la muda tu tutakuja kuona vitendo
 
Wewe upo dunia ya wapi? Satellite ndio hipima karibia kila kitu siku hizi hadi viwanja.
Kama camera za satellite zimeelekezwa kupitisha mpaka pembeni ya ziwa ujue wale wale waliokufanya mtumwa wanaihakikishia dunia kwamba hatuna mamlaka na hilo ziwa tena.

Ni suala la muda tu tutakuja kuona vitendo
Sasa wewe amini hizo satelite zako tulioko field tunajua
 
Sasa wewe amini hizo satelite zako tulioko field tunajua
Amiri jeshi wenu siku akiwaambia mrudi nyuma kilomita 20 kwa maana mpo ndani ya nchi nyingine utapinga?

Aliyekupitisha kuwa mwanajeshi alikosea sana
 
daah upana wa 20km ni kutoka mwenge to daraja la kigamboni na urefu wa 220km ni dar to moro. huu ni utani sasa
 
Amiri jeshi wenu siku akiwaambia mrudi nyuma kilomita 20 kwa maana mpo ndani ya nchi nyingine utapinga?

Aliyekupitisha kuwa mwanajeshi alikosea sana
Wewe hujui kuwa Google imenakili Ramani ya Waingereza? Au unazani satelite inajichorea yenyewe
 
Si tuingie vitani tu zipigwa aisee Kwan kuna tatizo gan majeshi tunayo tatizo nn aisee tunapiga mpaka mji mkuu na makao makuu ya malawi au tupeleke bibalaka huko waingie madalakani tubadili mipaka
Lowassa tu ndio alithubuti kumtishia yule mama
 
Kama ipo hivyo siku zote mbona Tanzania tunafanya shughuli zetu kama kawaida kwenye hilo ziwa?

Ingekua uongeayo ni kweli, basi tusingedhubutu kufanya shuguli za kiuchumi kwenye hilo ziwa
Huujui huu mgogoro Upo siku nyingi tangu enzi za Nyerere na Ndio maana shughuli zinaendelea.
 
Kama wanajiamini Ziwa lote ni lao waanze kufanya mishe mishe zao ziwa zima waone MOTO [emoji91][emoji91]
Wanachofanya wao ni vita ya kisayansi. Nyie subirini hapo hapo hiyo vita yenu ya kishamba ya mabunduki.
Nataka niwaambie hapo ndio tujijue sisi bado hata uelewa tu tunashuka kwa kasi kwenda chini. Hata Malawi wametupiga bao sasa. Tumekazana tu kutekana humu humu ndani.
Sisi tumepanga wanajeshi mpakani. Malawi wanaendelea taratibu kujimilikisha ardhi yetu kisheria kwenye jumuia za kimataifa
 
Back
Top Bottom