Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Napendekeza madereva wa magari ya abiria wawe na elimu angalau ya kidato cha nne na ufaulu mzuri
Watu 11 wamepoteza maisha na wengine 44 wamejeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya A-N Coach kupata ajali katika eneo la Luanjilo Wilaya ya Mbeya Vijijini.Ajali hiyo imetokea alfajiri ya leo Ijumaa, Septemba 6, 2024 baada ya basi hilo lililokuwa likitoka Mbeya kwenda Tabora kupinduka wakati likilikwepa lori, kisha kutumbukia mtaroni.
Mganga wa Mkuu wa Hosptali ya Wilaya ya Chunya, Dk Darson Andrew amethibitisha kupokea idadi ya hiyo na vifo huku akieleza kati ya majeruhi 44 wanne wana hali mbaya na watapewa rufaa kupelekwa Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.
Pia soma Mbeya: Basi la Kampuni ya Shari lapata ajali Mbarali, Watu 9 wapoteza maisha, Polisi wamshikilia Dereva
Kanda ya kusini na kaskazini ni nadra sana kusikia ajali kulinganisha na nyanda za juu kusini.Walishaweka wazi humu kuwa wao ni wapenda mbio na basi zao ni chapa Scania tu ndiyo wanapenda.
Why kusiwe na jitihada za lazima kunusuru maisha ya watu?Ni miuondo mbinu mibovu sana, ndugu yangu hata hivyo ni Mungu tu anasaidia kwa hizi route za Mbeya-Tabora
Barabara za Nyanda za juu zipo milimani.Kanda ya kusini na kaskazini ni nadra sana kusikia ajali kulinganisha na nyanda za juu kusini.
Wapumzike kwa amani
Ni ajali tu na mda wao ulikuwa umefika lakini kama ni elimu dereva aliefariki anaelimu za zaid, kama ntakuwa sijasajau alisomea Malaysia na alikuwa mbobevu katika ufundi pia na uendeshajiNapendekeza madereva wa magari ya abiria wawe na elimu angalau ya kidato cha nne na ufaulu mzuri