FEDHA ZA MAUZAUZA
1.
Tulikuwa kijiweni, tukizogoa zogoa,
Umbeya tukipigieni, tukiyapisha masaa,
Bia tamu tukinyweni, pia soka kichambua,
Fedha za mauzauza, menitia ulemavu.
2.
Mara mtu akapita, shanga nyingi zi shingoni,
Kati yetu akamwita, machache kiulizweni,
Akaja bila kusita, karibu...