Zuio Kwa WaTZ: Wahi Ubalozi wa USA Kabla haijala Kwako Kama Ulishinda Viza ya Kukupa Makazi ya Kudumu Marekani

Zuio Kwa WaTZ: Wahi Ubalozi wa USA Kabla haijala Kwako Kama Ulishinda Viza ya Kukupa Makazi ya Kudumu Marekani

DocJayGroup

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2020
Posts
1,654
Reaction score
3,346
Kila mwaka, Marekani inatoa makazi ya kudumu kwa watu 50,000 kupitia mchezo wa bahati nasibu. Mchezo huo, unachezwa kuanzia mwanzoni mwa mwezi Oktoba hadi Mwanzoni mwa mwezi Novemba. Leo hii, Serikali ya Marekani imetangaza kwamba waTanzania wote watazuiliwa kwenda Marekani kupitia bahati na sibu hiyo. Kuzuiwa huko kutaanza tarehe February 22. Kwa hio kama ulishinda mwaka jana, basi wahi ubalozini sasa hivi upate viza yako ya kukupatia makazi ya kudumu USA, kabla ya hio tarehe ambapo ndio waTZ watazuiliwa. Serikali ya Marekani haijasema sababu halisia ya kufanya hilo.

Pamoja na Tanzania, nchi ya Sudan nayo imezuiliwa viza hio ya bahati na sibu. Nchi 2 nyingine za Afrika za Eritrea na Nigeria zimepigwa nyundo kali Zaidi ambapo wamezuia aina zote za visa zinazomruhusu mtu kuishi na kufanya kazi Marekani.

IMG-20200131-WA0004.jpg
 
Wamalizane na Iran kwanza sio wanatafuta pa kutokea
 
Utawala wa nchi umekuwa wa Ki-dikteta hata mataifa mengine wanashtuka kweli tumerudi nyuma.
 
Kila mwaka, Marekani inatoa makazi ya kudumu kwa watu 50,000 kupitia mchezo wa bahati nasibu. Mchezo huo, unachezwa kuanzia mwanzoni mwa mwezi Oktoba hadi Mwanzoni mwa mwezi Novemba. Leo hii, Serikali ya Marekani imetangaza kwamba waTanzania wote watazuiliwa kwenda Marekani kupitia bahati na sibu hiyo. Kuzuiwa huko kutaanza tarehe February 22. Kwa hio kama ulishinda mwaka jana, basi wahi ubalozini sasa hivi upate viza yako ya kukupatia makazi ya kudumu USA, kabla ya hio tarehe ambapo ndio waTZ watazuiliwa. Serikali ya Marekani haijasema sababu halisia ya kufanya hilo.

Pamoja na Tanzania, nchi ya Sudan nayo imezuiliwa viza hio ya bahati na sibu. Nchi 2 nyingine za Afrika za Eritrea na Nigeria zimepigwa nyundo kali Zaidi ambapo wamezuia aina zote za visa zinazomruhusu mtu kuishi na kufanya kazi Marekani.

View attachment 1343071
Mkuu kwani Kazuiliwa Makonda peke yake Au Taifa zima?
Kuna Hiyo ramani hapo Juu mjumbe katupia Nchi zilizopigwa Ban 2018 na Nchi mpya Ban! Tanzania ikiwemo,
Sasa Kama Nchi tayari ilikuwa Imepigwa Ban? Ina maana gani kumpiga Makonda Ban wakati tayari ulishaipiga Ban Nchi yake?
Nieleweshe Mkuu!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu kama Nimesoma mahali,kuwa Hii bani haitahusisha Watu wanaoenda Kupata Matibabu,watalii,Wanaofanya Nazi,nk,
Ila ni Immigrants tuu,na watu wanaoenda kwa Muda!
Nisahihishe kama nimekosea!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kwani Kazuiliwa Makonda peke yake Au Taifa zima?
Kuna Hiyo ramani hapo Juu mjumbe katupia Nchi zilizopigwa Ban 2018 na Nchi mpya Ban! Tanzania ikiwemo,
Sasa Kama Nchi tayari ilikuwa Imepigwa Ban? Ina maana gani kumpiga Makonda Ban wakati tayari ulishaipiga Ban Nchi yake?
Nieleweshe Mkuu!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
Marekani ina viza za aina mbili kuu. Aina ya kwanza, inamfanya mtu anakuwa na karibu haki zote kama raia (immigrant visa), na ya pili haimpi haki na anatakiwa kuondoka USA muda wa visa ukiisha (mtalii, viza ya biashara, mwanafunzi nk).

Makonda amepigwa marufuku kabisa kwa asilimia zote viza za aina zote. Eritrea na Nigeria wamepigwa marufuku viza zote hizo za immigrant visas. Katioa immigrant visas pia ina aina tofauti, kwa Tanzania tumepigwa marufuku visa inaitwa Dv Lottery visa ambayo mtu unaipata kwa kucheza hio bahati nasibu.

Kwa hio kwa waTz, bado unaweza kuomba visa kama wewe unaenda kusoma, kutalii nk. Ila kwa ujumla, mambo yatakuwa magumu kwa waTz. Kwa hio mtu ni kwenda ubalozini ukiwa uko fiti kwelikwelii
 
Back
Top Bottom