23% tu ya wanafunzi ndiyo wanamudu lugha ya kiingereza kidato cha kwanza sekondari

23% tu ya wanafunzi ndiyo wanamudu lugha ya kiingereza kidato cha kwanza sekondari

Hata waalimu watanzania 10% hawamudu lugha ya kiingereza itakua je kwa wanafunzi iwe 23% wewe pitia mashuleni usikilize kiingereza cha hao waalimu.
Tema mate chini, sio 10%, ni 7% ndio wanamudu kiingereza tena sio kile fasaha bali ni kile cha kigugumizi chenye the the the. Mbaya zaidi hata Udsm kuna lecturer wengi tu viingereza vyao vimepindapinda sana, imagine PhD hamfikii kijana wangu wa Form 3.

Tukitaka tuwe wazuri ktk lugha basi tukubali kiingereza kifundishwe kuanzia std 1 . Shida hao walimu watatoka wapi!!? Labda tuagize Kenya na Uganda .

Dr......wa Udsm usiwe na wasiwasi siwezi kukutaja humu kuwa kiingereza chako ni cha kuungaunga, japo ulinisumbua sana nusu ni rudie mwaka
 
. Shida hao walimu watatoka wapi!!? Labda tuagize Kenya na Uganda .

Naunga mkono wakati huu wa mpito kukazania lugha ya kigeni Tanzania ipande basi serikali iajiri waalimu toka nchi jirani ulizotaja pamoja na za Malawi, Zambia, Zimbabwe kwa wingi kisha baada ya miaka 20 ya mkakati huu nchi itakuwa na watanzania mahiri ktk lugha hiyo ya kigeni ktk nyanja / kada zote za jamii ikiwemo waalimu wa shule zote za kata / serikali na private za chekechea msingi, sekondari na wahadhiri wa vyuo vikuu.


Hili linawezekana maana mfano nchi ya Rwanda imefanikiwa kubadili kutoka lugha ya kiFaransa tu na kuongeza umahiri wa matumizi ya lugha ya Kiingereza katika shule na vyuo vya elimu ya Juu.

Rwanda kuwa na lugha nne zinazofundishwa shuleni

"Haina maana lugha hii haikuwepo na wala haina uhusiano wa kuchaguliwa kwa Waziri Mushikiwabo hapana huo ni uzushi mtupu na ndiyo maana tunasema tunaimarisha. Kuimarisha maana yake ni unaimarisha kitu ambacho kilikuwepo. Jjitihada hizi ni mojawapo ya mchakato mzima wa kutathmini jinsi lugha zinavyofundishwa kuanzia kule chini."

Lakini wanafunzi wa shule ya sekondari ya Lycee de Kigali jijini Kigali wametoa maoni tofautitofauti. Mmoja amesema "Masaa ya kujifunza kifaransa yalikuwa machache ikiliganishwa na yale ya kiingereza." mwenzake mwengine naye ameongeza akisema:

"Ilikuwa haitoshi kwa muda tuliokuwa tunajifunza lakini kwa vyovyote tulijitahidi kuzingatia hayo tulokuwa tunafundishwa."

Kwa uamuzi huu sasa ni dhahiri kwamba lugha nne za Kiswahili, Kingereza, Kifaransa na Kinyarwanda zitakuwa zinafundishwa kwa kiwango sawa nchini Rwanda hali inayowapa wanafunzi fursa kwenye lugha hizi muhimu ulimwenguni ..... Soma zaidi Azma ya Rwana : Rwanda kuimarisha lugha ya Kifaransa – DW – 25.10.2018

Kipindi cha Ukoloni
Nchi ya Rwanda ilitawaliwa na watawala wawili wa kikoloni: Mjerumani kuanzia mwaka 1898 – 1916 na Mbelgiji kuanzia mwaka 1916 – 1962. Serikali hizi mbili kila moja ilikuwa na uamuzi wa kipekee kuhusiana na lugha ya Kiswahili pamoja na lugha nyingine nchini Rwanda. Uamuzi huo ndiyo msingi wa kuwapo au kutokuwapo kwa utashi wa kisiasa katika kipindi hiki.
3.1.1 Wakati wa Utawala wa Wajerumani
Mtawala huyu ndiye aliyeitumia lugha ya Kiswahili kwa mara ya kwanza kama lugha rasmi na lugha ya utawala nchini Rwanda (Kimenyi, 2003; MINEDUC, 2010; Niyibizi, 2014). Hii haina maana kwamba Kiswahili kililetwa Rwanda kwa mara ya kwanza na Wajerumani kwani lugha ya Kiswahili ilikuwapo nchini humo hata kabla ya utawala wa Wajerumani. Hii ni kutokana na ukweli kwamba misafara ya biashara kutoka pwani ya Afrika Mashariki ilifika Rwanda na nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Kongo kabla ya utawala wa Mjerumani (Niyibizi, 2014).
Kutokana na Kiswahili kuwa lugha rasmi na lugha ya kiutawala, shule nyingi katika kipindi hiki zilifundisha lugha ya Kiswahili na masomo mengine (Republic of Rwanda, 1999; Kimenyi, 2003)3. Lugha za Kiswahili na Kijerumani ndizo pekee zilizofundishwa kama somo katika shule ya kwanza kabisa nchini Rwanda iliyojulikana kama Shule ya Nyanza. Shule hii ilianzishwa na Wajerumani katika eneo la Nyanza kwenye Jimbo la Kusini (Niyibizi, 2014). Utashi wa kisiasa wa utawala wa Wajerumani unaonekana katika kuipangia lugha ya Kiswahili dhima maalumu. Pia serikali hii ya kikoloni ilishiriki katika kuongeza idadi ya watumiaji wa lugha ya Kiswahili nchini humo. Hili lilifanyika kwa kuhakikisha kuwa Kiswahili kinafundishwa pia katika shule zilizokusudiwa kwa ajili ya watoto wa viongozi. Jitihada hizi ziliifanya lugha ya Kiswahili kupata hadhi kubwa miongoni mwa watumiaji wake na jamii yote kwa ujumla katika koloni hili la Mjerumani. Utashi huu wa kisiasa uliopendelea lugha ya Kiswahili ulichochewa zaidi na Rwanda kuwa sehemu ya koloni la Mjerumani la Afrika Mashariki. Katika makoloni mengine, hususan Tanganyika, lugha ya Kiswahili ilikuwa imestawi zaidi na hivyo kumlazimisha Mjerumani aitumie kama lugha ya utawala na mawasiliano rasmi.
3.1.2 Wakati wa Utawala wa Wabelgiji
Baada ya Vita vya Kwanza vya Dunia, Mjerumani alipoteza himaya zake. Hii ilitokana na kushindwa vita. Hivyo, Rwanda ilikoma kuwa chini ya utawala wa Wajerumani baada ya vita hivi, na utawala wa Ubelgiji ukachukua nafasi. Mfalme wa Ubelgiji akawa mtawala mpya wa Rwanda kuanzia mwaka 1916 – 1962. Mabadiliko haya yalikuwa na athari kubwa kwa lugha ya Kiswahili. Athari hiyo ilitokana na marufuku iliyowekwa dhidi ya lugha ya Kiswahili. Marufuku hii ilihusu kukataza lugha ya Kiswahili kutumika kama lugha rasmi na lugha ya utawala. Kufikia mwaka 1929, Kiswahili kiliondolewa kuwa lugha ya kufundishia katika shule za msingi na sekondari. Hoja hii inadhihirishwa na Ntawigira (1997) kama anavyonukuliwa na Kimenyi (2003: 4) akisema:
Mnamo mwaka wa 1929 Kiswahili kilifutwa kama lugha ya kufundishia katika shule za msingi na zile za upili… Mnamo mwaka 1929, mkaguzi wa ufundishaji wa kikoloni kutoka Leopordiville (Kinshasa), alisema kwamba hakukuwepo fursa ya kuendelea kutumia Kiswahili.
Dondoo hili linaonesha namna Wabelgiji walivyoshiriki kurudisha nyuma ustawi mkubwa wa lugha ya Kiswahili uliokuwa umefikiwa katika kipindi cha utawala wa Wajerumani. Dondoo hili pia linaonesha kwamba ndani ya miaka 13 ya utawala wao Wabelgiji waliweza kukiondoa Kiswahili kama lugha ya kufundishia. Je, kwa nini utawala wa Wabelgiji ulikosa utashi wa kisiasa wa kustawisha Kiswahili nchini Rwanda?
Marufuku hii inaweza kutokana na mambo mawili. Jambo la kwanza ni kutaka kuonesha kwa vitendo mabadiliko ya kiutawala. Hivyo huenda ilikusudiwa kuonesha kuwa sasa kuna mabadiliko ya kiutawala ili kuleta utii zaidi kwa utawala mpya. Utaratibu huu wa mabadiliko ya lugha, kupitia sera za lugha, umejitokeza katika nchi nyingi, kwa nia ya kujitenga na kale na kujenga taswira mpya ya mwanzo mpya (Steflja, 2012). Jambo la pili linahusiana na kuihusisha au kuifungamanisha lugha ya Kiswahili na dini ya Kiislamu (Bujra, 2002). Wabelgiji kwa kiwango kikubwa walifungamana na dini ya Kikristo, hususan madhehebu ya Kikatoliki. Jambo hili lilitosha kuwa sababu ya msingi ya kuipiga marufuku lugha ya Kiswahili.
Baada ya Kiswahili kuondoshwa katika mfumo wa elimu, Kifaransa kilipewa hadhi ya juu na kuwa lugha rasmi na lugha ya kiutawala. Lakini pia kilianza kutumika kama lugha ya kufundishia katika shule (taz. Niyibizi, 1980 katika Niyirora, 2013:5). Hivyo lugha ya Kiswahili ilianza kupoteza hadhi yake na ilianza kutumiwa na watu duni au watu wa chini kama vile Waislamu, vibarua, na wafanyabiashara (Kimenyi, 2003). Waislamu katika kipindi cha utawala wa Wabelgiji walikuwa katika kipindi kigumu kutokana na Uislamu wao. Hawakupata fursa ya kupata elimu na hivyo kukosa kuajiriwa katika kazi mbalimbali za serikali ambazo zilionekana kuwa na hadhi ya juu. Kutokana na matumizi ya Kiswahili kushamiri miongoni mwa Waislamu, ambao walitazamwa kama watu duni, lugha ya Kiswahili pia ikajikuta ikitazamwa kama lugha duni.
Sababu nyingine ya kushuka kwa hadhi ya Kiswahili ni ukatili wa “Abasemyi” (Wanyarwanda wachache waliokuwa na uwezo wa kuzungumza lugha ya Kiswahili). Watu hawa walitumiwa na watawala wa Kibelgiji kama wakalimani kufanikisha mawasiliano kati ya watawala na wenyeji. Wakalimani hawa walitumiwa na Wabelgiji kuanzia mwaka 1916 hadi 1919. Katika kipindi hiki, walijipatia utajiri mkubwa kutokana na marupurupu yao; pia, walijihusisha katika kuwapiga na kuwaibia raia (Republic of Rwanda, 1999). Hivyo basi, kwa mazingira haya ilikuwa ni rahisi lugha ya Kiswahili kuhusishwa na unyang’anyi. Kutokana na uamuzi wa kimakusudi wa serikali ya Wabelgiji kuhusiana na sera ya lugha, lugha ya Kiswahili haikupata nafasi ya kustawi. Ijapokuwa Kiswahili kiliendelea kuwapo Rwanda kutokana na Uislamu, biashara, na kuzungukwa na watumiaji wa lugha ya Kiswahili, kipindi hiki kinatajwa kama kipindi cha udumavu wa Kiswahili nchini humo.
 
Mwanza, Tanzania

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - Elimu - wizara ya TAMISEMI Dr. Charles Enock Msonde na Dr. Lyabwene Mtahabwa - kamnishna wa elimu kutoka wizara ya elimu wahimiza waalimu wa darasa la kwanza na darasa la tatu shule ya msingi wawe mahiri ktk masomo yao huku vigezo vya lazima kwa waalimu viwe digrii yenye matokeo ya daraja la ufaulu wa juu vya elimu ya juu ya Chuo Kikuu
video : source : millard ayo

Habari hiyo muhimu juu ya yanayojiri katika hatua za kujaribu kuleta Mapinduzi ya elimu yalifahamika katika mkutano wa maafisa elimu wa mikoa na halmashauri kuhusu njia gani zitumike kubadili hali hiyo ya sasa hasa ktk kuwajengea msingi imara wa uwezo wa masomo ya kuhesabu, kuandika, hisabati, lugha ya taifa kiswahili na lugha ya kigeni kwani katika umri huo mdogo wa darasa la kwanza na la tatu katika elimu ya msingi ndiyo itawajengea msingi mzuri wa kielimu kwenda mbele.

N.B
Waalimu wengi wa chekechea na shule za msingi nchi za Scandinavia na Ulaya huwa na elimu za Ph.D na masters ili kuwajenga watoto wadogo vizuri kuelimu

Bado wapo pale pale tuuu ! Wabadilishe kwanza namna zinavyo patikana degree huko vyuoni ili kuwe na degree zenye tija

Lakini pia ambacho hawakijui ni kwamba ufahuru mkubwa sio kigezo kikubwa sana katika kumfanya mtoto aelewe, cha msingi mwalimu anauwezo wa kufundisha na watoto wakafundishika? Pili jee? Watoto wenyewe katika makuzi na malezi yao wana lelewa katika misingi ya kufundishika kirahisi ,

Ni upumbavu na ujinga msomi kabisa wa daraja lake kuchukua nchi za scandinavia kama case study na kutaka ya scandinavia yawe aplied huku ambako hadi sasa watoto wanatoka katika familia ambazo hata uhakika wa kula mlo wa siku moja hawana , anatembea over 7kms kwenda shule tena na kandambili rangi tofauti,

Hebu tuache .huu ujinga kulinganisha nchi zilizo endelea zilizo weza kukabiliana na over population ili kumudu provision of social services na kinchi kama tanzania ambacho tunazaliana kama panya wakati ni maakini

hawa ma professor hawa hebu watupishe kwanza maana kwanza unaweza kukuta tangu azaliwe hajawahi hata kunya porini au hata choo cha shimo hivyo wanadhani watanzania wote wana enjoy maisha kama wapi upanga na oysterbay
 
Umahiri wa kiingereza ni tatizo la kitaifa hata kwenye ualimu kuna nafuu sana bcoz kiingereza chao ni chakufundishia but in fluent speaking specifically kwenye maongezi ya kawaida nakubali hawako mahiri but ulishawahi kuwasikia mawaziri wetu wakiongea kiingereza tena wengine wana mpaka PhD
Mawaziri wenyewe stress tupu hahahaa nakumbuka kile kingereza cha joyce ndalichako 🤣🤣🤣🤣🤣
 
Tuwasikilize hawa wanataaluma wawili Dr. Charles Enock Msonde naibu katibu mkuu TAMISEMI sekta ya elimu na kamishna wa elimu wa wizara ya Elimu Dr. Lyabwene Mtahabwa kusisitiza umuhimu wa kiingereza katika kupata elimu yenye maarifa mapana
Hii ni dhana potofu na ya kipuuzi kabisa toka Kwa watu wanaojiita "wasomi"...

Kiingereza ni lugha sawasawa tu kama kilivyo kiswahili..

Ujinga ni watu wawili wajinga kuamua kulazimisha kuwasiliana kwa lugha wasiojua. Matokeo yake ni kuwa watu hawa hawataelewana. Hii ndiyo hali ya mwanafunzi na mwalimu wa Tanzania. Wanatumia lugha ya Kiingereza wasioijua vyema kufundisha a...!

Huo kama siyo ujinga ni Nini eti??
maana kiswahili kina maneno machache yanayobeba dhama maalum ya sayansi, sheria, utabibu, fizikia ndiyo maana lugha kubwa duniani zimekopa maneno ya maeneo ya kitaaluma, sayansi n.k toka lugha za Kigiriki, kilatini..
Mawazo potofu na ya kipuuzi tena toka kwa wanaojiita "wasomi".

JIBU LA HOJA YAKO: Si kweli...!!!

Kiswahili ni lugha iliyo sawa tu na lugha nyingine yoyote kikiwemo Kiingereza. Kiswahili Kwa wanaokijua kiswahili na Kiingereza Kwa wanaojua Kiingereza.

Kiswahili kina misamiati yote utakayo katika nyanja zote za maisha iwe ni siasa, uchumi, sayansi, utsbibu, elimu viumbe hai, ubaharia, sheria nk nk
Tujiulize je kiSwahili mbali ya kuwa lugha iliyonikita zaidi ktk maeneo machache tu kama kuwezesha Mawasiliano mepesi na kutumika katika mashairi na tenzi.
Unaandika kwa hisia tu kwa kuwa ndivyo ulivyofundishwa kwa kukaririshwa na walimu wako waliokufundisha kwenye shule zenu hizi wakikudanganya kuwa Kiswahili hakina misamiati mingi kwa kuwa eti;

Hutumika kwa mawasiliano mepesi..!!!!???
====Sijui hata unamaanisha Nini hapa===!
====mawasiliano magumu (ambayo ni kinyume cha mepesi) ni yepi hayo eti===?
Hutumika kwenye tenzi na mashairi..!!!????
====Na hapa sijui umefyatua nini tu===!!
====Je, una maana kichina, kijapan, kiarabu, kurusi nk ni lugha isiyotumika kwenye mashairi na tenzi??
Je lugha ya kiswahili na mapungufu yake haya inaweza kutumika kama lugha za Mandarini, Kijapani, Kingussie kufundisha utabibu, bailojia, fizikia, molekula, uhandisi, uwakili, internal medicine, Nishati ya Nuklia n.k
bagamoyo, lugha ya kiswahili Haina shida wala upungufu wowote. Mwenye shida na mapungufu ni wewe mwenye fikra potofu za namna hiyo..

Kila lugha inajitosheleza yenyewe ili mradi inaeleweka na jamii yote ya watu hao wazungumzao lugha hiyo...

Na pale inapoonekana imepungugua, basi inaweza kukopa au kuazima maneno toka lugha nyingine. Na kiuhalisia kiswahili chetu kipo hivyo...

Hata Kiingereza, kimekopa au kimetohoa maneno mengi toka lugha zingine mfano Kifaransa, kiarabu, kigiriki, kiyunani, Kiyahudi nk nk
Mfano masuala haya kweli yanaweza yanafundishika ktk kiswahili kwa sasa upande wa utabibu / uganga na ukapikika kitaaluma ?
  • Medical cell biology and genetics.
  • Pathological processes.
  • Health behaviours, musculoskeletal, respiratory and digestive systems.
  • Evidence based medicine and research methods.
  • Clinical procedural skills.
  • Ethics and law in clinical practice.
  • Mechanisms of drug action.
  • Biology of disease
Absolutely, Yes...!

Yanaweza kufundishwa Kwa lugha yoyote na mtu anayeelewa lugha hiyo akapokea maarifa kwa kiwango stahili na ukamilifu wake....

Ni kazi moja tu inahitajika. Nayo ni kuyatafsiri maneno hayo kwenda ktk lugha ya waliokusudiwa na kuweka wazi maana/mantiki iliyo ktk terms hizo...

That's all. Hakuna kingine hapo...

Otherwise, wewe bagamoyo ndiye utuambie kwanini unadhani hayawezekani?

Mfano, unaifahamu Biblia Takatifu wewe? Kwa taarifa yako tu ni kuwa, hicho kitabu hicho kimetafsiriwa kwa lugha zote za dunia hii..!!

Kwanini kimetafsiriwa kwa Kila lugha za hapa duniani?

Jibu ni rahisi tu. Kwamba, ni ili ujumbe na maarifa yaliyomo kwenye kitabu hicho yasomwe na kueleweka na watu wote duniani kwa Kila mtu na lugha yake...!

Kama Hilo limewezekana, kwanini isiwe kwenye VITABU vya elimu dunia Kwa ajili ya jamii???

Ukipata jibu la SWALI hilo☝️☝️☝️☝️, njoo tuzungumze
 
Back
Top Bottom