A BITTER TRUTH: Kwanini watu weusi walishindwa kwenda Ulaya/Amerika (Ughaibuni) kuwachukua wazungu (Whites) kisha kuwaleta Afrika kuwafanya watumwa?

Hata wasipotufuata fuata tutapigana tu shida yetu kubwa tuna tamaa sana na roho mbaya tutamalizana wenyewe kwa wenyewe
Mkuu kuna mambo mengine haya epukiki kabisa hata ufanyeje! huko Mbinguni shetani alishikwa na tamaa akatamani kiti cha Mungu akashawishi theluthi 2 ya Malaika wote wakaasi mpakaleo wanateseka kwa mawazo Ulaya wao waliuana sana huko nyuma, wwi, wwii ni shida, achilia mbali ile ya Napoleon Bonaparte, juzijuzi tu Hx inasema Hitre aliua wazungu Miliion 50, yaani km Bongo yote.

Berlin conf. illiitshwa na wao wenyewe ili wasipigane hovyo, wakagawana Africa kwa maelewano mpaka leo! ni maeneo yao hati za umiliki ziko Vatican, ulishawahi sikia zimebadilishwa mkuu? wanayaita sijui Jumuiaya ya Madola. Mfaransa hagusi! na wao wana utaratibu aliyeanzisha ukorofi na akashindwa vita anawalipa wenzake, Germany ililipa ufaransa. USA lipaJapan
 
Mbona pia kulikuwa na white slaves from Spain,Italy na Europe walikuwa wanauzwa Morocco,Algeria na Libya ila wengi wao walikuwa Christian wanatekwa na Arabs...nyuma ya pazia history tunayosoma kuhusu slave trade imegeuzwa geuzwa haina ukweli vitu vingi vimefichwa ambavyo tungevijua wa Afrika vita kubwa ingetokea.
 
Wazungu walizijua shida mapema ...mfano ufinyu wa ardhi ambao watoke kutafuta mahali pengine ( ndo kuzaliwa kwa Amerika, Australia, New Zealand...) wengi wao walitamani sana kufika India mfano Vasco Dagama mpelelezi wa kireno yeye alitafuta njia ya kufika India akajikuta ameishia Africa na ndo alikuwa chanzo cha wareno kuja uku.

Kingine sisi Africa nadhani jamii nyingi za kale hazikuwa na utaratibu wa kwenda mbali zaid kutafuta maisha mengine ...kiufupi ni Kwamba wazungu walijua mambo mengi ambapo uku kwetu Africa yalikuwa ni mageni, mfano hao mababu hawakujua kuhusu umeme, bunduki, kuhusu magari ...wakati wenzetu walikuwa tayari wana wanasayansi kama Isaacs Newtown, Galileo, Wakina Telsa, Da Vinci, na wengineo wengi, sisi tulikuwa na akina kinjekitile ngwale, zwangendaba, mputa maseko, chief msuvero...

Kingine namna ya kutawala katika jamii nyingi za kiafrica pia ilichangia kuweza kutawaliwa kirahisi sana.
 
Sababu hasa ni ufinyu wa ardhi pamoja na malighafi ili kukidhi mahitaji ya viwanda vyao maana wao walipiga hatua mapema.
 
Kwanini mzungu awe mbali kidogo? Huu ndio msingi wa swali langu. Ina maana wazungu wapo very intelligent tangia zamani sana na ndio maana wanatawala dunia mpaka sasa?
Tofauti ni Kwamba bara ulaya wakati huo ilikuwa ni tabu tupu na shida nyingi, maana ardhi ilikuwa ndogo na kila mtawala aliitaka, sasa uku kwetu mambo yalikua shwari kabisa ..hakuna shida wala njaa mvua ni uwakika. Kiufupi matatizo waliyopitia wale jamaa yaliwapa namna ya kuweza kupambana ili kukidhi mahitaji yao.
 
Lakini hata hao mwarabu, wachina wahindi wamezizidi pia nchi nyingi za africa kimaendeleo ilhali na wao walitawaliwa na wazungu. Tatizo nini apo? Au namna ya kutawala ilikuwa tofauti?
 
Bila shaka wao walishindwa kuishi na matatizo/changamoto hivyo kila wakitatua changamoto/tatizo kinatokea kitu kipya (nimechoka/sipendi kutembea umbali mrefu basi nitaunda baiskeli, baiskeli haiwezi kubeba vitu vizito na haina Kasi pia natumia nguvu nyingi basi nitaunda gari yenye injini na yenye uwezo mkubwa kushinda baiskeli).

huku sisi tulizigeuza changamoto/matatizo kuwa kitu cha kawaida na kukizoea hivyo ikapelekea kuridhika na maisha hayo,hayo.
tukawa tunaishi ili siku ziende tu.
lakini kama ingekuwa kinyume chake basi history ingekuwa kinyume chake pia.

shida/changamoto ukizitafutia ufumbuzi basi lazima uendelee kwenye kila nyanja ya maisha yako.
 
Hakika umenena vema kaka
 
Kama nimemuelewa mleta hoja nikama anasema muafrika ndio wakwanza kuumbwa /kuwepo. Sasa iweje yeye asiwe na hivyo vyote ulivyotaja. ?
 
Kwa sababu hawakuhitaji wafanyakazi wa ziada, (surplus labour) waliridhika na walichokizalisha kwa wakati ule.
Kwamba wao waliamini maisha yatabaki vile vile tuuu? . Kama ndivyo uwezo wao wa kufikiria ulikua na upungufu
 
Kwa akili hizi kweli? . Tugundue nini[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Utumwa upo kila eneo la maisha yetu ni kutofkiri sawasawaa tuuu ndio kunatufanya tusijue kua maisha bila utumwa hayaendi.

Mfano. Kua na mbunge anae lipwa mamilioni kwa mwezi tena hata akiwa na elimu ya darasa la pili. Huku kuna mwalimu mwenye digrii anaelipwa laki tano, huo sio mfumo wa kitumwa. ?
 
Hapo ndio ujue akili zetu zilivyo, pale kabla ya hao wachina kuanza ujenzi na kuweka hiyo round about foleni ilikua balaaa.

Unajiuliza hawa wasomi wetu hata tuu kuweka hiyo round about walishindwa. ?
 
Na hapa ndio hoja ya mleta uzi ilipo.
 
Mkuu umezungumza ukweli,ila Watanzania wachache sana watakuelewa.Wengi wana macho lakini hawaoni,wana masikio lakini hawasikii.umejaribu kuelimisha lakini
 
Hili hata hailihitaji mjadala, ni ukweli usiopingika wazungu wanatuzidi kiakili, walituzidi enzi za mababu zetu na wanatuzidi hadi leo sisi wajukuu.
Ujerumani ya vita vya pili vya dunia inaweza ikagaragaraza Afrika yote ya leo kasoro Afrika Kusini maana kule kuna mzungu.
Waafrika sisi ni mzigo dunia hii, kazi kuzaliana tu.
 
Hitajiko la malighafi na nguvu kazi huko kwao ndio chachu iliyowapelekea kuja Africa .wakati sisi hatukuwa na mahitaji hayo kwa kiasi kikubwa hivyo tako zetu zililia bwata. Kama ilivyo mchukue mtoto wa masaki na uwanja wa fisi uwapambanishe basi utapata majibu.. n.b wazungu walianza kutawalana na kutumikishana wenyewe kwa wenyewe na kutokana na hali ngumu za kimazingira na kimaisha kiujumla mfumo wao ulikuwa strongest to survive hivyo waligaa gaa sana kutafuta ukuu ili wazidi kujiimarisha wakati sisi tukilewa neema ambayo wenzetu hawakuwa nayo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…