4% ya mapato kwenda Zanzibar kama Hoja ya Muungano

4% ya mapato kwenda Zanzibar kama Hoja ya Muungano

Unajua Sky Eclat watu huwa wanajadili hata wasichokifahamu! Mleta mada mwenyewe amekurupuka kulalamika badala ya kuishia kuuliza swali yeye ametafasiri moja kwa moja kwamba kinachogawanwa ni pato la Taifa (kitu ambacho ni ujinga kuhoji!). Malalamiko ya Zanzibar yamekuwa kwenye kupunjwa fedha za misaada ambayo kwenye hati za muungano imetamkwa namna watakavyogawana hiyo misaada, sasa mama amekuja kuhakikisha makubaliano yanatekelezwa!
Hili likitekelezwa litaimarisha Muungano.
 
Iwe msaada ama mkopo Zanzibar haipaswi kupata asilimia 4

Asilimia 4 kwa Zanzibar ni nyingi kwa hoja kuu mbili:

Moja: asilimia ya pato la Zanzibar katika pato jumla la nchi nzima ni chini ya hiyo 4

Mbili: asilimia ya wakazi wa Zanzibar katika total population ya milioni 59 ni chini ya hiyo 4
Yaani! ndugu zetu wa damu! the 4% tunayogaiwa wazanzibari na ambayo ni haki yetu imewatowa roho kiasi hiki? tuwaeleweje ndugu zetu nyie?
 
chapwa24 Sheria inaitaka serekali ya muungano iipatie Zanzibar 4.5% ya misaada yote pamoja na Bakia la Pato la Muungano.
Swali la kwanza ni kua Bakia la pato la Muungano ni lipi? Pato la muungano ni yale mapato yote yanayokusanywa na jamhuri katika mambo ambayo yamo ndani ya muungano kisheria.
Inavyotakiwa ni kuwa baada ya mapato yote kukusanywa, fedha inatakiwa itumike kwenye Budget ya mambo ya muungano, fedha yote itakayobakia inatakiwa igawanywe kwa washirika wa muungano. Kwahiyo Zanzibar wanatakiwa wapate 4.5% na Bara wapate 95.5%
Mfano: kama mapato ya mwaka ya source zote za Muungano ni milioni 120. Halafu Matumizi ya muasuala ya Muungano kuanzia mishahara pamoja na miradi mambo mengine ni milioni 20. Kwahiyo itabakia milion 100, Sasa hiyo mia itatakiwa igaiwe Zanzibar wachukue milioni 4.5 na Bara wachukue milion 95.5. Sasa tatizo lnakuja kuwa Bara hawajawahi kuwalipa Zanzibar stahiki yao ya mgao wa mapato kwa miaka yote hiyo. Pesa zote wanachukua wao, na ndio mana Zanzibar wanalalamika na ndio moja katika kero kubwa za muungano.

Swali jengine linalokujia wewe ni, Kwanini Zanzibar wapewe mgao wa fedha wakati wewe huuoni mchango wao kwenye hayo mapato?

Mtu yoyote anaetaka kuja Tanzania anlipia visa, Pesa ya visa direct inaingia kwenye mfuko wa Muungano. Zanzibar kwa mwaka kunakwenda watalii wasiopungua laki 3, hawa malipo ya visa zao zote zinachukuliwa na Bara, Zanzibar haifidika na hela visa ya watalii wanaokwenda kwao.

Ma company yote ta TZ, kuanzia ya mitandao ya simu, ving'amuzi, Mabenk na mengineyo, Yanasajiliwa Bara, lakini yanafika mpaka Zanzibar kutoa huduma bila kulipa kodi yoyote kule Zanzibar. Yani ni hivi Voda wanalipa Kodi Bara lakini wanatoa huduma mpaka Zanzibar. Fedha wanazolipia za kodi ni kwa ajili ya kutoa huduma mpaka Zanzibar, ila sasa TRA hawagawi mgao wa fedha zinazotokana na makampuni kwa Zanzibar.

Hiyo ni mifano miwili na ipo mengi tu kwenye kila sekta inayohusu Muungano.

Kwa kifupi wanachokifanya Serekali ya SMT, ni wizi wa mchana kabisa, Kila mwaka wanawaibia Zanzibar karibu 1 trillion. kwa kipindi cha miaka kumi kiharaka haraka Zanzibar wanaidai Tanzania fedha isiyopungua Trillion 10.
Asante mkuu kwa huu ufafanuzi. Hata hivo kama mzanzibari nimejisikia vibaya sana na masimango ya ndugu zetu hawa kwa kitu kidogo sana kama 4%. Ambapo kiukweli Zanzibar kama ingeachwa vitu hivi viingie ndani yake bila ya kupitia kwenye muungano, Zanzibar ingefaidika mno. Leo hii watanganyika wanaona kama vile hii 4% ni fadhila na upendeleo na kwamba Zanzibar haistahiki nayo! Na ndio maana ni vyema Zanzibar ikawa na mamlaka yake kamili.
 
Huu Muungano ni mzigo Kwa Tanganyika Kwa 100% . Kifo cha JPM kimeturudisha nyuma miaka kimaendeleo. JPM Bora angemchaguaga Hussein Mwinyi kuwa vice president wa Tanzania. Kwenye katiba ibadilishwe na iseme akifa rais basi prime minister ndio awe rais. Hapa Tanganyika tunavuja Jasho kwaajili ya kuwanufaisha wazanzibar. Huu ni Muungano mbovu kuwahi kutokea duniani
Kama vipi iwachieni Zanzibar ijitawale.
 
Zanzibar haichangii chochote, yeye mwenyewe Samia mshahara wake na marupurupu yote ni jasho la watanganyika

TRA ipo zanzibar lakini inakusanya mapato kwenye maeneo chache sana, na kisha mapato yote huachwa Zanzibar (hakuna shilingi inayokusanywa Zanzibar huvuka maji)
Acha uongo, tra ukusanye mapato znz alaf yote yaachwe znz basi itakua tra yenu ya kikundi cha majambazi
 
Kama mzanzibari, na kwa masimango haya, how I wish lisitekelezwe ili iendelee kuwa chachu kwa wazanzibari kudai Zanzibar yao!
Nimekuelewa, tatizo waliotaka Muungano walifikiria tu kujilinda ili Sultan asirudi kutawala maana alishataarishiwa msaada wa kijeshi kutoka Oman.
 
Ukitathimi kwa kina utagundua iyo 4% inatoka Tanganyika kwenda Zanzibar.

Ni kama vile Tanganyika inalipia gharama za muungano.
Huku ni kuchoshana tu na sisi tutaanza kudai mirabaa ya Ubuyu wa Tangawizi, viladu na mashelisheli.
 
kuna kipindi nilisikia wanalalamika kuwa ukiagiza bidhaa toka zenji, inakuwa imelipiwa ushuru zenji lakini ikifika dsm inalipiwa tena. ina maana kule wana ushuru wa kikwao na wana makusanyo ya pesa ya kikwao.
 
Usichokifahamu ni kwamba TRA wanakusanya kodi hadi Zanzibar. Ndio maana sheria inataka 4% ya mapato yote Tanzania iende Zanzibar. Tena hio 4% kwa maoni yangu ni ndongo ingepaswa walau 15%.
Mi naona kuweka vitu simple Zanzibar iwe na ZRA, iwe inakusanya mapato yenyewe ila shida sasa kwenye kugaramia shughuli za muungano itabidi Zanzibar ichangie. Au shughuli za muungano zipunguzwe zaidi ibaki moja tu ya Ulinzi.
 
chapwa24 Sheria inaitaka serekali ya muungano iipatie Zanzibar 4.5% ya misaada yote pamoja na Bakia la Pato la Muungano.
Swali la kwanza ni kua Bakia la pato la Muungano ni lipi? Pato la muungano ni yale mapato yote yanayokusanywa na jamhuri katika mambo ambayo yamo ndani ya muungano kisheria.
Inavyotakiwa ni kuwa baada ya mapato yote kukusanywa, fedha inatakiwa itumike kwenye Budget ya mambo ya muungano, fedha yote itakayobakia inatakiwa igawanywe kwa washirika wa muungano. Kwahiyo Zanzibar wanatakiwa wapate 4.5% na Bara wapate 95.5%
Mfano: kama mapato ya mwaka ya source zote za Muungano ni milioni 120. Halafu Matumizi ya muasuala ya Muungano kuanzia mishahara pamoja na miradi mambo mengine ni milioni 20. Kwahiyo itabakia milion 100, Sasa hiyo mia itatakiwa igaiwe Zanzibar wachukue milioni 4.5 na Bara wachukue milion 95.5. Sasa tatizo lnakuja kuwa Bara hawajawahi kuwalipa Zanzibar stahiki yao ya mgao wa mapato kwa miaka yote hiyo. Pesa zote wanachukua wao, na ndio mana Zanzibar wanalalamika na ndio moja katika kero kubwa za muungano.

Swali jengine linalokujia wewe ni, Kwanini Zanzibar wapewe mgao wa fedha wakati wewe huuoni mchango wao kwenye hayo mapato?

Mtu yoyote anaetaka kuja Tanzania anlipia visa, Pesa ya visa direct inaingia kwenye mfuko wa Muungano. Zanzibar kwa mwaka kunakwenda watalii wasiopungua laki 3, hawa malipo ya visa zao zote zinachukuliwa na Bara, Zanzibar haifidika na hela visa ya watalii wanaokwenda kwao.

Ma company yote ta TZ, kuanzia ya mitandao ya simu, ving'amuzi, Mabenk na mengineyo, Yanasajiliwa Bara, lakini yanafika mpaka Zanzibar kutoa huduma bila kulipa kodi yoyote kule Zanzibar. Yani ni hivi Voda wanalipa Kodi Bara lakini wanatoa huduma mpaka Zanzibar. Fedha wanazolipia za kodi ni kwa ajili ya kutoa huduma mpaka Zanzibar, ila sasa TRA hawagawi mgao wa fedha zinazotokana na makampuni kwa Zanzibar.

Hiyo ni mifano miwili na ipo mengi tu kwenye kila sekta inayohusu Muungano.

Kwa kifupi wanachokifanya Serekali ya SMT, ni wizi wa mchana kabisa, Kila mwaka wanawaibia Zanzibar karibu 1 trillion. kwa kipindi cha miaka kumi kiharaka haraka Zanzibar wanaidai Tanzania fedha isiyopungua Trillion 10.
1. pesa ya visa: hivi kweli itakuwa nyingi kiasi hicho? manake hata bara kuna watalii wengi wanakuja.

2. makampuni ya simu:- naona zanzibar hapo wanafaidika kwa kupata huduma zao, kwasababu kama isingekuwa bara sidhani kama kungekuwa na kampuni la simu lingeenda kwao kugombania wateja chini ya milioni moja. kwahiyo wanapata huduma za simu kwa mgongo wa population ya bara, hapo washukuru wasilaumu. kama vipi wapige marufuku yasitoe huduma kule kama wataweza.

3. zaidi ya yote, wazanzibar bara wengi sana sana na binafsi huwa nawaona ni watz wala si wazazibar, pamoja na kwamba wao huwa wanapenda kujionyesha ni wa kisiwani sio wa uku. wanafaidika na chochote kinachofanywa na serikali ya muungano. sasa kama raia wao wanakula matunda ya muungano, utasemaje wanatudai? wanatudai chakula ambacho tulipokitenga hadi watoto wao wamekula? na kwanini sisi hatumiliki ardhi kisiwani wakati wao wanamiliki ardhi hadi migodi bara?
 
Mi naona kuweka vitu simple Zanzibar iwe na ZRA, iwe inakusanya mapato yenyewe ila shida sasa kwenye kugaramia shughuli za muungano itabidi Zanzibar ichangie. Au shughuli za muungano zipunguzwe zaidi ibaki moja tu ya Ulinzi.
yaani, kila mmoja akusanye mapato kwenye nafasi yake. kama ni watalii wanaenda zanzibar, wakatoe visa pale zanzibar kwasababu si nchi ile? kama ni kukusanya mapato basi kuwe na ZRA ya kwao, nchi mbili zikusanye mapato kila mmoja kwa nafasi yake halafu kila mmoja sasa achangie kwenye muungano.

litakalotokea hapo, zanzibar hawatakuwa na cha kukusanya zaidi ya visa za watalii kimuungano. mitandao ya simu watabaki na zantel yao tu ambao haitakuwa na faida kwasababu ya pupulation ya kisiwani, ni ndogo kufanya biashara hizo, the same applies kwa mabenki. tuishie kusema muungano unawafaidisha pande zote mbili na zanzibar inafaidika nao indirectly na wanakula kwa mgongo wetu sana.
 
Binafsi sina shida kama hiyo 4% itahusisha mapato na madeni. Kama ni mapato tu, hapo kuna tatizo.
Kwahiyo na hili deni letu la taifa la 71tr wao pia wanachangia asilimia ngapi?..au tunagawana nusu kwa nusu.[emoji28][emoji28]

Kimsingi huu muungano ni pasua kichwa..vizenji tegemezi zaidi ya chawa..bado vinataka pasu huu ni upuuzi.

Leo hii vi zenji vikija huku ni free kwa kila jambo..ila mbara aakienda huko ubaguzi kuanzia akishuka bandarini..mara kitambulisho cha ukaazi..ni ushezi tu...harafu tunajiita watanzania etu tuna muungano.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ni zamu ya watanganyika kulalamika!!

Zanzibar wamelalama Hadi vichwa vinauma, lakini yote Kwa yote, huo mgao usiwe tu wa mapato ya ndani, upole wote wa watanganyika Mbona utaisha hivi karibuni!!!
 
unataka tugawane deni? hahaaha, kwahiyo kama kuna mikopo tulichukua na hatukuwapatia, ile mikopo hadi leo tunadaiwa trillion 70 kwa mfano, itabidi kama wao wakitaka tuwapatie mgao wa mkopo huo wakubali kuchukua na mgao wa kulipa deni lake. asilimia 4% ya deni la taifa inakuwa ngapi i li wenzetu pia waje wadaiwe.
 
Mnapoungana kuna vitu unapata na vingine unapoteza, hizi kero za muungano ni ubinafsi wa kufikiri kwanini mimi napoteza hiki.
Muungano pamoja na kwamba uko kikatiba pia ni sera ya Chama tawala bahati mbaya viongozi na wanachama wengi wa chama tawala hawajui kwanini chama chao kina sera ya muundo wa serikali mbili wa muungano matokeo yake kila kiongozi anaamua kwa utashi wake.
Mara zote kero za muungano huwa zinahusu Zanzibar ukiondoa swala la kwenda visiwani kwa passport.
Ni vema tukawa na muundo ama wa serikali tatu au moja kuliko muundo wa sasa kwani tukiwa na serikali hizo mambo ya mgawo wa asilimia 4 yataondoka na kero kama mafuta lisiwe swala la muungano pia litaondoka na hata migawo ya asilimia au kwanini huchangii pia vitaondoka.
 
Abstract

One hundred and nineteen states signed the Law of the Sea Convention in Jamaica in December 1982. This Convention will enable coastal states inter alia to extend their jurisdiction over living and nonliving resources to 200 miles from their coastlines. Tanzania has consistently supported the concept of the Exclusive Economic Zone but has not yet claimed its own. This paper examines considerations of law and policy relevant to the requirements of a developing country in preparation of an EEZ claim. It shows that the notion of “grabbing jurisdiction”; with its implication of unilateralism in disregard of the law is certainly mistaken so far as Tanzania is concerned. It seems clear that many ratifications of the Convention will be delayed, and for a period of time at least careful attention will have to be paid to state practice grounded in national legislation extending jurisdiction to 200 miles as well as to bilateral and regional agreements. It is on the basis of scrutiny and evaluation of ongoing and unfolding state practice that a state is able to determine its obligations based on international law and to define its policies.​
 
Kwanza hii asilimia 4 ipo zamani kidogo na siyo jana au juzi.

Pili ni kwamba share ya Zanzibar katika kuanzisha BoT ilikuwa hailipwi, bara wanaipiga kimya kimya kwa miaka mingi.

Unalalamika kwamba ukifika Zanzibar unaonekana kama ni mgeni fulani hivi, hiyo ni kawaida hata kwa Wazanzibar walioko bara, na hata kwa wewe mwenyewe ukenda kwenye mkoa au wilaya siyo asili yako lazima utajulikana tu.
To upompoma wako..mbara ni mgeni huko hatambuliki..ndio mana kuna kitambulisho cha ukaazi..kukipata mpka ukae miaka mitatu..sasa hii ni Tanzania au malawi..kwani NIDA haitoshi?

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom