4% ya mapato kwenda Zanzibar kama Hoja ya Muungano

4% ya mapato kwenda Zanzibar kama Hoja ya Muungano

Unapoambiwa watanzania tupo milion 60+.
unaelewa nini?.
au wanzibar sio watanzania?
unataka tugawane deni? hahaaha, kwahiyo kama kuna mikopo tulichukua na hatukuwapatia, ile mikopo hadi leo tunadaiwa trillion 70 kwa mfano, itabidi kama wao wakitaka tuwapatie mgao wa mkopo huo wakubali kuchukua na mgao wa kulipa deni lake. asilimia 4% ya deni la taifa inakuwa ngapi i li wenzetu pia waje wadaiwe.
 
chapwa24 Sheria inaitaka serekali ya muungano iipatie Zanzibar 4.5% ya misaada yote pamoja na Bakia la Pato la Muungano.
Swali la kwanza ni kua Bakia la pato la Muungano ni lipi? Pato la muungano ni yale mapato yote yanayokusanywa na jamhuri katika mambo ambayo yamo ndani ya muungano kisheria.
Inavyotakiwa ni kuwa baada ya mapato yote kukusanywa, fedha inatakiwa itumike kwenye Budget ya mambo ya muungano, fedha yote itakayobakia inatakiwa igawanywe kwa washirika wa muungano. Kwahiyo Zanzibar wanatakiwa wapate 4.5% na Bara wapate 95.5%
Mfano: kama mapato ya mwaka ya source zote za Muungano ni milioni 120. Halafu Matumizi ya muasuala ya Muungano kuanzia mishahara pamoja na miradi mambo mengine ni milioni 20. Kwahiyo itabakia milion 100, Sasa hiyo mia itatakiwa igaiwe Zanzibar wachukue milioni 4.5 na Bara wachukue milion 95.5. Sasa tatizo lnakuja kuwa Bara hawajawahi kuwalipa Zanzibar stahiki yao ya mgao wa mapato kwa miaka yote hiyo. Pesa zote wanachukua wao, na ndio mana Zanzibar wanalalamika na ndio moja katika kero kubwa za muungano.

Swali jengine linalokujia wewe ni, Kwanini Zanzibar wapewe mgao wa fedha wakati wewe huuoni mchango wao kwenye hayo mapato?

Mtu yoyote anaetaka kuja Tanzania anlipia visa, Pesa ya visa direct inaingia kwenye mfuko wa Muungano. Zanzibar kwa mwaka kunakwenda watalii wasiopungua laki 3, hawa malipo ya visa zao zote zinachukuliwa na Bara, Zanzibar haifidika na hela visa ya watalii wanaokwenda kwao.

Ma company yote ta TZ, kuanzia ya mitandao ya simu, ving'amuzi, Mabenk na mengineyo, Yanasajiliwa Bara, lakini yanafika mpaka Zanzibar kutoa huduma bila kulipa kodi yoyote kule Zanzibar. Yani ni hivi Voda wanalipa Kodi Bara lakini wanatoa huduma mpaka Zanzibar. Fedha wanazolipia za kodi ni kwa ajili ya kutoa huduma mpaka Zanzibar, ila sasa TRA hawagawi mgao wa fedha zinazotokana na makampuni kwa Zanzibar.

Hiyo ni mifano miwili na ipo mengi tu kwenye kila sekta inayohusu Muungano.

Kwa kifupi wanachokifanya Serekali ya SMT, ni wizi wa mchana kabisa, Kila mwaka wanawaibia Zanzibar karibu 1 trillion. kwa kipindi cha miaka kumi kiharaka haraka Zanzibar wanaidai Tanzania fedha isiyopungua Trillion 10.
Hakuna pesa mtalipwa..tumewasamehe madeni mengi achlilia mbali umeme...mnakula bure bado mnataka kutupangia aina ya chakula ch akuwalisha?.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu huyu mama sometimes naona amekuja kutuchanganya tu, hii huruma anayoiweka mbele badala ya kutumia akili atatuumiza, hao wazanzibar wenzake wana bunge, mahakama, serikali, jeshi, kuonesha kwamba wana mamlaka wanajitegemea, sasa hii kuwabeba beba mara umeme, bado tuwagawie 4% maana yake nini?
Hivi huwa nawaza, huu Muungano wa nchi mbili kuwa nchi mbili badala ya kuwa nchi moja sijui tumeutoa wapi. Wanajificha kwenye kero za Muungano,hakuna cha kero wala nini ni watu waoga kuamua kama tuwe nchi moja au kila mtu kivyake.
 
Kama vipi iwachieni Zanzibar ijitawale.
Zanzibar ilikuwa nchi huru kabla ya Muungano, lakini ni mali halali ya Sultan wa Oman. Muungano ni ukuta tu uliojengwa kumzuia mwenye chake asidai haki yake aliyodhurumiwa na mapinduzi MATUKUFU. Zanzibar mkiona vema kujitenga mjue Sultani anaweza kuja kudai chake kama hajasamehe.
 
unfortunately, amini usiamini, mafuta zenji hakuna. na kama yapo, yapo kidogo sana, na kama yakiwepo zenji basi na bara yapo. hata gesi tu hawajagundua. binafsi, ninaamini kama tunataka muungano, tuungane kabisa kabisa tuwe nchi moja, hata hoja ya kuwa na marais wawili kwenye nchi moja hii huwa naona ni ukakasi.

ila kama kweli kuna mafuta zanzibar, ni haki wayatumie wao tu, na sisi gas na mafuta na helium etc zitumike huku tu. Zanzibar kama wakipata mafuta kweli wataendelea sana, kama wakipata kitu cha kuwaingizia hela wataendelea sana kwasababu nchi yao ni ndogo kuiendeleza ni rahisi. hata hivyo.

wamejaa sana bara na ninapenda wajae zaidi ndio maana ya muungano, ila sisi sasa kwenda kwao tunaonekana wageni fulani hivi. tukija ndani ya hoja, ni kitu gani hiki kinachotakiwa kugawanywa? isije kuwa wana hoja ya msingi halafu inafunikwa.
Mafuta na gesi yapo vizuri tu Zanzibar, katika jambo moja ambalo limesababisha yasichimbwe, ni uroho wa JMT kutaka yawe ya Muungano. Tangu lini rasilimali za sehemu moja zikawa za Muungano ila za upande mwengine zisiwe za Muungano? Lengo ni nini?

Mimi nasema Mafuta yasichimbwe, yaachwe huko huko yalipo mpaka Zanzibar ipate kiongozi anaetaka maendeleo sio hawa wa mfano waliotoka serikali kina Balozi Sua Mbaya Idi, kazi yao ilikuwa kufanya ufisadi tu!
 
Mafuta na gesi yapo vizuri tu Zanzibar, katika jambo moja ambalo limesababisha yasichimbwe, ni uroho wa JMT kutaka yawe ya Muungano. Tangu lini rasilimali za sehemu moja zikawa za Muungano ila za upande mwengine zisiwe za Muungano? Lengo ni nini?

Mimi nasema Mafuta yasichimbwe, yaachwe huko huko yalipo mpaka Zanzibar ipate kiongozi anaetaka maendeleo sio hawa wa mfano waliotoka serikali kina Balozi Sua Mbaya Idi, kazi yao ilikuwa kufanya ufisadi tu!
kwahiyo, kama zanzibar kuna mafuta, unaamini bara hakuan mafuta? yaani mafuta yawepo tu pale zanzibar na kwenye bahari yetu kuanzia mtwara kwenye gas hadi Tanga kusiwe na mafuta? au unaamini umiliki wa bahari zanzibar wanamiliki ukanda wote? kama zanzibar kuna mafuta na bara nako kuna mafuta tena na gas pia. ila kwa haki, bila kumung'unya maneno, mafuta ya Zanzibar yanatakiwa yakiendeleze kisiwa kile,na gas na mafuta na madini ya bara hayatakiwi kugawiwa hata sent kwa wazenji, hiyo ni haki. nakubaliana nao.

kitu kizuri ni kwamba, zanzibar pakiendelea, bara patafaidia pia, hivyo kama kuna vitu vinavyoweza kuwasaidia kuendelea, tunatakiwa kuwaunga mkono.
 
Kuna hoja nimekuta watu wanaongea, ni kuhusu kile ambacho mama amesema waziri wa fedha akakae na mwenzake wajadili na kusuluhisha katika kero za muungano. Ninaupenda sana Muungano,ninauunga mkono. lakini, nilijiuliza kitu kimoja, mimi kama mtu wa bara sitaki tupigwe pia kama wazenji wasivyopenda kupigwa.

1. hivi Zanzibar inachangia kitu gani kwenye kwa Tz bara kinachowastahilisha tuwagawie hiyo asilimia? Bara inafaidika nini toka Zanzibar?

2. Mgao unaoongelewa ni wa misaada toka nje, au ni mapato ya nchi (pato la madini bara, TRA, navitu vyote vya bara)?

3. kama ni mapato ya nchi, kwani TRA haipo Zanzibar ya kikwaokwao?

4. proportion ya wingi wa watu + ukubwa wa eneo vinazingatiwaje wakati wa kugawa pato ya muungano?

5. kwanini marais waliopita walikuwa hawashughulikii hilo jambo, kulikuwa na kitu gani walichokiona? including one of them who was Zanzibari.

6. kwa anayeelewa, naomba anieleweshe hili jambo kwasababu kama vile tu zanji wasivyopenda kupigwa, mimi kama mtu wa bara pia sipendi na sikubali.

Naongea hivi kwasababu watu wanavyoongea mtaani wanaongea kama vile kwasababu mama ni mzanzibar basi wanaona wazanzibar wanaweza kupitisha vitu vingi sana ambavo vilikuwa havipiti kwa awamu za nyuma ambazo nyingi hazikushikwa na rais wa zanzibar.

MWISHO: siongei kwa ubaya, wala kwa unafiki, ila ninaongea kinachoongelewa mitaani. Ninamwamini mama atafanya makubwa. Ila naamini tunatakiwa kuwa na busara ya hali ya juu kwasababu kuna mambo tunaweza kufanya tukifikiri tunajenga muungano kumbe ndio tunauweka kwenye mazingira ya kubomoka kabisa.
Kwani Chato ilikuwa inachangia nini kwenye pato la Taifa mpaka ikapelekewa mbuga ya wanyama,uwanja wa ndege na ikulu??
 
1. hivi Zanzibar inachangia kitu gani kwenye kwa Tz bara kinachowastahilisha tuwagawie hiyo asilimia? Bara inafaidika nini toka Zanzibar?
ilichangia BOT 12% kama sikosei, hadi dakika hii haijawahi kupata faida kutoa hio 12% iliowekeza hapo kwenye BOT.

2. Mgao unaoongelewa ni wa misaada toka nje, au ni mapato ya nchi (pato la madini bara, TRA, navitu vyote vya bara)?
Misaada/Mikopo kutoka nje

3. kama ni mapato ya nchi, kwani TRA haipo Zanzibar ya kikwaokwao?
Hi ni bodi ya mapato ya Tanzania na sio Zanzibar, nafikiri unajua sasa pesa yake inaungia akaunti ya nani.

4. proportion ya wingi wa watu + ukubwa wa eneo vinazingatiwaje wakati wa kugawa pato ya muungano?
Zimeungana nchi, sio ukubwa wa eneo au wingi wa watu.

5. kwanini marais waliopita walikuwa hawashughulikii hilo jambo, kulikuwa na kitu gani walichokiona? including one of them who was Zanzibari.
Hakukuwa na lengo la kuisaidia wala kutaka kuona Zanzibar ikipiga maendeleo, kuendelea kwa Zanzibar ilikuwa mwiba kwao. Lengo ni kujimilikisha na kujifaidisha kile walichokuwa nacho wazanziba, BAHARI.
 
Nilichogundua humu kuna watu hawawezi hata kupewa uongozi wa family, yaani watu wengi wanaongea kiunafiki na inaonyeshea wamezoea maisha ya wizi na uongouongo, kama wao wamekubaliana hivyo tokea enzi sasa kinachowauma ni nini? Kwann hio 4% inawauma na still hamjawapa? Kwanza mnatakiwa mpiganie hayo matrillioni wanayoyachukua kina kingwala na wenzake yarudishwe, mnatakiwa mpiganie ufisadi mkubwa unaofanywa na ccm kwa mfano miradi ya ndege nk, mkishakupapatua huo ufisadi mtapata zaidi ya 4%, yaani znz wanahaki ya kupata zaidi ya 4% sio mnataka kuwadhulumu
 
kwahiyo, kama zanzibar kuna mafuta, unaamini bara hakuan mafuta? yaani mafuta yawepo tu pale zanzibar na kwenye bahari yetu kuanzia mtwara kwenye gas hadi Tanga kusiwe na mafuta? au unaamini umiliki wa bahari zanzibar wanamiliki ukanda wote? kama zanzibar kuna mafuta na bara nako kuna mafuta tena na gas pia. ila kwa haki, bila kumung'unya maneno, mafuta ya Zanzibar yanatakiwa yakiendeleze kisiwa kile,na gas na mafuta na madini ya bara hayatakiwi kugawiwa hata sent kwa wazenji, hiyo ni haki. nakubaliana nao.

kitu kizuri ni kwamba, zanzibar pakiendelea, bara patafaidia pia, hivyo kama kuna vitu vinavyoweza kuwasaidia kuendelea, tunatakiwa kuwaunga mkono.
Hatuna tatizo ikiwa mna mafuta kila chochoro hapo tanganyika. Tatizo tulokuwa nalo na nyinyi ni kuyataka Mafuta ya Zanzibar kuwa ya Muungano, ilhali ya kwenu hamutaki yawe ya Muungano. Kwanini Almasi, Dhahabu na madini mengine yasiwe ya Muungano?

Hio 4% hatupewi na mafuta pia JMT inataka kuyachukua?!!!
 
chapwa24 Sheria inaitaka serekali ya muungano iipatie Zanzibar 4.5% ya misaada yote pamoja na Bakia la Pato la Muungano.
Swali la kwanza ni kua Bakia la pato la Muungano ni lipi? Pato la muungano ni yale mapato yote yanayokusanywa na jamhuri katika mambo ambayo yamo ndani ya muungano kisheria.
Inavyotakiwa ni kuwa baada ya mapato yote kukusanywa, fedha inatakiwa itumike kwenye Budget ya mambo ya muungano, fedha yote itakayobakia inatakiwa igawanywe kwa washirika wa muungano. Kwahiyo Zanzibar wanatakiwa wapate 4.5% na Bara wapate 95.5%
Mfano: kama mapato ya mwaka ya source zote za Muungano ni milioni 120. Halafu Matumizi ya muasuala ya Muungano kuanzia mishahara pamoja na miradi mambo mengine ni milioni 20. Kwahiyo itabakia milion 100, Sasa hiyo mia itatakiwa igaiwe Zanzibar wachukue milioni 4.5 na Bara wachukue milion 95.5. Sasa tatizo lnakuja kuwa Bara hawajawahi kuwalipa Zanzibar stahiki yao ya mgao wa mapato kwa miaka yote hiyo. Pesa zote wanachukua wao, na ndio mana Zanzibar wanalalamika na ndio moja katika kero kubwa za muungano.

Swali jengine linalokujia wewe ni, Kwanini Zanzibar wapewe mgao wa fedha wakati wewe huuoni mchango wao kwenye hayo mapato?

Mtu yoyote anaetaka kuja Tanzania anlipia visa, Pesa ya visa direct inaingia kwenye mfuko wa Muungano. Zanzibar kwa mwaka kunakwenda watalii wasiopungua laki 3, hawa malipo ya visa zao zote zinachukuliwa na Bara, Zanzibar haifidika na hela visa ya watalii wanaokwenda kwao.

Ma company yote ta TZ, kuanzia ya mitandao ya simu, ving'amuzi, Mabenk na mengineyo, Yanasajiliwa Bara, lakini yanafika mpaka Zanzibar kutoa huduma bila kulipa kodi yoyote kule Zanzibar. Yani ni hivi Voda wanalipa Kodi Bara lakini wanatoa huduma mpaka Zanzibar. Fedha wanazolipia za kodi ni kwa ajili ya kutoa huduma mpaka Zanzibar, ila sasa TRA hawagawi mgao wa fedha zinazotokana na makampuni kwa Zanzibar.

Hiyo ni mifano miwili na ipo mengi tu kwenye kila sekta inayohusu Muungano.

Kwa kifupi wanachokifanya Serekali ya SMT, ni wizi wa mchana kabisa, Kila mwaka wanawaibia Zanzibar karibu 1 trillion. kwa kipindi cha miaka kumi kiharaka haraka Zanzibar wanaidai Tanzania fedha isiyopungua Trillion 10.
Nimegundua humu jamvini huwa tunachangia amma kwa ushabiki au kwa kutokujua baadhi ya mambo. Afadhali umetoa mwanga. Chanzo cha mgao huu ni wakati EAC liyovunjika 1977 ilipokuwa inagawa mali zake kwa washirika. utakumbuka mgao wa Zanzibar uliingizwa Tanzania. Akatafutwa mshauri elekezi ambaye alishauri Zanzibar ipewe 4.5%. Bahati mbaya Serikali ikaamua 4% kwa kila jambo. Wakati tunadai hiyo 4% ni kubwa, pamoja na ufafunuzi huu, kuna jambo halisemwi na huwa hatutaki lisemwe; kwamba wakati wa kuanzisha BOT mwaka 1967 Zanzibar ilichangia 11.5% ya mtaji wa benki hiyo. Tokea wakati huo hakuna mgao wowote uliotolewa kwa Zanzibar kama mwanahisa mshirika mkubwa wa benki hiyo. Nadhani wakati tukijifaragua kwa dharau na kejeli tufike mahala tuukubali ukweli kwamba katika hili Zanzibar imedhulumiwa, inadhulumwa na itaendelea kudhulumiwa kwa jina kulinda muungano ikiwa hatutachukua hatua kurekebisha uendeshaji wa mambo yetu. Tuseme basi
 
Halafu huyu mama sometimes naona amekuja kutuchanganya tu, hii huruma anayoiweka mbele badala ya kutumia akili atatuumiza, hao wazanzibar wenzake wana bunge, mahakama, serikali, jeshi, kuonesha kwamba wana mamlaka wanajitegemea, sasa hii kuwabeba beba mara umeme, bado tuwagawie 4% maana yake nini?
Jeshi lipi walilonalo? Vile ni vikosi tu havina hadhi yakuitwa jeshi maana majeshi ni suala la muungano.
Hiyo asilimia 4 huenda ni mapato yatokanayo na biashara za nje ama mambo ya nje kama misaada nakadhalika kwakuwa masuala ya kimataifa ni ya muungano.
 
Yaani! ndugu zetu wa damu! the 4% tunayogaiwa wazanzibari na ambayo ni haki yetu imewatowa roho kiasi hiki? tuwaeleweje ndugu zetu nyie?
[emoji23] [emoji23] [emoji23] Wakati kingwala na wenzake wanakula zaidi ya hizo %4 but wanawacha wadunde kitaa ila znz ambayo inachangia pato wasipewe, hawa jamaa waajabu sijapata kuona na hawasarifiki
Mm siko znz ila napenda kuongea ukweli kama anavyoongea TL
 
Halafu huyu mama sometimes naona amekuja kutuchanganya tu, hii huruma anayoiweka mbele badala ya kutumia akili atatuumiza, hao wazanzibar wenzake wana bunge, mahakama, serikali, jeshi, kuonesha kwamba wana mamlaka wanajitegemea, sasa hii kuwabeba beba mara umeme, bado tuwagawie 4% maana yake nini?
Acha roho mbaya wewe.
 
Back
Top Bottom