2pac alifanya harakati za kudai haki na kuelimisha jamii, Notorious Big aliedanganya maisha yake na kuimba uhuni pekee, anamsogelea kwa kipi?

" Mimi ni mtu mzima Nina akili ndiyo maana nimetoka, Mambo yakuniletea ushauri kwenye bata unanikosea " diamond platnumz single chorus in Amen song. 😳😳😳
 
Huyo Biggie kwa Pac alikuwa wakawaida.
 
Hakuna anayeshushiwa heshima hapo,ila kwenye wawili ni lazima mmoja awe zaidi ya mwingine.
 
Kimuzi kwangu mimi Pac alikuwa mtu mbadi.
 
Utamvuruga mwana mbaya.
 
Hahah kuna makuzi itakuwa umepitia ya mabroo.

Sasa unashindwaje kuelewa jumbe kutoka kwa pac, nas, biggie, alafu unawaelewa kelele za kina lil nani sijui, inashangaza kwa kweli.

But anyways kila zama na mambo yake.
Yah kiasi.. kuna Mjomba wangu mmoja amefariki kwa sasa. Yeye aliathirika na MADAWA ya kulevya, so enzi za uhai wake alikuwa anapiga sana ngoma za HIP HOP, na Reggae sana sana.. kuna baadhi ya nyimbo hizo mpaka leo hii (Takribani 15yrs) sijawahi zisikia popote pale nje ya CD zake alizokuwa anatumia.

Alikuwa very deep....

Mie nilikuwa obsessed na Mziki aliokuwa anaupiga home. And that time DSTV ndio ilikuwa imeingia ingia so ile TRACE ORIGINAL ndio ilikuwa yamoto.. so nikawa napata OLD SCHOOL vibes pia na New school vibes.
 
Mkisema BINGWA wa FLOW ni BIG ntawashangaa sana maana kwa RECORDS zangu sidhan kama kuna mtu MTAMU/MTAALAM wa kuflow zaidi ya SNOOP Double G Y.

Muhasisi wa DOGGY style flow.. anashuka bars kama hataki... na bingwa wa chorus kwa upande wangu ni NATE DOGG...

Apart from yeye kuimba ila pia alikuwa anawaandikia watu chorus.. na alikuwa very humbleee.......
 
I see, may his soul rest in heaven.
 
Niqqas knows kila kichwa na mantiki yake, hujiulizi ni kwanini pac na big walikuwepo wengi,
sema sipendi kuwapambanisha hawa mabraza kila mmoja ana mchango wake, kivyake
you damn right, that was my point.
 
Huyo Biggie kwa Pac alikuwa wakawaida.
Hii 'wakaida' ndio ninapowaona nyie jamaa ni wajabu sana and again i call this disrespect if you knw wat i mean.

I agree to disagree, na simlazimishi mtu amkubali biggie over pac or vice versa ila maneno kama hayo sidhani kama ni sahihi na ya mtu anaejua hip hop, inahitaji uwe punguani kumuona biggie wa kawaida, regadlessly! (excuse my language)
 
gangster hip hop ilichagizwa sana na NWA, na ndio maana vijana wa west waliishi humo. I personally not a big fan wa gangstar hip hop and dats why with all due respect sio fan wa west coast licha ya mziki mzuri waliofanya, i respect that.

Eastside!
 
Sijui hizi charts mbalimbali wanaangaliaga vigezo vipi lakn iko ivo, sawa na Ile chart ya Billboard ya Best rapper of all the time miaka kadhaa alikuwa pac asa hivi Jay-Z ni best ever.

View attachment 2763636
Si kwa kuwa yupo HAI na ni MWANACHAMA wa wale watu wenye NGUVU duniani.

Kumbuka 2PAC aliwapiga vita sana hao watu mpk akatoa album yake ya KILLUMINATI the 7 day theory..

JZ hana maajabu just refer ile Ngoma aliyoshirikishwa na SNOOP "I wanna rock" uone alivyokimbizwa mule.

JZ hana nyimbo hata moja ya kumpambanishia na Pac. JZ kwa upande wangu hata top 10 hapaswi kuonekana.
 
Ukweli unabaki hivyo,nina zaidi ya ngoma 30 za pac na kila nikizipiga masela kibao unyoosha mikono kwa mwamba Pac.Ngoma za Biggie nilizonazo hazizidi 5 na masela wakisikia wala hawastuki.
 
Mkuu una chuki binafsi. Jay asiwemo kwenye top 10?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…