23% tu ya wanafunzi ndiyo wanamudu lugha ya kiingereza kidato cha kwanza sekondari

23% tu ya wanafunzi ndiyo wanamudu lugha ya kiingereza kidato cha kwanza sekondari

Lugha ya kufundishia iwe kingereza toka chekechea hadi chuo kikuu.

Kiswahili kifundishwe kama somo toka chekechea hadi form six.

Tatizo kuna walimu kiduchu sana wa kiingereza.

Kung’ang’ania kiswahili kwa sababu za kizalendo ishapitwa na wakati.
Hata hivyo uzalendo wa kweli hakuna, ni mtindo wa unafiki, uongo na ufisadi umejaa.
Mimi nasema HAPANA..

Lugha ya kufundishia iwe hii tunayoita "LUGHA YA TAIFA" yaani KISWAHILI...

Honestly, Mimi nilishashindwaga kuelewa kwanini hasa tunaogopa kutumia lugha yetu ya Kiswahili tunayoielewa kutolea ElLIMU (yaani UJUZI na MAARIFA) kwa watoto wetu...

Lugha ya Kiingereza iwe ni somo la kawaida na mtu akitaka kuimudu, atumie bidii yake kujifunza....

Lakini MAARIFA na UJUZI yahamishwe toka kizazi hata kizazi kwa lugha inayoeleweka na pande zote mbili, yaani atoaye na apokeaye hayo maarifa na ujuzi...

Taifa lolote lililopuuza na kudharau component muhimu ya "lugha" kama sehemu ya utamaduni wake na kuuenzi utamaduni huo, lisahau milele kukua kisayansi na kiteknolojia na kisha kimaendeleo...!!

Tujifunze kwa nchi kama China, Japan, Ubelgiji, Korea, Urusi na zingine nyingi huko duniani wanaotumia lugha zao kutolea elimu. Mengi yamezagaa dunia nzima yakijenga mabarabara, madaraja, yaki - operate viwanda vya kila aina nk lakini mengi ya haya mamtu hata Kiingereza hayakijui...!!!

Tuwe tunapenda au hatupendi, sisi kama Taifa la bado tuko kwenye "ukoloni mamboleo wa lugha ya Kiingereza" na kwa maana hiyo, lugha ni kikwazo kikubwa cha kushindwa kwetu kupiga hatua za haraka za maendeleo ya sayansi na teknolojia hapa nchini kwetu...!!

Kosa lilifanyikaga toka mwanzo wa kuwekwa kwa misingi ya Taifa hili. Hayati Mwl Julius K. Nyerere na waasisi wenzake wa Taifa hili walikosea sana kutuwekea lugha mbili za kutolea elimu. Wangeamuaga tu toka mwanzo kuwa aidha iwe KIINGEREZA a KISWAHILI kuanzia chini mpaka juu. Lakini kwa mbili, it was a big mistake...

Hata hivyo, tunaweza kurekebisha sasa makosa hayo...!!
 
Mwanza, Tanzania

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - Elimu - wizara ya TAMISEMI Dr. Charles Enock Msonde na Dr. Lyabwene Mtahabwa - kamnishna wa elimu kutoka wizara ya elimu wahimiza waalimu wa darasa la kwanza na darasa la tatu shule ya msingi wawe mahiri ktk masomo yao huku vigezo vya lazima kwa waalimu viwe digrii yenye matokeo ya daraja la ufaulu wa juu vya elimu ya juu ya Chuo Kikuu
video : source : millard ayo

Habari hiyo muhimu juu ya yanayojiri katika hatua za kujaribu kuleta Mapinduzi ya elimu yalifahamika katika mkutano wa maafisa elimu wa mikoa na halmashauri kuhusu njia gani zitumike kubadili hali hiyo ya sasa hasa ktk kuwajengea msingi imara wa uwezo wa masomo ya kuhesabu, kuandika, hisabati, lugha ya taifa kiswahili na lugha ya kigeni kwani katika umri huo mdogo wa darasa la kwanza na la tatu katika elimu ya msingi ndiyo itawajengea msingi mzuri wa kielimu kwenda mbele.

N.B
Waalimu wengi wa chekechea na shule za msingi nchi za Scandinavia na Ulaya huwa na elimu za Ph.D na masters ili kuwajenga watoto wadogo vizuri kuelimu

Duh nimesoma CV ya huyo mwamba kweli yuko nondo....sounds kama ameokoka hivi... may God Bless him!
 
Hivi mlishawahi kukaa na kujadiri maslahi ya hawa waalimu?

Mwalimu analipwa 300k per month jumlisha mfumuko wa bei na hali mbaya hii ya maisha mnafikiri huo umahili atautoa wapi?

Mbunge ambaye elimu yake ni darasa la saba analipwa mil 12 na posho za vikao juu, lakini mwalimu mwenye diploma analipwa 400k na mnamuandama huyu mwalimu aongeze ufanisi autoe wapi?
Mkuu acha tu [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Wanataka iwe kiswahili hadi chuo kikuu hapo hapo mwanafunzi ajue kingereza. Hii nchi ngumu sana kuielewa.
 
Si mbaya kwa sababu tunakwenda kutumia kiswahili kuanzia chekechea hadi vyuo vikuu. so hao 77% wasiojua kiingeleza tuwaache tu wametuwahi kujua lengo letu.
 
Kimsingi hili ni Tatizo la Kujitakia. Ni upumbavu na utumwa kuendelea kung'ang'ania kutumia Kigeni kutolea maarifa.

Ni utumwa!
mbona mwanao unamsomesha FM Academia? acheni unafiki.
 
Usikariri bos sku english medium zipo mpaka vijijini
Hizo medium unazozisema wewe mwenyewe unajua kabisa sifa za kusoma hizo shule ni uwe na kipato. Kuwa kijijini haina maana zinafundisha wanakijiji wote waliopo hapo.
 
Kwenye daladala wanafunzi wanajadili walichosoma shuleni kwa kiswahili na neno mojamoja la kiingereza linatamkwa kiaina. Kweli tuna shida na lugha ya malkia.
 
Tujifunze kwa nchi kama China, Japan, Ubelgiji, Korea, Urusi na zingine nyingi huko duniani wanaotumia lugha zao kutolea elimu.

Tuwasikilize hawa wanataaluma wawili Dr. Charles Enock Msonde naibu katibu mkuu TAMISEMI sekta ya elimu na kamishna wa elimu wa wizara ya Elimu Dr. Lyabwene Mtahabwa kusisitiza umuhimu wa kiingereza katika kupata elimu yenye maarifa mapana maana kiswahili kina maneno machache yanayobeba dhama maalum ya sayansi, sheria, utabibu, fizikia ndiyo maana lugha kubwa duniani zimekopa maneno ya maeneo ya kitaaluma, sayansi n.k toka lugha za Kigiriki, kilatini.

Tujiulize je kiSwahili mbali ya kuwa lugha iliyonikita zaidi ktk maeneo machache tu kama kuwezesha Mawasiliano mepesi na kutumika katika mashairi na tenzi.

Je lugha ya kiswahili na mapungufu yake haya inaweza kutumika kama lugha za Mandarini, Kijapani, Kingussie kufundisha utabibu, bailojia, fizikia, molekula, uhandisi, uwakili, internal medicine, Nishati ya Nuklia n.k

Mfano masuala haya kweli yanaweza yanafundishika ktk kiswahili kwa sasa upande wa utabibu / uganga na ukapikika kitaaluma ?


  • Medical cell biology and genetics.
  • Pathological processes.
  • Health behaviours, musculoskeletal, respiratory and digestive systems.
  • Evidence based medicine and research methods.
  • Clinical procedural skills.
  • Ethics and law in clinical practice.
  • Mechanisms of drug action.
  • Biology of disease
 
Tanzania ni taifa la watu wasiojielewa. Bungeni wanaendsha mijadala kwa kiswahili, wananchi wanaongea kiswahili, inakuaje watoto wetu wafundishwe Kwa lugha ya kigeni?! Prof. Mkenda, waziri wa elimu twambie inakuaje watoto wetu wanafundishwa Kwa lugha ya kigeni, inakuaje? Tutaendelea kuwa watumwa wa lugha za kigeni mpaka lini?
 
Waalimu wamelinganisha % na Ile 23% ya mchongo ongezeko la mishahara.
 
Tuwasikilize hawa wanataaluma wawili Dr. Charles Enock Msonde naibu katibu mkuu TAMISEMI sekta ya elimu na kamishna wa elimu wa wizara ya Elimu Dr. Lyabwene Mtahabwa kusisitiza umuhimu wa kiingereza katika kupata elimu yenye maarifa mapana maana kiswahili kina maneno machache yanayobeba dhama maalum ya sayansi, sheria, utabibu, fizikia ndiyo maana lugha kubwa duniani zimekopa maneno ya maeneo ya kitaaluma, sayansi n.k toka lugha za Kigiriki, kilatini.

Tujiulize je kiSwahili mbali ya kuwa lugha iliyonikita zaidi ktk maeneo machache tu kama kuwezesha Mawasiliano mepesi na kutumika katika mashairi na tenzi.

Je lugha ya kiswahili na mapungufu yake haya inaweza kutumika kama lugha za Mandarini, Kijapani, Kingussie kufundisha utabibu, bailojia, fizikia, molekula, uhandisi, uwakili, internal medicine, Nishati ya Nuklia n.k

Mfano masuala haya kweli yanaweza yanafundishika ktk kiswahili kwa sasa upande wa utabibu / uganga na ukapikika kitaaluma ?


  • Medical cell biology and genetics.
  • Pathological processes.
  • Health behaviours, musculoskeletal, respiratory and digestive systems.
  • Evidence based medicine and research methods.
  • Clinical procedural skills.
  • Ethics and law in clinical practice.
  • Mechanisms of drug action.
  • Biology of disease
Hakuna Lugha Isiyojitosheleza duniani, na Hakuna Lugha iliyo juu ya nyingine duniani.
Ni ukoloni tu na utumwa unaojaribu kupandikiza kasumba hasi juu ya Lugha Fulani na chanya kwa Lugha nyingine.
 
Tanzania ni taifa la watu wasiojielewa. Bungeni wanaendsha mijadala kwa kiswahili, wananchi wanaongea kiswahili, inakuaje watoto wetu wafundishwe Kwa lugha ya kigeni?! Prof. Mkenda, waziri wa elimu twambie inakuaje watoto wetu wanafundishwa Kwa lugha ya kigeni, inakuaje? Tutaendelea kuwa watumwa wa lugha za kigeni mpaka lini?
Kingereza ni muhimu mno ni muhimu mno mno na mno
 
Hakuna Lugha Isiyojitosheleza duniani, na Hakuna Lugha iliyo juu ya nyingine duniani.
Ni ukoloni tu na

Inabidi lugha ya kiSwahili ifanyiwe namna ili iweze kwenda na hitaji hilo la kutumika kama lugha ya kufundishia vyuo vikuu.

Wataalamu wakusanyike na kukisuka kiswahili kwa ajili ya kufundishia masomo yote ya elimu ya juu na zoezi hilo litachulua miaka angalau 10 kama kweli kutakuwepo juhudi za dhati kabisa kiSwahili kiwe ktk viwango kama vya lugha ya Kifaransa, Kiingereza, Mandarin n.k

Fizikia ya Nyuklia:

Module 1: (BAS) will be devoted to the basic knowledge required on general Physics, and Complementary/Interdisciplinary courses adapted to the chosen path (notably atomic and plasma physics, quantum mechanics, computing and numerical methods, basic nuclear physics, basic lab in nuclear physics). These courses will be concentrated in the first semester, and include topics as Advanced Quantum Mechanics, Structure of Matter, Basic Nuclear Physics: theory and laboratory and Computing and Numerical Methods.

Module 2: allows students to follow 3 paths: Experimental/large accelerators (EXP), Theoretical (THEO), or Applied/small accelerators (APP). This module will give the specialized focus of the Master curriculum towards fundamental or applied nuclear physics. Fundamental physics includes either an experimental or a theoretical focus. Applied physics is especially focussed on biomedical applications, but also includes fundamentals in accelerators technology, archaeometry, monitoring ....
 
Sln, Kama tunahitaji watoto waongee au wapate idea ya kizungu Tuanze na awali huko na sio darasa la 3 kama sasa,iwekwe mikakati ya kiushindani na ki motisha kuhakikisha juhudi binafsi za kusoma lugha zinafikiwa
Hii ndo sln...

Ila si kwa nchi hii.. Watu masaa ishina nne wanawaza kuibia nchi..
 
Kosa lilifanyikaga toka mwanzo wa kuwekwa kwa misingi ya Taifa hili. Hayati Mwl Julius K. Nyerere na waasisi wenzake wa Taifa hili walikosea sana kutuwekea lugha mbili za kutolea elimu. Wangeamuaga tu toka mwanzo kuwa aidha iwe KIINGEREZA a KISWAHILI kuanzia chini mpaka juu. Lakini kwa mbili, it was a big mistake...
✔️✔️
 
Back
Top Bottom