A God can be a mere theory, nothing more

A God can be a mere theory, nothing more

Huenda nisimwelewe au kumfahamu vizuri Mungu nnayemwamini, na huenda nikawa na maswali mengi kuhusu huyu Mungu nnayemwamini kuliko haya ya ndugu yangu Mashaxizo ila hayo yote hayajawahi kunishawishi niamini kwamba Mungu hayupo.

Pili, misingi ya imani ya Ukristo na Uislam iko tofauti sana mkuu licha ya baadhi ya mambo kuwepo kwenye Quran na Biblia takatifu. Mfano, kwa imani yangu Kifo cha Yesu na kufuguka kwake ndio msingi na nguzo ya imani yangu ya ki Kristo wakati Quran inapinga kufa kwa Yesu.

Hoja ya dini kuja kwa lengo la kututawala, Je, hizi dini zililetwa Afica tu na haziko huko kwa hao waliotutawala? na siku hizi hazipo tena huko kwa sababu lengo lao lilikua ni kututawala ambapo kazi ya dini itakua imemaliza umuhimu wake?

Na kwanini tuhoji kwamba kwanini Mungu anaacha mabaya au maovu yatokee kana kwamba tunataka huyu Mungu afanye kazi kama tunavyotaka sisi wanadamu? Ni sawa na wewe unapesa zako umeamua kuwekeza kwenye miradi ya aina flani na kununua gari za aina unayoitaka wewe kisha mtu mwingine ambaye hata hajui wewe unapanga kitu gani na aanze kukukosoa kwamba haufanyi sawa kisa, haujafanya kama anayofikiria yeye wewe unaweza kufanya.

Nimependa kichwa cha hii habari kwamba "...can be a mere theory...." ikimaanisha inaweza ikawa hivyo au isiwe hivyo.
 
Mashaxizo unaelekea kuwa ATHEIST taratibu na nilikuwa naliona hili kila nikikusoma......mtihani huu unao alafu nina hakika DINI yako hujaisoma vilivyo unaisomea mitandaoni ukichanganya ni twist za atheists wengine wamekuweza.....

POOR YOU...

unahitaji msaada mkubwa wa kuondokana na hili UNAWEZA KUNI PM nikusaidie
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mashaxizo ingekuwa vizuri kama ungejaribu kutaja vigezo ambavyo kwako unaona ni muhimu kwa kutambua dini iliyosahihi.

1- Mungu ni mjuzi/anajua yote. Akisema uongo huyo hajui anachokiongea so huyo si Mungu.

2- God is reasonable one. akiact or kufundisha unreasonably huyo si Mungu.

3- Mungu hana ubaguzi na anapenda watu wote. akifanya kinyume huyo si Mungu.

4- Ni hakimu wa haki. akifanya kinyume huyo si Mungu.

5- Sheria za Mungu yanakwenda na wakati na kutekelezeka, ikiwa kinyume huyo si Mungu.

Kwa mtazamo wangu ni sifa hizo kuu.
 
Last edited by a moderator:
"...Na hapo ndipo niliposema kwamba anaweza kuwepo but sie huyu anaeongelewa na Muslims and Christians."

Hapa umehit the spot sasa from my perspective na research yangu nliofanya first of all napinga sana ile story ya dunia ilivoumbwa, adam na hawa mara bustani ya edeni mara nyoka akawadanganya wakala mti wa kati , nyoka kulaaniwa na kutambaa sasa kama ni shetani alimwingilia nyoka kosa lake liko wapi na kama laana alipewa nyoka tu nin kilifanya wanyama wengine waache kuongea hizo ni story tu mtu aliandika kwa mtazamo wake a couple thousand years ago saivi kuna well elaboration ya theories kuexplain jinsi planet inavojitengeneza so kama dini ingeanza leo basi kuna namna wangelifitisha hili kwenye maandiko na yakaeleweka ila tatizo maandiko they're so old kwanin usiambiwe mafuriko yalitokea dunia nzima eti viumbe vili survive kisa kila kimoja kilibebwa kwenye boti flani!! Really?! ... Au mtu mweusi chanzo chake ni laana kuna mtu alimchungulia mzazi uzao wake uwe wa giza ndo ngozi hii nyeusi ilipoanzia seriously?! Ukieza kuamini hiyo story utaishi utumwani miaka yako yote sijawahi kuikubali hii kauli(chanzo cha mtu mweusi) kuanzia nlivokua mdogo nlivoeleZwa hivyo nlikataa mimi kua ni laana...haya lets drop that ninavoamini kama kweli Huyu Mungu ana exist basi sisi wanadamu pengine hatujajua ukuu wake if God is infinity how can his creation be less huu ukuu wa Mungu hautoshi kusmamiwa na vitabu vitatu vilivoandikwa karne ya kwanza kama Mungu kweli yupo na ukuu wake una exist hata sasa inabidi kuwe na a new body of knowledge inayoelezea ukuu wake currently na continuously

Then tunaambiwa mtume aliuita mwezi na kuugawa ukawa vipande viwili kwenye viganja vyake, infact wanauchulia mwezi kama mpira wa netball. then tunaambiwa Mungu kapanga kila kitu but ujinga unaendelea duniani haambiwi yeye ni source. watakao kwenda mbinguni na motoni tunaambiwa ameshawapanga.

Yaani hizi dini zinauongo kiasi kwamba hata uyo Mungu kama yupo, huko aliko anacheka sana!!!
 
Yawezekana ukawa sahihi, ila ukumbuke hata sie tunajazana makanisani na msikitini ila wengi wetu hatuna ufahamu na MUNGU tunayemwabudu.

Na huo ndio ukweli tumeadopt hako kamchezo tulikoletewa na wakoloni na wale waliotuuza.

Then nimegundua wale wasiojua maandiko ndio wanaimani sana.
 
..then tunaambiwa Mungu kapanga kila kitu but ujinga unaendelea duniani haambiwi yeye ni source. watakao kwenda mbinguni na motoni tunaambiwa ameshawapanga.

Yaani hizi dini zinauongo kiasi kwamba hata uyo Mungu kama yupo, huko aliko anacheka sana!!!

Naona umeushtukia uongo uliopo kwa jina la imani.

Hapa utaelewa kwa nini saa nyingine mtu unaona unyamaze tu, watu wakishavaa jezi ni ligi na ushabiki.
 
Tatizo lako ni kwamba unatumia logic kwa mambo mabayo yanataka Metaphysical approach ili kuyaelewa.Ukitumia logic kwenye mambo ya kiimani ni sawa tu na kumbiza kuvuli chako mwenyewe....utapoteza muda tuu na hutapata majibu ya kufaa!

Kwaiyo mkuu unataka kusema God ni unreasonable?

Then kwenye hiyo theory ya metaphysics mbona inakataa uwepo wake? na hao wanatumia metaphysics kukubali uwepo wa Mungu wanatumia tu reasoning.
 
Naona umeushtukia uongo uliopo kwa jina la imani.

Hapa utaelewa kwa nini saa nyingine mtu unaona unyamaze tu, watu wakishavaa jezi ni ligi na ushabiki.

Aisee ktk dini watu wanadanganywa sana, wengi huingia uoga wakiambiwa habari za motoni na story za watu walioangamizwa.
 
Laiti kama ungejua nguvu na Mamlaka ya Jina la Mungu unalolitaja taja Bila Heshima na Adabu usinge andika uzi wako huu.

Binadamu ni kiumbe dhaifu sana, Hata awe vipi upeo wake wa kutambua na kufikiri ni mdogo sana kuweza kutambua Mamlaka zote za Mungu.

Ikiwa ni hivyo hao wanaedai yupo wamemtambuaje?
Anyway you have free chance to choose either to believe on God or Devil.

Jiulize tu swali hili dogo,... Mtu anawezaje kufanya miujiza??
Soma point no. 9 ktk thread Mkuu.
Kwa mfano wakina Chriss Angel, David Blain(Google kwa kujua zaidi) na wengine wengi...! Waliwahi kutamba ulimwenguni kwa kufanya miujiza kwa nguvu za shetani.

So kama mtu anaweza kutumia nguvu za shetani kufanya miujiza basi kwa namna yoyote Mungu anaetajwatajwa yupo na anatenda miujiza vilevile.
Mkuu unaweza kuelezea shetani ni nani? ni kiumbe?
 
Huenda nisimwelewe au kumfahamu vizuri Mungu nnayemwamini, na huenda nikawa na maswali mengi kuhusu huyu Mungu nnayemwamini kuliko haya ya ndugu yangu Mashaxizo ila hayo yote hayajawahi kunishawishi niamini kwamba Mungu hayupo.

Pili, misingi ya imani ya Ukristo na Uislam iko tofauti sana mkuu licha ya baadhi ya mambo kuwepo kwenye Quran na Biblia takatifu. Mfano, kwa imani yangu Kifo cha Yesu na kufuguka kwake ndio msingi na nguzo ya imani yangu ya ki Kristo wakati Quran inapinga kufa kwa Yesu.

Hoja ya dini kuja kwa lengo la kututawala, Je, hizi dini zililetwa Afica tu na haziko huko kwa hao waliotutawala? na siku hizi hazipo tena huko kwa sababu lengo lao lilikua ni kututawala ambapo kazi ya dini itakua imemaliza umuhimu wake?

Na kwanini tuhoji kwamba kwanini Mungu anaacha mabaya au maovu yatokee kana kwamba tunataka huyu Mungu afanye kazi kama tunavyotaka sisi wanadamu? Ni sawa na wewe unapesa zako umeamua kuwekeza kwenye miradi ya aina flani na kununua gari za aina unayoitaka wewe kisha mtu mwingine ambaye hata hajui wewe unapanga kitu gani na aanze kukukosoa kwamba haufanyi sawa kisa, haujafanya kama anayofikiria yeye wewe unaweza kufanya.

Nimependa kichwa cha hii habari kwamba "...can be a mere theory...." ikimaanisha inaweza ikawa hivyo au isiwe hivyo.

Yah! kichwa kinasomeka vizuri.
Hata mimi naweza kusema Mungu yupo based on certain definition but Mungu wa waislamu na wakiristo hawezi kuwa Mungu coz ni muongo, unreasonable na anajicontradict.

Najua utashangaa mkuu but research yangu imeniridhisha hayo.
 
Mashaxizo unaelekea kuwa ATHEIST taratibu na nilikuwa naliona hili kila nikikusoma......mtihani huu unao alafu nina hakika DINI yako hujaisoma vilivyo unaisomea mitandaoni ukichanganya ni twist za atheists wengine wamekuweza.....

POOR YOU...

unahitaji msaada mkubwa wa kuondokana na hili UNAWEZA KUNI PM nikusaidie

Mkuu dini nimeisoma madrasa, nikasisoma kwenye darsa msikitini, nikaisoma shule na kuifanyia mitihani, hata chuo nimesoma ...... na shariah.

Unaposema dini nimeisoma mitandaoni hunitendei haki mkuu. vizuri umekubali kwamba hata post zangu za mwamzo ulikua unaziona, hukutaka tu kusema kwamba nilipinga ububusa and be unreasonable kisa dini imesema.

Anyway, unaweza ukawa sahihi na hisia zako kwa mtazamo wako or mtazamo wa kiimani. naweza kuja pm but nahisi hutopata kuwaamsha na wengine. Kuna maswali nimeuliza hapo kwa mada unaweza kunisaidia majibu mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Aisee ktk dini watu wanadanganywa sana, wengi huingia uoga wakiambiwa habari za motoni na story za watu walioangamizwa.

Sema wewe. Sisi tunaonekana vichaa.

Najua watu wanotambua hizo habari za motoni ni uongo na story nzima ni uzushi lakini wanakwenda kuswali kwa sababu dini kwao imekuwa kama therapy.

Hawakubali kukubali uhalisia wa maisha kwamba life is not fair. Hivyo mtu anaona akiswali kidogo shida zake zinapungua na anakua na amani fulani.
 
Ikiwa ni hivyo hao wanaedai yupo wamemtambuaje?

Soma point no. 9 ktk thread Mkuu.

Mkuu unaweza kuelezea shetani ni nani? ni kiumbe?

Ikiwa umeziweka akili zako kukataa uwepo wa Mungu hata uambiwe nini hautoelewa/utajifanya kutoelewa....

ikiwa mganga anaweza kukufanyia mazingaombwe/Viini macho Basi vise versa is true vilevile kwamba kuna alie zaidi ya vyote Katika Dunia hii..Nae Ni MUNGU.

Usidanganywe na akili zako zilizokuzwa na kupaliliwa na Theories, Principles na Ujuvi mdogo sana wa watu wa Dunia hii ambao nao wana uelewa finyu kuhusu Mwenyezi MUNGU.

Kumbbuka kama unataka kukubaliana na Mimi Kuhusu uwepo wa Mungu Kubali kwanza kwamba Ujuzi, Akili, Maarifa na vyote unavyojivunia ni Finyu, na hafifu.

Human Knowledge has Big Limitations to revel presence of God Only Faith can work through it.
 
Yah! kichwa kinasomeka vizuri.Hata mimi naweza kusema Mungu yupo based on certain definition but Mungu wa waislamu na wakiristo hawezi kuwa Mungu coz ni muongo, unreasonable na anajicontradict.Najua utashangaa mkuu but research yangu imeniridhisha hayo.
Hapana kaka, sijashangaa nafikiri unanielewa misimamo yangu kama nnavyoielewa yako na hatujawahi kwaruzana.Huu mjadala ungeweza kutufikirisha na kusaidia watu kutafakari juu ya Mungu. Kama tu watu wangekuja na maandiko na maelezo ya kujitosheleza kuhusu Mungu wanae mwamini.Narudia tena, naamini Mungu yupo licha ya kutokumwelewa kiufasaha, lakini hata tunapokua kwenye ibada hua najaribu kufikiriaJe, hivi katika watu hawa wote kila mmoja ana uelewa sawa au ufaham sawa kuhusu Mungu anaemwabudu? Hapo naongelea watu ambao wako kwenye kusanyiko moja achilia mbali dini au dhehebu lingine.
 
1- Mungu ni mjuzi/anajua yote. Akisema uongo huyo hajui anachokiongea so huyo si Mungu.

2- God is reasonable one. akiact or kufundisha unreasonably huyo si Mungu.

3- Mungu hana ubaguzi na anapenda watu wote. akifanya kinyume huyo si Mungu.

4- Ni hakimu wa haki. akifanya kinyume huyo si Mungu.

5- Sheria za Mungu yanakwenda na wakati na kutekelezeka, ikiwa kinyume huyo si Mungu.

Kwa mtazamo wangu ni sifa hizo kuu.

Sasa hizo ni sifa za kutambua dini sahihi au hizo ni za Mungu?
 
Laiti kama ungejua nguvu na Mamlaka ya Jina la Mungu unalolitaja taja Bila Heshima na Adabu usinge andika uzi wako huu.

Binadamu ni kiumbe dhaifu sana, Hata awe vipi upeo wake wa kutambua na kufikiri ni mdogo sana kuweza kutambua Mamlaka zote za Mungu.





Hapa mimi ndo nlikua napataka hii inaonesha dhahiri watu walivo na uelewa mdogo wa Mungu basi kama hamtujui Mungu kwakua sisi ni wadhaifu sana na yeye alie Mkuu sana its safe to say kuna mambo ya uongo tunayompakazia Mungu wetu na huenda yanayotokana na huo udhaifu wetu na ukuu wake tuendeleeni kujitahidi kumtafuta Mungu tusichoke tena bila woga tukazane
 
Sema wewe. Sisi tunaonekana vichaa.

Najua watu wanotambua hizo habari za motoni ni uongo na story nzima ni uzushi lakini wanakwenda kuswali kwa sababu dini kwao imekuwa kama therapy.

Hawakubali kukubali uhalisia wa maisha kwamba life is not fair. Hivyo mtu anaona akiswali kidogo shida zake zinapungua na anakua na amani fulani.

Kwani ukweli ni upi ambao unakufanya wewe useme hayo mambo ya motoni ni uongo?
 
Hapa mimi ndo nlikua napataka hii inaonesha dhahiri watu walivo na uelewa mdogo wa Mungu basi kama hamtujui Mungu kwakua sisi ni wadhaifu sana na yeye alie Mkuu sana its safe to say kuna mambo ya uongo tunayompakazia Mungu wetu na huenda yanayotokana na huo udhaifu wetu na ukuu wake tuendeleeni kujitahidi kumtafuta Mungu tusichoke tena bila woga tukazane

Kumbuka kwa sisi wakristu tunashauriwa kumwomba roho mtakatifu atusaidie kuweza kumjua vyema huu Mungu, Bila yeye ni Ngumu kumfahamu Yehova Muweza wa yote.

usitegemee akili zako mweyewe, tumwombe yeye atuwezeshe kuweza kumjua zaidi.
 
Mkuu when i was Muslim niliuliza swali hilo kwa mashehe wakaanza kunipa siasa kwamba Mungu alituma mitume jamii zote! teh teh, nilipouliza ni Mtume gani alietumwa nje ya far east wakaniambia Mungu hakutaka tu kuwataja kwenye kitabu kitakatifu! But unaweza kujiuliza mbona hakuna historia yoyote au kitabu cha historia kinachoonesha nje na far east kulikua na hayo mafundisho? Hapo unaambiwa Mungu ndie ajuae!!!!

Swali hilo hilo nililileta hapa jf atleast kuskia na mawazo ya wakiristo bu ile mada ilifika page tano bila jibu.
Kwa nini tanzania haijawahi kutawaliwa na mnyakusa ni kwamba hakuna wasomi, kwa nini kwa nini ujerumani haijawahi kutawaliwa na mweusi hakuna weusi waliosoma kule...
 
Back
Top Bottom