23% tu ya wanafunzi ndiyo wanamudu lugha ya kiingereza kidato cha kwanza sekondari

23% tu ya wanafunzi ndiyo wanamudu lugha ya kiingereza kidato cha kwanza sekondari

SASA TUKIWAAMBIA WALIMU KUWA WAJIONGEZA WANATUPIGA MAJUNGU


WALIMU WA KIIINGEREZA NI KICHEKESHO
 
Hivi mlishawahi kukaa na kujadiri maslahi ya hawa waalimu?
Mwalimu analipwa 300k per month jumlisha mfumuko wa bei na hali mbaya hii ya maisha mnafikiri huo umahili atautoa wapi?
Mbunge ambaye elimu yake ni darasa la saba analipwa mil 12 na posho za vikao juu, lakini mwalimu mwenye diploma analipwa 400k na mnamuandama huyu mwalimu aongeze ufanisi autoe wapi?
Hakuna mwalimu anayelipwa kiasi hicho.
Una lengo la kupotosha umma kwa maslahi yako.
 
Unategemea mtoto kwenye foundation level (shule za msingi)

Na mbaya zaidi waalimu lugha ya taifa ya Kiswahili pia hawaimudu vilivyo, hivyo kufundisha kuhesabu, hisabati, kuandika maneno sanifu ya kiswahili n.k pia ni mtihani mkubwa maana lugha ya kiswahili wanayoitumia waalimu inashindwa kuleta mantiki kirahisi ktk bongo za watoto.
 
Na mbaya zaidi waalimu lugha ya taifa ya Kiswahili pia hawaimudu vilivyo, hivyo kufundisha kuhesabu, hisabati, kuandika maneno sanifu ya kiswahili n.k pia ni mtihani mkubwa maana lugha ya kiswahili wanayoitumia waalimu inashindwa kuleta mantiki kirahisi ktk bongo za watoto.
Ndio iko hivyo mwisho wa siku wanalaumiwa watoto kuwa wanafeli. Hatari sana.
 
Hakika ndivyo ilivyo...

Tatizo ni mfumo mzima wa elimu yetu unaobebwa na msingi wa lugha..

Nenda shule zetu za sekondari iwe za mjini au vijijini, ambako tunaambiwa lugha ya kufundishia ni Kiingereza, lakini cha ajabu ni kuwa language competence ya walimu hawa kwa zaidi ya 90% iko below average.

Yaani kwa lugha rahisi na ya moja kwa moja ni kuwa, walimu hawa hawamudu kabisa lugha ya kiingereza kiasi cha kupewa nafasi ya kufundisha wengine na wengi wa walimu hawa eti ni university graduates..

Na maana yake ni kuwa tatizo hili lipo kuanzia huku chini kwenye grassroots (kindergarten & primary school levels) mpaka huko University level...

Na huko kindergarten & primary school level, hakuna walimu competent wa lugha ya lugha ya kiingereza...!!
Tatizo la kiingereza ni lakitaifa ,watanzania hata baadhi ya malecturers hawapo vizuri kwenye ngeli
 
Huwezi ukasoma shule za Tz Hadi chuo kikuu ukaelewa kingereza kwa ufasaha , sisi baadhi yetu tulisoma Uganda ndo tumeweza kidogo kuongea kimalkia
Uongo

Tanzania watoto kibao English medium.za Tanzania wa chekechea ns Primary wanaongea kingereza kilichonyooka kibao
 
lugha ya kiswahili ibaki kama somo katika ngazi zote za elimu
 
Hata waalimu watanzania 10% hawamudu lugha ya kiingereza itakua je kwa wanafunzi iwe 23% wewe pitia mashuleni usikilize kiingereza cha hao waalimu.
... mwalimu mmoja anafundisha utitiri wa watoto. By the way, hiyo 23% ya wanaomudu kiingereza booster ni English medium schools otherwise ingekuwa 3%!
 
Huwezi ukasoma shule za Tz Hadi chuo kikuu ukaelewa kingereza kwa ufasaha , sisi baadhi yetu tulisoma Uganda ndo tumeweza kidogo kuongea kimalkia
Waliosoma Tz miaka ya 50, 60 na robo 70 walikimudu vizuri kiingereza kabla siasa za kijinga za ujamaa hazijaingia nchini.
 
Kujua kuzungumza lugha na ku Imaster vizuri ni mchakato unaoanzia nyumbani unaenda shuleni nk,

Mfumo wetu tulio wengi si rahisi kuimaster lugha hii ya 3 vizuri,

Mfano watoto wa vijijini huko huwa wanaanza na lugha mama,alafu kiswahili kwa taabu,tena wengi wao kiswahili kinaanza ukiwa darasa la 4 huko,na kumbuka kuwa kiswahili kinazungumzwa na jamii kubwa,

Sasa unakuja kumsuprize na lugha ya watu ambayo inampasa aikariri kwa muda wa dk 80 za ufundishaji,Then kwingine huko aendelee na lugha yake kunakuelewa hapo0?

Na sio wanafunzi wa sekondari tu,nenda mpaka wanafunzi wa vyuo vikuu wengi tu,kizungu ni tatizo

Sln, Kama tunahitaji watoto waongee au wapate idea ya kizungu Tuanze na awali huko na sio darasa la 3 kama sasa,iwekwe mikakati ya kiushindani na ki motisha kuhakikisha juhudi binafsi za kusoma lugha zinafikiwa

Sent from my SM-G950F using JamiiForums mobile app
 
Umahiri wa kiingereza ni tatizo la kitaifa hata kwenye ualimu kuna nafuu sana bcoz kiingereza chao ni chakufundishia but in fluent speaking specifically kwenye maongezi ya kawaida nakubali hawako mahiri but ulishawahi kuwasikia mawaziri wetu wakiongea kiingereza tena wengine wana mpaka PhD
Mimi nimewahi kusikia wakiongea, kina Joyce Ndalichako, Jpm etc. Mbona kiingereza kizuri tuu? 🤣🤣🤣
 
Serikali ibadilishe mitaala iwe ya Kiingeleza na Kiswahili....

Lugha ya kufundishia iwe kingereza toka chekechea hadi chuo kikuu.

Kiswahili kifundishwe kama somo toka chekechea hadi form six.

Tatizo kuna walimu kiduchu sana wa kiingereza.

Kung’ang’ania kiswahili kwa sababu za kizalendo ishapitwa na wakati.
Hata hivyo uzalendo wa kweli hakuna, ni mtindo wa unafiki, uongo na ufisadi umejaa.
 
Anayo point ya msingi sana, wataalamu wanasema kuna umri fulani wa mtoto ambapo ni rahisi zaidi kujifunza lugha. Kiingereza kifundishwe na wabobezi kwenye kipindi hicho (chekechea mpaka darasa la tatu)
Hili mimi nililiona mapema nikapeleka mtoto shule ambayo hataongea kiswahili mpaka likizo. Leo hii anashuka ngeli kama maji tu shwaaaa. Wakati baba yake the the the kibao. Uko sahihi
 
Tatizo la kiingereza ni lakitaifa ,watanzania hata baadhi ya malecturers hawapo vizuri kwenye ngeli
Kimsingi hili ni Tatizo la Kujitakia. Ni upumbavu na utumwa kuendelea kung'ang'ania kutumia Kigeni kutolea maarifa.

Ni utumwa!
 
Hivi mlishawahi kukaa na kujadiri maslahi ya hawa waalimu?

Mwalimu analipwa 300k per month jumlisha mfumuko wa bei na hali mbaya hii ya maisha mnafikiri huo umahili atautoa wapi?

Mbunge ambaye elimu yake ni darasa la saba analipwa mil 12 na posho za vikao juu, lakini mwalimu mwenye diploma analipwa 400k na mnamuandama huyu mwalimu aongeze ufanisi autoe wapi?
Nakubaliana na wewe kuwa Walimu wanalipwa mshahara kidogo sana.
Lakini kwa mfano mwalimu ambaye si mahiri wa kingereza, hata ukimlipa milioni moja atamudu hiyo lugha?!

Tatizo limetengenezwa na utaratibu wa kuchukua wanafunzi waliofeli au ambao hawakufanya vizuri sana kusomea kozi ya ualimu.
 
Back
Top Bottom