1. Ninalo wazo bunifu,
Ila mwenzenu nahofu,
Wapo wenye nia chafu,
Wanoweza nizulia.
2. Ninaposhusha usuli,
Uhusuo serikali,
Wenye hiba na adili,
Wao wataupindua.
3. Watazua yaso mana,
Ambayo sijayanena,
Hivyo nawaomba sana,
Muje nihahakikishia.
4. Ikiwa tatoa wazo,
Lililokidhi vigezo,
Mtakuwa...