Ahsante sana mkuu 'Bush...'. Mada za namna hii ndizo zingeheshimika sana katika jukwaa kama hili hapa JF.Sikuwa nafahamu kwamba huyu Tundu Lissu ana Ushawishi Mkubwa namna hii sio tu leo ambapo tunamuona kwenye Jukwaa la Siasa bali kazi ya kutetea Nchi, Taifa na Wanachi wake ameianza Zamani ktk Ujana wake woote.
Kwamba Tundu Lissu anaweza kuwa na Influence kwenye Tasisi kubwa kama baraza la Taifa la kiislam BAKWATA, Baraza la Kikristo Tanzania CCT, Tanzania Episcopal Council TEC, Legal and Human Right Centre(LHRC) na miamba wengine wa Uchumi ktk taasisi mbalimbali kama University of Dar Es Salaam.
Ushiriki wa Taasisi kubwa za namna hii katika uchambuzi, utafiti na hatimaye ku ripoti taarifa hizi za Uchimbaji wa madini ya Dhahabu Tanzania umetokana na ukweli kwamba;
1. Mwenyezi Mungu ndiye aliyeumba Tanzania na vitu vyote vilivyomo.
2. Kwamba Mungu alipomuumba Mwanadamu alitaka aishi maisha ya ukamilifu na utajiri hivyo kila alipo Mwanadamu kuna vyanzo vya uchumi vinavyomuwezesha kuishi na Kustawi.
Wame quote kitabu cha Zaburi 24: 1.
Katika Utafiti na matokeo yao waligundua mambo makuu matatu.
1. Migodi ya Dhahabu inatoa kiasi kidogo cha mapato ya Kodi
2.Usiri Mkubwa kwenye miradi ya madini na hivyo hatari ua kuwepo mazingira ya Rushwa
3.Watu na wananchi jirani katika migodi hii hawananufaiki chochote na wanazidi kuwa maskini.
Mada mahususi
1. The Tax System and its Hidden subsidies
2. Alleged Tax Evasion
3. Democracy and Transparency
4. Local economic development
Uhondo unapatikana zaidi ukiangalia jinsi walivyochambua mapato na uvunaji wa madini ya Dhahabu kutoka migodi ifuatayo
➡️AngroGold Ashanti, kampuni inayomilikiwa kwa ubia wa Ghana na South Africa hawa wanamiliki migodi ya GGM huko Geita
➡️Barrick- hii ya Wakanada wanamiliki mgodi wa Bulyankulu
➡️Australian company wanaomiliki Migodi ya Dhahabu ya North Mara under East African Gold Mines brand.
Pia wameongelea "The Buzwagi contract"
Ktk takwimu zao kwenye majedwali mbali mbali wame extraxt data na taarifa kutoka kwenye vyanzo mbali mbali ikiwemo
Tume ya Taifa ya Madini, Wizara ya Nishati na Madini, Tanzaniani Chamber of Mines, Tanzania Revenue Authority TRA.
Jambo lingine lilonishangaza ktk ripoti hii ni kuwa matatizo yanayotokana na migogoro na Machimbo ya madini ya Dhahabu yanafanana ktk Nchi nyingi za Africa, ambapo inaonekana baadhi ya viongozi ktk nchi hizo wanashirikiana na wezi wa kigeni na kudidimiza wananchi wao.
Basi mwisho wakamaliza na Recomendations zao.
Walitoa mapendekezo 7.
Ukitazama kwa umakini ni Copy and Paste ya zile za Tume ya Uchunguzi ya Prof Usoro na Prof Mruma.
Hii ni repoti ya mwaka 2008 toleo la pili.
Wakati nikisoma maelezo yako, nikawa naingiwa na dukuduku la kutaka nikwambie usipige stori ndefu, tuwekee tune wenyewe. Kumbe hapo mwisho umefanya kweli.
Nchi yetu Tanzania sasa kuna ombwe kubwa sana la wasomi/wana siasa wa aina ya Tundu Lissu. Watu wameweka elimu zao pembeni na kujikita katika kuwa maroboti tu ya kutumiwa na wanasiasa hata wasiokuwa na kitu kichwani.
Katika mawaziri tulio nao/tuliowahi kuwa nao, ni wangapi wametumia taaluma zao hata kuchapisha tu makala kwenye gazeti la kawaida?
Kwa hiyo, ninapoona mtu, kama Tundu Lissu akijipambanua kuwa tofauti kabisa na wengi wengine, hiyo inanipa matumaini makubwa. Ni muhimu taifa letu lirudi kwenye misingi yake. Watu watumie elimu waliyo nayo katika kulijenga taifa hili.
Sijawahi kuona andiko lolote la maana toka kwa:
Kikwete; kabudi, Samia, Nchemba Madilu, na wengi wengine wanaotupigia kelele kila siku Bungeni na kwenye Baraza la Mawaziri, CCM na kwingineko.
Naheshimu, uwezo wa Zitto Kabwe (ukiweka mbali siasa zake).
Kwa hiyo, Tundu Lissu ni tofauti kubwa sana na hawa wengine wote kwa sasa.