1963: Rais wa Jamhuri ya Tanganyika, Julius Nyerere akiweka pini katika koti la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. U Thant


Unasogeza tu magoli Mohammed. Hii unataka kutuaminisha kuwa Dar es Salaam nzima uliyejua habari za Abdul Sykes ni wewe tu?

Mimi nimesema Earle E Seaton, mwanasheria mzaliwa wa Bermuda, alumni wa Howard University alialikwa na Thomas Marealle kuja Tanganyika baada ya kukutana nae London, Uingereza. Walikutana wakati Seaton anasomea sheria London University na Thomas Marealle akiwa anasoma London School of Economics. Wewe unaleta ya DAVID Marealle na kuwa alipokewa na Abbas Sykes Dar es Salaam? David na Thomas wapi na wapi?

Kama vile wewe unavyozungumzia benz ya Sykes, mimi naweza kukuambia kuwa nilikuwa napanda benz ya mzee John Rupia.

Sasa kama unajua kuwa kuna mikutano ilifanyika Welfare kwa Hamza Mwapachu kwa nini ulitaka kutuaminisha kuwa mikutano yote ilifanyika kwa Abdul Sykes peke yake? Unajichanganya mwenyewe.

Unasema Katiba ya TANU ni ya Labour Party wakati awali ulituambia kuwa Seaton alimshauri mwandishi wa katiba hiyo, Abdul Sykes a copy ya Nkrumah ili ikubaliwe na wazungu! Nkrumah alikuwa Labour Party? Chama cha CPP ni cha Gold Coast, na katiba yake na ya Labour Party ya Uingereza ilitumiwa na Nyerere kutayarisha draft ya Katiba ya TANU. Na hili nimelisema.

Unasema wasingeweza kufanya mikutano kwa Amir Jamal kwa sababu alijiunga na TANU 1958. Unajuaje kama hakuwa shabiki wa TANU wa chinichini kabla ya kujiunga rasmi? Unataka kutuambia kuwa wakati unaozungumzia waafrika walikuwa wanazuiwa kwenda kwa wahindi? Na mikutano ilipamba moto baada ya TANU kuzaliwa na haikuishia Anatouglou na Jangwani.

Wakina Kimambo waliandika Historia ya nchi yetu wakati tunaimba " zidumu fikra sahihi za Mwenyekiti wetu" kwa hiyo si ajabu wao kumkuza sana Nyerere na kuwapuuza watu kama Abdul Sykes na wengine. Mmojawapo wa watu waliochangia sana kuimarika kwa TANU ni Oscar Kambona ambae alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa TANU aliambiwa kuwa mshahara wake utatokana na wanachama atakaowaingiza kwenye chama. Leo nani anamtaja? Nani hata anajua mke wake Flora aliishia wapi? Wakina Sykes wana mtaa, lakini Kambona hata kichochoro hana. Na ingekuwa ni kwa sababu ya kesi ya uhaini basi hata Bibi Titi asingekuwa na mtaa!

Ishara kubwa ya mtu aliye elimika ni kukubali kukosolewa, kurekebisha alichokiandika kama taarifa nyingine zitatokeza nakutambua kuwa anachojua yeye ni sehemu tu ya ukweli uliopo. Hata Stephen Hawkins hakuwahi kusema hakuna mtu wa kumfundisha lolote kuhusu physics. Alikuwa anajifunza kila siku kutoka kwa walimwengu wenzake.

Kuna article imeandikwa na N.J. Westcott inayoitwa " An East African Radical : The Life of Erica Fiah" katika Journal of African History ya mwaka 1981. Sijui Westcott alipewa na nani habari za Fiah?

Amandla...

Bwana Mdogo Fundi Mchundo

cc. Nguruvi3
 
Makala...
Hii makala niliweka wakati wa majuma yale tukifanya kumbukumbu ya miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika.

Nimeunganisha hapa kukuambia kuwa yapo mengi ya kuzingatia hii leo kutoka historia kama hizi:

MIAKA 60 YA UHURU WA TANGANYIKA: KISA KILICHOWALIZA WANAWAKE WANNE PEMBENI YA JULIUS NYERERE WAKATI WA KUPIGANIA UHURU

''Kwa kuwa umependa kumbukumbu hizi za nyumbani kwetu Gerezani basi nataka nikupe kisa kilicholeta taharuki kubwa ambayo naelezwa haijapata kutokea katika historia ya TANU na Nyerere labda hadi Baba wa Taifa anaaga dunia.

Siku za mwanzo za TANU viongozi wake walikuwa wakiwa na jambo zito la kujadili walikuwa wakikutana nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu.

Walikuwa wakimaliza shughuli basi inakuwa chakula na vinywaji kujipongeza.
Siku hiyo baada ya kikao wakala chakula cha mchana.

Baada ya kula ghafla Nyerere akaanza kulalamika kuwa tumbo linamkata.
Nyerere akawa anajipindua huku na huku kwa maumivu.

Siku zote TANU walikuwa wakiishi chini ya hofu ya Nyerere kudhuriwa na maadui wa TANU lakini katika chakula kile cha nyumbani kwake hapakuwa na hofu kwani chakula chake kilikuwa kinatoka Kariakoo na kwa watu maalum ambao Market Master, Abdul Sykes akiwafahamu na Mzee Mshume na ndiye akikinunua, mpelekaji wa chakula hicho kwa Mama Maria alikuwa dereva wa TANU, Said Kamtawa maarufu kwa jina Said TANU.

Nyerere kalala kwenye kochi anaugulia na taharuki ikazuka na minong'ono haikuweza kukwepeka.

Nyerere kalishwa sumu!
Sumu Nyerere alishwe nyumbani kwa Abdul Sykes?

Uani jikoni walikuwa mama yake Nyerere Bi. Mgaya, Mama Maria, mama yake Abdul Sykes Bi. Mruguru bint Mussa, mkewe Abdul Sykes, Mama Daisy.

Bi. Mgaya hakuweza kustahamili alipoona wanaume ingia toka kule ndani.

Aliposikia kuwa Nyerere anaumwa baada ya kula chakula kitu cha kwanza kilichomjia ni kuwa mwanae kalishwa sumu akawa sasa mikono kichwani analia na kutembea ua mzima.

Bi. Mgaya anasema Kizanaki na anachanganya na Kiswahili.
Ikawa patashika nguo kuchanika kumtuliza.

Wote waliokula chakula kile walikuwa salama na hawa ni watu waliokuwa wakijuana vizuri na wakiaminiana mwisho wa imani.

Nani anaweza kupenya nyumbani kwa Abdul akampa sumu Nyerere?

Nani?

Mama Daisy ndiye alikua akinihadithia alipomaliza aliinamisha kichwa akasema, ''Mwanangu Mohamed, Abdul na Nyerere wametoka mbali sana na walikuwa zaidi ya ndugu.''

Iko siku nitakileta hapa kisa cha sanduku la fedha la Abdul Sykes kama nilivyokipokea kutoka kwa Bi. Mwamvua bint Mrisho maarufu kwa jina la Mama Daisy.

Picha ya kwanza ni mama yake Julius Nyerere Bi. Mugaya Nyag'ombe, Bi. Mruguru bint Mussa Mohamed mama yake Abdul Sykes, Ally na Abbas, Mama Maria Nyerere na Bi. Mwamvua bint Mrisho.''

Hivi ndiyo dunia ilivyo.
Mtu anaweza leo akawakejeli hawa wazee wetu apendavyo.

Hakuna wa kumzuia.

Leo ni zaidi ya miaka 70 imepita toka haya yatokee na aliye hai katika hawa ni Mama Maria Nyerere peke yake.

Namshuru Allah kuwa nimeihifadhi historia hii kwa sauti yangu nikihadithia yote na kwa kalamu yangu.

 
Ahsante sana, angalia hapo kati ya Thomas na David. Hajui tofauti ya hawa wawili na hataki kujifunza
Sasa kama unajua kuwa kuna mikutano ilifanyika Welfare kwa Hamza Mwapachu kwa nini ulitaka kutuaminisha kuwa mikutano yote ilifanyika kwa Abdul Sykes peke yake? Unajichanganya mwenyewe.
Tena alitumia neno ''yote'' hakuacha nafasi
Hataki kukubali kuwa Nyerere ali tranform chama kutoka Familia kuwa wanachama
Sijui ana uhakika gani kama hakukuwa na 'underground'' yeye anaamini zilikuwepo kwa Sykes tu
Kambona hakutendewa haki!
Ishara kubwa ya mtu aliye elimika ni kukubali kukosolewa, kurekebisha alichokiandika kama taarifa nyingine zitatokeza nakutambua kuwa anachojua yeye ni sehemu tu ya ukweli uliopo.
Mohamed hakubali kukosolewa na hapa inatia shaka sana. Moja ya kazi za academician ni kukubali kukosolewa, kukubali mitazamo tofauti na kukubali kukutokubaliana kwa heshima na adabu
Hizi habari za ''hawa wanifundishe, mimi nina.. ' ni grandiose zisizo na haiba ya 'academics'

Bado tunauliza, Salum Abdallah babu yake Mohamed Said alikuwa na cheo gani TRAU?
 
uliaFather of the nation legacy Yake inapotea hivi hivi View attachment 2064310View attachment 2064311View attachment 2064312
Dive,
Nakuwekea picha za Mwalimu ambazo nimeweza kuzikusanya katika utafiti wangu na kuandika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika nikienda nyuma sana miaka ya mwanzoni wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika.

Kuna yeyote anaejua historia za wazalendo hawa wake kwa waume atupe historia zao?:


Kulia Ali Msham na aliyekaa kwenye meza ni Mwalimu Julius Nyerere.


Kulia Julius Nyerere, John Rupia na Sheikh Suleiman Takadir na hao waliosimama nyuma ni Bantu Group wahamaishaji na walinzi wa viongozi wakiwa na silaha za jadi


Kulia Haruna Taratibu, Saadan Abdu Kandoro, Julius Nyerere,
Sheikh Mohamed Ramia na Idd Faiz Mafungo

Kulia Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bi. Titi Mohamed kushoto Bi. Titi bin Mzee na katikati Julius Nyerere wakimsindikiza safari ya kwanza UNO





 
Acha Umbea.

Unafikiri ni wewe tu mwenye kufahamu historia ya Upatikanaji wa Uhuru wa Tanganyika, akiandika mwingine eti anaokoteza.

Nitaanza kukukumbusha Uongo wako wote humu, hata ule wa idadi ya wabunge
 
Msaada wanaJF, kuna picha ya Salum Abdallah. Nani anajua huyu Mzee alikuwa na wadhifa gani TRAU?
 
So what, nawewe umeokoteza picha eeh

Chuo cha Kivukoni waliandika vizuri sana Historia ya TANU na upatikanaji wa Uhuru wa Tanganyika

Haya mengine ni kudhihirisha Udini wako tu, huku wapo wasomi wawezao kuchambua mambo kwa kina na kutathmini.
 
Msaada wanaJF, kuna picha ya Salum Abdallah. Nani anajua huyu Mzee alikuwa na wadhifa gani TRAU?
We we wee....!

Kuna jamaa alishamuuliza huyu Mzee hilo swali, Mzee atalikwepa mpaka mwisho, hebu atuwekee picha ya Baba yake na hasa akiwa hapo Ofisini TRAU.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Katika picha anazoleta Mohamed Said hapo juu hakuna mpya hata moja
Kila uzi anaweka picha hizo hizo, sasa mtu atajiuliza ni kwanini?

Jibu ni rahisi anatumia picha ni ''bamboozle'' yaani kama kiini macho pale hoja inapomfika pabaya

Kwa mfano, hutamuona akirudisha picha ya Babu yake Salum Abdallah kwavile tayari amebaini hana jibu ni upi wadhifa wa Mzee wake?

Pili anataka kufifisha hoja ya Fundi Mchundo kuhusu Thomas na David

Na mwisho amebaini Benz si deal wapo waliotumia nyakati hizo

Someni between the lines wanaJF, si kumeza tu! chambua mchele na mashudu
 
Mimi nilishamfahamu siku nyingi, kuna vitu anavikwepa sana na ndio maana hawezi kuquote maneno yangu KABISA na hadhubutu.

Btw, nasikia Baba yake alikuwa Mwl. wa Madrassat na akamfundisha hadi Nyerere Madrassa [emoji23]

Kwa Bahati mbaya JKN akabaki na Ukatoliki wake wakamchukia sana.
 
We we wee....!

Kuna jamaa alishamuuliza huyu Mzee hilo swali, Mzee atalikwepa mpaka mwisho, hebu atuwekee picha ya Baba yake na hasa akiwa hapo Ofisini TRAU.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Mumepatikana Na Nyerere wenu , vitabu vyenu vya kanisa vikimsifu Tu baada ya kumtumia Kama kibaraka wao. Mzee kawatolea ukweli mnakwenda mbio . Si mtunge vyengine vya kumsuta Mzee Mohammed mnalia Lia nini
 

Nani kawakataza kitabu chenu ?
Wasomaji tupo
 
Azarel na Jagina huu mjadala ni ' Civil and secular'' tafadhalini epukeni hoja za udini.
Uvumilivu ni kitu muhimu

Kinachojadiliwa hapa ni Historia.
 
Azarel na Jagina huu mjadala ni ' Civil and secular'' tafadhalini epukeni hoja za udini.
Uvumilivu ni kitu muhimu

Kinachojadiliwa hapa ni Historia.
Ni kitu gani mnachosema kuwa Mzee Mohammed ni mdini kwani Nyerere hakuwa mdini ?
 
KAMWE...!!!

This man was an Icon and he still is

The whole World knows and appreciate him

Ni waswahili wachache tu wakishalewa wali wa manjano wanakuja kuwehuka huku

😝😝😝😝😝
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…