ZPC Muliro: Mtu yeyote atakayetoa taarifa zitakazosaidia kukamatwa mtuhumiwa wa ujambazi akiwa na silaha atazawadiwe Shilingi 2 Milioni.

ZPC Muliro: Mtu yeyote atakayetoa taarifa zitakazosaidia kukamatwa mtuhumiwa wa ujambazi akiwa na silaha atazawadiwe Shilingi 2 Milioni.

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
4,016
Reaction score
6,759
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema mtu yeyote atakayetoa taarifa zitakazosaidia kukamatwa mtuhumiwa wa ujambazi akiwa na silaha atazawadiwa Sh2 milioni.

Hayo yameelezwa leo Jumatano Juni 23, 2021 na Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Jumanne Muliro katika mkutano wake na waandishi wa habari.

Amesema lengo ni kuendeleza operesheni hadi pale vitendo vya uhalifu vitakapokoma huku akihidi kuwa watakaotoa taarifa hizo hawatatajwa.

"Mwenye taarifa zinazohusu jambazi ziwe sahihi na ambazo zitafanikisha kumkamata akiwa na silaha donge hilo litatolewa palepale baada ya kufanikisha kumkamata kwa siri,” amesema.
 
Hivi hawa Polisi uwezo wao wa kufikiri umeishia wapi?hivi kweli huo ndio mwisho wao wa kufikiri,.....mwisho wao wa kutumia uwezo wa akili zao??!

Je wanajua madhara ya hili wanalolifanya?Je wameshasahau nini kilifanyika wakati wa mkuu wa upelelezi aliekuwa anaitwa Zombe,kama sikosei,hala Dar

Kufanya Watanzania tuanze kuchunguzana ni kitu kibaya sana..

Nakumbuka kuna wakati Polisi walipewa agizo la kuuwa mtu yoyote anaehusishwa na ujambazi

matokeo yake wafanya biashara wa dhahabu wasiokuwa na hatia yoyote waliuliwa kikatili na Polisi kwa kusingiziwa majambazi..

Polisi kuwaruhusu raia wachunguzane ni sawa na kuruhusu raia waanze kulipizana visasi,raia waanza kuwajaza Polisi habari za uongo,ni kufanya raia waanze kuogopana

Kwa umasikini tulionao milioni mbili ni pesa nyingi sana,raia wataanza kuwalisha Polisi habari za uongo ili wapate hizo pesa

Kule Marekani ni kosa kubwa kwa Polisi kitumia "informer" kwa kupata habari zake,ijapokuwa wako wanaotumia informers kisirisiri

Polisi wa Marekani hawaruhusiwi kutumia mainfoma kwa sababu kama nilizozitaja hapo juu

Polisi waache kutaka easy solutions,easy answers,waache kucheza na maisha ya Watanzania..
 
Wale traffic wa barabarani haturuhusiwi kuwaripoti walau kwa malipo kiduchu?

Raia wanaweza kusaidia upatikanaji wa taarifa. Lakini askari wao wana mafunzo. Kupambana na uhalifu kunahitaji weledi sana na siyo kwa njia kama hizi hasa kwa jamii iliuojaa chuki, umaskini na visasi.
 
Hivi hawa Polisi uwezo wao wa kufikiri umefikiri umeishia wapi

Je wanajua madhara ya hili wanalofanya?Je wameshasahau nini kilifanyika wakati wa mkuu wa upelelezi Zombe

Kufanya Watanzania tuanze kuchunguzana ni kitu kibaya sana..

Nakumbuka kuna wakati Polisi walipewa agizo la kuuwa mtu yoyote anaehusishwa na ujambazi

matokeo yake wafanya biashara wa dhahabu wasiokuwa na hatia yoyote waliuliwa kikatili na Polisi kwa kusingiziwa majambazi..

Polisi kuwaruhusu raia wachunguzane ni sawa na kuruhusu raia waanze kulipizana visasi,raia waanza kuwajaza Polisi habari za uongo,ni kufanya raia waanze kuogopana

Kwa umasikini tulionao milioni mbili ni pesa nyingi sana,raia wataanza kuwalisha Polisi habari za uongo ili wapate hizo pesa

Kule Marekani ni kosa kubwa kwa Polisi kitumia "informer" kwa kupata habari zake,ijapokuwa wako wanaotumia informers kisirisiri

Polisi wa Marekani hawaruhusiwi kutumia mainfoma kwa sababu kama nilizozitaja hapo juu

Polisi waache kutaka easy solutions,easy answers,waache kucheza na maisha ya Watanzania..
Hatuna Jeshi la Polisi tuna genge la waganga njaa, wao wanasema hilo Jw nao wasemeje, Fire nao wasemeje, PCCB nao
 
Back
Top Bottom