50 People Who Are Screwing Up Tanzania

50 People Who Are Screwing Up Tanzania

Status
Not open for further replies.
Huyo no. 15 mbona haonekani? Nashauri ubadilishe rangi yake ifanane na wengine au kama ni kinara basi weka nyekundu

No. 15 ni invisible but inasomeka mkuu...! Huyo ndie kamanda mkuu a.k.a Mh. Dr. Col. Mr P.
 
Mkuu Sonara,

Serikali ipi hiyo unayoizungumzia!!! Ya Kikwete?????? Ni kichekesho unless umetoka usingizini na hujui kinachoendelea Tanzania la sivyo, nina wasiwasi majibu yako yanalengo lililofichika!!!!

Tiba
 
Hao hawamuwezi Kikwete hata dakika moja ,Kikwete ni mtu mkimya sana sana ,na hatari ya mtu mkimya ni kubwa kuliko yule anaepiga makelele,maana mtu mkimya anakuwa alert kwa kila step anayochukua,japo ataonekana hajui au mtamuona zezeta lakini hesabu zake haziendi upande,anapanga ,anayajua,na kuelewa ni wakati gani anahitaji kuchukua hatua ili kuidhibiti hali. Hivyo hao akina Rostam na wengine inakuwa kama wadudu waliokuwemo ndani ya sufuria kubwa ,hivyo Kikwete aliepo juu anawaona na kuwatazama movement zao na nani anataka kutoka kwenye sufuria atamuona tena kwa urahisi zaidi ,natumai umepata picha halisi ,hivyo Kikwete anayatazama haya yanayofanywa kwa upole kabisa akiamini watu watajirekebisha intime kabla hajaamua kuwarudisha ndani ya sufuria kwa yule anaekuja juu akiamua kutaka kutoka ndani ya sufuria ,kwa ufupi hawa watu wamewekwa ndani ya kona au uangalizi na kila hatua wanayofanya inadhibitiwa na kupimwa kwa kina na malengo yake,kiasi kwa walipo wanaonekana wamo katika kugombea ukubwa wao kwa wao,hivyo Kikwete analielewa hilo ,na wao kama ndugu lazima mkubwa amuheshimu mdogo ,sasa wanapotokea ndugu kupigana inabidi uwawache ili mmoja aweze kumuheshimu mwenziwe.
Kikwete ni Raisi ambae amekuwa mvumilivu sana kiasi kuwa uvumilivu wake unaonekana kuwa umepita mipaka ,lakini anaamini kuwa kila mtu atauona ukweli wa anayoyafanya na atajirekebisha hivyo tunaweza kumuweka katika kundi la watu wenye subira.Na ndivyo nimuonavyo mimi kwa upande wangu ,ni mtu ambae anaweza kukasirika mpaka akabadilika rangi lakini mwisho wake hurudisha hasira zake na kuwa katika uvumilivu na ndio tunavyokwenda nae he is a man of GOD & we can do nothing to force him to take action by our makelele.
Hata Mtume wetu Muhammad alikuwa mpole sana kuna sehemu alipigwa mawe na yakamtoa ngeu na damu,malaika alimshukia na kumwambia sema tuwafanye nini wale watu ,Mtume akawaombea dua tu na hakuwatakia waadhibiwe. Hivyo wavumilivu ni watu wa aina hawawezi kabisa kufuata matakwa ya mtu mwengine katika kuchukua hatua.

Usitudanganye umakini na ukimya wa Kikwete ni upi unaotuambia nao?EL ni makini sana kuliko Kikwete,Amini usiamini anachokizungumza Mmaroroi ni sahihi sana.Kwa gharama yoyote Lowasa yuko tayari kutaka madaraka ya kuongoza nchi.Na nikuambie hujui aliko Lowasa na kambi yake wakati huu ,na wanachokifanya wala hujui.Pia ukumbuke mtu huyo huyo Lowasa ndiye alikuwa behind Wanamtandao na kumweka Kikwete madarakani.Sasa hoja siyo nani makini au mkiya bali NCHI ISIINGIZWE MATATANI KWA UFISADI WA MAFISADI!!!Lowasa yuko na atakuwa tayari kumwaga damu ili aingie madarakani kwa udhaifu wa aliyeko madarakani.Kwa hiyo ni vyema tukachukua tahadhari kabla ya shari.
 
Usiwe na jazba unaushahidi wowote wa kubainisha hilo au ni chuki tu hao watu sioni kama wanamakosa hadi sasa. hivi tuseme iwe ni wewe ndio umeona hilo vyombo vya dola halioni hicho kitu na kama ingekuwa hali ipo hivyo ulivyo isema basi sidhani kama serekali ingewachia watu hao wa 3 wafanye hayo wakati serekali inauwezo wa kuwashuhulikia na sifikiri serekali ingekubali nchi kuchafuliwa lakini kwa hali inavyokwenda nahisi hata serekali inajuwa kuwa hao watu wanazuliwa tu

Waua nchi na wauza nchi muna sura nyingi
Asante kwa kujitambulisha, unaturahisishia kazi wazalendo
 
Na ukiangalia ni watanzania wenzetu waliopata kusoma kwa fedha za watanzania na kisha kupewa madaraka na kuyatumia vibaya madaraka yao.

ongeza na wajumbe wa shina wa CCM, wanauza viwanja mara mbilimbili huko serikali za mitaani na wanasumbuaa kweli watanzania wenzao
 
Mfumwa hatukuelewi. We nani katika hao unaona hastahili au una mjomba wako katika hao?
 
Na ukiangalia ni watanzania wenzetu waliopata kusoma kwa fedha za watanzania na kisha kupewa madaraka na kuyatumia vibaya madaraka yao.

ongeza na wajumbe wa shina wa CCM, wanauza viwanja mara mbilimbili huko serikali za mitaani na wanasumbuaa kweli watanzania wenzao

Jamani tuache wivu, mtu akiwa na hela kidogo kwetu tayari huyo ni fisadi! Ndiyo maana Tanzania tunazidi kurudi nyuma. Hao tunaowaita mafisadi ndo wajasilimali kwani bila wao tusingekuwa na Mbezi Beach, Masite ya Tegeta, masaki, Makongo Juu na kadhalika.

Tujifunze kutoka kwa wenzetu Wakenya. Kibaki, Odinga, Kenyatta nk ni matajiri wakubwa wanaomiliki mali nyingi na wanasaidia katika kukuza ajira.

Huku kwetu, hao mafisadi mnaowasema hata nyumba ya kupangisha hawana!! Umasikini ndo unatusumbua.

Nakubaliana na wale wanaosema kuwa mafisadi wa nchi hii ni wewe na mimi, period!
 
Napendekeza shortlist zaidi ya 50 halafu tukipiga kura ndio wabaki hao 50 ili kuondoa walioonewa! Ongezea James E. Sinclair,Chairman & CEO,Tanzanian Royalty Exploration Corporation swahiba mkubwa wa mkulu!
 
Apson Mwang'onda
Rostam Azizi
Ben Mkapa
Rajab Maranda
Johnson wa EPA
Abdallah Kinana
Peter Serukamba
Subhash Patel
Manji
Chavda
Vithlan

.....hawa wote kuna sifa moja wana share mnaijua hiyo?
 
Maximo ....kwa kushindwa kuchukua kombe la Challenge,na kwa kushindwa kuipeleka Stars 2010.. ha ha ha ha aaaa
 
Pius Msekwa
Tuendeleze list
Wakuu, nimemwongezea Spika wa zamani mzee Msekwa. Nimekumbushwa na mdau pembeni kuwa anastahili kuwepo kwenye list.

Kama kuna niliyemwonea kwenye hii list naomba mnifahamishe tumwondoe.

6 screwers missing 🙁
 
Kuchafuana maana yake nini mfumwa au yupi wewe kati ya hao unaona hawastahili. Au nawe unakuwa kama wale waandishi wa NeW Habari(2006) wanaomtetea RA na kumuona msafi wakati nasikia anawafanyia ufisadi hata wao kuwapa titles za consultants ili akwepe kodi yav TRA. Muulize Muhingo kama halijui hilo.

Mungu ibariki Africa
 
Maximo ....kwa kushindwa kuchukua kombe la Challenge,na kwa kushindwa kuipeleka Stars 2010.. ha ha ha ha aaaa

ha,ha kwani yeye ndio alikuwa akicheza. Ndio maaana nakubaliana kabisa na mwana Jf aliyesema namba one katika list ni sisi wenyewe wananchi
 
Hi,

Hiyo list imetumia vigezo gani, mbona watu wengine hawamo, au just if have ever appeared in newspaper then you are part of MAFISADI.

Mh!!!!
 
Mimi nafikiri tuanze na wananchi wenyewe.

We are actually screwing ourselves for allowing CCM to rule our country!!!!!!!!!!!!!!!
 
Duh Kazi kweli kweli...

Ingependeza kama ungekuja na list ya watu kama 100 ili tuwa-shortlist wabaki 50....hivi kuna watakaodai wameonewa...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom