11 wafariki dunia, 44 wajeruhiwa kwa ajali ya basi Mbeya

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274

Watu 11 wamepoteza maisha na wengine 44 wamejeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya A-N Coach kupata ajali katika eneo la Luanjilo Wilaya ya Mbeya Vijijini.​

Ajali hiyo imetokea alfajiri ya leo Ijumaa, Septemba 6, 2024 baada ya basi hilo lililokuwa likitoka Mbeya kwenda Tabora kupinduka wakati likilikwepa lori, kisha kutumbukia mtaroni.


Mganga wa Mkuu wa Hosptali ya Wilaya ya Chunya, Dk Darson Andrew amethibitisha kupokea idadi ya hiyo na vifo huku akieleza kati ya majeruhi 44 wanne wana hali mbaya na watapewa rufaa kupelekwa Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.


Pia soma Mbeya: Basi la Kampuni ya Shari lapata ajali Mbarali, Watu 9 wapoteza maisha, Polisi wamshikilia Dereva
 
Wasiojulikana ili kutimiza lengo lao la kafara za uchaguzi sasa wamebadilisha Mechanism.
 
Wimbi la ajali lomeendelea kutisa Mkoa wa Mbeya ambapo mapema Leo Alfajiri kumetokea ajali eneo la Lwanjilo Wilayani Chunya Mkoani Mbeya ambapo watu 14 wamepoteza maisha na wengine 44 kujeruhiwa kufuatia ajali ya bus la AN Classic kutoka Mbeya kwenda Tabora.

View: https://www.instagram.com/p/C_kgPlwNdxo/?igsh=MWl3MTNtaHA3MjYwZg==
My Take
Je Serikali na Polis Wameshindwa kuja na Sheria ya kuwafilosi na kuwanyonga madereva Wazembe?

R.I.P ndugu wote,majeruhi mpone haraka.

View: https://x.com/tanroas/status/1831987363943198805?t=hDdgDeof1XaKBqLZsmszog&s=19
Pia soma Mbeya: Basi la Kampuni ya Shari lapata ajali Mbarali, Watu 9 wapoteza maisha, Polisi wamshikilia Dereva
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…