23.10.2016: Toto Africa Vs Simba S.C

Naamini leo tunashinda,tena goli nyingi.Hata wakaze leo lazima waachie tu.
 
Naamini leo tunashinda,tena goli nyingi.Hata wakaze leo lazima waachie tu.
Mkuu.. Machinjioni wanatokaje?! Leo tunawapatia full dose, ili wakawasimulie na wenzao.
 
Kikosi cha Simba S.C kinachoanza leo;

1. Vicent Angban
2. Javier Bukungu
3. Mohamed Hussein
4. Method Mwanjale
5. Juuko Murshid
6. Jonas Mkude
7. Muzamiru Yassin
8. Mwinyi Kazimoto
9. Frederic Blagnon
10. Mohamed Ibrahim
11. Shiza Kichuya

SUB: Denis (GK), Hamadi Juma, Novatus Lufunga, Jamal Mnyate, Said Ndemla, Ibrahim Ajibu na Laudit Mavugoal.
 
haya yatakuwa maajabu ya dunia, yaani tutafune MBAO ngumu za mpingo tushindwe kula pilau????

huu utakuwa ujinga sasa!
Mechi imeanza?
Kama imeanza matokeo please
 
Dakika ya 24: Simba wanafanya shambulizi kali,Blagnon anabaki yeye na kipa lakini anababaika na kuupaisha mpira baada ya kutokea kugongana kwa wachezaji wa Simba.

Dakika ya 19: Simba wanapata kona baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Mohamed Ibrahim, Kichuya anapiga kona lakini inaokolewa.
 
Dakika ya 27: Toto wanafanya shambulizi kali, Lusajo anashindwa kutumia nafasi baada ya kubabaika akiwa mbele ya lango la Simba.

Dakika ya 26: Simba wanapata kona nyinfine, Kichuya anapiga lakini inaokolewa.
 
Reactions: PNC
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…