mtoto wa mchungaji
JF-Expert Member
- Oct 24, 2020
- 279
- 480
Akihojiwa kupitia EATV live, Kilikuwa kipindi kizuri hasa ukiangalia ile kombinesheni ya wadada hawa wawili yani Da Salama kama mnavyo mjua na Da Zuhura wakiwa pamoja mezani na Da Salama anavyomchimba kumtaka ya ndani na nje. Mahojiano yalikuwa mazuri sana kwani Da Salama anajaribu kumchimba Zuhura ambaye anaakili sana namna anavyojibu maswali ya Salama.
Kiukweli walijadiliana mengi sana lakini mimi nimeyaona mawili kuwa ya muhimu, yaani uchumi na mahusiano. Kiuchumi Zuhura alikuwa anasema kuwa maisha ya London ni magumu sana ukilinganisha na hapa bongo (Dar), na amekiri kuwa na wakati mgumu kwa ndugu, jamaa na marafiki ambao wamekuwa hawaelewi maisha ya London. Nilivyomwelewa kuna baadhi ya jamaa huwa akirudi wanamtolea macho kumtoa mchuzi wakidhani anamihela mingi, yaani maisha yake wanayatafsiri kwa kumwangalia kupitia runinga anavyo waka mtoto.
Da zuhura alikuwa anajaribu kutoa ufafanuzi wa gharama za maisha kama kulipia televisheni (ching'amuzi) chaneli kama laki 3 za kibongo kwa kadirio la chini kwa mwezi, kodi ya nyumba alisema iko juu sana, sikumwelewa vizuri lakini alikuwa anamaanisha inachajiwa kwa siku yaani kama huku basi umeenda zile gesti za kibongo za buku 50 au 60 hivi, hina kuwa kama 1,800,000/= kwa mwezi. Na ieleweke kuwa kule London unapohamia katika nyumba unabeba nguo zako tu, tofauti na huku Bongo mtu akihamia katika nyumba aliyopanga anabeba mpaka fuso inajaa wakati mwingine anarudia. Kwa Londoni kila kitu unakikuta ndani mpaka vijiko unavikuta.
Pia tofauti na uku unalipa chumba umeme na maji kule ni vyote vipo ila kimeongezeka kingine, kinaitwa gesi, na kina kazi zaidi ya kupikia nayo pia huwezi kuishi bila hiyo na ipo juu vile vile.
Maji amesema pia yapo juu, yaani bili ya maji London iko juu, lakini kunasheria kali Uingereza hairuhusiwi kumkatia mtu maji hata kama hajalipa bili ya maji tofauti na Bongo, hapa DAWASA wanang'oaga mpaka bomba lote wakibeba mita.
Hivyo dadetu ambaye ni mzaliwa wa hapa hapa mchangani leo ametoa ufafanuzi huo na kukiri kuwa kusevu ni ngumu sana, hivyo msimchukulie poa anapambana na hali yake.
Salama alipotaka kujua kuhusu maswala ya mahusiano yake binafsi kama kawaida alitumia engo nyingi na ndefu za kiswahili, nilimsikia Salama akisema sasa maisha umesema ni magumu lakini nasikia mtu akiwa na mpenzi huwa wanasaidiana maisha huko si kama huku bongo kuna vibenten (Salama alikejeli) ndipo Zuhura akaingia katika 3 zake na kusema kule Uingereza kugawa majukumu ni pasu pasu hakuna kukwepa hata kama una mshahara mdogo majukumu hayajui hilo.
Ndipo salama akamdondoshea swali pale pale kuwa vipi wewe umeolewa na una watoto, chakushangaza Zuhura bila kupepesa macho wala kumung'unya maneno akajibu hana mume bado anatafuta, na anamwomba Allah apate mume.
Jamani kwa wale mnaojua Zuhura wa BBC hana mume anatafuta na ameonyesha hamu ya kuolewa na mtanzania mwenzake. Mimi mtoto wa mchungajia tayari nilisha oa na kanisa limetwambia mke mmoja tu hivyo mimi nashusha udende kazi kwenu.
Mtoto wa mchungaji.
Kiukweli walijadiliana mengi sana lakini mimi nimeyaona mawili kuwa ya muhimu, yaani uchumi na mahusiano. Kiuchumi Zuhura alikuwa anasema kuwa maisha ya London ni magumu sana ukilinganisha na hapa bongo (Dar), na amekiri kuwa na wakati mgumu kwa ndugu, jamaa na marafiki ambao wamekuwa hawaelewi maisha ya London. Nilivyomwelewa kuna baadhi ya jamaa huwa akirudi wanamtolea macho kumtoa mchuzi wakidhani anamihela mingi, yaani maisha yake wanayatafsiri kwa kumwangalia kupitia runinga anavyo waka mtoto.
Da zuhura alikuwa anajaribu kutoa ufafanuzi wa gharama za maisha kama kulipia televisheni (ching'amuzi) chaneli kama laki 3 za kibongo kwa kadirio la chini kwa mwezi, kodi ya nyumba alisema iko juu sana, sikumwelewa vizuri lakini alikuwa anamaanisha inachajiwa kwa siku yaani kama huku basi umeenda zile gesti za kibongo za buku 50 au 60 hivi, hina kuwa kama 1,800,000/= kwa mwezi. Na ieleweke kuwa kule London unapohamia katika nyumba unabeba nguo zako tu, tofauti na huku Bongo mtu akihamia katika nyumba aliyopanga anabeba mpaka fuso inajaa wakati mwingine anarudia. Kwa Londoni kila kitu unakikuta ndani mpaka vijiko unavikuta.
Pia tofauti na uku unalipa chumba umeme na maji kule ni vyote vipo ila kimeongezeka kingine, kinaitwa gesi, na kina kazi zaidi ya kupikia nayo pia huwezi kuishi bila hiyo na ipo juu vile vile.
Maji amesema pia yapo juu, yaani bili ya maji London iko juu, lakini kunasheria kali Uingereza hairuhusiwi kumkatia mtu maji hata kama hajalipa bili ya maji tofauti na Bongo, hapa DAWASA wanang'oaga mpaka bomba lote wakibeba mita.
Hivyo dadetu ambaye ni mzaliwa wa hapa hapa mchangani leo ametoa ufafanuzi huo na kukiri kuwa kusevu ni ngumu sana, hivyo msimchukulie poa anapambana na hali yake.
Salama alipotaka kujua kuhusu maswala ya mahusiano yake binafsi kama kawaida alitumia engo nyingi na ndefu za kiswahili, nilimsikia Salama akisema sasa maisha umesema ni magumu lakini nasikia mtu akiwa na mpenzi huwa wanasaidiana maisha huko si kama huku bongo kuna vibenten (Salama alikejeli) ndipo Zuhura akaingia katika 3 zake na kusema kule Uingereza kugawa majukumu ni pasu pasu hakuna kukwepa hata kama una mshahara mdogo majukumu hayajui hilo.
Ndipo salama akamdondoshea swali pale pale kuwa vipi wewe umeolewa na una watoto, chakushangaza Zuhura bila kupepesa macho wala kumung'unya maneno akajibu hana mume bado anatafuta, na anamwomba Allah apate mume.
Jamani kwa wale mnaojua Zuhura wa BBC hana mume anatafuta na ameonyesha hamu ya kuolewa na mtanzania mwenzake. Mimi mtoto wa mchungajia tayari nilisha oa na kanisa limetwambia mke mmoja tu hivyo mimi nashusha udende kazi kwenu.
Mtoto wa mchungaji.