8/02/2015: Yanga vs Mtibwa match preview and live coverage

Umeenda kabila gani vile?

Yalaaaaaaah!!! kumbe upo hai mkuu Masuke!!!!, Nikajua umedondoka pale taifa baada ya kuona timu ya wananchi ilivyokuwa inawanyanyasa wale wakulima wa miwa wa kutoka kule Manungu!! Habar za kuadimika!!!
 
Umeenda kabila gani vile?

Nakuwa Msukuma Masuke, sasa tumemaliza wewe Yanga, mimi Msukuma powa kabisa.
Hatubadilishi ndio tayari imepitishwa hii, mimi kubadili kabila si mchezo. Karibu sana Yanga.
 
Last edited by a moderator:
Yalaaaaaaah!!! kumbe upo hai mkuu Masuke!!!!, Nikajua umedondoka pale taifa baada ya kuona timu ya wananchi ilivyokuwa inawanyanyasa wale wakulima wa miwa wa kutoka kule Manungu!! Habar za kuadimika!!!
Siku ile mimi nilikuwa kimataifa zaidi, muda huo mnawanyanyasa Mtibwa nilikuwa nimepumzika kusubiri mtanange mkali kati ya Ivory Coast na Ghana ambao nilijua ungechukua muda mrefu na kweli ikatokea.
 
Nakuwa Msukuma Masuke, sasa tumemaliza wewe Yanga, mimi Msukuma powa kabisa.
Hatubadilishi ndio tayari imepitishwa hii, mimi kubadili kabila si mchezo. Karibu sana Yanga.
Kubadilisha kabila kunaendana na kujua tamaduni, mila na miiko ya kabila husika, endapo utaniambia baadhi ya miiko, baadhi ya tamaduni, baadhi ya mila za kisukuma na kuniambia umechagua jina gani na ukoo gani wa kisukuma then i will have to think about the offer of becoming Yanga supporter for at most one match.
 
Last edited by a moderator:

Uwiii hayo mambo mengi sana, Masuke kama ni la ukoo nachukua hilohilo lako lol...
Mila najua hiyo ya chagulaga. Kuchunga ng'ombe, miiko hapo ndio nisaidie eeh.
Yanga tunapokea shabiki mpya leo, karibu tena...
 
Uwiii hayo mambo mengi sana, Masuke kama ni la ukoo nachukua hilohilo lako lol...
Mila najua hiyo ya chagulaga. Kuchunga ng'ombe, miiko hapo ndio nisaidie eeh.
Yanga tunapokea shabiki mpya leo, karibu tena...

Umeshindwa mtihani huu inaonekana huna nguvu ya ushawishi, ngoja nikuitie hawa ndugu zangu wanaweza kukusaidia. Makoye Matale, sembo na Crashwise hebu njoni huku mjaribu kumpa tuition huyu mtu maana tunataka kumuasili ili ajiunge na wananzengo. Mpeni darasa kuhusu utamaduni, mila na miiko yetu.
 
Last edited by a moderator:

Mkuu Masuke wewe ni ndugu katika kabila letu na Bantu lady ni dada katika Yanga yetu. Na-declare conflict of interests katika mjadala huu, hence no comment.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Masuke wewe ni ndugu katika kabila letu na Bantu lady ni dada katika Yanga yetu. Na-declare conflict of interests katika mjadala huu, hence no comment.

Lengo ni kumpa machache yanayohusiana na kabila letu ili ikionekana anaelewa nitaamini kweli amedhamiria kubadili kabila hivyo nitaona inawezekana hivyo na mimi nitaweza kuwasupport vijana wa jangwani siku mtakapokutana na wale wa Botswana.
 
Lengo ni kumpa machache yanayohusiana na kabila letu ili ikionekana anaelewa nitaamini kweli amedhamiria kubadili kabila hivyo nitaona inawezekana hivyo na mimi nitaweza kuwasupport vijana wa jangwani siku mtakapokutana na wale wa Botswana.

Kumbe unakuwa Yanga kwa mechi moja tu? Mkuu Masuke hapo nami nakuwa Msukuma kwa siku hiyo tu hahahahahahaaaa.
Uwe Yanga jumla ndio nami nitakuwa Msukuma jumla. Ila hiyo janja yako, nabaki na ukurya wangu mmmh
 
Last edited by a moderator:
nashukuru nimerudi salama, hongereni kwa ushindi mnono sana...............mimesoma Gazeti nimemkubali sana Ngassa ingawa inaonekana bado mashabiki wa simba na Yanga washamba sana
 
sikupenda Nagsaa kuzomewa wala Okwi kuzomewa akitolewa nje baada ya kupigwa kiwiko ...............nakumbuka Chelsea walimshangilia sana Lampard Man City ilipocheza darajani, nadhani shida ya tafsiri tu hapa
 
Kumbe unakuwa Yanga kwa mechi moja tu? Mkuu Masuke hapo nami nakuwa Msukuma kwa siku hiyo tu hahahahahahaaaa.
Uwe Yanga jumla ndio nami nitakuwa Msukuma jumla. Ila hiyo janja yako, nabaki na ukurya wangu mmmh

Tatizo ni nini unajua Bantu lady, Mimi kuwa Yanga nahitaji kama elfu ishirini tu za kununua jezi zao lakini wewe kuwa Msukuma inahitaji ujue vitu vingi sana ambavyo kwa sasa naamini huvijui sasa ikitokea mimi nimekubali offer hiyo kwa kigezo cha kwamba umebadili kabila itakula kwangu maana utakuwa msukuma bandia ile mbaya.

Nimekwambia japo uchague hata jina lako tu maana sisi hata kama ungekuwa na haya majina ya kizungu lazima utakuwa na jina la nyumbani tena yanaweza kuwa hata mawili moja la upande wa baba na lingine la upande wa mama.
 
Last edited by a moderator:
nashukuru nimerudi salama, hongereni kwa ushindi mnono sana...............mimesoma Gazeti nimemkubali sana Ngassa ingawa inaonekana bado mashabiki wa simba na Yanga washamba sana

Mkuu ulikuwa wapi? Sisi mashabiki wa Yanga siyo washamba bali mashabiki wa Simba kwa mujibu wa Rage ni 'mbumbumbu'.
 
Mkuu ulikuwa wapi? Sisi mashabiki wa Yanga siyo washamba bali mashabiki wa Simba kwa mujibu wa Rage ni 'mbumbumbu'.
nilienda kwa palizi la ufuta.......uache unazi sasa, Rage alipata alichotaka kwenye michezo kama anavyitaka sasa Malinzi na Tenga................Yanga walimozmea Okwi.................
 
Uwiiii kuna watu wametoka usingizini muda huu!!!
Aibu imeshapita haya anzeni mmoja baada ya mwingine kurudi, karibuni jukwaani hivi kikaragosi changu Komeo Lachuma uko wapi? Nahitaji kucheka hebu ukuje haraka.
Umepata na msaidizi huyu OKW BOBAN SUNZU
 
Last edited by a moderator:
nilienda kwa palizi la ufuta.......uache unazi sasa, Rage alipata alichotaka kwenye michezo kama anavyitaka sasa Malinzi na Tenga................Yanga walimozmea Okwi.................

Usijali Mkuu, kwa niaba ya wanazi wenzangu wa Yanga, naomba radhi kwa kitendo kile.

Nanyi wanazi wa Simba mlimzomea Tambwe na wengine mkadai kuwa yule beki hana hatia, kwa kuwa kafungiwa mechi 3 kama Morris, mmoja wenu atuombe radhi pia kwa kitendo kile kisichokuwa cha uanamichezo.
 
...namsubiri mchambuzi mahiri wa soka revocatus Kashanga akitabiri mechi ya Yanga na BDF XI...
 
Last edited by a moderator:
Sasa mkuu Masuke nimekuwekea full nondo, jina langu nitaitwa Nshoma.
Upande wa baba itakuwa Jongh'eka na upande wa mama ni Ngh'ungulu hata kutamka siwezi hahahahahaaaa!!!

Haya mila sasa huwa wanapiga magoti wakati wa kusalimia eeh, mdogo kumuanza kumsalimia mkubwa, mnatambika na kulima kwa ng'ombe.
Pia huwa mnao mke zaidi ya mmoja sijui hii inakuaje aah.
Halafu sijui naanza jisikiaje, miye kuwa msukuma aaah kama sitaki vile. Hivi naanzaje kuhama kabila kwanza hahahaaaa.
Ila karibu Yanga na ndio tayari kuanzia leo Masuke ni Yanga, nimeshakamilisha usajili hapo juu!!!
 
Last edited by a moderator:
Hayo majina kiboko, jina la Nshoma ni common sana ila hayo mawili ni balaa.

Baadhi ya mila na Tamaduni:


  • Wanawake kupiga magoti wakati wanasalimia.
  • Wanawake kupiga magoti anapokuwa anampa maji ya kunywa mkubwa wake.
  • Kulima na ng'ombe ni kazi ya wanaume lakini kama familia haina wanaume wengi ni ruksa kwa wanawake kufanya kazi hiyo.
  • Kuchunga ng'ombe ni kazi ya wanaume.
  • Kutunza watoto ni kazi ya wanawake.
  • Mwanaume anaweza kuoa wanawake wengi.
  • Ikitokea binti amezaa kabla ya kuolewa mtoto hupewa ubini wa mjomba wake.
  • Ikitokea umetorosha binti na bahati mbaya akafa kabla hujatoa mahari lazima ulipie maiti ndo izikwe.
  • Mama akifariki wakati wa kujifungua kina mama wenzake hukusanyika na kuchukua vitu vingi (hata mimi sivijui maana ni siri ya wanawake) wanaenda navyo na kuvitupa kijiji kinachofuata uelekeo wa ziwa au mto mkubwa na hapa ikitokea mwanaume(hata mtoto mdogo wa kiume) umekutana na hilo kundi la wanawake unaweza kuuawa, wenyewe wanaamimi mwanamme ndo chanzo cha mwanamke mwenzao kufa. kina mama huficha ndani watoto zao wa kiume.
  • Mwanamke aliyeolewa akichelewa kupata mtoto mjomba wake lazima aende afanye tambiko kwenye familia ile na kuacha kondoo jike, mara nyingi kondoo aliyeachwa akizaa na huyu mama kizazi hufunguka.

  • Kuna makundi mawili ya upinzani, kama hauko kundi hili lazima utakuwa kundi fulani, makundi ni Bagika na Bagalu, ama unakuwa ngika ama unakuwa ngalu; Wewe Bantu lady umechagua kuwa kundi?
  • Mwanaume aliyeoa kwenye familia fulani anatakiwa kuwa na heshima kwa wana familia wote including watoto wadogo hasa wa kiume.

Baadhi ya miiko:
  • Ni marufuku kuoana ndugu na ikitokea mmeoana na mkazaa bila kujuana lazima mfanyiwe tambiko na mwanamme lazima atoe faini.
  • Ni marufuku vijana wadogo kujihusisha na mambo ya mapenzi pamoja na kunywa pombe.

Yanatosha hayo kwa leo, mengine siyakumbuki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…